2 Nyakati 23 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

2 Nyakati 23:1-21

Uasi Dhidi Ya Athalia

(2 Wafalme 11:4-20)

123:1 2Fal 11:4Katika mwaka wa saba, Yehoyada akaonyesha nguvu zake. Alifanya agano na wakuu wa vikosi vya mamia: yaani Azaria mwana wa Yerohamu, Ishmaeli mwana wa Yehohanani, Azaria mwana wa Obedi, Maaseya mwana wa Adaya, na Elishafati mwana wa Zikri. 223:2 Hes 35:2-5; Za 112:5Wakazunguka katika Yuda yote na kukusanya Walawi na viongozi wa jamaa za Israeli kutoka miji yote. Walipofika Yerusalemu, 323:3 2Fal 11:17; 2Sam 7:12; 1Fal 2:4; Za 89:29; 1Fal 9:5; 2Nya 6:16; 7:18; 21:7kusanyiko lote likafanya agano na mfalme katika Hekalu la Mungu.

Yehoyada akawaambia, “Mwana wa mfalme atatawala, kama Bwana alivyoahidi kuhusu wazao wa Daudi. 423:4 1Nya 9:25; Lk 1:8-9Basi hivi ndivyo iwapasavyo kufanya: Theluthi yenu makuhani na Walawi ambao mnaingia zamu siku ya Sabato mtalinda milangoni, 523:5 Mdo 3:2theluthi yenu mtalinda jumba la kifalme, na theluthi nyingine mtalinda Lango la Msingi. Walinzi wengine wote mwe ndani ya nyua za Hekalu la Bwana. 623:6 1Nya 23:28-29; Hes 16:5; Zek 3:7; 2Fal 11:6-7; Ezr 8:28Hakuna mtu yeyote ataingia katika Hekalu la Bwana isipokuwa makuhani na Walawi walioko kwenye zamu. Wao wanaweza kuingia kwa sababu ni watakatifu, lakini watu wengine wote itawapasa kulinda kile walichoamriwa na Bwana. 7Walawi watajipanga kumzunguka mfalme, kila mtu akiwa na silaha zake mkononi. Mtu mwingine yeyote aingiaye Hekaluni lazima auawe. Kaeni karibu na mfalme popote aendapo.”

823:8 2Fal 11:9; 1Nya 24:1Walawi na watu wote wa Yuda wakafanya kama vile kuhani Yehoyada aliagiza. Kila mmoja akawachukua watu wake, wale waliokuwa wakiingia zamu siku ya Sabato na wale waliokuwa wakienda mapumziko, kwa sababu kuhani Yehoyada hakuruhusu kikosi chochote kiondoke. 9Kisha akawapa wakuu wa vikosi vya mamia mikuki na ngao kubwa na ndogo zilizokuwa za Mfalme Daudi, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu. 10Akawapanga walinzi wote kumzunguka mfalme, kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi mwake, karibu na madhabahu na Hekalu, kuanzia upande wa kusini hadi upande wa kaskazini mwa Hekalu.

1123:11 Kut 25:16; Kum 17:18; 2Sam 16:16; Kut 31:18; Isa 8:16-20; 1Sam 10:24Yehoyada na wanawe wakamtoa Yoashi mwana wa mfalme nje na kumvika taji. Wakampa nakala ya agano na kumtangaza kuwa mfalme. Wakamtia mafuta na kupaza sauti, wakisema, “Mfalme aishi maisha marefu!”

12Athalia aliposikia kelele za watu wakikimbia na kumsifu mfalme, akawaendea watu katika Hekalu la Bwana. 1323:13 1Fal 1:41; 7:15; 18:17-18; Rum 2:3Athalia akaangalia, tazama alikuwepo mfalme akiwa amesimama karibu na nguzo yake kwenye ingilio. Maafisa na wapiga tarumbeta walikuwa kando ya mfalme, nao watu wote wa nchi walikuwa wanashangilia na kupiga tarumbeta na waimbaji wakiwa na vyombo vya uimbaji, walikuwa wakiongoza nyimbo za sifa. Ndipo Athalia akararua mavazi yake na kupiga kelele, akisema, “Uhaini! Uhaini!”

1423:14 Hes 5:2; 19:14Kuhani Yehoyada akawatuma majemadari wa vikosi vya mamia, waliokuwa viongozi wa jeshi, na kuwaambia: “Mleteni nje kati ya safu, na mkamuue kwa upanga yeyote anayemfuata.” Kwa kuwa kuhani alikuwa amesema, “Msimuulie ndani ya Hekalu la Bwana.” 1523:15 Neh 3:28; Yer 31:40; Mwa 9:5; 2Nya 22:10; Mt 7:2Kwa hiyo wakamkamata alipofika kwenye ingilio la Lango la Farasi katika viwanja vya jumba la mfalme wakamuulia hapo.

1623:16 2Nya 34:31; Neh 9:38; 2Nya 15:12; Kum 5:2-3; 2Fal 11:17; 2Nya 19:10; Ezr 10:3Kisha Yehoyada akafanya agano kwamba yeye na watu wote na mfalme watakuwa watu wa Bwana. 1723:17 Kum 13:6-9; 2Fal 10:23; 11:18; 18:4; 2Nya 34:4-7Kisha watu wote wakaenda kwenye hekalu la Baali na kulibomoa. Wakavunjavunja madhabahu pamoja na sanamu na kumuua Matani kuhani wa Baali mbele ya hayo madhabahu.

1823:18 1Nya 23:28-32; 2Nya 5:5; Kut 29:38; Hes 28:2; 1Nya 23:6Kisha Yehoyada akaweka uangalizi wa Hekalu la Bwana mikononi mwa makuhani, waliokuwa Walawi, ambao Mfalme Daudi alikuwa amewagawa ili wahudumu hekaluni kwa ajili ya kutoa sadaka za kuteketezwa za Bwana kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, kwa kushangilia na kuimba kama Daudi alivyokuwa ameagiza. 1923:19 1Nya 9:22Pia akawaweka mabawabu kwenye malango ya Hekalu la Bwana ili kwamba kwa vyovyote asije akaingia mtu yeyote aliye najisi.

2023:20 2Fal 15:25; 11:19Akawachukua majemadari wa mamia, watu waheshimiwa, viongozi wa watu pamoja na watu wote wa nchi na kumteremsha mfalme kutoka Hekalu la Bwana. Wakaingia kwenye jumba la mfalme kupitia Lango la Juu na kumkalisha mfalme kwenye kiti cha enzi, 2123:21 2Nya 22:1; 1Sam 11:15; Za 58:10; Mit 11:10; 1Fal 1:40; 2Fal 11:20; Mit 29:2nao watu wote wa nchi wakafurahi. Mji ukatulia kwa sababu Athalia alikuwa ameuawa kwa upanga.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

歷代志下 23:1-21

耶何耶大立約阿施為猶大王

1第七年,耶何耶大發憤圖強,召來一些百夫長與他們立約。他們是耶羅罕的兒子亞撒利雅約哈難的兒子以實瑪利俄備得的兒子亞撒利雅亞大雅的兒子瑪西雅,以及細基利的兒子以利沙法2他們走遍猶大各城,把利未人和以色列的各族長召集到耶路撒冷3全體會眾到上帝的殿中與王立約。耶何耶大對他們說:「王的兒子當做王!這是耶和華對大衛子孫的應許。 4你們要這樣做,在安息日值班的祭司和利未人要撥出三分之一的人把守各門, 5三分之一的人把守王宮,三分之一的人把守基址門,所有民眾要留在耶和華殿的院子裡。 6只有祭司和供職的利未人可以進耶和華的殿,因為他們是聖潔的。其他人一律不准進殿。所有的人都要遵守耶和華的吩咐。 7利未人要手持兵器護衛在王周圍。凡擅自進殿的,一律處死。無論王去哪裡,你們都要緊隨左右。」

8於是,利未人和所有猶大人遵令而行,各自帶來在安息日值班和休班的屬下,因為耶何耶大祭司沒有讓他們休班。 9耶何耶大祭司把上帝殿中大衛王的矛槍和大小盾牌交給百夫長。 10耶何耶大安排眾人手持兵器,從殿右到殿左,在祭壇和殿周圍護衛王。 11耶何耶大及其眾子領王子出來,給他戴上王冠,把約書交給他,膏立他為王。眾人高呼:「願王萬歲!」

亞她利雅被處死

12亞她利雅聽到人們奔走稱頌王的聲音,便走進耶和華的殿,到眾人那裡。 13她看見王站在門口的柱旁,百夫長和吹號的人侍立在王左右,眾人都歡呼吹號,歌樂手用各種樂器帶領眾人歌唱頌揚,便撕裂衣服,喊道:「反了!反了!」 14耶何耶大祭司認為不可在耶和華的殿裡處死亞她利雅,便命令帶兵的百夫長出來,對他們說:「把她帶出去並用刀殺死所有跟隨她的人。」 15他們抓住她,把她帶到馬匹進出王宮的入口,在那裡殺了她。

耶何耶大的改革

16耶何耶大讓民眾和王與他一起立約,要做耶和華的子民。 17於是,民眾出去拆毀了巴力廟,砸碎祭壇和偶像,在壇前殺了巴力的祭司瑪坦18耶何耶大大衛的吩咐,讓利未祭司負責耶和華殿裡的事務。大衛曾吩咐利未祭司在耶和華的殿中司職,照摩西的律法向耶和華獻燔祭,歡呼歌唱。 19耶何耶大還派門衛把守耶和華殿的各門,禁止一切不潔淨的人入內。 20他率領百夫長、貴族、首領和全體民眾護送王從耶和華的殿下來,經上門進入王宮,擁立王登上王位。 21民眾都歡喜快樂,城裡安定,因為亞她利雅已死在刀下。