2 Nyakati 20 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 20:1-37

120:1 1Nya 4:41Ikawa baada ya jambo hili, Wamoabu na Waamoni, pamoja na baadhi ya Wameuni wakaja ili wapigane vita na Yehoshafati.

220:2 Mwa 14:7; Wim 1:14; Yos 15:62; 1Sam 23:29Watu fulani wakaja wakamwambia Yehoshafati, “Jeshi kubwa linakuja dhidi yako kutoka Edomu tokea ngʼambo ile nyingine ya Bahari.20:2 Yaani Bahari ya Chumvi. Tayari liko Hasason-Tamari” (yaani En-Gedi). 320:3 Es 4:16; Isa 58:6; Amu 20:26; Ezr 8:21-23; 1Sam 7:6; Yer 36:9; Yn 3:5Yehoshafati akaogopa, akaazimu kumtafuta Bwana, na akatangaza kwa Yuda wote kufunga. 420:4 Yoe 1:14Watu wa Yuda wakakusanyika pamoja ili kutafuta msaada kutoka kwa Bwana. Wakaja kutoka kila mji wa Yuda ili kumtafuta.

5Kisha Yehoshafati akasimama katika kusanyiko la Yuda na Yerusalemu katika Hekalu la Bwana, mbele ya ua mpya, 620:6 Mt 6:9; Kum 4:39; 1Fal 8:23; 1Nya 29:11-12; Yos 2:11; Isa 57:15; Za 47:2; 62:11; Yer 27:5; Dan 4:17; Mt 6:13akasema:

“Ee Bwana, Mungu wa baba zetu, si wewe ndiwe uliye Mungu mbinguni? Si wewe ndiwe utawalaye juu ya falme zote za mataifa? Uweza na nguvu viko mkononi mwako, wala hakuna yeyote awezaye kushindana nawe. 720:7 Isa 41:8; Yak 2:23; Mwa 17:7; Kut 6:7Je, si wewe, Ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa nchi hii mbele ya watu wako Israeli, ukawapa wazao wa Abrahamu, rafiki yako, hata milele? 820:8 2Nya 6:20-28Wameishi ndani yake na humo wamekujengea mahali patakatifu kwa ajili ya Jina lako, wakisema: 920:9 1Fal 8:33-37; 2Nya 6:28-29‘Kama maafa yakitujia, ikiwa ni upanga, hukumu, tauni, au njaa, tutasimama mbele zako, mbele ya Hekalu hili ambalo limeitwa kwa Jina lako na kukulilia katika shida yetu, nawe utatusikia na kutuokoa.’

1020:10 Hes 20:14-21; Kum 2:4-6, 9, 18-19“Lakini sasa hawa watu wa kutoka Amoni, Moabu na Mlima Seiri, ambao hukuwaruhusu Israeli wazivamie nchi zao wakati walitoka Misri, hivyo wakageukia mbali nao na hawakuwaangamiza, 1120:11 Za 83:1-12tazama jinsi wanavyotulipa kwa kuja kututupa nje ya milki uliyotupa sisi kuwa urithi. 1220:12 2Kor 3:5; Amu 11:27; Mik 7:7; Za 12:1-2; 1Sam 3:13; Za 46:7-11; Ufu 19:11; Za 25:15Ee Mungu wetu, je, wewe hutawahukumu? Kwa kuwa sisi hatuna uwezo wa kukabiliana na jeshi hili kubwa linalokuja kutushambulia. Sisi hatujui la kufanya, bali macho yetu yanakutazama wewe.”

13Watu wote wa Yuda pamoja na wake zao, watoto wao na wadogo wao wakasimama pale mbele za Bwana.

1420:14 Hes 11:25; 24:2; 1Nya 12:18; 2Nya 15:1; 24:20Ndipo Roho wa Bwana akaja juu ya mtu mmoja jina lake Yahazieli mwana wa Zekaria, mwana wa Benaya, Mwana wa Yeieli, mwana wa Matania, Mlawi mzao wa Asafu alipokuwa amesimama katika kusanyiko.

1520:15 2Nya 32:7; Kut 14:13-14; Za 91:8; Kum 1:29; 31:6-8Akasema: “Sikilizeni, enyi Yuda wote nanyi nyote mkaao Yerusalemu, nawe Mfalme Yehoshafati! Hili ndilo Bwana asemalo kwenu, ‘Msiogope wala msifadhaike kwa sababu ya jeshi hili kubwa. Kwa maana vita hivi si vyenu, bali ni vya Mungu. 16Kesho shukeni kukabiliana nao. Watakwea kwa kupandia Genge la Sisi, nanyi mtawakuta mwisho wa bonde, kabla ya Jangwa la Yerueli. 1720:17 Hes 14:9; 2Nya 15:2; Kut 14:13; 2Nya 32:8; Za 46:7-11; Isa 8:10; Amo 5:14Hamtahitaji kupigana vita hivi. Kaeni kwenye nafasi zenu, simameni imara na mkaone wokovu Bwana atakaowapatia, enyi Yuda na Yerusalemu. Msiogope, wala msifadhaike. Kesho tokeni mwende mkawakabili, naye Bwana atakuwa pamoja nanyi.’ ”

1820:18 Mwa 24:26; Kut 4:31Yehoshafati akainamisha uso wake chini, nao watu wote wa Yuda na Yerusalemu wakaanguka chini ili kuabudu mbele za Bwana. 19Ndipo baadhi ya Walawi kutoka kwa Wakohathi na kwa wana wa Kora wakasimama na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sauti kuu sana.

2020:20 Isa 7:9; Mwa 39:3; Mit 16:3; Rum 8:31; Isa 26:3; Yn 11:40; 14:1Asubuhi na mapema wakaondoka kuelekea Jangwa la Tekoa. Walipoanza safari, Yehoshafati akasimama akasema, “Nisikilizeni, enyi Yuda, na watu wa Yerusalemu! Mwaminini Bwana Mungu wenu, hivyo mtathibitika, wasadikini manabii wake nanyi mtafanikiwa. 2120:21 1Nya 16:29; 2Nya 5:13; Za 136:1Alipomaliza kushauriana na watu, Yehoshafati akawaweka watu wa kumwimbia Bwana na kumsifu katika utukufu wa utakatifu wake walipokuwa wametangulia mbele ya jeshi, wakisema:

“Mshukuruni Bwana

kwa kuwa upendo wake wadumu milele.”

2220:22 Amu 7:22; 2Nya 13:13; 1Sam 14:20Walipoanza kuimba na kusifu, Bwana akaweka waviziao dhidi ya watu wa Amoni, Moabu na wale wa Mlima Seiri waliokuwa wamekuja kuishambulia Yuda, nao wakashindwa. 2320:23 Mwa 19:38; 2Nya 21:8; Eze 38:21Watu wa Amoni na Moabu wakawainukia watu wa Mlima Seiri ili kuwaua na kuwaangamiza kabisa. Baada ya kumaliza kuwachinja watu wa Seiri, wakaangamizana wao kwa wao.

2420:24 Isa 37:36; Yer 33:5; Kut 14:13Yuda walipofika katika mnara wa ulinzi wa jangwani, wakaliangalia lile jeshi kubwa, wakaona ni maiti tupu zimetapakaa ardhini, wala hakuna yeyote aliyenusurika. 25Hivyo Yehoshafati na watu wake wakaenda kujitwalia nyara kutoka kwao, nao wakakuta humo wingi wa mifugo, mali, nguo na vitu vya thamani, ambavyo vilikuwa vingi zaidi ya vile walivyoweza kuchukua. Wakakusanya nyara kwa siku tatu kwa sababu zilikuwa nyingi mno. 26Siku ya nne wakakusanyika katika Bonde la Beraka20:26 Bonde la Beraka maana yake Bonde la Kusifu. kwa maana huko ndiko walikomsifu Bwana. Ndiyo sababu linaitwa Bonde la Beraka mpaka leo.

2720:27 Neh 12:43Kisha watu wote wa Yuda na Yerusalemu, wakiongozwa na Yehoshafati, wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kwa kuwa Bwana alikuwa amewasababisha wafurahi juu ya adui zao. 28Wakaingia Yerusalemu na kwenda hekaluni mwa Bwana wakiwa na vinubi, zeze na tarumbeta.

2920:29 Mwa 35:5; Kum 2:25; 14:14; 2Nya 17:10Hofu ya Mungu ikazipata falme zote za nchi waliposikia jinsi Bwana alivyokuwa amepigana dhidi ya adui za Israeli. 3020:30 2Nya 15:15; 1Nya 22:9; Ay 34:29Ufalme wa Yehoshafati ukawa na amani, kwa kuwa Mungu wake alikuwa amemstarehesha pande zote.

Mwisho Wa Utawala Wa Yehoshafati

(1 Wafalme 22:41-50)

3120:31 1Fal 22:41Hivyo Yehoshafati akatawala Yuda. Alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, akatawala katika Yerusalemu kwa miaka ishirini na mitano. Mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi. 32Alienenda katika njia za Asa baba yake wala hakwenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana. 3320:33 2Nya 12:14; 17:6Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa, na watu wakawa bado hawajaelekeza mioyo yao kwa Mungu wa baba zao.

3420:34 1Fal 16:1-3Matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu cha Yehu mwana wa Hanani, ambazo zimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli.

3520:35 2Nya 16:3; 19:1-3Hatimaye Yehoshafati mfalme wa Yuda akafanya urafiki na Ahazia mfalme wa Israeli ambaye alifanya maovu sana. 3620:36 1Fal 22:49Akaungana naye kutengeneza meli nyingi za kwenda Tarshishi,20:36 Au: za biashara (ona pia 1Fal 10:22; 22:48; 2Nya 9:21; Isa 2:16; 60:9). nazo zilitengenezwa huko Esion-Geberi. 3720:37 1Fal 9:26; 2Nya 9:21; Mwa 10:4; 1Fal 10:22Ndipo Eliezeri mwana wa Dodavahu wa Maresha akatoa unabii dhidi ya Yehoshafati, akasema, “Kwa kuwa umeungana na Ahazia, Bwana ataangamiza vile mlivyotengeneza.” Zile meli zikavunjika na hazikuweza kungʼoa nanga ili kwenda Tarshishi.

New International Version

2 Chronicles 20:1-37

Jehoshaphat Defeats Moab and Ammon

1After this, the Moabites and Ammonites with some of the Meunites20:1 Some Septuagint manuscripts; Hebrew Ammonites came to wage war against Jehoshaphat.

2Some people came and told Jehoshaphat, “A vast army is coming against you from Edom,20:2 One Hebrew manuscript; most Hebrew manuscripts, Septuagint and Vulgate Aram from the other side of the Dead Sea. It is already in Hazezon Tamar” (that is, En Gedi). 3Alarmed, Jehoshaphat resolved to inquire of the Lord, and he proclaimed a fast for all Judah. 4The people of Judah came together to seek help from the Lord; indeed, they came from every town in Judah to seek him.

5Then Jehoshaphat stood up in the assembly of Judah and Jerusalem at the temple of the Lord in the front of the new courtyard 6and said:

Lord, the God of our ancestors, are you not the God who is in heaven? You rule over all the kingdoms of the nations. Power and might are in your hand, and no one can withstand you. 7Our God, did you not drive out the inhabitants of this land before your people Israel and give it forever to the descendants of Abraham your friend? 8They have lived in it and have built in it a sanctuary for your Name, saying, 9‘If calamity comes upon us, whether the sword of judgment, or plague or famine, we will stand in your presence before this temple that bears your Name and will cry out to you in our distress, and you will hear us and save us.’

10“But now here are men from Ammon, Moab and Mount Seir, whose territory you would not allow Israel to invade when they came from Egypt; so they turned away from them and did not destroy them. 11See how they are repaying us by coming to drive us out of the possession you gave us as an inheritance. 12Our God, will you not judge them? For we have no power to face this vast army that is attacking us. We do not know what to do, but our eyes are on you.”

13All the men of Judah, with their wives and children and little ones, stood there before the Lord.

14Then the Spirit of the Lord came on Jahaziel son of Zechariah, the son of Benaiah, the son of Jeiel, the son of Mattaniah, a Levite and descendant of Asaph, as he stood in the assembly.

15He said: “Listen, King Jehoshaphat and all who live in Judah and Jerusalem! This is what the Lord says to you: ‘Do not be afraid or discouraged because of this vast army. For the battle is not yours, but God’s. 16Tomorrow march down against them. They will be climbing up by the Pass of Ziz, and you will find them at the end of the gorge in the Desert of Jeruel. 17You will not have to fight this battle. Take up your positions; stand firm and see the deliverance the Lord will give you, Judah and Jerusalem. Do not be afraid; do not be discouraged. Go out to face them tomorrow, and the Lord will be with you.’ ”

18Jehoshaphat bowed down with his face to the ground, and all the people of Judah and Jerusalem fell down in worship before the Lord. 19Then some Levites from the Kohathites and Korahites stood up and praised the Lord, the God of Israel, with a very loud voice.

20Early in the morning they left for the Desert of Tekoa. As they set out, Jehoshaphat stood and said, “Listen to me, Judah and people of Jerusalem! Have faith in the Lord your God and you will be upheld; have faith in his prophets and you will be successful.” 21After consulting the people, Jehoshaphat appointed men to sing to the Lord and to praise him for the splendor of his20:21 Or him with the splendor of holiness as they went out at the head of the army, saying:

“Give thanks to the Lord,

for his love endures forever.”

22As they began to sing and praise, the Lord set ambushes against the men of Ammon and Moab and Mount Seir who were invading Judah, and they were defeated. 23The Ammonites and Moabites rose up against the men from Mount Seir to destroy and annihilate them. After they finished slaughtering the men from Seir, they helped to destroy one another.

24When the men of Judah came to the place that overlooks the desert and looked toward the vast army, they saw only dead bodies lying on the ground; no one had escaped. 25So Jehoshaphat and his men went to carry off their plunder, and they found among them a great amount of equipment and clothing20:25 Some Hebrew manuscripts and Vulgate; most Hebrew manuscripts corpses and also articles of value—more than they could take away. There was so much plunder that it took three days to collect it. 26On the fourth day they assembled in the Valley of Berakah, where they praised the Lord. This is why it is called the Valley of Berakah20:26 Berakah means praise. to this day.

27Then, led by Jehoshaphat, all the men of Judah and Jerusalem returned joyfully to Jerusalem, for the Lord had given them cause to rejoice over their enemies. 28They entered Jerusalem and went to the temple of the Lord with harps and lyres and trumpets.

29The fear of God came on all the surrounding kingdoms when they heard how the Lord had fought against the enemies of Israel. 30And the kingdom of Jehoshaphat was at peace, for his God had given him rest on every side.

The End of Jehoshaphat’s Reign

31So Jehoshaphat reigned over Judah. He was thirty-five years old when he became king of Judah, and he reigned in Jerusalem twenty-five years. His mother’s name was Azubah daughter of Shilhi. 32He followed the ways of his father Asa and did not stray from them; he did what was right in the eyes of the Lord. 33The high places, however, were not removed, and the people still had not set their hearts on the God of their ancestors.

34The other events of Jehoshaphat’s reign, from beginning to end, are written in the annals of Jehu son of Hanani, which are recorded in the book of the kings of Israel.

35Later, Jehoshaphat king of Judah made an alliance with Ahaziah king of Israel, whose ways were wicked. 36He agreed with him to construct a fleet of trading ships.20:36 Hebrew of ships that could go to Tarshish After these were built at Ezion Geber, 37Eliezer son of Dodavahu of Mareshah prophesied against Jehoshaphat, saying, “Because you have made an alliance with Ahaziah, the Lord will destroy what you have made.” The ships were wrecked and were not able to set sail to trade.20:37 Hebrew sail for Tarshish