2 Nyakati 15 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

2 Nyakati 15:1-19

Asa Afanya Matengenezo

115:1 Hes 24:4; Amu 3:10; 2Nya 24:20; 2Sam 23:2; 2Nya 20:14; 2Pet 1:21Roho wa Bwana akamjia Azaria mwana wa Odedi. 215:2 Yak 4:8; 2Nya 20:17; Kum 31:17; 1Nya 28:9; Ebr 12:25; 2Nya 33:12-13; Yer 29:13; Mt 7:7; 2Nya 12:1-3; Rum 11:1-2Akatoka ili kumlaki Asa na kumwambia, “Nisikilizeni, Asa na Yuda wote na Benyamini. Bwana yu pamoja nanyi mkiwa pamoja naye. Kama mkimtafuta, ataonekana kwenu, lakini kama mkimwacha yeye, naye atawaacha ninyi. 315:3 Law 10:11; Mao 2:9; Amo 8:11; Hos 3:4Kwa muda mrefu Israeli walikuwa hawana Mungu wa kweli, walikuwa hawana kuhani wa kuwafundisha na wala hawakuwa na sheria. 415:4 Kum 4:29Lakini katika taabu yao walimrudia Bwana, Mungu wa Israeli na kumtafuta, naye akaonekana kwao. 515:5 Amu 19:20; Zek 8:10; Amu 5:6Katika siku hizo hapakuwa na amani kwa yeyote aliyesafiri, kutoka wala kuingia, kwa kuwa wakazi wote wa nchi walikuwa katika machafuko makubwa. 615:6 Mt 24:7; Isa 19:2; Mk 13:8Taifa moja lilipigana na taifa lingine na mji mmoja ukapigana na mji mwingine, kwa sababu Mungu alikuwa anawahangaisha kwa taabu za kila aina. 715:7 1Sam 24:19; Mit 14:14; Rut 2:12; Za 58:11; Mt 5:12-46; Lk 6:35; Kol 3:24Lakini kwa habari yenu ninyi, kuweni hodari wala msikate tamaa, kwa kuwa mtapata thawabu kwa kazi yenu.”

815:8 2Nya 13:19; 8:12; 1Fal 8:64Asa aliposikia maneno haya na unabii wa Azaria mwana wa Odedi nabii, akajipa moyo. Akaziondoa sanamu zote zilizokuwa machukizo katika nchi yote ya Yuda na Benyamini na kutoka miji aliyoiteka ya vilima vya Efraimu. Akakarabati madhabahu ya Bwana iliyokuwa mbele ya ukumbi wa Hekalu la Bwana.

915:9 2Nya 11:16-17Kisha akakutanisha Yuda wote, Benyamini na watu kutoka Efraimu, watu wa Manase na Simeoni waliokuwa wanaishi miongoni mwao, kwa maana idadi kubwa walikuwa wamemjia kutoka Israeli walipoona kwamba Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye.

10Basi wakakusanyika huko Yerusalemu mwezi wa tatu katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Asa. 1115:11 2Nya 14:13-15Wakati huo wakamtolea Bwana dhabihu za ngʼombe 700, kondoo na mbuzi 7,000 kutoka zile nyara walizoteka. 1215:12 2Fal 11:17; 2Nya 23:16; Neh 10:29; 1Nya 16:11; 2Fal 23:3; 2Nya 34:31Wakafanya agano kumtafuta Bwana, Mungu wa baba zao kwa moyo wao wote na kwa roho yao yote. 1315:13 Kut 22:20; Kum 13:9-16Wale wote ambao hawangemtafuta Bwana, Mungu wa Israeli wangelazimika kuuawa, akiwa mdogo au mkubwa, mwanaume au mwanamke. 14Wakamwapia Bwana kwa sauti kuu, kwa kupiga kelele, tarumbeta na kwa mabaragumu. 1515:15 Kum 4:29; 1Nya 22:9; 2Nya 14:7Yuda wote wakafurahia kile kiapo kwa sababu walikuwa wameapa kwa moyo wao wote. Wakamtafuta Mungu kwa bidii, naye akaonekana kwao. Kwa hiyo Bwana akawastarehesha pande zote.

1615:16 Kut 34:13; 2Nya 14:2-5; 1Fal 15:2, 10Mfalme Asa akamwondolea Maaka mama yake wadhifa wake kama mama malkia kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo, akaivunjavunja na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni. 1715:17 2Fal 12:3; 1Fal 3:2-4; Kum 12:7; 1Fal 15:14; 2Nya 14:3-5Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika Israeli, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote. 18Akaleta ndani ya Hekalu la Mungu fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.

19Hapakuwepo vita tena mpaka mwaka wa thelathini na tano wa utawala wake Asa.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

历代志下 15:1-19

亚撒的改革

1上帝的灵降在俄德的儿子亚撒利雅身上, 2他便出来迎接亚撒,对他说:“亚撒啊,所有的犹大人和便雅悯人啊,请听我说!你们若顺从耶和华,祂必与你们同在。你们若寻求祂,祂必让你们寻见。你们若背弃祂,祂必离弃你们。 3以色列人已经许久没有真神,没有祭司教导,也没有律法。 4然而,他们在患难时归向以色列的上帝耶和华,寻求祂,祂就让他们寻见。 5那时,人们出入不得平安,因为各地都有动乱。 6邦国毁灭邦国、城邑毁灭城邑,因为上帝用各样灾难扰乱他们。 7但你们要刚强,不要双手发软,因为你们必因所行的得奖赏。”

8亚撒听了俄德的儿子亚撒利雅先知的预言,就鼓起勇气铲除犹大便雅悯全境及他在以法莲山区夺取的各城邑中的可憎神像,并在耶和华殿的走廊前重修耶和华的祭坛。

9当时,有许多以法莲人、玛拿西人和西缅人看见亚撒的上帝耶和华与他同在,就从以色列来投奔他,寄居在犹大亚撒把他们和所有的犹大人与便雅悯人都招聚在一起。 10亚撒执政第十五年三月,他们聚集在耶路撒冷11当天,他们从掳物中取出七百头牛和七千只羊献祭给耶和华。 12他们与他们祖先的上帝耶和华立约,要全心全意地寻求祂。 13凡不寻求以色列的上帝耶和华的,无论男女老幼,一律处死。 14他们高声向耶和华起誓,并吹响号角。 15犹大人都为所起的誓而欢喜快乐,因他们诚心起誓、诚意寻求耶和华,耶和华就让他们寻见,并赐他们四境平安。

16亚撒王还废除了他祖母玛迦的太后之位,因为她造了可憎的亚舍拉神像。亚撒把她可憎的神像砍倒、打碎,放在汲沦溪烧掉。 17他虽然没有清除以色列的丘坛,但一生忠于耶和华。 18他把自己和父亲奉献的金银及器皿都带到上帝的殿里。

19从那时直到亚撒执政第三十五年,国中都没有战争。