2 Nyakati 13 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 13:1-22

Abiya Mfalme Wa Yuda

(1 Wafalme 15:1-8)

1Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu, Abiya akawa mfalme wa Yuda, 213:2 2Nya 11:20; 1Fal 15:6naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka, binti Urieli wa Gibea.

Basi kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu. 3Abiya aliingia vitani na jeshi la watu 400,000 wenye uwezo wa kupigana, naye Yeroboamu akapanga jeshi dhidi ya Abiya akiwa na jeshi la watu 800,000 wenye uwezo.

413:4 Yos 18:22; 1Nya 11:1Abiya akasimama juu ya Mlima Semaraimu, katika nchi ya vilima ya Efraimu, naye akasema, “Yeroboamu na Israeli yote, nisikilizeni mimi! 513:5 2Sam 7:13; 1Nya 17:12; Law 2:13; Hes 18:19; Amu 11:21-24; Eze 43:24; 1Sam 16:13; Za 89:20; Lk 1:31-33Hamfahamu kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi na wazao wake ufalme juu ya Israeli milele kwa Agano la chumvi? 613:6 1Fal 11:26; 12:20; 2Nya 10:19Hata hivyo Yeroboamu mwana wa Nebati afisa wa Solomoni mwana wa Daudi, aliasi dhidi ya bwana wake. 713:7 Amu 9:4; Za 26:4; Mdo 17:5; Mit 12:11Baadhi ya watu wasiofaa kitu, wabaya kabisa walimkusanyikia na kumpinga Rehoboamu mwana wa Solomoni alipokuwa kijana mdogo asiyekuwa na uamuzi, asiye na nguvu za kuweza kupingana nao.

813:8 Za 68:25; 1Nya 25:10-24; 2Nya 29:2513:8 Kut 32:4; 1Fal 12:28; Hos 8:6“Hata sasa unapanga kupingana na ufalme wa Bwana ambao uko mikononi mwa wazao wa Daudi. Kweli ninyi ni jeshi kubwa nanyi mnazo ndama za dhahabu Yeroboamu alizozitengeneza kuwa miungu yenu. 913:9 2Nya 11:14-15; Kut 29:35-36; Gal 4:8; Yer 2:11Lakini je, hamkuwafukuza makuhani wa Bwana, wana wa Aroni na Walawi na kujifanyia makuhani wenu wenyewe kama yafanyavyo mataifa ya nchi nyingine? Yeyote anayekuja kujiweka wakfu akiwa na ndama dume na kondoo dume saba aweza kuwa kuhani wa kile ambacho ni miungu kwenu.

10“Lakini kwetu sisi, Bwana ndiye Mungu wetu, wala hatujamwacha. Makuhani wanaomtumikia Bwana ni wana wa Aroni, nao Walawi wakiwasaidia. 1113:11 Kut 29:39; 2Nya 2:4; Law 24:2-6; 1Nya 9:24; Kut 27:20-21Kila asubuhi na jioni wao hutoa sadaka za kuteketezwa na kufukiza uvumba wa harufu nzuri kwa Bwana. Wao huweka mikate juu ya meza safi kwa taratibu za kiibada na kuwasha taa kwenye kinara cha dhahabu kila jioni. Sisi tunazishika kanuni za Bwana Mungu wetu. Lakini ninyi mmemwacha Mungu. 1213:12 Hes 10:8-9; Amu 2:15; Mdo 5:39; Kum 20:4; Yos 5:4; Za 20:7; Ay 15:25-26; Mdo 9:4-5Mungu yu pamoja nasi, yeye ndiye kiongozi wetu. Makuhani wake wakiwa na tarumbeta zao watapiga baragumu ya vita dhidi yenu. Watu wa Israeli, msipigane dhidi ya Bwana, Mungu wa baba zenu, kwa maana hamtashinda.”

1313:13 2Nya 20:22; Yos 8:9Basi Yeroboamu alikuwa ametuma jeshi kuzunguka nyuma ya Yuda ili kwamba akiwa mbele ya Yuda, jeshi liwavizie kwa nyuma. 1413:14 1Nya 5:20; 2Nya 18:31Basi Yuda wakageuka na kuona kwamba wanashambuliwa mbele na nyuma. Ndipo wakamlilia Bwana. Makuhani wakapiga tarumbeta zao, 1513:15 2Nya 14:12; Hes 32:4nao watu wa Yuda wakapaza sauti ya kilio cha vita. Katika kupiga kelele za vita, Mungu akawafukuza Yeroboamu na Israeli wote mbele ya Mfalme Abiya na Yuda. 1613:16 2Nya 16:8Waisraeli wakakimbia mbele ya Yuda, naye Mungu akawatia Israeli mikononi mwao. 17Abiya na watu wake wakawachinja kwa machinjo makuu, hata wakawepo majeruhi 500,000 miongoni mwa watu wenye uwezo wa Israeli. 1813:18 1Nya 5:20; Za 22:5; Amu 8:28; 2Fal 18:5; 2Nya 16:8-9; 20:20Watu wa Israeli walitiishwa katika tukio lile, nao watu wa Yuda wakawa washindi kwa sababu walimtegemea Bwana, Mungu wa baba zao.

1913:19 Yos 15:9; Yn 11:54Abiya akamfuatia Yeroboamu na kuteka miji ya Betheli, Yeshana na Efroni kutoka kwake, pamoja na vijiji vinavyoizunguka miji hiyo. 2013:20 1Sam 25:38; Eze 24:16; Mdo 12:23; 1Sam 26:10; 1Fal 14:20Yeroboamu hakupata nguvu tena wakati wa utawala wa Abiya. Naye Bwana akampiga Yeroboamu akafa.

21Lakini Abiya akapata nguvu. Alioa wanawake kumi na wanne na alikuwa na wana ishirini na wawili na binti kumi na sita.

2213:22 2Nya 9:29; 12:15Matukio mengine ya utawala wa Abiya, pamoja na mambo aliyofanya na aliyosema, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.

New International Reader’s Version

2 Chronicles 13:1-22

Abijah King of Judah

1Abijah became king of Judah. It was in the 18th year of Jeroboam’s rule over Israel. 2Abijah ruled in Jerusalem for three years. His mother’s name was Maakah. She was a daughter of Uriel. Uriel was from Gibeah.

There was war between Abijah and Jeroboam. 3Abijah went into battle with an army of 400,000 capable fighting men. Jeroboam lined up his soldiers against them. He had 800,000 able troops.

4Abijah stood on Mount Zemaraim. It’s in the hill country of Ephraim. Abijah said, “Jeroboam and all you Israelites, listen to me! 5The Lord is the God of Israel. Don’t you know that he has placed David and his sons after him on Israel’s throne forever? The Lord made a covenant of salt with David. The salt means the covenant will last for all time to come. 6Jeroboam, the son of Nebat, was an official of David’s son Solomon. But he refused to obey his master. 7Some worthless and evil men gathered around him. They opposed Solomon’s son Rehoboam. At that time Rehoboam was young. He couldn’t make up his mind. He wasn’t strong enough to stand up against those men.

8“Now you plan to stand up against the kingdom of the Lord. His kingdom is in the hands of men in David’s family line. It’s true that you have a huge army. You have the statues of the golden calves that Jeroboam made to be your gods. 9But you drove out the priests of the Lord, the sons of Aaron. You also drove out the Levites. You appointed your own priests. That’s what the people of other nations do. Anyone can come and set himself apart. All he has to do is sacrifice a young bull and seven rams. Then he becomes a priest of gods that aren’t really gods at all!

10“But the Lord is our God. We haven’t deserted him. The priests who serve the Lord belong to the family line of Aaron. The Levites help them. 11Every morning and evening the priests bring burnt offerings and sweet-smelling incense to the Lord. They set out the holy bread on the table. That table is ‘clean.’ They light the lamps on the gold lampstand every evening. We always do what the Lord our God requires in his law. But you have deserted him. 12God is with us. He’s our leader. His priests will blow their trumpets. They will sound the battle cry against you. People of Israel, don’t fight against the Lord. He’s the God of your people who lived long ago. You can’t possibly succeed.”

13Jeroboam had sent some troops behind Judah’s battle lines. He told them to hide and wait there. He and his men stayed in front of Judah’s lines. 14Judah turned and saw that they were being attacked from the front and from the back. Then they cried out to the Lord. The priests blew their trumpets. 15The men of Judah shouted the battle cry. When they did, God drove Jeroboam and all the Israelites away from Abijah and Judah. 16The Israelites ran away from them. God handed Israel over to Judah. 17Abijah and his troops wounded and killed large numbers of them. In fact, 500,000 of Israel’s capable men lay dead or wounded. 18So at that time the Israelites were brought under Judah’s control. The people of Judah won the battle over them. That’s because they trusted in the Lord, the God of their people.

19Abijah chased Jeroboam. He captured from him the towns of Bethel, Jeshanah and Ephron. He also captured the villages around them. 20Jeroboam didn’t get his power back during the time of Abijah. In fact, the Lord struck Jeroboam down, and he died.

21But Abijah grew stronger. He married 14 wives. He had 22 sons and 16 daughters.

22The other events of Abijah’s rule are written down. The things he did and said are written in the notes of Iddo the prophet.