2 Nyakati 1 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 1:1-17

Solomoni Aomba Hekima

(1 Wafalme 3:1-15)

11:1 1Fal 2:26; 2Nya 12:1; Mwa 39:2; Hes 14:43; 1Nya 29:25; Mwa 21:22; 1Nya 17:8; Mt 28:20Solomoni mwana wa Daudi alijiimarisha kwenye milango yote! Katika ufalme wake, kwa kuwa Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye, naye akamfanya mkuu mno.

21:2 1Nya 28:1; 2Nya 29:20; 30:2Ndipo Solomoni akasema na Israeli wote, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, waamuzi na viongozi wote katika Israeli, pamoja na wakuu wa jamaa. 31:3 Law 17:4; Kut 36:8; 40:18; 1Fal 3:4Naye Solomoni na kusanyiko lote wakakwea mpaka mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni, kwa kuwa huko ndiko Hema la Kukutania la Mungu lilipokuwa, ambalo Mose mtumishi wa Bwana alikuwa amelitengeneza huko jangwani. 41:4 2Sam 6:2, 17; 1Nya 15:25Basi Daudi alikuwa amelipandisha Sanduku la Mungu kutoka Kiriath-Yearimu mpaka mahali alipokuwa amepatengeneza kwa ajili yake, kwa sababu alikuwa amesimamisha hema kwa ajili ya hilo Sanduku huko Yerusalemu. 51:5 Kut 38:2; 31:2; 1Nya 13:3Lakini yale madhabahu ya shaba ambayo Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, alikuwa ametengeneza yalikuwa huko Gibeoni mbele ya Maskani ya Bwana Mungu, hivyo Solomoni na kusanyiko lote walimtafuta Mungu huko. 61:6 1Fal 3:4Solomoni akapanda huko yalikokuwa madhabahu ya shaba mbele za Bwana katika Hema la Kukutania, na kutoa dhabihu 1,000 za sadaka za kuteketezwa juu yake.

71:7 2Nya 7:12; Isa 58:9; 1Fal 3:5; Mit 3:5Usiku ule Mungu akamtokea Solomoni na kumwambia, “Omba lolote utakalo nikupe.”

81:8 1Nya 23:1; 28:5Solomoni akamjibu Mungu, “Umemwonyesha baba yangu Daudi fadhili nyingi, nawe umeniweka niwe mfalme mahali pake. 91:9 2Sam 7:25; 1Fal 8:25; Mwa 12:2Sasa, Bwana Mungu, ahadi yako kwa baba yangu Daudi na ithibitike, kwa kuwa umenifanya mimi mfalme juu ya watu ambao ni wengi kama mavumbi ya nchi. 101:10 Hes 27:17; Mit 8:15-16; Kum 31:2; 1Fal 3:9; Za 119:34; Mit 3:13; Yak 1:5Nakuomba unipe mimi hekima na maarifa, ili niweze kuongoza watu hawa, kwa kuwa ni nani awezaye kutawala hawa watu wako walio wengi hivi?”

111:11 Kum 17:17; 1Sam 16:7; 1Fal 3:11; 8:18Mungu akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa jambo hili ndilo shauku ya moyo wako na hukuomba mali, utajiri au heshima, wala kifo kwa ajili ya adui zako, nawe kwa kuwa hukuomba maisha marefu, bali umeomba hekima na maarifa ili kuongoza watu wangu ambao nimekufanya uwe mfalme juu yao, 121:12 1Nya 29:12-25; Neh 13:26; Efe 3:20; 2Nya 9:22; Za 34:9-10; Mt 6:33; Mhu 2:9kwa hiyo utapewa hekima na maarifa. Tena nitakupa pia mali, utajiri na heshima, ambavyo hakuna mfalme yeyote aliyekuwepo kabla yako amewahi kuwa navyo, na hakuna yeyote baada yako atakayekuwa navyo.”

Fahari Ya Solomoni

(1 Wafalme 10:26-29)

13Ndipo Solomoni akaenda mpaka Yerusalemu kutoka mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni, kutoka mbele ya Hema la Kukutania. Naye akatawala Israeli.

141:14 1Sam 8:11; 1Fal 9:19; 4:26Solomoni akakusanya magari ya vita na farasi. Alikuwa na magari 1,400 na farasi 12,000, ambayo aliyaweka katika miji ya magari na mengine akawa nayo huko Yerusalemu. 151:15 1Fal 9:28; Isa 60:5; Ay 22:24; 1Fal 10:27Mfalme akafanya fedha na dhahabu kuwa vitu vya kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani. 16Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka Kue.1:16 Yaani Kilikia. Wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue. 171:17 Wim 1:9Waliagiza magari kutoka Misri kwa bei ya shekeli 6001:17 Shekeli 600 za fedha ni sawa na kilo 7. za fedha, na farasi kwa shekeli 150.1:17 Shekeli 150 ni sawa na kilo 1.7. Pia waliwauza nje kwa wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.

Swedish Contemporary Bible

2 Krönikeboken 1:1-17

Salomos regering

(1:1—9:31)

Salomo ber Gud om vishet

(1 Kung 3:4-15)

1Salomo, Davids son, hade nu etablerat sin kungamakt, och Herren, hans Gud, var med honom och gjorde honom mycket mäktig.

2Salomo talade till hela Israel, till både högre och lägre officerare, alla domare och alla ledare i Israel, familjeöverhuvuden. 3Salomo och hela församlingen gick till offerplatsen i Givon, där Guds uppenbarelsetält var, som Herrens tjänare Mose hade gjort i öknen. 4Men Guds ark hade David flyttat från Kirjat-Jearim till den plats han hade ställt i ordning åt den; han hade satt upp ett tält åt den i Jerusalem. 5Men kopparaltaret, som Besalel, Uris son och Hurs sonson, hade gjort, stod framför Herrens boning i Givon. Nu uppsökte Salomo och de församlade det. 6Salomo gick upp till kopparaltaret inför Herren i uppenbarelsetältet och offrade 1 000 brännoffer på det.

7Den natten uppenbarade sig Gud för Salomo och sa: ”Be mig om vad du vill, så ska du få det!”

8Salomo svarade Gud: ”Du har visat stor nåd mot min far David och gjort mig till kung efter honom. 9Herre Gud, uppfyll nu ditt löfte till min far David, för du har gjort mig till kung över ett folk som är lika talrikt som stoftet på jorden. 10Ge mig nu vishet och kunskap, så att jag kan leda detta folk, för vem kan styra ditt folk som är så stort?”

11Gud svarade Salomo: ”Därför att din största önskan var detta, och därför att du inte bad om rikedom, välfärd och ära eller dina fienders liv, och inte heller ett långt liv, utan om vishet och kunskap för att kunna leda mitt folk, som jag har gjort dig till kung över –  12därför ska jag ge dig vishet och kunskap. Jag ska också ge dig mer rikedom, välfärd och ära än någon kung någonsin haft före dig eller någonsin kommer att ha.”

13Sedan begav sig Salomo till Jerusalem från offerplatsen i Givon, från uppenbarelsetältet, och han regerade över Israel.

Salomos oerhörda rikedom

(1 Kung 10:26-29; 2 Krön 9:25-28)

14Salomo samlade också vagnar och hästar. Han hade 1 400 vagnar och 12 000 hästar, dels i vagnstäderna, dels hos kungen i Jerusalem. 15Silvret och guldet var tack vare Salomo lika vanligt i Jerusalem som sten, och cederträ lika vanligt som mullbärsfikonträ i Låglandet. 16Salomos hästar köptes i Egypten1:16 Eller Musri, jfr 1 Kung 10:28 med not. och Kuve. Kungens uppköpare importerade dem från Kuve. 17Varje vagn som de importerade från Egypten kostade 600 siklar silver och en häst 150 siklar1:17 7,2 kilo … 1,6 kilo En sikel=12 gram.. De exporterade dem också till hettiternas och araméernas kungar.