1 Wathesalonike 5 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

1 Wathesalonike 5:1-28

Kuweni Tayari Kwa Siku Ya Bwana

15:1 Mdo 1:7; 1The 4:9Basi, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira hatuna haja ya kuwaandikia, 25:2 1Kor 1:8; 2Pet 3:10kwa kuwa mnajua vyema kwamba siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajapo usiku. 35:3 Yer 6:14; Yn 16:21, 22; Mt 24:39; Lk 21:34, 35Wakati watu wanaposema, “Kuna amani na salama,” maangamizi huwajia ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwanamke mwenye mimba; nao hakika hawatatoroka.

45:4 Mdo 26:18; 1Yn 2:8Bali ninyi, ndugu, hampo gizani hata siku ile iwakute ghafula kama mwizi. 55:5 Rum 13:12; Efe 5:9Ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi si wana wa giza wala wa usiku. 65:6 Rum 13:11Kwa hiyo basi, tusilale kama watu wengine walalavyo, bali tukeshe na kuwa na kiasi. 75:7 Lk 21:34, 36; Rum 13:13; 1Kor 15:34Kwa kuwa wote walalao hulala usiku na wale walewao hulewa usiku. 85:8 Isa 59:17; Efe 6:14, 16, 17Lakini kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, basi tuwe na kiasi, tukijivika imani na upendo kama dirii kifuani na tumaini letu la wokovu kama chapeo. 95:9 2The 2:13-14Kwa maana Mungu hakutuita ili tupate ghadhabu bali tupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo. 105:10 2Kor 5:15Yeye alikufa kwa ajili yetu ili hata kama tuko macho au tumelala, tupate kuishi pamoja naye. 115:11 1The 4:18Kwa hiyo farijianeni na kujengana, kama vile mnavyofanya sasa.

Maagizo Ya Mwisho, Salamu Na Kuwatakia Heri

125:12 1Tim 5:17; Ebr 13:17Sasa tunawaomba, ndugu, waheshimuni wale wanaofanya kazi kwa bidii miongoni mwenu, wale ambao wana mamlaka juu yenu katika Bwana na ambao wanawaonya. 135:13 Mk 9:50; 2The 3:6-11; Rum 14:1Waheshimuni sana katika upendo kwa ajili ya kazi zao. Ishini kwa amani ninyi kwa ninyi. 145:14 2The 3:11, 12; Ebr 12:12; Rum 4:1; 15:1Nasi twawasihi, ndugu, waonyeni walio wavivu, watieni moyo waoga, wasaidieni wanyonge na kuwavumilia watu wote. 155:15 1Pet 3:9; Gal 6:10; Efe 4:32Angalieni kuwa mtu asimlipe mwenzake maovu kwa maovu, bali siku zote tafuteni kutendeana mema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.

165:16 2Kor 6:10; Flp 4:4Furahini siku zote; 175:17 Lk 18:1; 21:36; Rum 12:12; Efe 6:18; Kol 4:12ombeni bila kukoma; 185:18 Efe 5:20; Kol 3:17shukuruni kwa kila jambo, kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu.

195:19 Efe 4:30Msiuzime moto wa Roho Mtakatifu; 205:20 1Kor 14:1-40msiyadharau maneno ya unabii. 215:21 1Kor 14:29; 1Yn 4:1Jaribuni kila kitu. Yashikeni yaliyo mema. 225:22 1The 4:12Jiepusheni na uovu wa kila namna.

235:23 Rum 15:33; Ebr 4:12; 1The 3:13; 2:19Mungu mwenyewe, Mungu wa amani, awatakase ninyi kabisa. Nanyi mhifadhiwe roho zenu, nafsi zenu na miili yenu, bila kuwa na lawama katika Bwana wetu Yesu Kristo. 245:24 Rum 8:28; 1Kor 1:9; Hes 23:19; Flp 1:6Yeye aliyewaita ni mwaminifu naye atafanya hayo.

255:25 Kol 4:3; 2The 3:1; Ebr 13:18; Efe 6:9Ndugu, tuombeeni. 26Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu. 27Nawaagizeni mbele za Bwana mhakikishe kuwa ndugu wote wanasomewa barua hii.

28Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi. Amen.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

帖撒罗尼迦前书 5:1-28

主来的日子

1弟兄姊妹,这件事会在什么日期、什么时候发生,不必我写信告诉你们, 2因为你们已经清楚知道,主的日子会像夜间的贼一样突然临到。 3当人们正在说一切平安稳妥的时候,灾祸会像产痛临到孕妇一样突然临到他们,他们将无法逃脱。

4然而,弟兄姊妹,你们不是活在黑暗里,因此那日子不会像贼一样突然临到你们。 5你们都是光明之子,白昼之子。我们既不属于黑夜,也不属于黑暗。 6所以不要像其他人一样沉睡,要警醒戒备, 7因为睡觉的人是在夜里睡,醉酒的人是在夜里醉。 8我们既属于白昼,就应当保持清醒,要把信心和爱心当作护心镜遮胸,把得救的盼望当作头盔戴上。 9因为上帝不是预定我们受惩罚,而是预定我们靠着主耶稣基督得救。 10主替我们死,使我们无论是醒是睡5:10 “是醒是睡”或译“是生是死”。,都可以与祂同活。 11所以,你们要彼此鼓励、互相造就,正如你们一向所做的。

劝勉与问候

12弟兄姊妹,我劝你们要敬重那些在你们当中辛勤工作、在主里领导和劝诫你们的人。 13因为他们的工作,你们要怀着爱心格外敬重他们。你们要彼此和睦相处。 14弟兄姊妹,我劝你们要告诫懒惰的人,鼓励灰心的人,扶持软弱的人,耐心对待所有的人。 15你们要小心,谁都不可冤冤相报,总要彼此善待,也要善待众人。

16要常常喜乐, 17不断地祷告, 18凡事谢恩,因为这是上帝在基督耶稣里给你们的旨意。

19不要抑制圣灵的感动, 20不要轻视先知的信息。 21凡事都要小心察验,持守良善的事, 22杜绝所有的恶事。

23愿赐平安的上帝亲自使你们完全圣洁!愿祂保守你们的灵、魂、体,使你们在主耶稣基督再来的时候无可指责! 24呼召你们的主是信实可靠的,祂必为你们成就这事。

25弟兄姊妹,请为我们祷告。 26要以圣洁的吻问候众弟兄姊妹。 27我奉主的名吩咐你们把这封信读给所有弟兄姊妹听。

28愿我们主耶稣基督的恩典与你们同在!