1 Wathesalonike 3 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

1 Wathesalonike 3:1-13

Timotheo Atumwa Kwenda Thesalonike

13:1 Mdo 17:15; 1The 3:5; Mdo 17:14Kwa hivyo tulipokuwa hatuwezi kuvumilia zaidi, tuliamua tubaki Athene peke yetu. 23:2 Mdo 16:1; 1Kor 3:9; 2Kor 2:12Tukamtuma Timotheo ambaye ni ndugu yetu na mtumishi mwenzetu wa Mungu katika kuieneza Injili ya Kristo, aje kuwaimarisha na kuwatia moyo katika imani yenu, 33:3 Mdo 9:16; 14:22ili mtu yeyote asifadhaishwe na mateso haya. Mnajua vyema kwamba tumewekewa hayo mateso. 43:4 1The 2:14; Mdo 14:22Kwa kweli, tulipokuwa pamoja nanyi tuliwaambia mara kwa mara kwamba tutateswa na imekuwa hivyo kama mjuavyo. 53:5 Mt 4:3; Gal 2:2; Flp 2:16Kwa sababu hii nilipokuwa siwezi kuvumilia zaidi, nilimtuma mtu ili nipate habari za imani yenu. Niliogopa kwamba kwa njia fulani yule mjaribu asiwe amewajaribu, nasi tukawa tumejitaabisha bure.

Taarifa Ya Timotheo Ya Kutia Moyo

63:6 Mdo 18:5Lakini sasa Timotheo ndiyo tu amerejea kwetu kutoka kwenu na ameleta habari njema kuhusu imani yenu na upendo wenu. Ametuambia kwamba siku zote mnatukumbuka kwa wema na kwamba mna shauku ya kutuona kama vile sisi tulivyo na shauku ya kuwaona ninyi. 7Kwa hiyo, ndugu zetu, katika dhiki na mateso yetu yote tumefarijika kwa sababu ya imani yenu. 83:8 1Kor 16:13Sasa kwa kuwa hakika tunaishi, kwa kuwa ninyi mmesimama imara katika Bwana. 93:9 1The 1:2; 2:19, 20Je, tutawezaje kumshukuru Mungu kiasi cha kutosha kwa ajili yenu, kutokana na furaha tuliyo nayo mbele za Mungu wetu kwa sababu yenu? 103:10 2Tim 1:3; 1The 2:17Usiku na mchana tunaomba kwa bidii ili tupate kuwaona tena na kujaza kile kilichopungua katika imani yenu.

113:11 1The 3:13; Flp 4:20Basi Mungu wetu na Baba yetu mwenyewe na Bwana wetu Yesu atengeneze njia ya sisi kuja kwenu. 123:12 1Kor 1:8; 1The 2:19Bwana na auongeze upendo wenu na kuuzidisha kati yenu na kwa wengine wote, kama vile tulivyo na upendo mwingi kwenu. 13Tunamwomba Mungu aimarishe mioyo yenu ili msiwe na lawama katika utakatifu mbele za Mungu wetu aliye Baba yetu wakati wa kuja kwake Bwana Yesu pamoja na watakatifu wote.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

帖撒羅尼迦前書 3:1-13

1最後我們無法再忍受思念之苦,就決定我們留在雅典, 2提摩太去你們那裡。他在傳揚基督福音的事工上是我們的弟兄、上帝的同工。他去是要鼓勵你們,使你們信心堅定, 3免得有人因遭受這些患難而動搖,因為你們知道我們必遭受患難。 4我們在你們那裡時曾預先告訴過你們,我們會遭遇患難,你們知道後來果然如此。 5因此,我無法再等下去了,就派提摩太到你們那裡看看你們的信心如何,免得那誘惑人的誘惑了你們,使我們的心血都白費了。

喜聞佳訊

6現在,提摩太剛從你們那裡回來,把有關你們信心和愛心的好消息告訴了我們。他說你們常常思念我們,很想見到我們,就像我們渴望見到你們一樣。 7弟兄姊妹,你們的信心使我們在萬般困苦和患難中得到了激勵。 8得知你們靠著主堅定不移,我們現在無比振奮。 9你們使我們在上帝面前感到非常喜樂,我們該怎樣為你們感謝上帝呢? 10我們晝夜懇切禱告,渴望能見到你們,彌補你們信心的不足之處。

11願我們的父上帝和主耶穌引領我們到你們那裡。 12願主使你們彼此之間的愛和對他人的愛一齊增長,甚至滿溢出來,就像我們愛你們一樣。 13這樣,願我們的主耶穌帶著祂的眾聖徒再來時,使你們心裡剛強,在我們的父上帝面前完全聖潔,無可指責。