1 Wathesalonike 2 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

1 Wathesalonike 2:1-20

Huduma Ya Paulo Huko Thesalonike

12:1 1The 1:5-9Ndugu zangu, kwa kuwa ninyi wenyewe mnajua ya kwamba kuja kwetu kwenu hakukuwa bure, 22:2 Mdo 16:22; Flp 1:30kama vile mjuavyo, tulikuwa tumeteswa na kutukanwa huko Filipi, lakini hata hivyo, kwa msaada wa Mungu wetu, tulikuwa na ujasiri wa kuwaambia Injili ya Mungu ingawa kulikuwa na upinzani mkubwa. 32:3 2Kor 2:17Kwa maana himizo letu halikutokana na hila wala nia mbaya au udanganyifu. 42:4 Gal 2:7; 1:10Kinyume chake, tulinena kama watu tuliokubaliwa na Mungu tukakabidhiwa Injili. Sisi hatujaribu kuwapendeza wanadamu bali kumpendeza Mungu, yeye ayachunguzaye mawazo ya ndani sana ya mioyo yetu. 52:5 Mdo 20:33; Rum 1:9Kama mjuavyo, hatukuja kwenu kwa maneno ya kujipendekeza au maneno yasiyo ya kweli ili kuficha tamaa mbaya: Mungu ndiye shahidi yetu. 62:6 1Kor 9:1-2Wala hatukuwa tunatafuta sifa kutoka kwa wanadamu, wala kutoka kwenu au kwa mtu mwingine awaye yote.

Kama mitume wa Kristo tungaliweza kuwa mzigo kwenu, 72:7 1The 2:11; 1Kor 2:3; 9:22; 2Kor 1:4; 7:6, 7lakini tulikuwa wapole katikati yenu, kama mama anayewatunza watoto wake wadogo. 82:8 2Kor 12:15; 1Yn 3:16Tuliwapenda sana kiasi kwamba tulifurahia kushirikiana nanyi, si Injili ya Mungu tu, bali hata maisha yetu, kwa sababu mlikuwa wa thamani mno kwetu. 92:9 Mdo 18:3; 2Kor 11:9; 2The 3:8Ndugu zetu, mnakumbuka juhudi yetu na taabu yetu. Tulifanya kazi usiku na mchana, ili tusimlemee mtu yeyote wa kwenu wakati tulipokuwa tunawahubiria Injili ya Mungu.

102:10 2Kor 1:12Ninyi wenyewe ni mashahidi na Mungu pia, jinsi tulivyokuwa watakatifu, wenye haki na wasio na lawama miongoni mwenu ninyi mlioamini. 112:11 1Kor 4:14Maana mnajua kwamba tuliwatendea kila mmoja wenu kama vile baba awatendeavyo watoto wake. 122:12 Efe 4:1Tuliwatia moyo, tuliwafariji na kuwahimiza kuishi maisha yampendezayo Mungu, anayewaita katika Ufalme na utukufu wake.

132:13 Ebr 4:12Nasi pia tunamshukuru Mungu bila kukoma kwa sababu mlipolipokea neno la Mungu mlilosikia kutoka kwetu, hamkulipokea kama neno la wanadamu, bali mlilipokea kama lilivyo hasa, neno la Mungu, litendalo kazi ndani yenu ninyi mnaoamini. 142:14 Gal 1:22; Mdo 17:5; 2The 1:4Kwa maana ninyi ndugu zetu, mlifanyika wafuasi wa makanisa ya Mungu yaliyoko ndani ya Kristo Yesu katika Uyahudi. Mlipata mateso yale yale kutoka kwa watu wenu wenyewe kama vile makanisa hayo yalivyoteswa na Wayahudi, 152:15 Mdo 2:23; Mt 5:12wale waliomuua Bwana Yesu na manabii, nasi wakatufukuza pia. Watu hao walimchukiza Mungu na tena ni adui wa watu wote, 162:16 Mdo 13:45-50; Mt 23:32wakijitahidi kutuzuia tusizungumze na watu wa Mataifa ili kwamba wapate kuokolewa. Kwa njia hii wanazidi kujilundikia dhambi zao hadi kikomo. Lakini hatimaye ghadhabu ya Mungu imewafikia.

Paulo Atamani Kuwaona Wathesalonike

172:17 1Kor 5:3; Kol 2:5; 1The 3:10Lakini ndugu zetu, tulipotenganishwa nanyi kwa kitambo kidogo (ingawa kutengana huko kulikuwa kwa mwili tu, si kwa moyo), tulizidi kuwa na shauku kubwa kuwaona uso kwa uso. 182:18 Mt 4:10; Rum 1:13; 15:22Maana tulitaka kuja kwenu, hasa mimi Paulo, nilitaka kuja tena na tena, lakini Shetani akatuzuia. 192:19 Flp 4:1; 2Kor 1:14; Mt 16:27; 1The 3:13Kwa maana tumaini letu ni nini, au furaha yetu au taji yetu ya kujisifia mbele za Bwana Yesu Kristo wakati wa kuja kwake? Je, si ni ninyi? 202:20 2Kor 1:14Naam, ninyi ndio fahari yetu na furaha yetu.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

帖撒羅尼迦前書 2:1-20

保羅在帖撒羅尼迦的工作

1弟兄姊妹,你們自己知道,我們那次探望你們並沒有白費。 2你們也知道,我們之前在腓立比遭受了迫害和凌辱,但仍然不顧強烈的反對,靠著我們的上帝放膽向你們傳揚祂的福音。 3我們的勸勉並非出於謬誤、不良動機或詭詐。 4我們得到了上帝的恩准來承擔福音的責任,所以才這樣傳,不是要取悅人,而是要取悅鑒察我們內心的上帝。

5你們知道,我們沒有花言巧語奉承人,也沒有心存貪念,上帝可以為我們作證。 6我們不求得到你們或其他任何人的讚揚, 7雖然身為基督的使徒,我們理當受到尊重。我們反而像母親撫育嬰兒一樣溫柔地對待你們。 8我們深愛你們,對你們有深厚的感情,不僅樂意把上帝的福音傳給你們,甚至把生命給你們也在所不惜。

9弟兄姊妹,你們一定記得我們的勞苦和艱難。我們一面向你們傳上帝的福音,一面晝夜辛勤工作,免得成為你們任何人的負擔。 10我們怎樣以聖潔、公義、純全的方式對待你們眾信徒,你們自己可以作證,上帝也可以作證。 11你們也知道,我們對待你們就像父親對待自己的孩子一樣。 12我們安慰你們,勸勉你們,督促你們,叫你們行事為人對得起上帝,祂呼召你們進入祂的國度和榮耀。

13我們也不住地感謝上帝,因為你們從我們這裡聽了上帝的道後就接受了,確信這不是人的道理,而是上帝的道。這道正在你們信的人心裡發揮作用。

14弟兄姊妹,你們的遭遇和猶太地區上帝在基督耶穌裡的眾教會的遭遇一樣。你們受到了自己同胞的迫害,他們也受到了猶太人的迫害。 15這些猶太人殺死了主耶穌和眾先知,又迫害我們。他們不但冒犯上帝,還與所有的人為敵, 16阻止我們傳福音給外族人,唯恐他們得救。這些人惡貫滿盈,上帝的烈怒終於臨到了他們頭上。

保羅渴望去帖撒羅尼迦

17弟兄姊妹,我們身體暫時與你們分離,心靈卻與你們在一起。我們非常渴望見到你們,並想方設法與你們會面。 18我們想去你們那裡,我保羅也一次又一次地想去,只是遭到撒旦的攔阻。 19我們主耶穌再來的時候,我們在祂面前的盼望、喜樂和可誇耀的冠冕是什麼呢?不就是你們嗎? 20因為你們是我們的榮耀和喜樂。