1 Wakorintho 16 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wakorintho 16:1-24

Changizo Kwa Ajili Ya Watakatifu

116:1 Mdo 24:17; 9:13; 16:6Basi kuhusu changizo kwa ajili ya watakatifu: Kama nilivyoyaagiza makanisa ya Galatia, fanyeni vivyo hivyo. 216:2 Mdo 20:7; 2Kor 9:4-5Siku ya kwanza ya kila juma, kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha, kulingana na mapato yake na fedha hizo aziweke akiba, ili nitakapokuja pasiwe na lazima ya kufanya mchango. 316:3 2Kor 3:1; 8:18-19Kwa hiyo nitakapowasili, nitawapa wale mtakaowachagua barua za kuwatambulisha, ili kuwatuma wapeleke zawadi zenu huko Yerusalemu. 416:4 2Kor 8:4, 19Kama ikionekana ni vyema na mimi niende, basi hao watu watafuatana nami.

Mahitaji Binafsi

516:5 1Kor 4:19; Mdo 16:9Baada ya kupitia Makedonia nitakuja kwenu, maana ninakusudia kupitia Makedonia. 616:6 Rum 15:24; Tit 3:13Huenda nitakaa nanyi kwa muda, au hata kukaa nanyi kipindi chote cha baridi, ili mweze kunisaidia katika safari yangu, popote niendapo. 716:7 Mdo 18:21Kwa maana sitaki niwaone sasa na kupita tu; natarajia kuwa nanyi kwa muda wa kutosha, kama Bwana akipenda. 816:8 Mdo 18:19; 2:1Lakini nitakaa Efeso mpaka wakati wa Pentekoste, 916:9 Mdo 14:27; 2Kor 2:12; Kol 4:3; Ufu 3:8; Mdo 19:9kwa maana mlango mkubwa umefunguliwa kwangu kufanya kazi yenye matunda, nako huko kuna adui wengi wanaonipinga.

1016:10 Mdo 16:1; 19:22; Rum 16:21; Flp 2:20, 22; 1The 3:2Ikiwa Timotheo atakuja kwenu, hakikisheni kwamba hana hofu yoyote akiwa nanyi, kwa sababu anafanya kazi ya Bwana, kama mimi nifanyavyo. 1116:11 1Tim 4:12; 2Kor 1:16; 3Yn 6; Mdo 19:9Basi asiwepo mtu atakayekataa kumpokea. Msafirisheni kwa amani ili aweze kunijia tena. Namtarajia pamoja na ndugu.

1216:12 Mdo 18:24; 1Kor 1:12Basi kwa habari za ndugu yetu Apolo, nimemsihi kwa bidii aje kwenu pamoja na hao ndugu. Ingawa alikuwa hapendi kabisa kuja sasa, lakini atakuja apatapo nafasi.

Maneno Ya Mwisho

1316:13 1Kor 1:8; 2Kor 1:21; Gal 5:1; Flp 1:27; 1The 3:8; Tit 1:9; Efe 6:10Kesheni, simameni imara katika imani, fanyeni kiume, kuweni mashujaa kuweni hodari. 1416:14 1Kor 14:1Fanyeni kila kitu katika upendo.

1516:15 1Kor 1:6; Rum 16:5; Mdo 18; 12; 24; 17; 9:13Ninyi mnajua kwamba watu wa nyumbani mwa Stefana ndio waliokuwa wa kwanza kuamini katika Akaya, nao wamejitoa kwa ajili ya kuwahudumia watakatifu. Ndugu nawasihi, 1616:16 1The 5:12; Ebr 13:17mjitie katika kuwahudumia watu kama hawa na kila mmoja aingiaye kwenye kazi na kuifanya kwa bidii. 1716:17 2Kor 11:9; Flp 2:30Nilifurahi wakati Stefana, Fortunato na Akaiko walipofika, kwa sababu wamenipatia yale niliyopungukiwa kutoka kwenu. 1816:18 Rum 15:32; Flp 1:7; 2:29Kwa kuwa waliiburudisha roho yangu na zenu pia. Watu kama hawa wanastahili kutambuliwa.

Salamu Za Mwisho

1916:19 Mdo 2:9; 18:2; Rum 16:5Makanisa ya Asia yanawasalimu. Akila na Prisila,16:19 Prisila kwa Kiyunani ni Priska, hivyo tafsiri nyingine zimemuita Priska. pamoja na kanisa lililoko nyumbani kwao wanawasalimu sana katika Bwana. 2016:20 Rum 16:16; 2Kor 13:12; 1Pet 5:14Ndugu wote walioko hapa wanawasalimu. Salimianeni kwa busu takatifu.

2116:21 Gal 6:11; Kol 4:18; 2The 3:17Mimi, Paulo, naandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe.

2216:22 Efe 6:24; Rum 9:3; Ufu 22:20Kama mtu yeyote hampendi Bwana Yesu Kristo, na alaaniwe. Bwana wetu, njoo.16:22 Kwa Kiaramu ni Marana tha.

2316:23 Rum 16:20Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.

24Upendo wangu uwe nanyi nyote katika Kristo Yesu. Amen.

Hoffnung für Alle

1. Korinther 16:1-24

Unterstützung für die notleidende Gemeinde in Jerusalem und Briefschluss

(Kapitel 16)

Hilfe für die Gemeinde in Jerusalem

1Zum Schluss will ich noch etwas zur Geldsammlung für die Christen in Jerusalem sagen. Führt sie so durch, wie ich es auch für die Gemeinden in Galatien angeordnet habe. 2An jedem Sonntag soll jeder von euch dafür so viel Geld zurücklegen, wie es ihm möglich ist. Dann braucht ihr mit dem Sammeln nicht erst anzufangen, wenn ich komme. 3Gleich nach meiner Ankunft sollen dann Männer aus eurer Gemeinde, die ihr für zuverlässig erachtet, das Geld nach Jerusalem bringen. Ich werde ihnen Empfehlungsschreiben für unterwegs mitgeben. 4Sollte es nötig sein, werde ich selbst mit ihnen reisen.

Weitere Reisepläne

5Ich werde zu euch kommen, sobald ich die Gemeinden in der Provinz Mazedonien besucht habe. Dort will ich mich nicht lange aufhalten; 6aber bei euch möchte ich eine Zeit lang bleiben, vielleicht sogar den ganzen Winter über. Es wäre gut, wenn ihr mich dann für die Weiterreise versorgen könntet. 7Wenn ich sehr bald zu euch käme, könnte ich euch nur auf der Durchreise besuchen. Aber das will ich nicht. Wenn der Herr es zulässt, hoffe ich, einige Zeit bei euch verbringen zu können. 8Bis Pfingsten bleibe ich noch in Ephesus. 9Hier hat mir Gott viele offene Türen geschenkt, um die rettende Botschaft zu verkünden, und dadurch haben zahlreiche Menschen zum Glauben gefunden; gleichzeitig sind auch viele Gegner da.

10Wenn Timotheus zu euch kommt, sorgt bitte dafür, dass er nicht entmutigt wird. Denn er arbeitet wie ich für den Herrn. 11Niemand darf ihn herablassend behandeln. Seht zu, dass ihr ihn für die Weiterreise versorgt und er sich dann in Frieden von euch verabschieden kann. Er soll unbeschwert wieder zu mir zurückkommen, denn wir alle erwarten ihn hier16,11 Oder; denn ich erwarte ihn und die Brüder, die mit ihm gereist sind.. 12Unseren Mitarbeiter Apollos habe ich immer wieder gebeten, euch mit den anderen Brüdern zu besuchen, aber er meinte, es sei jetzt nicht angebracht. Sobald sich eine andere Gelegenheit bietet, wird er kommen.

Grüße und Segenswünsche

13Seid wachsam und steht fest im Glauben! Seid entschlossen und stark! 14Bei allem, was ihr tut, lasst euch von der Liebe leiten.

15Noch eins, liebe Brüder und Schwestern: Ihr kennt doch Stephanas und alle, die bei ihm leben. Sie waren die ersten Christen in der Provinz Achaja und haben sich ganz für den Dienst in der Gemeinde zur Verfügung gestellt. 16Hört auf solche Leute und auf alle anderen, die mitarbeiten und ihr Bestes geben. 17Ich freue mich, dass Stephanas, Fortunatus und Achaikus zu mir gekommen sind. Sie haben mir darüber hinweggeholfen, dass ich nicht bei euch sein konnte. 18Ja, sie haben mir neuen Mut gegeben, so wie sie auch euch ermutigt haben. Nehmt euch diese Männer zum Vorbild!

19Die Gemeinden der Provinz Asia senden euch herzliche Grüße. Aquila und Priska lassen euch ebenfalls grüßen, zusammen mit der Gemeinde, die sich in ihrem Haus versammelt. Sie wissen sich durch Christus, den Herrn, mit euch verbunden.

20Auch die Brüder und Schwestern hier haben mich gebeten, euch zu grüßen. Grüßt einander mit dem Friedenskuss!

21Und hier noch mein Gruß an euch, den ich, Paulus, mit eigener Hand schreibe.

22Wer den Herrn nicht liebt, den soll Gottes Urteil treffen! Unser Herr, komm! 23Die Gnade unseres Herrn Jesus sei mit euch!

24Meine Liebe gilt euch allen. Ich bin durch Jesus Christus mit euch verbunden.