1 Wafalme 6 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wafalme 6:1-38

Solomoni Ajenga Hekalu

(2 Nyakati 3)

16:1 Ezr 4:15; 5:17Katika mwaka wa 480 baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa utawala wa Solomoni katika Israeli, katika mwezi wa Zivu, ambao ndio mwezi wa pili, alianza kujenga Hekalu la Bwana.

2Hekalu hilo Mfalme Solomoni alilojenga kwa ajili ya Bwana lilikuwa na urefu wa dhiraa sitini,6:2 Dhiraa 60 ni sawa na mita 27. upana wa dhiraa ishirini6:2 Dhiraa 20 ni sawa na mita 9. na kimo cha dhiraa thelathini6:2 Dhiraa 30 ni sawa na mita 13.5. kwenda juu. 36:3 Ezr 3:10; Hag 2:3Baraza ya mbele ya Hekalu ilienea dhiraa ishirini kulingana na upana wa Hekalu na kujitokeza dhiraa kumi mbele ya Hekalu. 46:4 1Fal 6:36; Ezr 7:20; Isa 60:6; Za 68:29Akatengeneza madirisha membamba yenye vidirisha vidogo vya juu katika Hekalu. 56:5 1Nya 29:2; Yer 27:18-22; Ezr 5:14Akafanyiza vyumba vya pembeni kulizunguka Hekalu lote vikishikamana na kuta za Hekalu na za Patakatifu pa Patakatifu. 66:6 Ezr 5:3Ghorofa ya chini kabisa ilikuwa na upana wa dhiraa tano,6:6 Dhiraa 5 ni sawa na mita 2.25. ya kati ilikuwa dhiraa sita na ya tatu ilikuwa dhiraa saba.6:6 Dhiraa saba ni sawa na mita 3.15. Kuzunguka ukuta wa nje wa Hekalu akapunguza ukuta pande zote ili boriti zisishikane kwenye kuta za Hekalu.

7Katika kujenga Hekalu, yalitumika tu mawe yaliyochongwa huko machimboni, wala hakuna nyundo, patasi au chombo kingine chochote cha chuma kilichosikika sauti yake katika eneo la ujenzi wa Hekalu wakati lilipokuwa likijengwa.

86:8 1Sam 9:10Ingilio la ghorofa ya chini kabisa lilikuwa upande wa kusini wa Hekalu, ngazi ilielekea ghorofa ya kati na kutokea hapo ilielekea hadi ghorofa ya tatu. 9Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha, akiliweka paa za boriti na mbao za mierezi. 106:10 Ezr 7:23; Yer 29:7; Law 1:9; Mwa 8:21; 1Tim 2:1-2Mfalme Solomoni akajenga vyumba vya pembeni kuzunguka Hekalu lote. Kimo cha kila kimoja kilikuwa dhiraa tano. Navyo vilikuwa vimeunganishwa na Hekalu kwa boriti za mierezi.

116:11 Kum 21:22-23; Es 2:23; Ezr 7:26; Dan 2:5Neno la Bwana likamjia Solomoni kusema: 126:12 Kut 20:24; Kum 12:11; 1Fal 9:3; 2Nya 7:16; Za 132:13“Kwa habari ya Hekalu hili unalojenga, kama ukifuata amri zangu, ukatunza masharti yangu na kushika maagizo yangu yote na kuyatii, kwa kupitia wewe nitatimiza ahadi niliyomwahidi Daudi baba yako. 136:13 Ay 5:12; Ezr 4:9; Za 9:16; 1Kor 3:19Nami nitakaa miongoni mwa Waisraeli, nami sitawaacha watu wangu Israeli.”

146:14 Ezr 5:1; 7:1; Neh 2:1; Ezr 4:24Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha. 156:15 Zek 4:9Akazifunika kuta zake za ndani kwa mbao za mierezi, akizipigilia ukutani kuanzia sakafuni mwa Hekalu hadi kwenye dari na kufunika sakafu ya Hekalu kwa mbao za misunobari. 166:16 1Fal 8:63; 2Nya 7:15; Yn 10:22Akagawa dhiraa ishirini sehemu ya nyuma ya Hekalu kwa mbao za mierezi kuanzia kwenye sakafu hadi darini ili kufanya sehemu takatifu ya ndani, yaani Patakatifu pa Patakatifu. 176:17 2Sam 6:13; 1Nya 16:1-3; 2Nya 29:21; Hes 7:2-3; Ezr 8:25Ukumbi mkubwa uliokuwa mbele ya chumba hiki ndio ulikuwa na urefu wa dhiraa arobaini.6:17 Dhiraa 40 ni sawa na mita 18. 186:18 1Nya 24:1; 23:6; Hes 3:6-9; 8:9-11Hekalu ndani ilikuwa ya mierezi iliyonakshiwa mifano ya maboga na maua yaliyochanua. Kila kitu kilikuwa cha mwerezi, hakuna jiwe ambalo lilionekana.

196:19 Kut 12:11; Hes 28:16Ndani ya Hekalu akatengeneza sehemu takatifu ya ndani, kwa ajili ya kuweka Sanduku la Agano la Bwana. 206:20 2Nya 30:15-17; 35:11; Kut 12:25; 2Nya 29:34Sehemu takatifu ya ndani ilikuwa na upana, urefu na kimo cha dhiraa ishirini ndani kwa ndani. Akaifunika ndani kwa dhahabu safi, pia akaifunika madhabahu ya mierezi vivyo hivyo. 216:21 Kut 12:48; Za 93:5Solomoni akaifunika sehemu ya ndani ya Hekalu kwa dhahabu safi, naye akaitandaza mikufu ya dhahabu kutoka upande moja hadi ule mwingine mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, ambako palifunikwa kwa dhahabu. 226:22 Kut 12:17; Mit 21:1; Ezr 1:1Basi akafunika sehemu yote ya ndani kwa dhahabu. Pia akafunika madhabahu yale yaliyokuwa ndani ya Patakatifu pa Patakatifu kwa dhahabu.

23Katika Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza makerubi wawili kwa mzeituni, kila moja likiwa na dhiraa kumi6:23 Dhiraa 10 ni sawa na mita 4.5. kwenda juu. 24Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na bawa jingine dhiraa tano, hivyo urefu kutoka ncha ya bawa moja hadi ncha ya bawa jingine ulikuwa dhiraa kumi. 25Kerubi wa pili alikuwa na urefu wa dhiraa kumi pia, hivyo makerubi hao wawili walifanana kwa vipimo na kwa umbo. 26Kimo cha kila kerubi kilikuwa dhiraa kumi. 27Aliwaweka makerubi hao ndani ya Patakatifu pa Patakatifu pa Hekalu, mabawa yake yakiwa yamekunjuliwa. Bawa la kerubi mmoja liligusa ukuta mmoja, wakati bawa la yule mwingine liligusa ukuta mwingine, nayo mabawa yao mengine yaligusana katikati ya chumba. 28Akafunika wale makerubi kwa dhahabu.

29Juu ya kuta zote zilizozunguka Hekalu, za vyumba vya ndani na vya nje, zilipambwa kwa nakshi zilizokatwa za makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua. 30Pia alifunika sakafu zote za vyumba vya ndani na vya nje vya Hekalu kwa dhahabu.

31Kwa ingilio la Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza milango ya mbao za mzeituni, zikiwa na miimo na vizingiti vyenye umbo la pembe tano. 32Juu ya milango miwili ya mbao za mzeituni alinakshi makerubi, miti ya mitende pamoja na maua yaliyochanua na kufunika makerubi na miti ya mitende kwa dhahabu iliyofuliwa. 33Kwa njia iyo hiyo akatengeneza miimo yenye pande nne ya miti ya mizeituni, kwa ajili ya ingilio la ukumbi mkubwa. 34Kulikuwa na milango miwili iliyoweza kukunjuka iliyotengenezwa kwa mbao za msunobari na kila mmoja ulikuwa na bawaba ambazo zingeuwezesha kujikunja kila kipande juu ya kingine. 35Akanakshi makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua juu yake na kufunika kwa dhahabu iliyonyooshwa vizuri juu ya michoro.

36Tena akajenga ua wa ndani safu tatu za mawe yaliyochongwa na safu moja ya boriti za mierezi zilizorembwa.

37Msingi wa Hekalu la Bwana uliwekwa katika mwaka wa nne, katika mwezi wa Zivu, ndio mwezi wa tano. 38Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa Buli, ndio mwezi wa nane, Hekalu lilikamilika katika hatua zake zote kwa kufuatana na maelekezo yake Solomoni. Alilijenga kwa miaka saba.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

列王纪上 6:1-38

建造圣殿

1所罗门在做以色列王的第四年二月,即西弗月,开始为耶和华建殿。那时正是以色列人离开埃及后第四百八十年。 2所罗门王为耶和华建造的殿长二十七米,宽九米,高十三米半。 3殿前的门廊和殿一样宽九米,深四米半。 4殿有精致的窗户。 5靠殿墙、围着外殿和内殿又造了三层厢房, 6底层宽二点二五米,中层宽二点七米,上层宽三点一米。厢房的横梁都搭在殿墙突出的地方,免得插入殿墙。 7建殿的石头都在采石场凿好了,建殿的时候听不到锤子、斧头或其他铁器的响声。

8底层厢房的进口在殿的南面,沿着一道螺旋楼梯可以通到第二层和第三层。 9殿建成后,殿顶装上香柏木的梁木和木板。 10靠着殿墙所造的厢房每一层高二点二五米,用香柏木的梁木与殿墙接连起来。

耶和华的约

11耶和华对所罗门说: 12“关于你所建的这殿,若你遵行我的律例,顺从我的典章,谨守我的一切诫命,我必实现我对你父亲大卫的应许。 13我必住在以色列人当中,不抛弃我的以色列子民。”

14所罗门建造的殿落成了。 15殿里的墙壁和天花板都铺上了香柏木,地面都铺上了松木板。 16在殿的后部,从地面至天花板用香柏木板隔出长九米的内殿,就是至圣所。 17在至圣所外面是外殿,长十八米。 18殿内全部铺上香柏木,不露一点石头,香柏木上刻着野瓜和花朵的图案。 19殿的至圣所用来安放耶和华的约柜。 20至圣所长、宽和高都是九米,里面全贴上纯金,香柏木造的祭坛也包上纯金。 21殿内全部贴上纯金,至圣所前面有金链拦着。 22殿内都贴上纯金,至圣所内的祭坛也都包上纯金。

23至圣所里面放着两个橄榄木造的基路伯天使,各高四米半, 24各有两个二点二五米长的翅膀,双翅展开,两翅尖相距四点五米。 25两个基路伯的大小和形状一模一样, 26高度都是四点五米。 27他将两个基路伯安在至圣所内,两个基路伯展开翅膀,各有一个翅膀在至圣所的中央相接,另一个翅膀的尖端触到墙壁。 28这两个基路伯天使也包上金。

29内殿和外殿的墙壁都刻上基路伯天使、棕树和花朵的图案, 30地板是铺金的。 31至圣所的门、门楣和门柱都是橄榄木造的,门柱呈五角形。 32两扇用橄榄木造的门上都刻着基路伯天使、棕树和花朵的图案,并包上金。 33外殿的四角形门柱也是用橄榄木造的, 34两扇门是松木造的,每一扇门都分为可折叠的两片, 35上面刻着基路伯天使、棕树和花朵的图案,并包上金。 36内院的墙是由三层凿好的石头和一层香柏木建的。

37耶和华的殿在所罗门执政第四年的西弗月奠基, 38在他执政的第十一年的布勒月,即八月全部按规格建成,历经七年。