1 Wafalme 11 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version

1 Wafalme 11:1-43

Wakeze Solomoni

111:1 Kut 34:16; 1Fal 12:21, 31Hata hivyo, Mfalme Solomoni akawapenda wanawake wengi wa kigeni zaidi, mbali na binti Farao: wanawake wa Wamoabu, Waamoni, Waedomu, Wasidoni na Wahiti. 211:2 Kut 34:16; 1Fal 16:31Walitoka katika mataifa ambayo Bwana aliwaambia Waisraeli, “Msije mkaoana nao, kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu mgeukie miungu yao.” Hata hivyo, Solomoni akakaza kuwapenda. 311:3 Mwa 22:24; Mit 31:3Alikuwa na wake 700 mabinti wa uzao wa kifalme, na masuria 300, nao wake zake wakampotosha. 411:4 Kut 34:16; 1Nya 29:19Kadiri Solomoni alivyozidi kuzeeka, wake zake wakaugeuza moyo wake kuelekea miungu mingine, na moyo wake haukujitolea kikamilifu kwa Bwana Mungu wake, kama ulivyokuwa moyo wa Daudi baba yake. 511:5 Amu 2:13Solomoni akafuata Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, na Moleki11:5 Moleki au Milkomu ni mungu aliyekuwa akiabudiwa na Waamoni; alikuwa chukizo kwa sababu watoto walitolewa kafara kwake. mungu aliyekuwa chukizo la Waamoni. 611:6 Kum 4:25Kwa hiyo Solomoni akafanya uovu machoni pa Bwana; hakumfuata Bwana kikamilifu kama alivyofanya Daudi baba yake.

711:7 2Fal 23:13; Hes 21:29; Mdo 7:43Kwenye kilima mashariki mwa Yerusalemu, Solomoni akajenga mahali pa juu kwa ajili ya Kemoshi chukizo la Wamoabu, na kwa Moleki mungu chukizo la Waamoni. 8Akafanya hivyo kwa wake zake wote wa kigeni, ambao walifukiza uvumba na kutoa dhabihu kwa miungu yao.

911:9 1Fal 3:5Bwana akamkasirikia Solomoni kwa sababu moyo wake uligeuka mbali na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye alikuwa amemtokea mara mbili. 1011:10 1Fal 9:6; 6:12Ingawa alikuwa amemkataza Solomoni kufuata miungu mingine, Solomoni hakutii amri ya Bwana. 11Kwa hiyo Bwana akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa hii ndiyo hali yako na hukushika Agano langu na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme kutoka kwako na kumpa mmoja wa walio chini yako. 12Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi baba yako, sitafanya jambo hili wakati wa uhai wako. Nitaurarua kutoka mikononi mwa mwanao. 1311:13 2Sam 7:15; Kum 12:11Lakini pia sitaurarua ufalme wote kutoka kwake, bali nitampa kabila moja kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu na kwa ajili ya Yerusalemu, ambao nimeuchagua.”

Adui Za Solomoni

14Kisha Bwana akamwinua adui dhidi ya Solomoni, Hadadi, Mwedomu, kutoka ukoo wa ufalme wa Edomu. 1511:15 1Nya 18:12Huko nyuma wakati Daudi alipokuwa akipigana na Edomu, Yoabu jemadari wa jeshi, aliyekuwa amekwenda kuzika waliouawa, alikuwa amewaua wanaume wote waliokuwako Edomu. 16Yoabu na Waisraeli wote walikaa huko kwa miezi sita, mpaka walipomaliza kuwaangamiza wanaume wote huko Edomu. 17Lakini Hadadi, akiwa bado mvulana mdogo, alikimbilia Misri akiwa na baadhi ya maafisa wa Kiedomu waliokuwa wakimhudumia baba yake. 1811:18 Hes 10:12Wakaondoka Midiani wakaenda Parani. Basi wakichukua pamoja nao wanaume kutoka Parani, wakaenda Misri, kwa Farao mfalme wa Misri, ambaye alimpa Hadadi nyumba, ardhi na akampatia chakula.

19Farao akapendezwa sana na Hadadi hata akampa ndugu wa mkewe mwenyewe, Malkia Tapenesi, ili aolewe na Hadadi. 20Huyo ndugu wa Tapenesi akamzalia mwana aliyeitwa Genubathi, ambaye alilelewa na Tapenesi katika jumba la kifalme. Huko Genubathi aliishi pamoja na watoto wa Farao mwenyewe.

21Alipokuwa huko Misri, Hadadi alisikia kwamba Daudi amepumzika na baba zake na ya kwamba pia Yoabu aliyekuwa jemadari wa jeshi amekufa. Ndipo Hadadi akamwambia Farao, “Niruhusu niende ili niweze kurudi katika nchi yangu.”

22Farao akauliza, “Umekosa nini hapa, kwamba unataka kurudi katika nchi yako?”

Hadadi akajibu, “Hakuna, lakini niruhusu niende!”

2311:23 1Fal 5:4; 2Sam 8:3Mungu akamwinua adui mwingine dhidi ya Solomoni, Rezoni mwana wa Eliada, ambaye alikuwa amemkimbia bwana wake Hadadezeri, mfalme wa Soba. 2411:24 2Sam 8:5Akawakusanya watu, naye akawa kiongozi wa kundi la waasi, wakati Daudi alipoangamiza majeshi ya Soba; waasi walikwenda Dameski, mahali walipokaa na kumiliki. 2511:25 Mwa 10:22; 2Sam 10:19Rezoni alikuwa adui wa Israeli kwa muda wote alioishi Solomoni, ukiongezea matatizo yaliyosababishwa na Hadadi. Kwa hiyo Rezoni akatawala katika Aramu11:25 Yaani Shamu (ambayo leo ni Syria). na alikuwa mkatili kwa Israeli.

Yeroboamu Anaasi Dhidi Ya Solomoni

2611:26 2Nya 13:6Pia, Yeroboamu mwana wa Nebati aliasi dhidi ya mfalme. Alikuwa mmoja wa maafisa wa Solomoni, Mwefraimu kutoka Sereda, ambaye mama yake alikuwa mjane aliyeitwa Serua.

2711:27 1Fal 9:24Haya ndiyo maelezo ya jinsi alivyomwasi mfalme: Solomoni alikuwa amejenga Milo11:27 Milo maana yake Boma la Ngome. naye akawa ameziba mwanya katika ukuta wa mji wa Daudi baba yake. 2811:28 Rut 2:1; Mit 22:29Basi Yeroboamu alikuwa mtu shujaa na hodari, naye Solomoni alipoona jinsi kijana alivyofanya kazi yake, akamweka kuwa kiongozi wa kazi yote ya mikono ya nyumba ya Yosefu.

2911:29 1Fal 12:15; 14:2Karibu na wakati ule Yeroboamu alikuwa anatoka nje ya Yerusalemu, Ahiya nabii Mshiloni akakutana naye njiani, akiwa amevaa joho jipya. Hawa wawili walikuwa peke yao mashambani, 3011:30 1Sam 15:27naye Ahiya akachukua joho jipya alilokuwa amevaa akalirarua vipande kumi na viwili. 3111:31 1Fal 11:11; 1Sam 15:27Kisha akamwambia Yeroboamu, “Chukua vipande kumi kwa ajili yako, kwa kuwa hivi ndivyo Bwana, Mungu wa Israeli asemavyo: ‘Tazama, ninakwenda kuuchana ufalme kutoka mikononi mwa Solomoni na kukupa wewe makabila kumi. 3211:32 2Sam 7:15Lakini kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi na mji wa Yerusalemu, ambao nimeuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli, atakuwa na kabila moja. 3311:33 Amu 2:13; 1Fal 3:3Nitafanya hivi kwa sababu wameniacha mimi na kuabudu Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, Kemoshi mungu wa Wamoabu, na Moleki mungu wa Waamoni, nao hawakwenda katika njia zangu ili kufanya yaliyo sawa machoni pangu, wala kushika amri na sheria zangu kama Daudi, babaye Solomoni, alivyofanya.

34“ ‘Lakini sitauondoa ufalme wote kutoka mikononi mwa Solomoni, nimemfanya mtawala siku zote za maisha yake kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, niliyemchagua na ambaye aliyatunza maagizo na amri zangu. 35Nitauondoa ufalme kutoka mikononi mwa mwanawe na kukupa wewe makabila kumi. 3611:36 1Fal 12:17Nitampa mwanawe kabila moja ili kwamba Daudi mtumishi wangu awe na taa mbele zangu daima katika Yerusalemu, mji ambao nimeuchagua kuweka Jina langu. 3711:37 1Fal 14:7; 2Sam 3:21Hata hivyo, kukuhusu wewe Yeroboamu, nitakutwaa, nawe utatawala juu ya yote yale moyo wako unayotamani, utakuwa mfalme juu ya Israeli. 3811:38 Kum 12:25; 2Sam 3:15; Kut 1:21Ikiwa utafanya kila nitakalokuamuru, kuenenda katika njia zangu na kufanya yaliyo sawa mbele za macho yangu kwa kuzishika amri zangu na maagizo yangu kama alivyofanya Daudi mtumishi wangu, nitakuwa pamoja nawe. Nitakujengea ufalme utakaodumu kama ule niliomjengea Daudi, nami nitakupa Israeli. 39Nitawatesa wazao wa Daudi kwa ajili ya hili, lakini siyo milele.’ ”

4011:40 1Fal 12:2; 2Nya 10:2; 12:2Solomoni akajaribu kumuua Yeroboamu, lakini Yeroboamu akakimbilia Misri, kwa Mfalme Shishaki, naye akakaa huko mpaka Solomoni alipofariki.

Kifo Cha Solomoni

(2 Nyakati 9:29-31)

41Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, yote aliyoyafanya na hekima aliyoionyesha, je hayakuandikwa yote katika kitabu cha matendo cha Solomoni? 42Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu. 43Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.

New Russian Translation

3-я книга Царств 11:1-43

Соломон отворачивается от Господа

1Но, кроме дочери фараоновой, царь Соломон полюбил еще много других чужеземных женщин — моавитянок, аммонитянок, эдомитянок, сидонянок и хеттеянок. 2Они были из тех народов, о которых Господь сказал израильтянам: «Не роднитесь с ними браком, потому что они непременно обратят ваше сердце к своим богам». Соломона тянуло к ним. 3У него было семьсот жен царского рода и триста наложниц, и жёны сбили его с истинного пути. 4Когда Соломон состарился, жёны обратили его сердце к чужим богам, и оно перестало быть полностью преданным Господу, его Богу, каким было сердце Давида, его отца. 5Он пошел за Астартой11:5 Астарта. Богиня любви и плодородия, богиня-воительница., богиней сидонян, и Милхомом11:5 Милхом. Или: Молох— люди приносили этому божеству в жертву детей., омерзительным богом аммонитян. 6Соломон делал зло в глазах Господа, он не следовал за Господом полностью, как Давид, его отец.

7На холме к востоку от Иерусалима Соломон построил святилище11:7 Букв.: возвышенность. Кемошу11:7 Кемош. Божество, в жертвы которому приносились люди., омерзительному богу Моава, и Молоху, омерзительному богу аммонитян. 8То же самое он сделал для всех чужеземных жен, которые возжигали благовония и приносили жертвы своим богам.

9Господь разгневался на Соломона, потому что его сердце отвернулось от Господа, Бога Израиля, Который дважды являлся ему. 10Несмотря на то что Он запретил Соломону идти за чужими богами, Соломон не выполнил повеления Господа. 11И Господь сказал Соломону:

— Раз ты таков и не сохранил Моего завета и Моих установлений, которые Я повелел тебе соблюдать, Я непременно отниму у тебя царство и отдам его одному из твоих подданных. 12Но ради Давида, твоего отца, Я не сделаю этого при твоей жизни. Я вырву его из рук твоего сына. 13Но Я отниму у него не всё царство — Я оставлю ему один род ради Давида, Моего слуги, и ради Иерусалима, который Я избрал.

Враги Соломона

14Господь воздвиг Соломону врага — эдомитянина Гадада из царской семьи Эдома. 15Прежде, когда Давид был в Эдоме, начальник войска Иоав пришел хоронить погибших и перебил в Эдоме всех мужчин. 16Иоав и все израильтяне оставались там шесть месяцев, пока не истребили в Эдоме всех мужчин. 17Но Гадад — тогда еще лишь ребенок — бежал в Египет с некоторыми эдомскими приближенными, служившими его отцу. 18Они отправились в путь из страны Мадиана и пришли в пустыню Паран. Взяв с собой людей из Парана, они пришли в Египет, к фараону, царю Египта, который дал Гададу дом, пропитание и землю.

19Гадад был так угоден фараону, что тот дал ему в жёны сестру своей жены, царицы Тахпенесы. 20Сестра Тахпенесы родила ему сына Генувата, которого Тахпенеса вырастила в царском дворце. Генуват жил там вместе с детьми фараона.

21Будучи в Египте, Гадад услышал о том, что Давид упокоился со своими предками и что начальник войска Иоав умер. Тогда Гадад сказал фараону:

— Отпусти меня в мою страну.

22— Разве тебе чего-то недостает у меня, что ты так хочешь вернуться в свою страну? — спросил фараон.

— Нет, — ответил Гадад, — но все-таки отпусти меня!

23Бог воздвиг Соломону и другого врага — Резона, сына Элиады, который убежал от государя своего, Ададезера, царя Цовы. 24После того как Давид разбил войска Цовы, Резон собрал вокруг себя бунтовщиков и возглавил их. Они пришли в Дамаск, поселились там и сделали его царем Дамаска. 25Резон был врагом Израиля всё время, пока был жив Соломон, умножая зло, чинимое Гададом. Он правил страной Арам и презирал Израиль.

Пророчество Ахии о разделении царства

26Иеровоам, сын Навата, поднял мятеж против царя. Он был одним из приближенных Соломона, ефремит из Цереды, а матерью его была вдова по имени Церуа.

27Вот история о том, как он поднял мятеж против царя: Соломон построил укрепление Милло11:27 См. сноску к 9:15. и заделал брешь в стене Города Давида, своего отца. 28Иеровоам был очень сильным и храбрым, и когда Соломон заметил, как хорошо этот молодой человек исполняет свою работу, он поставил его над всеми подневольными работниками из дома Иосифа.

29В то время Иеровоаму случилось выйти из Иерусалима, и на пути его встретил пророк Ахия из Шило, одетый в новую одежду. Они были в том поле лишь вдвоем, 30и Ахия, взявшись за новую одежду, что была на нем, разорвал ее на двенадцать кусков. 31Затем он сказал Иеровоаму:

— Возьми десять кусков себе, потому что так говорит Господь, Бог Израиля: «Вот Я вырываю царство из руки Соломона и отдаю тебе десять родов. 32Но ради Моего слуги Давида и города Иерусалима, который Я избрал среди всех родов Израиля, у него будет один род. 33Я сделаю это, потому что они оставили Меня и поклонялись Астарте, богине сидонян, Кемошу, богу моавитян, и Милхому, богу аммонитян, и не следовали Моими путями, не делали того, что праведно в Моих глазах, и не соблюдали Мои установления и законы, как делал Давид, отец Соломона.

34Но Я заберу из рук Соломона не всё царство. Я сделал его правителем во все дни его жизни ради Давида, Моего слуги, которого Я избрал и который исполнял Мои повеления и установления. 35Я возьму царство из рук его сына и отдам тебе десять родов. 36Я дам один род его сыну, чтобы у Давида, Моего слуги, всегда был светильник передо Мной в Иерусалиме, в городе, который Я избрал, чтобы поместить там Мое имя. 37А тебя Я избираю, и ты будешь править всем, чем пожелает твое сердце, — ты будешь царем Израиля. 38Если ты будешь исполнять всё, что Я тебе велю, ходить Моими путями и делать то, что праведно в Моих глазах, исполняя Мои установления и повеления, как делал Мой слуга Давид, то Я буду с тобой. Я создам тебе такой же крепкий дом, как тот, что Я создал Давиду, и отдам тебе Израиль. 39Я накажу потомков Давида, но не навеки».

40Соломон пытался убить Иеровоама, но Иеровоам бежал в Египет к царю Шишаку и оставался там до смерти Соломона.

Смерть Соломона

(2 Пар. 9:29–31)

41Что же до прочих событий правления Соломона и всего, что он сделал, и его мудрости, то разве не записаны они в книге дел Соломона? 42Соломон правил в Иерусалиме всем Израилем сорок лет. 43Потом он упокоился со своими предками и был похоронен в Городе Давида, своего отца. А Ровоам, его сын, стал царем вместо него.