1 Timotheo 1 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

1 Timotheo 1:1-20

11:1 Tit 1:3; Kol 1:27Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na ya Kristo Yesu tumaini letu.

21:2 Mdo 16:1; 1Kor 4:17; 1The 2:11Kwa Timotheo, mwanangu halisi katika imani:

Neema, rehema na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.

Maonyo Dhidi Ya Walimu Wa Uongo

31:3 Mdo 18:19; Gal 1:6, 7Kama nilivyokusihi wakati nilipokwenda Makedonia, endelea kubaki Efeso, ili kwamba upate kuwaagiza watu wasiendelee kufundisha mafundisho ya uongo 41:4 1Tim 4:7; 2Tim 4:4; 1Tim 6:4wala wasitoe muda wao kwa hadithi za kubuniwa na orodha za majina ya vizazi visivyo na mwisho, ambazo huchochea mabishano badala ya mpango wa Mungu utokanao na imani. 51:5 2Tim 2:22; 1:5Kusudi la maagizo haya ni upendo utokao katika moyo safi, dhamiri njema na imani ya kweli. 61:6 1Tim 6:4, 20Watu wengine wamepotoka kutoka haya na kugeukia majadiliano yasiyo na maana kwa kuwa, 71:7 Efe 4:11; Ay 38:2wanataka kuwa walimu wa sheria, lakini hawajui mambo yale wanayosema wala hayo wanayoyatumainia kwa uthabiti.

81:8 Rum 7:12Tunajua kwamba sheria ni njema ikiwa inatumika kwa halali kama ilivyokusudiwa. 91:9 Gal 3:19; 5:23Lakini tunajua ya kuwa sheria si kwa ajili ya wenye haki, bali kwa ajili ya wavunja sheria na waasi, kwa ajili ya wasiomcha Mungu na wenye dhambi, wasio watakatifu na wanaokufuru; kwa wale wawauao baba zao au mama zao, kwa wauaji, 101:10 1Tim 6:3; 2Tim 1:13kwa wazinzi na wahanithi, kwa wale wauzao watu, na kwa waongo na waapao kwa uongo, na kwa chochote kingine kilicho kinyume na mafundisho ya kweli, 111:11 1The 2:4ambayo yanakubaliana na Injili ya utukufu wa Mungu anayehimidiwa, ambayo mimi nimewekewa amana.

Neema Ya Mungu Kwa Paulo

121:12 Flp 4:13Namshukuru Kristo Yesu Bwana wetu, aliyenitia nguvu, kwa sababu aliniona mwaminifu, akaniteua kwa kazi yake. 131:13 Mdo 8:3; 26:9Ingawa wakati fulani nilikuwa mwenye kukufuru, mtesaji na mwenye jeuri, lakini nilipata rehema kwa sababu nilitenda hivyo kwa kutojua na kutoamini kwangu. 141:14 Rum 5:20; 2Tim 1:13Neema ya Bwana wetu ilimiminwa juu yangu kwa wingi, ikiambatana na imani na upendo ulio katika Kristo Yesu.

151:15 1Tim 4:9; 2Tim 2:11Msemo huu ni wa kweli na unaostahili kukubalika, usemao kwamba: Kristo Yesu alikuja ulimwenguni kuokoa wenye dhambi, ambao mimi ndiye niliye mbaya kuliko wote. 161:16 1Tim 1:13; Rum 2:4; Yn 3:15; Mt 25:46Lakini kwa sababu hiyo nilipata rehema, ili katika mimi, niliyekuwa mwenye dhambi kuliko wote, Kristo Yesu apate kuonyesha uvumilivu wake usio na kikomo, ili niwe kielelezo kwa wale watakaomwamini na wapate uzima wa milele. 171:17 Ufu 15:3; Kol 1:15; Rum 11:36Basi Mfalme wa milele, asiye na mwisho, asiyeonekana, aliye Mungu pekee, apewe heshima na utukufu milele na milele. Amen.

181:18 1Tim 4:14; 2Tim 4:7Mwanangu Timotheo, ninakupa agizo hili, kwa kadiri ya maneno ya unabii yaliyosemwa kukuhusu, ili kwa kuyafuata upate kupigana vita vizuri, 191:19 1Tim 6:21; Mdo 23:1; 1Tim 6:21; 2Tim 2:18ukiishikilia imani na dhamiri njema, ambazo wengine wamevikataa, na hivyo wakaangamia kwa habari ya imani yao. 201:20 2Tim 2:17; 4:14; 1Kor 5:5Miongoni mwao wako Himenayo na Aleksanda, ambao nimemkabidhi Shetani ili wafundishwe wasije wakakufuru.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

提摩太前书 1:1-20

1保罗奉我们救主上帝和赐我们盼望的基督耶稣的命令,做基督耶稣的使徒, 2写信给因信主而做我真儿子的提摩太

愿父上帝和我们的主基督耶稣赐给你恩典、怜悯和平安!

谨防异端邪说

3我去马其顿的时候,曾经劝你继续留在以弗所,好命令那几个人不要传讲异端邪说, 4也不要沉迷于无稽之谈和冗长的家谱,因为这些事只会引起争论,无法帮助人凭信心认识上帝的计划。 5这命令的目的是为了爱,这爱来自于清洁的心、无愧的良心和真实无伪的信心。 6可惜有些人却偏离这些,转向空洞的谈论。 7他们想做律法教师,却不明白自己所谈论所主张的。

8我们知道,只要用得合宜,律法本是好的。 9因为律法并不是为义人设的,而是为了对付那些目无法纪、大逆不道、不敬畏上帝、犯罪作恶、不圣洁、贪恋世俗、杀害父母、行凶害命、 10淫乱、同性恋、拐卖人口、说谎、起假誓的人,以及其他违反正道的人。 11这正道来自当受称颂的上帝托付我传扬的荣耀福音。

感谢上帝的怜悯

12我感谢赐我力量的主基督耶稣,因为祂视我忠心可靠,派我事奉祂。 13尽管我从前是个亵渎上帝、迫害和侮辱信徒的人,但我仍然蒙了怜悯,因为那时我无知,还没有信耶稣。 14我们的主赐给我丰富的恩典,使我在基督耶稣里有信心和爱心。

15这句话千真万确、完全可信:“基督耶稣降世,为要拯救罪人。”在罪人中我是个罪魁, 16但我依然蒙了怜悯,因为基督耶稣要在我这个罪魁身上彰显祂无限的忍耐,使我做那些要信靠祂并得永生之人的榜样。

17愿尊贵、荣耀归给那位不朽的、肉眼不能见的万世君王——独一无二的上帝,直到永远。阿们!

18我儿提摩太啊,我依照从前有关你的预言,把这命令托付给你,好使你借此打美好的仗。 19你要持守信心和无愧的良心。有些人丧掉良心,结果他们的信仰就像船触了礁, 20其中有许米乃亚历山大。我已经把他们交给撒旦,使他们学到教训,不再说亵渎的话。