1 Samweli 3 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

1 Samweli 3:1-21

Bwana Amwita Samweli

13:1 1Sam 2:11; Za 74:9; Mao 2:9; Eze 7:26; Amo 8:11Kijana Samweli alihudumu mbele za Bwana chini ya Eli. Katika siku zile neno la Mungu lilikuwa adimu, hapakuwepo na maono mengi.

23:2 1Sam 4:15; Mwa 27:1Usiku mmoja Eli, ambaye macho yake yalikuwa yamefifia sana kiasi kwamba aliona kwa shida sana, alikuwa amelala mahali pake pa kawaida. 33:3 Kut 25:31-38; Law 24:1-4; 1Sam 1:9; Kum 10:1-5; 1Fal 6:19; 8:1Taa ya Mungu bado ilikuwa haijazimika, na Samweli alikuwa amelala Hekaluni3:3 Hekaluni maana yake ndani ya Maskani ya Bwana. mwa Bwana, ambapo Sanduku la Mungu lilikuwako. 43:4 Mwa 22:1; Kut 3:4Kisha Bwana akamwita Samweli.

Samweli akajibu, “Mimi hapa.” 5Naye akakimbia kwa Eli na kumwambia, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.”

Lakini Eli akasema, “Sikukuita; rudi ukalale.” Hivyo akaenda kulala.

6Bwana akaita tena, “Samweli!” Naye Samweli akaamka, kwenda kwa Eli na kusema, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.”

Eli akasema, “Mwanangu, sikukuita, rudi ukalale.”

73:7 1Sam 2:12; Hes 12:6; Mdo 19:2; Amo 3:7Wakati huu Samweli alikuwa bado hajamjua Bwana. Neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake.

8Bwana akamwita Samweli mara ya tatu, naye Samweli akaamka kwenda kwa Eli na kusema, “Mimi hapa, kwa kuwa umeniita.”

Ndipo Eli akatambua kuwa Bwana alikuwa akimwita kijana. 9Hivyo Eli akamwambia Samweli, “Nenda ukalale, na kama akikuita, sema, ‘Nena Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikiliza.’ ” Hivyo Samweli akaenda na kulala mahali pake.

103:10 Kut 3:4; Za 85:8; Mdo 9:6Bwana akaja akasimama hapo, akiita kama mara zile nyingine, “Samweli! Samweli!”

Kisha Samweli akasema, “Nena Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikiliza.”

113:11 2Fal 21:12; Ay 15:21; Yer 19:3Naye Bwana akamwambia Samweli: “Tazama, nipo karibu kufanya kitu katika Israeli ambacho kitafanya masikio ya kila mmoja atakayesikia yawashe. 123:12 1Sam 2:27-36Wakati huo nitatimiza dhidi ya Eli kila kitu nilichonena dhidi ya jamaa yake, kuanzia mwanzo mpaka mwisho. 133:13 1Fal 1:6; 1Sam 2:12Kwa kuwa nilimwambia kwamba ningehukumu jamaa yake milele kwa sababu ya dhambi aliyoijua, wanawe kumkufuru Mungu, naye akashindwa kuwazuia. 143:14 1Sam 2:25; Law 15:30-31; Isa 22:14; Hes 12:6; Yer 7:16; Ebr 10:26-31Kwa hiyo, nikaapa kuhusu nyumba ya Eli, ‘Hatia ya nyumba ya Eli kamwe haitaweza kufidiwa kwa dhabihu au sadaka.’ ”

153:15 1Sam 3:2Samweli akalala mpaka asubuhi, kisha akafungua milango ya nyumba ya Bwana. Aliogopa kumwambia Eli yale maono, 16lakini Eli akamwita na kumwambia, “Samweli mwanangu.”

Samweli akamjibu, “Mimi hapa.”

173:17 1Fal 22:14; Yer 23:28; 38:14; 42:4; Rut 1:17; 1:17; Mt 26:63Eli akamuuliza, “Ni nini alichokuambia? Usinifiche. Bwana na ashughulike nawe, tena kwa ukali, kama utanificha chochote alichokuambia.” 183:18 Amu 10:15; 2:16; Mwa 18:25; 1Sam 16:10-12; Isa 39:8; 1Pet 5:6Kwa hiyo Samweli akamwambia kila kitu, bila kumficha chochote. Ndipo Eli akasema, “Yeye ni Bwana; na afanye lile lililo jema machoni pake!”

193:19 Mwa 21:22; Hes 14:43; Amu 13:24; 1Sam 9:6; Mwa 39:2Bwana alikuwa pamoja na Samweli alipokuwa akikua, na hakuacha hata moja ya maneno yake lianguke chini. 203:20 Amu 20:1; Kum 18:22; Eze 33:33; Amu 20:1Nao Israeli wote kuanzia Dani hadi Beer-Sheba wakatambua kuwa Samweli amethibitishwa kuwa nabii wa Bwana. 213:21 Mwa 12:7; Hes 12:6; Amo 3:7Bwana akaendelea kutokea huko Shilo, na huko kujidhihirisha kwa Samweli kwa njia ya neno lake.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

撒母耳记上 3:1-21

主呼召撒母耳

1撒母耳跟着以利事奉耶和华。那时候,耶和华的话语稀少,异象也不多。 2一天晚上,老眼昏花的以利正睡在自己的房里。 3上帝的灯还没有熄灭,撒母耳睡在耶和华的殿内,那里有上帝的约柜。 4耶和华呼唤撒母耳撒母耳答道:“我在这里!” 5他跑到以利跟前,说:“我来了,你叫我吗?”以利说:“我没有叫你,你去睡吧。”于是,他就回去睡觉。 6耶和华又呼唤撒母耳撒母耳起来到以利跟前,说:“我来了,你叫我吗?”以利答道:“孩子,我没有叫你,回去睡吧。” 7那时,撒母耳还不认识耶和华,耶和华的话还没有向他显明。 8耶和华第三次呼唤他,撒母耳起来,到以利面前,说:“我来了,你叫我吗?”这时候,以利才明白原来是耶和华在呼唤这孩子。 9他就吩咐撒母耳说:“你回去睡吧,要是再呼唤你,你就说,‘耶和华啊,请吩咐,仆人恭听。’”于是,撒母耳就回去睡下。 10耶和华来站在那里,再次像刚才一样呼唤:“撒母耳撒母耳!”撒母耳答道:“请吩咐,仆人恭听。” 11耶和华对撒母耳说:“我要在以色列做一件令人震惊的事。 12到时候,我要应验我说的有关以利家的一切预言。 13我对以利说过我要永远惩罚他家,因为他知道自己的儿子亵渎我,却没有约束他们。 14所以,我向以利家起誓说,‘靠祭物或礼物绝不能赎去以利家的罪恶。’”

15撒母耳在床上躺到天亮,然后起来打开耶和华的殿门。他不敢把异象告诉以利16以利叫他:“撒母耳,我的孩子。”撒母耳答道:“我在这里。” 17以利说:“耶和华对你说了什么?你不要向我隐瞒。如果你隐瞒一句,愿上帝重重地惩罚你。”

18撒母耳就一五一十地告诉了他。以利说:“祂是耶和华,祂看怎样好,就怎样行吧。” 19撒母耳渐渐长大,耶和华与他同在,使他所说的话没有一句落空。 20别示巴,全以色列的人都知道撒母耳被立为耶和华的先知。 21耶和华继续在示罗显现,用自己的话启示撒母耳