1 Samweli 20 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

1 Samweli 20:1-42

Daudi Na Yonathani

120:1 1Sam 24:9; 22:23; 23:15; 24:11; 25:29; Za 40:14; 54:3; 63:9; 70:2Kisha Daudi akakimbia kutoka Nayothi huko Rama akamwendea Yonathani na kumuuliza, “Kwani nimefanya nini? Kosa langu ni nini? Nimemkosea baba yako kwa jinsi gani, hata kwamba anajaribu kuuondoa uhai wangu?”

220:2 Mwa 44:7; Yos 22:29Yonathani akajibu, “La hasha! Hutakufa! Tazama, baba yangu hafanyi kitu chochote, kikubwa au kidogo, bila kuniambia mimi. Kwa nini anifiche hili? Sivyo ilivyo!”

320:3 Kum 6:13Lakini Daudi akaapa na kusema, “Baba yako anajua kabisa kwamba nimepata kibali mbele yako, naye amesema moyoni mwake, ‘Yonathani sharti asilijue hili, la sivyo atahuzunika.’ Lakini kweli kama Bwana aishivyo na kama uishivyo, kuna hatua moja tu kati yangu na mauti.”

4Yonathani akamwambia Daudi, “Chochote unachotaka nifanye, nitakufanyia.”

520:5 Hes 10:10; 25:11; 1Sam 9:12; 2Fal 4:23; 1Nya 23:31; 2Nya 2:4; Ezr 3:5; Neh 10:33; Za 81:3; Isa 1:13; Eze 45:17; 46:6; Za 55:13; Yn 8:59Basi Daudi akamwambia, “Angalia, kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo, nami inanipasa kula chakula pamoja na mfalme; lakini niache niende kujificha shambani mpaka kesho kutwa. 620:6 1Sam 17:58; 1:3; 16:4; 9:12Kama baba yako akiona ya kuwa sipo, mwambie, ‘Daudi aliniomba sana ruhusa kuwahi Bethlehemu, mji wake wa nyumbani, kwa sababu dhabihu ya mwaka inafanywa huko kwa ajili ya ukoo wake wote.’ 720:7 1Sam 10:27; 25:17; 18:11; Kum 1:23Kama akisema, ‘Ni vyema sana,’ basi mtumishi wako yu salama. Lakini kama akikasirika, unaweza kuwa na hakika kwamba anakusudia kunidhuru. 820:8 1Sam 18:3; 23:18; 2Sam 14:32; Yos 2:14; Rut 1:8Lakini kwa habari yako wewe, mtende wema mtumishi wako, kwa sababu mmeingia kwenye agano pamoja naye mbele za Bwana. Kama nina hatia, basi niue wewe mwenyewe! Kwa nini unikabidhi kwa baba yako?”

9Yonathani akasema, “La hasha! Kama ningekuwa na kidokezo kidogo kwamba baba yangu amekusudia kukudhuru wewe, je, nisingekuambia?”

10Daudi akamuuliza, “Je, nani atakayeniambia kama baba yako atakujibu kwa ukali?”

11Yonathani akamwambia, “Njoo, twende shambani.” Basi wakaenda huko pamoja.

1220:12 1Sam 19:3; Yos 22:22Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Ninakuahidi kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli, hakika nitamchunguza baba yangu wakati kama huu kesho kutwa! Kama ameweka utaratibu wa kufaa kukuhusu wewe, je, sitakutumia ujumbe na kukufahamisha? 1320:13 Rut 1:17; 1Sam 16:18; 18:12Lakini ikiwa baba yangu amenuia kukudhuru, Bwana na anishughulikie kwa ukali, iwapo sitakufahamisha na kukuaga uende salama. Bwana na awe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na baba yangu. 14Lakini nitendee wema usiokoma kama ule wa Bwana siku zote za maisha yangu, ili nisije nikauawa, 1520:15 1Sam 24:21; 2Sam 9:7; Mwa 21:23wala usiuondoe wema wako kwa jamaa yangu, hata kama ni wakati ule Bwana atakapokuwa amekatilia mbali kila adui wa Daudi kutoka kwenye uso wa dunia.”

1620:16 1Sam 18:1-3; 25:22-23; Yos 22:23; 2Sam 4:7; 21:8Basi Yonathani akafanya agano na nyumba ya Daudi, akisema: “Bwana na awaangamize adui za Daudi.” 1720:17 Yos 9:18; 1Sam 18:3; 2Sam 1:26Naye Yonathani akamtaka Daudi athibitishe tena kiapo chake cha kumpenda, kwa sababu Yonathani alimpenda Daudi kama nafsi yake mwenyewe.

18Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Kesho ni sikukuu ya Mwezi Mwandamo. Itajulikana kwamba haupo kwa kuwa kiti chako kitakuwa hakina mtu. 1920:19 1Sam 19:2Kesho kutwa, inapokaribia jioni, nenda mahali pale ulipojificha wakati tatizo hili lilipoanza na usubiri karibu na jiwe la Ezeli. 2020:20 2Fal 13:15Nitapiga mishale mitatu kando yake, kama kwamba nilikwenda kulenga shabaha. 2120:21 Kum 6:13; 10:20; Isa 65:16; Yer 4:2Kisha nitamtuma mvulana na kumwambia, ‘Nenda ukaitafute mishale.’ Kama nikimwambia, ‘Tazama mishale iko upande huu wako! Uilete hapa,’ basi uje, kwa sababu hakika kama Bwana aishivyo, wewe ni salama, hakuna hatari. 22Lakini kama nikimwambia huyo mvulana, ‘Angalia, mishale iko mbele yako,’ basi inakupasa uondoke, kwa sababu Bwana amekuruhusu uende zako. 2320:23 Mwa 31:50Kuhusu yale tuliyozungumza wewe na mimi: kumbuka, Bwana ndiye shahidi kati yako wewe na mimi milele.”

2420:24 Hes 10:10; Mit 27:12Basi Daudi akajificha shambani, na sikukuu ya Mwezi Mwandamo ilipowadia, mfalme akaketi ili ale. 2520:25 1Sam 14:50Akaketi mahali pake pa kawaida karibu na ukuta, kuelekeana na Yonathani, naye Abneri akaketi karibu na Mfalme Sauli, lakini kiti cha Daudi kilikuwa wazi. 2620:26 Law 15:5; 1Sam 16:5; Law 6:2; 7:21; Hes 19:16; 1Kor 15:33; 2Kor 6:17; Efe 2:1-3; 5:11Sauli hakusema chochote siku ile kwa kuwa alifikiri, “Kuna kitu cha lazima kimetokea kwa Daudi ambacho kimemfanya najisi asihudhurie karamuni, hakika yeye yu najisi.” 27Lakini siku iliyofuata, siku ya pili ya mwezi, kiti cha Daudi kilikuwa wazi tena. Kisha Sauli akamwambia mwanawe Yonathani, “Kwa nini mwana wa Yese hajaja chakulani jana wala leo?”

28Yonathani akamjibu, “Daudi alinisihi sana nimpe ruhusa aende Bethlehemu. 2920:29 Mwa 8:20Alisema, ‘Niruhusu niende, kwa sababu jamaa yetu wana dhabihu mjini, na ndugu yangu ameniagiza niwepo huko. Kama nimepata kibali mbele yako, niruhusu niende kuona ndugu zangu.’ Hii ndiyo sababu hakuja mezani pa mfalme.”

30Hasira ya Sauli ikawaka dhidi ya Yonathani na kumwambia, “Wewe mwana wa mwanamke mkaidi na mwasi! Je, sijui kuwa umekuwa upande wa mwana wa Yese kwa aibu yako mwenyewe na kwa aibu ya mama yako aliyekuzaa? 3120:31 1Sam 23:17; 24:20Maadamu mwana wa Yese angali anaishi katika dunia hii wewe wala ufalme wako hautasimama. Sasa tuma aitwe umlete kwangu, kwa kuwa ni lazima afe!”

3220:32 1Sam 19:4-5; Mt 23:27; Mwa 31:36; Lk 23:22; Za 25:3; 69:4; Mit 14:25; 24:11; Mt 27:23; Yn 7:31; 15:25Yonathani akamuuliza baba yake, “Kwa nini auawe? Kwani amefanya nini?” 3320:33 1Sam 18:11, 17Lakini Sauli akamtupia Yonathani mkuki wake kwa nguvu ili amuue. Hapo ndipo Yonathani alipotambua kwamba baba yake alikusudia kumuua Daudi.

34Yonathani akainuka kutoka mezani kwa hasira kali. Siku ile ya pili ya mwezi hakula chakula, kwa kuwa alikuwa amehuzunishwa na vitendo vya aibu ambavyo baba yake alikuwa anamtendea Daudi.

35Kesho yake asubuhi Yonathani alikwenda shambani kukutana na Daudi. Alikuwa amefuatana na mvulana mdogo, 36naye Yonathani akamwambia yule mvulana, “Kimbia ukatafute mishale nitakayorusha.” Mvulana alipokuwa akikimbia, akarusha mishale mbele yake. 37Yule mvulana alipofika mahali pale ambapo mshale wa Yonathani ulipokuwa umeanguka, Yonathani akamwita, “Je, mshale hauko mbele yako?” 38Yonathani akampigia kelele, “Harakisha, nenda haraka! Usisimame!” Mvulana akaokota mshale na kurudi kwa bwana wake. 39(Mvulana hakujua chochote juu ya hayo yote; Yonathani na Daudi tu ndio waliojua.) 40Basi Yonathani akampa yule mvulana silaha zake na kumwambia, “Nenda, zirudishe mjini.”

4120:41 Mwa 33:3; Rut 2:10; 1Sam 24:8; 25:23; 2Sam 1:2Baada ya mvulana kwenda, Daudi akainuka kutoka upande wa kusini wa lile jiwe, naye akasujudu uso wake mpaka nchi mara tatu mbele ya Yonathani. Kisha kila mmoja akambusu mwenzake, wakalia pamoja. Lakini Daudi akalia zaidi.

4220:42 1Sam 1:17; Mdo 15:33; Mwa 40:14; 2Sam 1:26; Mit 18:24; Isa 48:1; Mwa 31:50; 1Sam 18:3; 2Sam 9; 1Yonathani akamwambia Daudi, “Nenda kwa amani, kwa kuwa tumeapiana kiapo cha urafiki kati yetu kwa jina la Bwana, tukisema, ‘Bwana ndiye shahidi kati yako na mimi, na kati ya wazao wako na wazao wangu milele.’ ” Kisha Daudi akaondoka, naye Yonathani akarudi mjini.

New International Version

1 Samuel 20:1-42

David and Jonathan

1Then David fled from Naioth at Ramah and went to Jonathan and asked, “What have I done? What is my crime? How have I wronged your father, that he is trying to kill me?”

2“Never!” Jonathan replied. “You are not going to die! Look, my father doesn’t do anything, great or small, without letting me know. Why would he hide this from me? It isn’t so!”

3But David took an oath and said, “Your father knows very well that I have found favor in your eyes, and he has said to himself, ‘Jonathan must not know this or he will be grieved.’ Yet as surely as the Lord lives and as you live, there is only a step between me and death.”

4Jonathan said to David, “Whatever you want me to do, I’ll do for you.”

5So David said, “Look, tomorrow is the New Moon feast, and I am supposed to dine with the king; but let me go and hide in the field until the evening of the day after tomorrow. 6If your father misses me at all, tell him, ‘David earnestly asked my permission to hurry to Bethlehem, his hometown, because an annual sacrifice is being made there for his whole clan.’ 7If he says, ‘Very well,’ then your servant is safe. But if he loses his temper, you can be sure that he is determined to harm me. 8As for you, show kindness to your servant, for you have brought him into a covenant with you before the Lord. If I am guilty, then kill me yourself! Why hand me over to your father?”

9“Never!” Jonathan said. “If I had the least inkling that my father was determined to harm you, wouldn’t I tell you?”

10David asked, “Who will tell me if your father answers you harshly?”

11“Come,” Jonathan said, “let’s go out into the field.” So they went there together.

12Then Jonathan said to David, “I swear by the Lord, the God of Israel, that I will surely sound out my father by this time the day after tomorrow! If he is favorably disposed toward you, will I not send you word and let you know? 13But if my father intends to harm you, may the Lord deal with Jonathan, be it ever so severely, if I do not let you know and send you away in peace. May the Lord be with you as he has been with my father. 14But show me unfailing kindness like the Lord’s kindness as long as I live, so that I may not be killed, 15and do not ever cut off your kindness from my family—not even when the Lord has cut off every one of David’s enemies from the face of the earth.”

16So Jonathan made a covenant with the house of David, saying, “May the Lord call David’s enemies to account.” 17And Jonathan had David reaffirm his oath out of love for him, because he loved him as he loved himself.

18Then Jonathan said to David, “Tomorrow is the New Moon feast. You will be missed, because your seat will be empty. 19The day after tomorrow, toward evening, go to the place where you hid when this trouble began, and wait by the stone Ezel. 20I will shoot three arrows to the side of it, as though I were shooting at a target. 21Then I will send a boy and say, ‘Go, find the arrows.’ If I say to him, ‘Look, the arrows are on this side of you; bring them here,’ then come, because, as surely as the Lord lives, you are safe; there is no danger. 22But if I say to the boy, ‘Look, the arrows are beyond you,’ then you must go, because the Lord has sent you away. 23And about the matter you and I discussed—remember, the Lord is witness between you and me forever.”

24So David hid in the field, and when the New Moon feast came, the king sat down to eat. 25He sat in his customary place by the wall, opposite Jonathan,20:25 Septuagint; Hebrew wall. Jonathan arose and Abner sat next to Saul, but David’s place was empty. 26Saul said nothing that day, for he thought, “Something must have happened to David to make him ceremonially unclean—surely he is unclean.” 27But the next day, the second day of the month, David’s place was empty again. Then Saul said to his son Jonathan, “Why hasn’t the son of Jesse come to the meal, either yesterday or today?”

28Jonathan answered, “David earnestly asked me for permission to go to Bethlehem. 29He said, ‘Let me go, because our family is observing a sacrifice in the town and my brother has ordered me to be there. If I have found favor in your eyes, let me get away to see my brothers.’ That is why he has not come to the king’s table.”

30Saul’s anger flared up at Jonathan and he said to him, “You son of a perverse and rebellious woman! Don’t I know that you have sided with the son of Jesse to your own shame and to the shame of the mother who bore you? 31As long as the son of Jesse lives on this earth, neither you nor your kingdom will be established. Now send someone to bring him to me, for he must die!”

32“Why should he be put to death? What has he done?” Jonathan asked his father. 33But Saul hurled his spear at him to kill him. Then Jonathan knew that his father intended to kill David.

34Jonathan got up from the table in fierce anger; on that second day of the feast he did not eat, because he was grieved at his father’s shameful treatment of David.

35In the morning Jonathan went out to the field for his meeting with David. He had a small boy with him, 36and he said to the boy, “Run and find the arrows I shoot.” As the boy ran, he shot an arrow beyond him. 37When the boy came to the place where Jonathan’s arrow had fallen, Jonathan called out after him, “Isn’t the arrow beyond you?” 38Then he shouted, “Hurry! Go quickly! Don’t stop!” The boy picked up the arrow and returned to his master. 39(The boy knew nothing about all this; only Jonathan and David knew.) 40Then Jonathan gave his weapons to the boy and said, “Go, carry them back to town.”

41After the boy had gone, David got up from the south side of the stone and bowed down before Jonathan three times, with his face to the ground. Then they kissed each other and wept together—but David wept the most.

42Jonathan said to David, “Go in peace, for we have sworn friendship with each other in the name of the Lord, saying, ‘The Lord is witness between you and me, and between your descendants and my descendants forever.’ ” Then David left, and Jonathan went back to the town.20:42 In Hebrew texts this sentence (20:42b) is numbered 21:1.