1 Samweli 19 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

1 Samweli 19:1-24

Sauli Ajaribu Kumuua Daudi

119:1 1Sam 18:1-9; Mit 27:4Sauli akamwambia mwanawe Yonathani na watumishi wake wote wamuue Daudi. Lakini Yonathani mwana wa Sauli alimpenda sana Daudi. 219:2 Mdo 23:16Yonathani akamwonya Daudi, akisema, “Baba yangu Sauli anatafuta nafasi ya kukuua. Ujilinde kesho asubuhi, nenda mahali pa siri na ukae huko. 319:3 1Sam 20:12Nitatoka na kukaa na baba yangu shambani mahali uliko. Nitazungumza naye juu yako, nami nitakueleza nitakachogundua.”

419:4 1Sam 20:32; 22:14; Mit 31:8-9; Yer 18:20; 1Sam 25:21; Mit 17:13; Mwa 42:22; 1Nya 6:22; Za 35:12; 109:5; Yer 18:20; 1Kor 8:12; 1Yn 3:15Yonathani akanena mema juu ya Daudi kwa Sauli baba yake na kumwambia, “Mfalme asitende mabaya kwa mtumishi wake Daudi; hajakukosea, aliyoyafanya yamekuwa ya faida sana kwako. 519:5 Amu 9:17; 1Sam 11:13; Mwa 31:36; Kum 19:10-13; 1Sam 17:49-50; 1Nya 11:14; Mt 27:4; Za 119:109; Mt 27:14Alihatarisha maisha yake alipomuua yule Mfilisti. Bwana akajipatia ushindi mkubwa kwa ajili ya Israeli wote, nawe uliuona na ukafurahi. Kwa nini basi utende mabaya kwa mtu asiye na hatia kama Daudi kwa kumuua bila sababu?”

6Sauli akamsikiliza Yonathani na kuapa hivi: “Hakika kama Bwana aishivyo, Daudi hatauawa.”

719:7 1Sam 16:21; 18:10Basi Yonathani akamwita Daudi na kumweleza mazungumzo yote. Akamleta kwa Sauli, naye Daudi akawa pamoja na Sauli kama kwanza.

8Vita vilitokea tena, naye Daudi akatoka na kupigana na Wafilisti. Akawapiga kwa nguvu nyingi hata wakakimbia mbele yake.

919:9 Amu 9:23; 1Sam 10:5; 16:14Lakini roho mbaya iliyoachiwa nafasi na Bwana ikaja juu ya Sauli alipokuwa ameketi katika nyumba yake akiwa na mkuki mkononi mwake. Daudi alipokuwa anampigia kinubi, 1019:10 1Sam 18:11; Ay 5:2; Za 5:6; Mit 1:16; 29:10Sauli akajaribu kumchomea Daudi ukutani kwa huo mkuki wake, lakini Daudi akauhepa huo mkuki wa Sauli ukakita ukutani. Usiku ule ule Daudi akakimbia na kuokoka.

1119:11 Za 59; Amu 16:2Sauli akatuma watu nyumbani mwa Daudi wailinde hiyo nyumba na kumuua asubuhi. Lakini Mikali, mkewe Daudi, akamwonya akisema, “Kama hukukimbia kuokoa maisha yako usiku huu, kesho yake utauawa.” 1219:12 Yos 2:15; Mdo 9:25; 2Kor 11:33Basi Mikali akamteremsha Daudi kupitia dirishani, naye akakimbia na kuokoka. 1319:13 Mwa 31:19; Amu 17:5Kisha Mikali akachukua kinyago, akakilaza kitandani, akakifunika kwa vazi na kukiwekea singa za mbuzi kichwani.

1419:14 Kum 1:19; Yos 2:4Sauli alipotuma watu kumkamata Daudi, Mikali akasema, “Yeye ni mgonjwa.”

15Kisha Sauli akatuma watu tena kumwona Daudi naye akawaambia, “Mleteni kwangu juu ya kitanda chake ili nipate kumuua.” 16Lakini wale watu walipoingia, kumbe ni kinyago tu kilichokuwa kitandani na kwenye kichwa kulikuwepo na singa za mbuzi.

1719:17 2Sam 2:22Sauli akamwambia Mikali, “Kwa nini umenidanganya mimi hivi na kumwacha adui yangu aende zake ili apate kuokoka?”

Mikali akamwambia, “Yeye aliniambia, ‘Niache niende zangu. Kwa nini nikuue?’ ”

1819:18 1Sam 7:17; Mit 17:17; Mal 2:7Daudi alipokuwa amekimbia na kuokoka, alimwendea Samweli huko Rama na kumwambia yale yote Sauli alimfanyia. Ndipo Daudi na Samweli wakaenda Nayothi kukaa huko. 19Habari zikamfikia Sauli kusema: “Daudi yuko Nayothi huko Rama.” 2019:20 Hes 11:25-29; 1Sam 10:5; Yoe 2:28; Yn 7:32, 45; 1Kor 14:3, 24, 25Basi Sauli akatuma watu kumkamata Daudi, lakini walipoona kundi la manabii wakitoa unabii, wakiwa pamoja na Samweli akiwa amesimama hapo kama kiongozi wao, Roho wa Mungu akaja juu ya watu wa Sauli, nao pia wakatoa unabii. 21Sauli akaelezwa juu ya hilo, naye akapeleka watu wengine zaidi, nao wakatoa unabii pia. Sauli akatuma watu mara ya tatu, nao pia wakatoa unabii. 22Mwishowe, yeye mwenyewe akaondoka kwenda Rama na kwenda hadi kwenye kile kisima kikubwa kilichoko huko Seku. Naye akauliza, “Wako wapi Samweli na Daudi?”

Wakasema, “Wako Nayothi huko Rama.”

2319:23 1Sam 10:13; Mwa 31:24; Hes 23:5; 24:2; Mit 21:1; Dan 4:35; Mt 7:22; Yn 11:51; 1Kor 13:2Hivyo Sauli akaenda Nayothi huko Rama. Lakini Roho wa Mungu akaja juu yake hata yeye, akawa anatembea huku anatoa unabii hadi akafika Nayothi. 2419:24 2Sam 6:20; Isa 20:2; 1Sam 15:35; 10:11; Mik 1:8; Mdo 9:21Akavua majoho yake na pia akatoa unabii mbele ya Samweli. Akalala hali hiyo ule mchana kutwa na usiku kucha. Hii ndiyo sababu watu husema, “Je, Sauli pia yumo miongoni mwa manabii?”

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

撒母耳记上 19:1-24

扫罗试图杀大卫

1扫罗吩咐他儿子约拿单和众臣仆去杀掉大卫。但约拿单非常喜爱大卫2便告诉他,说:“我父亲要杀你,明天早上你要小心,找个僻静的地方躲起来。 3我会出去和父亲站在你藏身的田间,跟他提你的事,然后把消息告诉你。” 4约拿单就在父亲面前替大卫说好话,他说:“王不要伤害大卫,他从来没有对不起王,他所做的使王大受益处。 5他冒着生命危险去杀非利士人,耶和华使以色列人大获全胜,当时你看见了,非常欢喜,现在为什么要犯罪,枉杀无辜的大卫呢?” 6扫罗听了约拿单的话,就凭永活的耶和华起誓说:“我不杀大卫。” 7约拿单叫来大卫,把经过告诉他,带他去见扫罗大卫又像以前一样伺候扫罗

8后来,战事再度爆发,大卫领兵与非利士人交战,大败敌人,杀得他们四散溃逃。 9一天,扫罗手里拿着矛正坐在家中,从耶和华那里来的邪灵降临在扫罗身上。大卫正在弹琴, 10扫罗想用矛把大卫刺透,钉在墙上,大卫躲开了,矛插在了墙上。大卫当晚逃走了。

11扫罗派人去监视大卫的家,要在早上杀死他。大卫的妻子米甲警告他说:“你如果今晚不逃命,明早必死无疑。” 12于是,她从窗口把大卫缒下去,让他逃走了。 13然后她把家中的神像放在床上,头枕在山羊毛的枕头上,盖上衣服。 14扫罗派人来捉拿大卫的时候,米甲说他病了。 15扫罗又派人去见大卫,并吩咐说:“把他连床一起抬来,我好杀他。” 16众人进去发现躺在床上的是一个神像,头枕在山羊毛的枕头上。 17扫罗米甲:“你为什么欺骗我,让我的敌人逃走?”米甲答道:“他说如果我不让他逃走,就杀了我。”

18大卫逃到住在拉玛撒母耳那里,把扫罗的所作所为告诉他。后来,他和撒母耳拿约住了下来。 19扫罗听说大卫拉玛拿约20就派人去捉拿他。扫罗的人看到一群先知在说预言,撒母耳在当中带领他们。上帝的灵也临到扫罗的人,他们也说起预言来。 21扫罗听说后又派人去,派去的人也说起预言来。扫罗第三次派人去,派去的人同样说起预言来。 22最后扫罗亲自前往拉玛,走到西沽的大井,问撒母耳大卫在哪里,有人说在拉玛拿约23扫罗便去拉玛拿约。上帝的灵临到扫罗,他就一边走一边说起预言来,一直到拉玛拿约24他脱下自己的衣服,在撒母耳面前说起预言来。他赤身躺了一天一夜。因此有句俗语说:“扫罗也在先知当中吗?”