1 Nyakati 21 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

1 Nyakati 21:1-30

Daudi Ahesabu Wapiganaji

(2 Samweli 24:1-25)

121:1 2Nya 18:21; 1Fal 22:20-22; Za 109:6; 2Nya 14:8; Ufu 12:9; 2Nya 25:5; Mt 4:2; Yn 13:2; Mdo 5:3Shetani akainuka dhidi ya Israeli na kumshawishi Daudi ahesabu watu wa Israeli. 221:2 1Nya 27:23-24Kwa hiyo Daudi akamwambia Yoabu na majemadari wa jeshi, “Nendeni mkawahesabu Waisraeli kuanzia Beer-Sheba mpaka Dani. Kisha nileteeni taarifa ili kwamba niweze kufahamu wako wangapi.”

3Yoabu akajibu, “Bwana na aongeze jeshi lake mara mia na zaidi. Mfalme bwana wangu, kwani hawa wote si raiya wa bwana wangu? Kwa nini bwana wangu unataka kufanya hivi? Kwa nini kuleta hatia juu ya Israeli?”

421:4 Mit 29:25; Mdo 5:29; 4:19; Mhu 8:4Hata hivyo, neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu; kwa hiyo Yoabu akaondoka na kuzunguka Israeli yote kisha akarudi Yerusalemu. 5Yoabu akampa Daudi jumla ya idadi ya watu wanaoweza kupigana. Katika Israeli kulikuwa na watu 1,100,000 ambao wangeweza kutumia upanga na katika Yuda watu 470,000.

621:6 Hes 1:47-49; 1Nya 27:24Lakini Yoabu hakuwahesabu Walawi na Wabenyamini, kwa sababu alichukizwa sana na amri ya mfalme. 7Amri hii ilikuwa mbaya machoni pa Mungu pia; hivyo akaiadhibu Israeli.

821:8 2Sam 24:10; Ay 42:6; Hos 14:2; Za 25:11; 51:1-3; Mit 28:13-14; 2Kor 7:10Kisha Daudi akamwambia Mungu, “Nimetenda dhambi kubwa kwa kufanya jambo hili. Sasa, ninakusihi, ondoa hatia ya mtumishi wako. Nimefanya jambo la kipumbavu sana.”

921:9 1Sam 22:5; 9:9Bwana akamwambia Gadi, mwonaji wa Daudi, 10“Nenda ukamwambie Daudi, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Ninakupa wewe uchaguzi wa mambo matatu. Nichagulie mojawapo nitakalotenda dhidi yako.’ ”

11Kwa hiyo Gadi akamwendea Daudi akamwambia, “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Chagua: 1221:12 Kum 32:24; Eze 30:25; Mwa 19:13; 2Sam 24:13miaka mitatu ya njaa, au miezi mitatu ya kushindwa na adui zako, ukipatwa na upanga wao, au siku tatu za upanga wa Bwana, yaani, siku tatu za tauni katika nchi na malaika wa Bwana akiangamiza kila mahali katika Israeli.’ Sasa basi, amua jinsi nitakavyomjibu yeye aliyenituma.”

1321:13 Neh 9:17; Za 6:4; 130:4-7; Mao 3:22; Za 100:5; 145:9; Yoe 2:13Daudi akamwambia Gadi, “Ninayo mahangaiko makubwa. Mimi na nianguke mikononi mwa Bwana kwa maana rehema zake ni kuu mno, lakini usiniache niangukie mikononi mwa wanadamu.”

1421:14 1Nya 27:24Basi Bwana akatuma tauni katika Israeli, watu 70,000 wa Israeli wakafa. 1521:15 Mwa 32:1; 2Sam 24:16; Mwa 6:6; Kut 32:14; Mwa 19:13; Yer 26:18; Mt 23:37-38; Amu 2:18Mungu akapeleka malaika kuangamiza Yerusalemu. Lakini malaika alipokuwa akifanya hivyo, Bwana akaona na akahuzunika kwa sababu ya maafa, akamwambia yule malaika aliyekuwa anaangamiza watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Bwana alikuwa amesimama katika sakafu ya kupuria nafaka ya Arauna21:15 Pia anaitwa Ornani kwa Kiebrania. Myebusi.

1621:16 Hes 14:5; Yos 7:6; 2Nya 3:1Daudi akayainua macho yake akamwona huyo malaika wa Bwana akiwa amesimama katikati ya mbingu na dunia, naye ameunyoosha upanga wake juu ya Yerusalemu tayari kuangamiza. Kisha Daudi na wazee, waliokuwa wamevaa nguo za gunia, wakaanguka kifudifudi.

1721:17 2Sam 7:8; Za 74:1; Yon 1:12Daudi akamwambia Mungu, “Je, si mimi ndiye niliyeamuru watu wahesabiwe? Mimi ndiye niliyetenda dhambi na kukosa. Hawa ni kondoo tu. Wamefanya nini? Ee Bwana, Mungu wangu, mkono wako na uwe juu yangu mimi na jamaa yangu, lakini usiache tauni hii iendelee juu ya watu wako.”

18Kisha malaika wa Bwana akamwamuru Gadi amwambie Daudi apande na kumjengea Bwana madhabahu kwenye sakafu ya kupuria nafaka ya Arauna Myebusi. 19Kwa hiyo Daudi akakwea, akalitii lile neno ambalo Gadi alikuwa amelisema katika jina la Bwana.

2021:20 Amu 6:11Arauna alipokuwa akipura ngano, akageuka akamwona yule malaika. Wanawe wanne waliokuwa pamoja naye wakajificha, yeye akaendelea kupura ngano. 21Kisha Daudi akakaribia, Arauna alipotazama na kumwona, akaondoka kwenye uwanja wa kupuria nafaka akamsujudia Daudi akiuinamisha uso wake ardhini.

2221:22 Hes 16:48; 25:8Daudi akamwambia, “Nipatie huu uwanja wako wa kupuria nafaka ili niweze kujenga madhabahu ya Bwana tauni ipate kukomeshwa katika watu. Niuzie kwa bei yake kamili.”

23Arauna akamwambia Daudi, “Uchukue huo uwanja. Mfalme bwana wangu na afanye lolote analopenda. Tazama, nitatoa maksai kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, vifaa vya kupuria kuwa kuni, pamoja na ngano kwa ajili ya dhabihu ya nafaka. Natoa hivi vyote.”

24Lakini Mfalme Daudi akamjibu Arauna, “La hasha! Lakini ninasisitiza kwamba nitalipa bei yake kamili. Sitachukua kilicho chako kwa ajili ya Bwana au kutoa sadaka ya kuteketezwa ambayo hainigharimu chochote.”

2521:25 2Sam 24:24Basi Daudi akamlipa Arauna shekeli za dhahabu 60021:25 Shekeli 600 za dhahabu ni sawa na kilo 7. kwa ajili ya ule uwanja. 2621:26 Kut 19:18; 2Nya 7:1Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu mahali hapo, na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Akamwita Bwana naye Bwana akajibu maombi yake kwa moto toka mbinguni juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa.

27Kisha Bwana akanena na yule malaika, naye akarudisha upanga wake katika ala yake. 28Wakati huo, Daudi alipoona kwamba Bwana amemjibu kule kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Arauna Myebusi, akatoa dhabihu huko. 2921:29 Yos 9:3; 1Fal 3:4; 1Nya 16:39Maskani ya Bwana ambayo Mose aliitengeneza kule jangwani, pamoja na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa wakati huo vilikuwa viko mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni. 3021:30 1Nya 13:12; Ay 13:21; 2Sam 6:9; Ay 21:6; Za 119:120Lakini Daudi hakuthubutu kuisogelea ili kumuuliza Mungu, kwa sababu aliuogopa upanga wa yule malaika wa Bwana.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

歷代志上 21:1-30

大衛統計人口

1撒旦起來攻擊以色列,挑動大衛統計以色列人的數目。 2大衛約押和其他軍中的首領說:「你們要去,從別示巴一直到,統計以色列的人口,然後回來稟告我,我好知道他們的數目。」 3約押說:「願耶和華使祂子民的人數比現在增加百倍。但我主我王啊,他們不都是你的僕人嗎?我主為什麼要這樣做?為什麼使以色列人陷於罪中呢?」 4但王不聽約押的規勸。約押只好出去,走遍以色列,然後回到耶路撒冷5將人數奏告大衛:全以色列有一百一十萬刀兵,猶大有四十七萬。 6約押沒有把利未人和便雅憫人算在其中,因為他厭惡王的這個命令。 7上帝也不喜悅這事,便降災給以色列人。 8大衛對上帝說:「我做這事犯了大罪。求你赦免僕人的罪,我做了極其愚昧的事。」 9耶和華對大衛的先見迦得說: 10「你去告訴大衛,我有三樣災禍,他可以選擇讓我降哪一樣給他。」

11迦得就來見大衛,對他說:「耶和華說,『你可以任選一樣: 12或三年的饑荒,或被敵人的刀擊敗並追殺三個月,或國中被耶和華的刀懲罰,就是三天的瘟疫,讓耶和華的天使在以色列全境施行毀滅。請你考慮好後告訴我,我好回覆那差我來的。』」 13大衛說:「我實在為難!不過我寧願落在耶和華的手中,也不願落在人的手中,因為耶和華有極大的憐憫。」

14於是,耶和華在以色列降下瘟疫,有七萬人死亡。 15上帝差遣天使去毀滅耶路撒冷。天使正要毀滅的時候,耶和華見了就心生憐憫,對施行毀滅的天使說:「夠了,住手吧!」當時,耶和華的天使正站在耶布斯阿珥楠的麥場上。 16大衛舉目看見耶和華的天使站在天地之間,手握著已出鞘的刀,指向耶路撒冷大衛和眾長老都身披麻衣,臉伏於地。 17大衛對上帝說:「吩咐統計人民數目的不是我嗎?是我犯了罪,做了惡事,這些百姓有什麼過錯呢?我的上帝耶和華啊,願你的手懲罰我和我的家族,不要把瘟疫降在你的子民身上。」

18耶和華的天使吩咐迦得去告訴大衛,他要在耶布斯阿珥楠的麥場上為耶和華建一座壇。 19大衛迦得奉耶和華之名所說的話去了麥場。 20那時,阿珥楠正在打麥子,他轉身看見了天使,跟他在一起的四個兒子都躲了起來。 21阿珥楠看見大衛來了,就從麥場出來,俯伏在地,向大衛下拜。 22大衛對他說:「請你將這塊麥場賣給我,我要在這裡為耶和華築一座壇,使民中的瘟疫止息。你全價賣給我吧。」 23阿珥楠說:「我主我王只管用我的麥場!我願獻出牛作燔祭,打麥的器具作柴,麥子作素祭,我願獻出這一切。」

24大衛王對他說:「不可,我一定要付你全價,我不要拿你的東西獻給耶和華,也不要把白白得來的獻作燔祭。」 25於是,大衛就用一百四十兩金子買了阿珥楠的麥場。 26大衛在那裡為耶和華建了一座壇,獻上燔祭和平安祭,並求告耶和華。耶和華垂聽了他的禱告,從天上降火在祭壇上, 27又命令天使收刀入鞘。

28大衛見耶和華在耶布斯阿珥楠的麥場上應允了他的禱告,就在那裡獻祭。 29那時候,摩西在曠野為耶和華所造的聖幕和燔祭壇都在基遍的邱壇。 30大衛因為懼怕耶和華天使的刀,不敢去那裡求問上帝。