1(المُحِبُّ): قَدْ جِئْتُ إِلَى جَنَّتِي يَا أُخْتِي، يَا عَرُوسِي، وَقَطَفْتُ مُرِّي مَعَ أَطْيَابِي، وَأَكَلْتُ شَهْدِي مَعَ عَسَلِي، وَشَرِبْتُ خَمْرِي مَعَ لَبَنِي.
(بَنَاتُ أُورُشَلِيمَ): كُلُوا أَيُّهَا الْخُلّانُ. اشْرَبُوا حَتَّى الانْتِشَاءِ أَيُّهَا المُحِبُّونَ.
2(الْمَحْبُوبَةُ): قَدْ نِمْتُ وَلَكِنَّ قَلْبِي كَانَ مُسْتَيْقِظاً. آهِ، اسْمَعُوا! هَا صَوْتُ حَبِيبِي قَارِعاً قَائِلاً: افْتَحِي لِي يَا أُخْتِي، يَا حَبِيبَتِي، يَا حَمَامَتِي، يَا كَامِلَتِي! فَإِنَّ رَأْسِي قَدِ ابْتَلَّ مِنَ النَّدَى وَشَعْرِي مِنْ طَلِّ اللَّيْلِ.
3فَقُلْتُ: قَدْ خَلَعْتُ ثَوْبِي فَكَيْفَ أَرْتَدِيهِ ثَانِيَةً؟ غَسَلْتُ قَدَمَيَّ فَكَيْفَ أُوَسِّخُهُمَا؟ 4مَدَّ حَبِيبِي يَدَهُ مِنْ كُوَّةِ الْبَابِ، فَتَحَرَّكَتْ لَهُ مَشَاعِرِي، 5فَنَهَضْتُ لأَفْتَحَ لَهُ بِيَدَيْنِ تَقْطُرَانِ مُرّاً، وَأَصَابِعَ تَفِيضُ عِطْراً عَلَى مِزْلاجِ الْبَابِ. 6فَتَحْتُ لِحَبِيبِي، لَكِنَّ حَبِيبِي كَانَ قَدِ انْصَرَفَ وَعَبَرَ فَفَارَقَتْنِي نَفْسِي حِينَ ابْتَعَدَ. بَحَثْتُ عَنْهُ فَلَمْ أَجِدْهُ، دَعَوْتُهُ فَلَمْ يُجِبْ. 7وَجَدَنِي الْحُرَّاسُ الْمُتَجَوِّلُونَ فِي الْمَدِينَةِ، فَانْهَالُوا عَلَيَّ ضَرْباً فَجَرَحُونِي. نَزَعَ حُرَّاسُ الأَسْوَارِ رِدَائِي عَنِّي. 8أَسْتَحْلِفُكُنَّ يَا بَنَاتِ أُورُشَلِيمَ إِنْ وَجَدْتُنَّ حَبِيبِي أَنْ تُبَلِّغْنَهُ أَنِّي مَرِيضَةٌ حُبّاً.
9(بَنَاتُ أُورُشَلِيمَ): بِمَ يَفُوقُ حَبِيبُكِ الْمُحِبِّينَ أَيَّتُهَا الْجَمِيلَةُ بَيْنَ النِّسَاءِ؟ بِمَ يَفُوقُ حَبِيبُكِ الْمُحِبِّينَ حَتَّى تَسْتَحْلِفِينَا هَكَذَا؟
10(الْمَحْبُوبَةُ): حَبِيبِي مُتَأَلِّقٌ وَأَحْمَرُ، مُتَمَيِّزٌ بَيْنَ الآلَافِ. 11رَأْسُهُ ذَهَبٌ خَالِصٌ وَشَعْرُهُ مُتَمَوِّجٌ حَالِكُ السَّوَادِ كَلَوْنِ الْغُرَابِ. 12عَيْنَاهُ حَمَامَتَانِ عِنْدَ مَجَارِي الْمِيَاهِ، مَغْسُولَتَانِ مُسْتَقِرَّتَانِ فِي مَوْضِعِهِمَا. 13خَدَّاهُ كَخَمِيلَةِ طِيبٍ تَفُوحَانِ عِطْراً، وَشَفَتَاهُ كَالسَّوْسَنِ تَقْطُرَانِ مُرّاً شَذِيّاً. 14يَدَاهُ حَلَقَتَانِ مِنْ ذَهَبٍ مُدَوَّرَتَانِ وَمُرَصَّعَتَانِ بِالزَّبَرْجَدِ، وَجِسْمُهُ عَاجٌ مَصْقُولٌ مُغَشّىً بِالْيَاقُوتِ الأَزْرَقِ. 15سَاقَاهُ عَمُودَا رُخَامٍ قَائِمَتَانِ عَلَى قَاعِدَتَيْنِ مِنْ ذَهَبٍ نَقِيٍّ، طَلْعَتُهُ كَلُبْنَانَ، كَأَبْهَى أَشْجَارِ الأَرْزِ. 16فَمُهُ عَذْبٌ، وَكُلُّهُ مُشْتَهَيَاتٌ. هَذَا هُوَ حَبِيبِي وَهَذَا هُوَ خَلِيلِي يَا بَنَاتِ أُورُشَلِيمَ!
Mpenzi
15:1 Yoe 3:18; Wim 4:12; 4:16; Isa 55:1Nimekuja kwenye bustani yangu, dada yangu,
bibi arusi wangu;
nimekusanya manemane yangu pamoja
na kikolezo changu.
Nimekula sega langu la asali na asali yangu;
nimekunywa divai yangu na maziwa yangu.
Marafiki
Kuleni, enyi marafiki, mnywe;
kunyweni ya kutosha, ee wapenzi.
Shairi La Nne
Mpendwa
25:2 Efe 5:275:2 Mit 8:4; Wim 6:9; 4:7; 1:15Nililala lakini moyo wangu ulikuwa macho.
Sikiliza! Mpenzi wangu anabisha:
“Nifungulie, dada yangu, mpenzi wangu,
hua wangu, asiye na hitilafu.
Kichwa changu kimeloa umande,
na nywele zangu manyunyu ya usiku.”
3Nimevua joho langu:
je, ni lazima nivae tena?
Nimenawa miguu yangu:
je, ni lazima niichafue tena?
4Mpenzi wangu aliweka mkono wake kwenye tundu la komeo;
moyo wangu ulianza kugonga kwa ajili yake.
5Niliinuka kumfungulia mpenzi wangu,
mikono yangu ikidondosha manemane,
vidole vyangu vikitiririka manemane,
penye vipini vya komeo.
65:6 Wim 6:1-2; 3:15:6 Hos 5:15; Mao 3:8Nilimfungulia mpenzi wangu,
lakini mpenzi wangu alishaondoka;
alikuwa amekwenda zake.
Moyo wangu ulishuka kwa kuondoka kwake.
Nilimtafuta lakini sikumpata.
Nilimwita lakini hakunijibu.
75:7 Wim 3:3Walinzi walinikuta
walipokuwa wakifanya zamu za ulinzi mjini.
Walinipiga, wakanijeruhi,
wakaninyangʼanya joho langu,
hao walinzi wa kuta!
85:8 Wim 2:7; 1:14; 2:5Enyi binti za Yerusalemu, ninawaagiza:
kama mkimpata mpenzi wangu,
mtamwambia nini?
Mwambieni ninazimia kwa mapenzi.
Marafiki
9Je, mpendwa wako ni bora kuliko wengine namna gani,
wewe uliye mzuri kupita wanawake wote?
Je, mpendwa wako ni mzuri kuliko wengine, namna gani,
hata unatuagiza hivyo?
Mpendwa
105:10 Za 45:2Mpenzi wangu anangʼaa, tena ni mwekundu,
wa kuvutia miongoni mwa wanaume kumi elfu.
11Kichwa chake ni dhahabu safi kuliko zote,
nywele zake ni za mawimbi
na ni nyeusi kama kunguru.
125:12 Mwa 49:12; Wim 1:15Macho yake ni kama ya hua
kandokando ya vijito vya maji,
aliyeogeshwa kwenye maziwa,
yaliyopangwa kama vito vya thamani.
13Mashavu yake ni kama matuta ya vikolezo
yakitoa manukato.
Midomo yake ni kama yungiyungi
inayodondosha manemane.
145:14 Ay 28:6Mikono yake ni fimbo za dhahabu
iliyopambwa kwa krisolitho.
Mwili wake ni kama pembe ya ndovu iliyongʼarishwa
iliyopambwa na yakuti samawi.
155:15 1Fal 4:33; Wim 7:4Miguu yake ni nguzo za marmar
zilizosimikwa katika vitako vya dhahabu safi.
Sura yake ni kama Lebanoni,
bora kama miti yake ya mierezi.
165:16 Wim 4:3; 7:9; Yer 31:3; Rum 8:35Kinywa chake chenyewe ni utamu,
kwa ujumla yeye ni wa kupendeza.
Huyu ndiye mpenzi wangu, huyu ndiye rafiki yangu,
ee binti za Yerusalemu.