مزمور 19 – NAV & NEN

New Arabic Version

مزمور 19:1-14

الْمَزْمُورُ التَّاسِعُ عَشَرَ

لِقَائِدِ الْمُنْشِدِينَ. مَزْمُورٌ لِدَاوُدَ

1السَّمَاوَاتُ تُحَدِّثُ بِمَجْدِ اللهِ، وَالْفَلَكُ يُخْبِرُ بِعَمَلِ يَدَيْهِ 2بِذَلِكَ تَتَحَادَثُ الأَيَّامُ أَبْلَغَ حَدِيثٍ، وَتَتَخَاطَبُ بِهِ اللَّيَالِي. 3لَا يَصْدُرُ عَنْهَا كَلامٌ، لَكِنَّ صَوْتَهَا يُسمَعُ وَاضِحاً. 4انْطَلَقَ صَوْتُهُمْ إِلَى الأَرْضِ كُلِّهَا وَكَلامُهُمْ إِلَى أَقَاصِي الْعَالَمِ. جَعَلَ لِلشَّمْسِ مَسْكَناً فِيهَا، 5وَهِيَ مِثْلُ الْعَرِيسِ الْخَارِجِ مِنْ مُخْدَعِهِ، كَالْعَدَّاءِ الْمُبْتَهِجِ لِلسِّبَاقِ فِي الطَّرِيقِ. 6تَنْطَلِقُ مِنْ أَقْصَى السَّمَاوَاتِ، وَتَدُورُ إِلَى أَقَاصِيهَا، وَلَا شَيْءَ يَحْتَجِبُ مِنْ حَرِّهَا.

7شَرِيعَةُ الرَّبِّ كَامِلَةٌ تُنْعِشُ النَّفْسَ. شَهَادَةُ الرَّبِّ صَادِقَةٌ تَجْعَلُ الْجَاهِلَ حَكِيماً. 8وَصَايَا الرَّبِّ مُسْتَقِيمَةٌ تُفَرِّحُ الْقَلْبَ. أَمْرُ الرَّبِّ نَقِيٌّ يُنِيرُ الْعَيْنَيْنِ. 9مَخَافَةُ الرَّبِّ طَاهِرَةٌ ثَابِتَةٌ إِلَى الأَبَدِ، وَأَحْكَامُ الرَّبِّ حَقٌّ وَعَادِلَةٌ كُلُّهَا. 10إِنَّهَا أَشْهَى مِنَ الذَّهَبِ النَّقِيِّ، وَهِيَ أَحْلَى مِنَ الْعَسَلِ بَلِ الْقَطْرِ السَّائِلِ مِنْ أَقْرَاصِ الشَّهْدِ. 11عَبْدُكَ يَهْتَدِي بِها، وَفِي صَوْنِهَا ثَوَابٌ عَظِيمٌ. 12مَنْ يَتَنَبَّهُ إِلَى سَهَوَاتِهِ؟ مِنَ الْخَطَايَا الْخَفِيَّةِ خَلِّصْنِي، 13وَمِنَ الْكَبَائِرِ أَيْضاً احْفَظْ عَبْدَكَ، وَلَا تَدَعْهَا تَتَسَلَّطُ عَلَيَّ. عِنْدَئِذٍ أَكُونُ كَامِلاً وَأَتَبَرَّأُ مِنْ ذَنْبٍ عَظِيمٍ. 14لِتَكُنْ أَقْوَالُ فَمِي وَخَوَاطِرُ قَلْبِي مَقْبُولَةً لَدَيْكَ يَا رَبُّ، يَا صَخْرَتِي وَفَادِيَّ.

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 19:1-14

Zaburi 19

Utukufu Wa Mungu Katika Uumbaji

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

119:1 Isa 6:3; 40:22; Za 4:2; 97:6; 89:5; 50:6; 8:1, 6; 148:3; 103:22; Rum 1:19; Mwa 1:8Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu,

anga zahubiri kazi ya mikono yake.

219:2 Za 74:16Siku baada ya siku zinatoa habari,

usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.

3Hakuna msemo wala lugha,

ambapo sauti zao hazisikiki.

419:4 Rum 10:18; Za 104:2; Ay 36:29; Amu 5:31Sauti yao imeenea duniani pote,

nayo maneno yao yameenea

hadi miisho ya ulimwengu.

Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,

519:5 1Sam 17:4; Mhu 11:7; Yoe 2:16; Ay 36:29linafanana na bwana arusi

akitoka chumbani mwake,

kama shujaa afurahiavyo

kukamilisha kushindana kwake.

619:6 Kum 30:4; Za 11:3; Mhu 1:5Huchomoza upande mmoja wa mbingu,

na kufanya mzunguko wake

hadi upande mwingine.

Hakuna kilichojificha joto lake.

719:7 Yak 1:25; Kum 4:6; Za 1:2; 23:3; 93:5; 119:130, 138, 142, 144; 11:7Sheria ya Bwana ni kamilifu,

ikihuisha nafsi.

Shuhuda za Bwana ni za kuaminika,

zikimpa mjinga hekima.

819:8 Za 33:4; 38:10; 119:14, 128; Ezr 9:7; Neh 9:13; Rum 7:12Maagizo ya Bwana ni kamili,

nayo hufurahisha moyo.

Amri za Bwana huangaza,

zatia nuru machoni.

919:9 Mhu 12:13; Isa 33:6; Za 34:11; 111:10; 119:138; Mit 1:7Kumcha Bwana ni utakatifu,

nako kwadumu milele.

Amri za Bwana ni za hakika,

nazo zina haki.

1019:10 Ay 22:24; Eze 3:3; Mit 8:10; 1Sam 14:27; Za 119:72, 103Ni za thamani kuliko dhahabu,

kuliko dhahabu iliyo safi sana,

ni tamu kuliko asali,

kuliko asali kutoka kwenye sega.

1119:11 Mit 6:22Kwa hizo mtumishi wako anaonywa,

katika kuzishika kuna thawabu kubwa.

1219:12 Za 51:2; 90:8; Mhu 12:14Ni nani awezaye kutambua makosa yake?

Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.

1319:13 Hes 15:30; Mwa 6:9; Za 18:32; 119:133Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi,

nazo zisinitawale.

Ndipo nitakapokuwa sina lawama,

wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.

1419:14 Za 104:34; 18:31; Kut 6:6; Isa 44:6; Ay 19:25Maneno ya kinywa changu

na mawazo ya moyo wangu,

yapate kibali mbele zako, Ee Bwana,

Mwamba wangu na Mkombozi wangu.