התגלות 19 – HHH & NEN

Habrit Hakhadasha/Haderekh

התגלות 19:1-21

1לאחר מכן שמעתי קול אדיר שנשמע כקול המוני אנשים בשמים: ”הללויה! הודו לה׳! הישועה, הכבוד והעוז שייכים לאלוהינו, 2כי הוא שופט בצדק ובאמת. הוא העניש את הזונה הגדולה, אשר השחיתה את הארץ במעשי הזנות והניאוף שלה, ונקם את רצח עבדיו.“

3שוב ושוב קראו הקולות: ”הללויה! שריפתה תעלה עשן לעולם ועד!“

4עשרים־וארבעה הזקנים וארבע החיות נפלו על פניהם, השתחוו לאלוהים היושב על הכיסא וקראו: ”אמן! הללויה!“

5‏-6שוב שמעתי קול אשר נשמע כקול המון רב, כקול מים רבים, וקול רעמים חזקים. ”הללויה! כי אלוהינו, ה׳ צבאות, מולך! 7הבה נשמח, נגיל וניתן לו כבוד, כי הגיע מועד חתונת השה, וכלתו התכוננה לקראתו; 8ניתן לה ללבוש שמלה מאריג משובח, צח וטהור.“ (אריג משובח זה מסמל את מעשי הצדקה של בני־האלוהים).

9המלאך אמר אלי: ”כת‎וֹב: ברוכים המוזמנים אל חתונת השה.“ הוא הוסיף ואמר: ”אלה מילותיו של אלוהים עצמו!“

10נפלתי לרגליו כדי להשתחוות לו, אך הוא אמר אלי: ”קום, אל תשתחווה לי; אני עבד אלוהים כמוך וכאחיך המאמינים שנושאים את עדות ישוע. השתחווה לאלוהים! כי האמת שגילה ישוע היא שנתנה השראה לנביאים.“

11לאחר מכן ראיתי את השמים נפתחים וסוס לבן הופיע. שם רוכבו, ”נאמן ואמיתי“, והוא שופט ולוחם בצדק. 12עיניו כלהבת אש, על ראשו כתרים רבים, ועל מצחו כתוב שם שידוע לו בלבד. 13לבושו הוטבל בדם, ושמו נקרא ”דבר האלוהים“. 14צבאות השמים, לבושים מדים לבנים מאריג משובח וטהור, דהרו בעקבותיו על סוסיהם הלבנים.

15מפי הרוכב יצאה חרב חדה, שמיועדת להכות את הגויים שבהם ישלוט בשוט ברזל, וברגליו דרך את ענבי הזעם של ה׳ אלוהי צבאות. 16על בגדו ועל ירכו כתוב: ”מלך המלכים ואדון האדונים.“

17לאחר מכן ראיתי מלאך עומד לבדו באור השמש המסנוור. הוא קרא בקול אדיר אל כל העופות המעופפים במרכז השמים: ”בואו אל הסעודה הגדולה של אלוהים! 18בואו איכלו בשר מלכים, קציני־צבא, גנרלים, גיבורים; בשר סוסים ופרשים, בשר עבדים ובני־חורין, מקטן ועד גדול.“

19ראיתי את החיה, את מלכי הארץ ואת צבאותיהם נאספים יחד, כדי להילחם נגד הרוכב על הסוס ונגד צבאו. 20אולם החיה הרעה נתפסה, ויחד איתה נתפס נביא השקר (בדמות החיה השנייה), שחולל את הניסים והנפלאות בנוכחותה – ניסים שהתעו את נושאי אות החותם ואת המשתחווים לפסלה. החיה הרעה ונביא השקר הושלכו חיים לאגם האש שבוער בגופרית, 21וכל צבאם נהרג בחרב שיצאה מפי הרוכב על הסוס. ועופות השמים טרפו בתאווה את בשרם.

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 19:1-21

Shangwe Huko Mbinguni

119:1 Ufu 11:15; 7:10; 4:11Baada ya haya nikasikia sauti kama ya umati mkubwa mbinguni wakipiga kelele wakisema:

“Haleluya!

Wokovu na utukufu na uweza ni vya Mungu wetu,

219:2 Kum 32:43; Ufu 6:10kwa maana hukumu zake

ni za kweli na za haki.

Amemhukumu yule kahaba mkuu

aliyeuharibu ulimwengu kwa uzinzi wake.

Mungu amemlipiza kisasi

kwa ajili ya damu ya watumishi wake.”

319:3 Isa 34:10; Ufu 14:11Wakasema tena kwa nguvu:

“Haleluya!

Moshi wake huyo kahaba unapanda juu

milele na milele.”

419:4 Ufu 4:4-6; 5:14Wale wazee ishirini na wanne pamoja na wale viumbe wanne wenye uhai wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu, aliyekuwa ameketi kwenye kile kiti cha enzi. Wakasema kwa sauti kuu:

“Amen, Haleluya!”

519:5 Za 134:1; Ufu 11:18Kisha sauti ikatoka katika kile kiti cha enzi, ikisema:

“Msifuni Mungu wetu,

ninyi watumishi wake wote,

ninyi nyote mnaomcha,

wadogo kwa wakubwa!”

619:6 Ufu 11:15Kisha nikasikia sauti kama ya umati mkubwa, kama sauti ya maji mengi yaendayo kasi na kama ngurumo kubwa ya radi wakipiga kelele wakisema:

“Haleluya!

Kwa maana Bwana Mungu wetu Mwenyezi anatawala.

719:7 Mt 25:10; Efe 5:32; Ufu 21:2, 9Tufurahi, tushangilie

na kumpa utukufu!

Kwa maana arusi ya Mwana-Kondoo imewadia

na bibi arusi wake amejiweka tayari.

819:8 Ufu 15:4; 19:14; 15:6; Isa 61:10; Eze 44:17; Zek 3:4Akapewa kitani safi, nyeupe

inayongʼaa, ili avae.”

(Hiyo kitani safi inawakilisha matendo ya haki ya watakatifu.)

919:9 Ufu 1:19; Lk 14:15; Ufu 21:5; 22:6Ndipo malaika akaniambia, “Andika: ‘Wamebarikiwa wale walioalikwa kwenye karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo!’ ” Naye akaongeza kusema, “Haya ndiyo maneno ya kweli ya Mungu.”

1019:10 Ufu 22:8; Mdo 10:25, 26; Ufu 22:9; 12:17Ndipo nikaanguka kifudifudi miguuni pake ili kumwabudu, lakini yeye akaniambia, “Usifanye hivyo! Mimi pia ni mtumishi mwenzako pamoja na ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Mwabudu Mungu! Maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii.”

Aliyepanda Farasi Mweupe

1119:11 Ufu 6:2; 3:14; Kut 15:3Kisha nikaona mbingu imefunguka na hapo mbele yangu akiwepo farasi mweupe, ambaye yeye aliyempanda aliitwa Mwaminifu na Kweli. Yeye huhukumu kwa haki na kufanya vita. 1219:12 Ufu 1:14; 6:2; 2:17Macho yake ni kama miali ya moto na juu ya kichwa chake kuna taji nyingi. Ana jina lililoandikwa ambalo hakuna mtu yeyote anayelijua isipokuwa yeye mwenyewe. 1319:13 Isa 63:2, 3; Yn 1:1Amevaa joho lililochoviwa katika damu, na Jina lake ni “Neno la Mungu.” 1419:14 Ufu 19:8; 3:4; 17:14Majeshi ya mbinguni walikuwa wakimfuata, wakiwa wamepanda farasi weupe, hali wamevaa mavazi ya kitani safi, nyeupe na nzuri. 1519:15 Ufu 1:16; 12:5; 14:20; Isa 11:4; 2The 2:8; Za 2:9Kinywani mwake hutoka upanga mkali ambao kwa huo atayaangusha mataifa. “Atayatawala kwa fimbo yake ya utawala ya chuma.” Hulikanyaga shinikizo la mvinyo wa ghadhabu ya Mungu Mwenyezi. 1619:16 Ufu 17:14; 19:12; 1Tim 6:15Kwenye joho lake na paja lake pameandikwa jina hili:

Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana.

Mnyama Na Majeshi Yake Yashindwa

1719:17 Ufu 8:13; Eze 39:17Nami nikamwona malaika amesimama ndani kwenye jua, akaita ndege wote warukao angani kwa sauti kuu, “Njooni, kusanyikeni kwa ajili ya karamu kubwa ya Mungu, 1819:18 Eze 39:18-20ili mpate kula nyama ya wafalme na ya majemadari, ya mashujaa, ya farasi na ya wapanda farasi, nyama ya wanadamu, wote walio huru na watumwa, wadogo na wakubwa.”

1919:19 Ufu 16:14, 16Kisha nikamwona yule mnyama na wafalme wa dunia pamoja na majeshi yao wakiwa wamekusanyika pamoja ili kufanya vita dhidi ya yule aliyempanda farasi pamoja na jeshi lake. 2019:20 Ufu 16:13; 13:12; Dan 7:11; Ufu 21:8; 14:19Lakini yule mnyama akakamatwa pamoja na huyo nabii wa uongo ambaye alikuwa amefanya ishara kwa niaba ya huyo mnyama, ambaye kwa ishara hizi aliwadanganya wale waliopokea chapa ya huyo mnyama na kuiabudu sanamu yake. Hawa wawili wakatupwa wakiwa hai ndani ya ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti. 21Wale waliosalia waliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa yule aliyekuwa amempanda farasi nao ndege wote wakajishibisha kwa nyama yao.