הבשורה על-פי מרקוס 14 – HHH & NEN

Habrit Hakhadasha/Haderekh

הבשורה על-פי מרקוס 14:1-72

1יומיים לפני חג הפסח עדיין חיפשו ראשי הכוהנים וכמה ממנהיגי היהודים הזדמנות מתאימה לאסור את ישוע ולהוציאו להורג.

2”איננו יכולים לעצור אותו בפסח,“ אמרו לעצמם, ”מפני שהעם יעורר מהומות.“

3באותו זמן היה ישוע בבית־עניה, בביתו של שמעון המצורע. בשעת ארוחת הערב הופיעה אישה אחת עם פחית קטנה מלאה בשמן זך יקר מאוד. האישה הסירה את המכסה ויצקה את השמן על ראשו של ישוע.

4‏-5אחדים מן המסובים התמרמרו בינם לבין עצמם על ”הבזבוז“, כלשונם. ”מדוע את מבזבזת את השמן היקר הזה?“ התלוננו. ”יכולת למכור אותו ברווח, ואת הכסף לתת לעניים.“ 6”הניחו לה!“ נחלץ ישוע להגנתה.

”מדוע אתם מציקים לה? הלא היא עשתה מעשה טוב. 7העניים הנזקקים לעזרה נמצאים אתכם תמיד, ואתם יכולים לעזור להם בכל זמן שתרצו בכך, ואילו אני לא אשאר אתכם עוד זמן רב. 8היא עשתה מה שיכלה; היא משחה את גופי בשמן לפני קבורתי.

9”אני אומר לכם: בכל מקום שבו תוכרז הבשורה, תיזכר גם האישה הזאת, בזכות המעשה שעשתה.“

10לאחר מכן הלך יהודה איש־קריות, תלמידו של ישוע, אל ראשי הכוהנים כדי לתכנן את הסגרתו של ישוע.

11ראשי הכוהנים התלהבו ושמחו על כך שיהודה החליט להסגיר את ישוע, והבטיחו לתת לו כסף.

12ביום הראשון של חג הפסח, שבו הקריבו את זבח הפסח, שאלו התלמידים את ישוע היכן ברצונו לערוך את הסדר.

13ישוע שלח שניים מתלמידיו לירושלים, כדי לערוך את ההכנות הדרושות, ואמר: ”כשתלכו העירה יבוא לקראתכם אדם ובידו כד מים. לכו אחריו, 14היכנסו אל הבית שאליו ייכנס ואמרו לבעל הבית: ’רבנו שלח אותנו לראות את החדר שהכנת בשביל הסדר‘. 15הוא יוביל אתכם לחדר גדול שהכין למעננו בקומה השנייה, ושם תכינו את הסדר.“

16כשהגיעו השניים העירה הכול התרחש בדיוק כפי שאמר להם ישוע, והם הכינו את הסדר.

17ישוע ושאר התלמידים הגיעו לשם בערב. 18כשישבו לאכול בשולחן פתח ישוע ואמר: ”אמת אני אומר לכם, אחד מכם היושב עכשיו בינינו ואוכל איתנו יבגוד בי ויסגיר אותי.“

19התלמידים נמלאו צער רב, ושאלו: ”האם זה יהיה אני?“ 20”אחד מבין השנים־עשר שיטבול איתי את הלחם“, השיב ישוע. 21”בן־האדם הולך למות כפי שכתוב שצריך לקרות, אולם אני אומר לכם: אוי לו לאיש שיסגיר אותו; מוטב שלא היה נולד בכלל!“

22בעת הסעודה הוא לקח לחם (מצה), ברך עליו ופרס אותו לפרוסות. הוא הגיש את הפרוסות לתלמידיו ואמר: ”קחו, זהו גופי.“

23לאחר מכן לקח ישוע כוס יין, ברך, הגיש לתלמידיו וכולם שתו ממנה. 24”זהו דמי הנשפך למען רבים, דם הברית“, המשיך ישוע. 25”ואני אומר לכם שלא אשתה עוד יין עד היום שבו אשתה יין חדש במלכות האלוהים.“

26כל הנוכחים שרו מזמורי תהלים, ולאחר מכן הלכו להר הזיתים.

27”כולכם תעזבו אותי,“ אמר ישוע לתלמידיו, ”והרי כתוב: ’אכה את הרעה ותפוצין הצאן‘. 28אולם לאחר שאקום לתחייה אלך לגליל ואפגוש אתכם שם.“

29”יקרה מה שיקרה,“ קרא פטרוס, ”אני לעולם לא אעזוב אותך!“

30”דע לך, פטרוס,“ אמר ישוע, ”עד מחר בבוקר, לפני שיקרא התרנגול, אתה תתכחש לי שלוש פעמים.“

31”אני לעולם לא אתכחש לך, אפילו אם יהיה עלי למות יחד אתך!“ נשבע פטרוס, וכל האחרים גם אמרו כך.

32הם הגיעו לחורשת עצי־זית הנקראת ”גת־שמני“, וישוע אמר לתלמידיו: ”חכו לי כאן עד שאחזור. אני הולך להתפלל.“

33הוא לקח איתו את פטרוס, יעקב ויוחנן, ולפתע נמלא חרדה ומועקה מפני העומד לבוא עליו. 34”אני מתייסר עד מוות!“ אמר להם ישוע. ”חכו כאן… הישארו ערים….“

35הוא התרחק מהם מעט, כרע ברך על האדמה והתפלל שאלוהים יוותר לו על העומד לקרות לו, אם אכן אפשרי.

36”אבא,“ קרא ישוע, ”אתה כל יכול. אנא, הרחק ממני את כוס הייסורים. אולם לא כרצוני כי אם רצונך ייעשה!“

37לאחר מכן הוא חזר אל שלושת התלמידים ומצא אותם ישנים. ”שמעון,“ קרא ישוע לפטרוס, ”אתה ישן? האם לא יכולת להישאר ער שעה אחת בלבד? 38עמדו על המשמר והתפללו שלא תבואו לידי ניסיון. אני יודע שהרוח אכן רוצה, אבל גופכם חלש כל־כך!“

39ישוע הלך להתפלל שוב, וחזר על תחינתו לפני אלוהים. 40הוא חזר אל תלמידיו, וגם הפעם מצא אותם ישנים, כי עיניהם היו כבדות. הם לא ידעו כיצד לתרץ את הדבר.

41כשחזר אליהם ישוע בפעם השלישית הוא קרא: ”קומו! ישנתם מספיק? הגיעה השעה שבן־האדם יימסר לידי אנשים חוטאים. 42קומו, הבה נלך מכאן. הביטו, הנה מתקרב האיש שיסגיר אותי.“

43לפני שהספיק ישוע לסיים את דבריו הגיע למקום יהודה, אחד משנים־עשר התלמידים, ואיתו המון שנשלח מטעם ראשי הכוהנים והסופרים והזקנים. כולם היו מצוידים בחרבות ובמקלות.

44יהודה תיאם איתם מראש ואמר: ”אני אגש לישוע ואנשק אותו, כדי שתדעו מיהו ותוכלו לתפוס אותו ולהוביל אותו בלוית משמר.“ 45יהודה ניגש אליו. ”רבי!“ קרא יהודה כשהוא מחבק ומנשק אותו. 46ואז תפסו את ישוע ואסרו אותו. 47פטרוס שלף מיד את חרבו והכה באחד מהם שהתברר להיות משרתו של הכהן הגדול, וקיצץ את אוזנו.

48”מדוע אתם מתנפלים עלי בחרבות ובמקלות?“ שאל ישוע. ”האם אני פושע מסוכן? 49מדוע לא אסרתם אותי בבית־המקדש? הרי לימדתי שם בכל יום ויכולתם לתפוס אותי ללא התנגדות. אבל מה שכתוב צריך להתקיים.“

50בינתיים ברחו כל התלמידים. 51‏-52נער אחד שהתלווה לישוע לבש סדין בלבד. כשניסו לתפוס אותו, הנער השאיר את הסדין בידם וברח מפניהם ערום.

53ישוע נלקח אל בית הכוהן הגדול, ועד מהרה התאספו שם כל ראשי הכוהנים, הזקנים והסופרים. 54פטרוס הלך אחריהם במרחק מה ונכנס לחצר הכוהן הגדול. הוא התיישב בין המשרתים והתחמם ליד המדורה.

55ראשי הכוהנים וחברי הסנהדרין ניסו למצוא סיבה מספקת כדי להוציא את ישוע להורג, אך מאמציהם היו לשווא. 56עדי שקר רבים התנדבו להעיד נגדו, אולם עדויותיהם סתרו זו את זו.

57לבסוף קמו עדי שקר נוספים שהעידו: 58”שמענו אותו אומר: ’אני אהרוס את המקדש הזה שנבנה בידי אדם, ותוך שלושה ימים אקים מקדש אחר שאינו מעשה ידי אדם!‘ “ 59אולם עדות זאת גם לא הייתה מספקת.

60הכהן הגדול עמד באמצע החדר ושאל את ישוע: ”מה יש לך לומר להגנתך? מה יש לך לומר על כל ההאשמות נגדך?“ 61ישוע לא פצה את פיו, והכהן הגדול המשיך לשאול אותו: ”האם אתה המשיח בן־האלוהים?“

62”אני הוא,“ השיב ישוע, ”אתם עוד תראו את בן־האדם יושב לימין האלוהים, ובא בענני השמים.“

63הכהן הגדול התרגז מאוד וקרע את בגדיו מעליו. ”למה אנו זקוקים עוד?“ שאל בכעס. ”איננו זקוקים להוכחות נוספות! 64שמעתם את הגידופים שלו. מהו פסק־דינכם?“ הם הצביעו פה אחד בעד הוצאתו להורג.

65לאחר השמעת פסק־הדין החל קהל הנוכחים לירוק על ישוע ולהתעלל בו. הם קשרו את עיניו והכו אותו בכל גופו. ”נחש מי הכה אותך, נביא שכמותך?“ לעגו לו. גם השומרים שלקחו אותו משם הכו אותו באגרופים.

66‏-67כל אותו זמן היה פטרוס בחצר. אחת המשרתות בבית הכהן הגדול זיהתה את פטרוס שהתחמם ליד המדורה. היא הביטה בו בתשומת לב רבה והכריזה: ”אתה היית עם ישוע מנצרת!“ 68פטרוס הכחיש מיד את ההאשמה. ”אינני יודע כלל על מה את מדברת!“ אמר ועבר לקצה האחר של החצר.

לפתע נשמעה קריאת התרנגול.

69המשרתת ראתה אותו עומד שם ולא הרפתה ממנו. ”הנה אחד התלמידים של ישוע!“ קראה בקול.

70פטרוס שוב הכחיש את דבריה.

כעבור זמן מה קראו גם אלה שעמדו איתו ליד האש: ”הלא גם אתה אחד מהם? הרי יש לך מבטא גלילי!“

71פטרוס החל לקלל ונשבע: ”אני בכלל לא מכיר את האיש שעליו אתם מדברים!“

72באותו רגע קרא התרנגול בפעם השנייה.

לפתע נזכר פטרוס בדברי ישוע: ”לפני שיקרא התרנגול פעמיים, תתכחש לי שלוש פעמים.“ והוא פרץ בבכי.

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Marko 14:1-72

Shauri La Kumuua Yesu

(Mathayo 26:1-5; Luka 22:1-2; Yohana 11:45-53)

114:1 Yn 11:55; 13:1; Mt 12:14; 26:1-5; Lk 22:1-2Zilikuwa zimebaki siku mbili tu kabla ya Sikukuu ya Pasaka, na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwa wakitafuta njia ya kumkamata Yesu kwa hila na kumuua. 214:2 Mt 26:1-5; Lk 22:1-2Lakini walisema, “Tusilifanye jambo hili wakati wa Sikukuu, maana watu wanaweza wakafanya ghasia.”

Yesu Kupakwa Mafuta Huko Bethania

(Mathayo 26:6-13; Yohana 12:1-8)

314:3 Mt 21:17; Lk 7:37-39Yesu alikuwa Bethania nyumbani kwa Simoni aliyekuwa na ukoma. Wakati alipokuwa ameketi mezani akila chakula cha jioni, mwanamke mmoja aliingia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya nardo14:3 Nardo ni aina ya manukato yaliyotengenezwa kutokana na mimea yenye mizizi inayotoa harufu nzuri. safi ya thamani kubwa. Akaivunja hiyo chupa, akamiminia hayo manukato kichwani mwa Yesu.

4Baadhi ya watu waliokuwepo pale walikuwa wakisemezana wao kwa wao, “Upotevu huu wote ni wa nini? 5Mafuta haya yangeweza kuuzwa kwa zaidi ya dinari14:5 Dinari 300 ni sawa na mshahara wa kibarua wa siku 300. 300, na fedha hizo wakapewa maskini.” Wakamkemea vikali huyo mwanamke.

6Lakini Yesu akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Mwacheni! Yeye amenitendea jambo zuri sana. 714:7 Kum 15:11Maskini mtakuwa nao siku zote na mnaweza kuwasaidia wakati wowote mnaotaka. Lakini mimi hamtakuwa nami siku zote. 814:8 Yn 19:40Huyu mwanamke amenitendea lile aliloweza. Ameumiminia mwili wangu manukato ili kuniandaa kwa maziko yangu. 914:9 Mt 24:14; Mk 16:15Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”

Yuda Akubali Kumsaliti Yesu

(Mathayo 26:14-16; Luka 22:3-6)

1014:10 Mk 3:16-19; Mt 10:4; 26:14-16; Lk 23:3-6Kisha Yuda Iskariote, mmoja wa wale wanafunzi kumi na wawili, akaenda kwa viongozi wa makuhani ili kumsaliti Yesu kwao. 1114:11 Mt 26:14-16; Lk 22:3-6Walifurahi sana kusikia jambo hili na wakaahidi kumpa fedha. Hivyo yeye akawa anatafuta wakati uliofaa wa kumsaliti.

Yesu Ala Pasaka Na Wanafunzi Wake

(Mathayo 26:17-25; Luka 22:7-14, 21-23; Yohana 13:21-30)

1214:12 Kum 16:1-4; 1Kor 5:714:12 Mt 26:17-19; 22:7-13Siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, siku ambayo kwa desturi mwana-kondoo wa Pasaka huchinjwa, wanafunzi wa Yesu wakamuuliza, “Unataka twende wapi ili tukuandalie mahali pa kula Pasaka?”

1314:13 Mt 26:17-19; 22:7-13Basi akawatuma wawili miongoni mwa wanafunzi wake, akawaambia, “Nendeni mjini. Huko mtakutana na mwanaume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni. 1414:14 Mt 26:17-19; 22:7-13Mwambieni mwenye nyumba ile atakayoingia, ‘Mwalimu anauliza: Kiko wapi chumba changu cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka?’ 1514:15 Mdo 1:13; Mt 26:17-19; 22:7-19Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani, kilichopambwa tena kilicho tayari. Tuandalieni humo.”

1614:16 Mt 26:17-19; 22:7-19Wale wanafunzi wakaondoka na kwenda mjini, nao wakakuta kila kitu kama Yesu alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.

1714:17 Mt 26:20Ilipofika jioni, Yesu akaja pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili. 1814:18 Za 41:10Walipoketi mezani wakila, Yesu akawaambia, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti, mmoja anayekula pamoja nami.”

19Wakaanza kuhuzunika na kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi Bwana?”

2014:20 Yn 13:18-27Akawajibu, “Ni mmoja miongoni mwenu ninyi kumi na wawili, yule anayechovya mkate kwenye bakuli pamoja nami. 2114:21 Mt 8:20Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa.”

Kuanzishwa Kwa Meza Ya Bwana

(Mathayo 26:26-30; Luka 22:14-20; 1 Wakorintho 11:23-25)

2214:22 Mt 14:22Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni mle; huu ndio mwili wangu.”

2314:23 1Kor 10:16Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, nao wote wakanywa kutoka humo.

2414:24 Mt 26:28Akawaambia, “Hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi. 2514:25 Mt 3:2Amin, nawaambia, sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya katika Ufalme wa Mungu.”

2614:26 Mt 21:1Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.

Yesu Atabiri Kuwa Petro Atamkana

(Mathayo 26:31-35; Luka 22:31-34; Yohana 13:36-38)

2714:27 Zek 13:7Yesu akawaambia, “Ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa:

“ ‘Nitampiga mchungaji,

nao kondoo watatawanyika.’

2814:28 Mk 16:7Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”

2914:29 Mt 26:33-34; Lk 22:33, 34; Yn 13:37, 38Petro akasema, “Hata kama wengine wote watakuacha, mimi sitakuacha.”

3014:30 Lk 22:34; Yn 13:38Yesu akamwambia, “Amin, nakuambia; leo, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, wewe mwenyewe utanikana mara tatu.”

3114:31 Lk 22:33; Yn 13:37Lakini Petro akasisitiza zaidi, “Hata kama itabidi kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Nao wale wengine wote wakasema vivyo hivyo.

Yesu Aomba Katika Bustani Ya Gethsemane

(Mathayo 26:36-46; Luka 22:39-46)

3214:32 Mt 26:36; Lk 22:29; Yn 13:37Wakaenda mahali paitwapo Gethsemane. Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa, nami niende nikaombe.” 33Kisha akawachukua pamoja naye Petro, Yakobo na Yohana. Akaanza kuhuzunika sana na kutaabika. 3414:34 Yn 12:27Akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe.”

3514:35 Mk 14:41; Mt 26:18Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba kwamba kama ingewezekana saa hiyo ya mateso imwondokee. 3614:36 Rum 8:15; Gal 4:6; Mt 20:22; 26:39Akasema, “Abba,14:36 Abba ni neno la Kiaramu ambalo maana yake ni Baba; ni mtoto wa kuzaa tu angeweza kulitumia kwa baba yake. Baba, mambo yote yawezekana kwako. Niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali vile upendavyo wewe.”

37Akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, “Simoni, umelala? Je, hukuweza kukesha hata kwa saa moja? 3814:38 Mt 6:13; Rum 7:22-23Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”

39Akaenda tena kuomba, akisema maneno yale yale. 40Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito. Nao hawakujua la kumwambia.

4114:41 Mt 26:18Akaja mara ya tatu, akawaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Imetosha! Saa imewadia. Tazameni, Mwana wa Adamu anasalitiwa na kutiwa mikononi mwa wenye dhambi. 4214:42 Mt 26:46; Yn 18:1, 2Inukeni, twende zetu! Tazameni, msaliti wangu yuaja!”

Yesu Akamatwa

(Mathayo 26:47-56; Luka 22:47-53; Yohana 18:3-12)

4314:43 Mt 10:4Yesu alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale wanafunzi Kumi na Wawili, akatokea. Alikuwa amefuatana na umati wa watu wenye panga na marungu, waliokuwa wametumwa na viongozi wa makuhani, walimu wa sheria, na wazee.

44Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni, mkamchukue chini ya ulinzi.” 4514:45 Mt 23:7Mara Yuda akamjia Yesu na kusema, “Rabi.”14:45 Rabi ni neno la Kiebrania ambalo maana yake ni daktari, mwalimu au bwana. Walikuwa na madaraja matatu: La chini kabisa Rab (bwana), la pili Rabi (bwana wangu), na la juu kabisa Raboni (mkuu wangu, bwana wangu mkuu). Akambusu. 46Wale watu wakamkamata Yesu, wakamweka chini ya ulinzi. 47Ndipo mmoja wa wale waliokuwa wamesimama karibu aliuchomoa upanga wake na kumpiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.

4814:48 Mt 26:55; Lk 22:52Kisha Yesu akawaambia, “Mmekuja na panga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi? 4914:49 Mt 26:55; Isa 53:7-12Siku kwa siku nilikuwa pamoja nanyi nikifundisha Hekaluni, wala hamkunikamata. Lakini Maandiko sharti yatimie.” 5014:50 Za 88:8; Mk 14:27Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha, wakakimbia.

51Kijana mmoja, ambaye hakuwa amevaa kitu isipokuwa alijitanda nguo ya kitani, alikuwa akimfuata Yesu. Walipomkamata, 52alikimbia uchi, akaliacha vazi lake.

Yesu Mbele Ya Baraza La Wayahudi

(Mathayo 26:57-68; Luka 22:54-71; Yohana 18:13-24)

5314:53 Mt 26:57; Yn 18:13Wakampeleka Yesu kwa kuhani mkuu, nao viongozi wa makuhani wote, na wazee na walimu wa sheria wote wakakusanyika pamoja. 5414:54 Mt 26:3; Yn 18:18Petro akamfuata kwa mbali, hadi uani kwa kuhani mkuu. Huko akaketi pamoja na walinzi, akiota moto.

5514:55 Mt 5:22Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi14:55 Baraza la Wayahudi hapa ina maana ya Sanhedrin ambalo lilikuwa ndilo baraza la juu kabisa la utawala wa Kiyahudi, lililoundwa na wazee 70 pamoja na kuhani mkuu. lote wakatafuta ushahidi dhidi ya Yesu ili wapate kumuua. Lakini hawakupata jambo lolote. 56Wengi walitoa ushahidi wa uongo dhidi yake, lakini maelezo yao hayakukubaliana.

57Ndipo wengine wakasimama wakatoa ushahidi wa uongo dhidi yake, wakisema: 5814:58 Mk 15:29; Yn 2:19“Sisi tulimsikia akisema, ‘Mimi nitalibomoa Hekalu hili lililojengwa na wanadamu, na katika siku tatu nitajenga jingine ambalo halikujengwa na wanadamu.’ ” 59Lakini hata hivyo, ushahidi wao haukukubaliana.

6014:60 Mt 26:62Basi kuhani mkuu akasimama mbele yao, akamuuliza Yesu, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?” 6114:61 Isa 54:7; Lk 23:9; Mt 16:16; Yn 4:25-26Lakini Yesu akakaa kimya, hakusema neno lolote.

Kuhani mkuu akamuuliza tena, “Je, wewe ndiwe Kristo,14:61 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. Mwana wa Mungu Aliyebarikiwa?”

6214:62 Ufu 1:7; Dan 7:13Yesu akajibu, “Mimi ndimi. Nanyi mtamwona Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa kuume wa Mwenye Nguvu, na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”

6314:63 Hes 14:6; Mdo 14:14Kuhani mkuu akararua mavazi yake, akasema, “Tuna haja gani tena ya mashahidi zaidi? 6414:64 Law 24:16Ninyi mmesikia hayo makufuru. Uamuzi wenu ni gani?”

Wote wakamhukumu kwamba anastahili kifo. 6514:65 Mt 16:21Kisha baadhi ya watu wakaanza kumtemea mate; wakamfunga kitambaa machoni, wakampiga kwa ngumi na kumwambia, “Tabiri!” Walinzi wakamchukua na kumpiga makofi.

Petro Amkana Yesu

(Mathayo 26:69-75; Luka 22:56-62; Yohana 18:15-18, 25-27)

6614:66 Lk 22:55; Yn 18:16Petro alipokuwa bado yuko chini kwenye ua wa jumba la kifalme, tazama akaja mmoja wa watumishi wa kike wa kuhani mkuu. 6714:67 Mk 14:54; 1:24Alipomwona Petro akiota moto, akamtazama sana, akamwambia,

“Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu, Mnazareti.”

6814:68 Mk 14:30, 72Lakini Petro akakana, akasema, “Sijui wala sielewi unalosema.” Naye akaondoka kuelekea kwenye njia ya kuingilia.

6914:69 Mt 26:71; Lk 22:58; Yn 18:25Yule mtumishi wa kike alipomwona mahali pale, akawaambia tena wale waliokuwa wamesimama hapo, “Huyu mtu ni mmoja wao.” 7014:70 Mdo 2:7Lakini Petro akakana tena.

Baada ya muda kidogo wale waliokuwa wamesimama hapo karibu na Petro wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana wewe pia ni Mgalilaya!” 7114:71 Mk 14:30, 72Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui huyu mtu mnayesema habari zake!”

7214:72 Mk 14:30, 68; Mt 26:75; Mk 14:50Papo hapo jogoo akawika mara ya pili. Ndipo Petro akakumbuka lile neno Yesu alikuwa amemwambia: “Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.” Akavunjika moyo, akalia sana.