啟示錄 21 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

啟示錄 21:1-27

新天新地

1接著我看見一個新天新地,21·1 以賽亞書65·17因為以前的天地都消逝了,海洋也不復存在了。 2我又看見聖城新耶路撒冷從天上的上帝那裡降下,預備好了,像妝飾整齊等候新郎的新娘。 3我聽見從寶座中傳來響亮的聲音說:「看啊!上帝的居所設立在人間,祂要與人同住。他們要成為祂的子民,上帝要親自與他們同在,作他們的上帝。 4上帝要擦乾他們所有的眼淚,再沒有死亡、憂傷、哭泣和痛苦,因為以前的事都已成過去。」21·4 以賽亞書25·8

5坐在寶座上的那位說:「看啊!我已經將一切都更新了。你要將這一切記錄下來,因為這些話真實可信。」 6祂又對我說:「一切都成了!我是阿拉法,我是俄梅加;我是開始,我是終結。我要將生命泉的水白白賜給口渴的人。 7得勝者必承受這一切福分,我要作他的上帝,他要作我的兒子。 8至於那些膽怯的、不信的、行為可憎的、殺人的、淫亂的、行邪術的、拜偶像的和所有說謊的,他們的結局是被扔進硫磺火湖裡,這就是第二次的死。」

新耶路撒冷

9七位天使手裡拿著盛滿最後七災的七個碗,其中有一位來對我說:「你來,我要將新娘,就是羔羊的妻子指給你看。」 10我被聖靈感動,天使帶著我到一座高大的山上,將從天上的上帝那裡降下的聖城耶路撒冷指給我看。 11城中充滿上帝的榮光,璀璨如貴重的寶石,晶瑩如碧玉。 12-13城牆高大,有十二個城門,東、北、南、西每面三個門,每個城門都有一位天使把守,門上寫著以色列十二支派的名字。 14城牆共有十二塊基石,基石上有羔羊的十二位使徒的名字。

15那和我說話的天使拿了一根金量桿要丈量聖城、城牆和城門。 16聖城是正方形的,長寬相等。天使用量桿丈量那城,長、寬、高都是兩千二百公里21·16 「兩千二百公里」希臘文是「一萬二千司他町」。17他又丈量了城牆,按人的尺寸,也是天使的尺寸來算,是六十五米21·17 「六十五米」希臘文是「一百四十四肘」。厚。 18城牆是用碧玉砌成的,城本身是用純金造的,跟玻璃一樣明淨。 19城牆的基石用各種寶石裝飾:第一塊基石是碧玉,第二塊是藍寶石,第三塊是綠瑪瑙,第四塊是綠寶石, 20第五塊是紅瑪瑙,第六塊是紅寶石,第七塊是橄欖石,第八塊是水蒼玉,第九塊是黃寶石,第十塊是翡翠,第十一塊是紫瑪瑙,第十二塊是紫晶。

21十二個城門是用十二顆珍珠造的,每一個城門都是一顆珍珠,城中的街道是純金的,好像透明的玻璃一樣。

22我看見城中沒有聖殿,因為全能的主上帝和羔羊就是聖城的殿。 23聖城裡不需要太陽和月亮的光照耀,因為有上帝的榮光照耀,羔羊就是聖城的燈。 24萬民要在聖城的光中行走,地上的君王也要將他們的榮耀帶進聖城。 25城門整天都開著,那裡沒有黑夜。 26人們將列國的榮耀和尊貴帶進聖城。 27所有污穢的、做可憎之事的、撒謊的都不得進入聖城。唯有名字記錄在羔羊的生命冊上的人才有資格進去。

Kiswahili Contemporary Version

Ufunuo 21:1-27

Mbingu Mpya Na Nchi Mpya

121:1 Isa 65:17; 2Pet 3:13Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya, kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza vimekwisha kupita, wala hapakuwepo na bahari tena. 221:2 Ebr 11:10; 12:22Nikaona Mji Mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, ukiwa umeandaliwa kama bibi arusi aliyepambwa kwa ajili ya mumewe. 321:3 2Kor 6:16; Zek 2:10; Isa 8:8Nami nikasikia sauti kubwa kutoka kile kiti cha enzi ikisema, “Sasa makao ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atakaa pamoja nao. Yeye atakuwa Mungu wao nao watakuwa watu wake, naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. 421:4 Ufu 7:17; 1Kor 15:26; Isa 35:10; 65:19Atafuta kila chozi kutoka macho yao. Mauti haitakuwepo tena, wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu, kwa maana mambo ya kwanza yamekwisha kupita.”

521:5 Ufu 4:9; 20:11; 19:9Naye yule aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi akasema, “Tazama, nayafanya mambo yote kuwa mapya!” Kisha akasema, “Andika haya, maana maneno haya ni ya kuaminika tena ni kweli.”

621:6 Ufu 16:17; 1:8; 22:13; Yn 4:10Akaniambia, “Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Yeye aonaye kiu nitampa kunywa kutoka chemchemi ya maji ya uzima bila gharama yoyote. 721:7 Ufu 2:7; 2Sam 7:14Yeye ashindaye atayarithi haya yote, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu. 821:8 Za 5:6; Ufu 2:11Lakini waoga, wasioamini, wachafu, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, pamoja na waongo wote, mahali pao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.”

921:9 Ufu 15:1, 6, 7; 19:7Mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na yale mabakuli saba ya hayo mapigo saba ya mwisho akaja akaniambia, “Njoo, nami nitakuonyesha bibi arusi, yaani, mke wa Mwana-Kondoo.” 1021:10 Ufu 17:3; 1:10; Eze 40:2; Ufu 21:2Naye akanichukua katika Roho hadi kwenye mlima mkubwa na mrefu, akanionyesha ule Mji Mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu. 1121:11 Ufu 15:8; 4:6; Isa 60:1, 2; Eze 43:2; Ufu 21:23; 21:18, 19Ulikuwa ukingʼaa kwa utukufu wa Mungu kama kito chenye thamani sana, kama yaspi, safi kama kioo. 1221:12 Eze 48:30-34Ulikuwa na ukuta mkubwa, mrefu wenye malango kumi na mawili, pakiwa na malaika kumi na wawili kwenye hayo malango. Kwenye malango hayo yaliandikwa majina ya yale makabila kumi na mawili ya Israeli. 1321:13 Eze 48:31, 34Kulikuwa na malango matatu upande wa mashariki, matatu upande wa kaskazini, matatu upande wa kusini na matatu upande wa magharibi. 1421:14 Efe 2:20; Ebr 11:10; Mdo 1:2621:14 Ufu 11:1; Eze 40:3; Ufu 21:12Ukuta wa huo mji ulikuwa na misingi kumi na miwili, na juu yake yaliandikwa majina ya wale mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo.

15Huyo malaika aliyesema nami alikuwa na ufito wa dhahabu wa kupimia huo mji, malango yake na kuta zake. 1621:16 Eze 45:16; 48:16; 17Mji huo ulikuwa mraba, urefu wake ulikuwa sawa na upana wake. Akaupima huo mji kwa huo ufito akakuta una kama kilomita 2,200;21:16 Kilomita 2,200 hapa ni sawa na maili 1,200. urefu wake na upana wake na kwenda juu kwake vilikuwa sawa. 1721:17 Ufu 13:18Akaupima ukuta wake, ulikuwa na unene wa dhiraa 14421:17 Dhiraa 144 ni karibu mita 65. kwa kipimo cha kibinadamu ambacho huyo malaika alikuwa akikitumia. 1821:18 Ufu 21:11, 21Ukuta huo ulijengwa kwa yaspi hali mji wenyewe ulijengwa kwa dhahabu safi, ikingʼaa kama kioo. 1921:19 Kut 28:17-20Misingi ya kuta za mji huo zilipambwa kwa kila aina ya kito cha thamani. Msingi wa kwanza ulikuwa wa yaspi, wa pili yakuti samawi, wa tatu kalkedoni, wa nne zumaridi, 2021:20 Ufu 4:3wa tano sardoniki, wa sita akiki, wa saba krisolitho, wa nane zabarajadi, wa tisa yakuti manjano, wa kumi krisopraso, wa kumi na moja hiakintho, wa kumi na mbili amethisto. 2121:21 Ufu 21:12; Isa 54:12; Ufu 21:18Yale malango kumi na mbili yalikuwa ni lulu kumi na mbili, kila lango lilikuwa limetengenezwa kwa lulu moja. Barabara kuu ya mji huo ilikuwa ya dhahabu safi ingʼaayo kama kioo.

2221:22 Yn 4:21-23; Ufu 1:8; 5:6Sikuona Hekalu ndani ya huo mji kwa sababu Bwana Mungu Mwenyezi na Mwana-Kondoo ndio hekalu lake. 2321:23 Isa 24:23; 22:5Ule mji hauhitaji jua wala mwezi kuuangazia, kwa sababu utukufu wa Mungu ndio nuru yake na Mwana-Kondoo ndiye taa yake. 2421:24 Isa 60:3, 5Mataifa yatatembea yakiangaziwa na nuru yake na wafalme wa duniani wataleta fahari yao ndani yake. 2521:25 Isa 60:11; Zek 14:7; Ufu 22:5Malango yake hayatafungwa kamwe, kwa maana hakutakuwa na usiku humo. 2621:26 Ufu 21:24Utukufu na heshima za mataifa zitaletwa humo. 2721:27 Yoe 3:17; Ufu 22:14, 15Lakini kitu kichafu hakitaingia humo kamwe, wala mtu yeyote atendaye mambo ya aibu au ya udanganyifu. Bali watakaoingia humo ni wale tu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.