創世記 24 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

創世記 24:1-67

亞伯拉罕為以撒娶妻

1亞伯拉罕已經年邁,耶和華在一切事上都賜福給他。 2亞伯拉罕對負責他所有產業的老總管說:「請你把手放在我大腿底下, 3我要你憑掌管天地的上帝耶和華起誓,你不會找我所居之地的迦南女子做我兒子的妻子。 4你要回到我的家鄉,在我的親族中為以撒物色妻子。」 5老總管問他:「如果那女子不肯跟我到這裡來呢?我要把你兒子帶回你的家鄉嗎?」 6亞伯拉罕說:「你千萬不可帶我的兒子回那裡! 7因為帶領我離開父家和本鄉的天上的上帝耶和華,曾經向我說話,起誓應許把這片土地賜給我的後裔。祂必派天使在你前面引路,好讓你在那裡為我兒子找到妻子。 8如果那女子不肯跟你來,你也算履行了你向我起的誓,只是你不可帶我兒子回那裡。」 9於是,老總管就把手放在他主人亞伯拉罕的大腿底下,為這事向他起誓。

10老總管帶著主人的十匹駱駝和各種上好的禮物,啟程前往美索不達米亞,來到拿鶴住的城。 11黃昏,婦女們出來打水的時候,他讓駱駝跪在城外的井旁, 12然後禱告說:「我主人亞伯拉罕的上帝耶和華啊,求你施恩給我家主人亞伯拉罕,讓事情今天能夠成就。 13現在,我站在這泉水旁,城裡的女子正出來打水。 14如果我對哪個少女說『請放下你的水罐,讓我喝點水』,如果她說『請喝,我也打水給你的駱駝喝』,願那女子做你為自己的僕人以撒選定的妻子。這樣,我就知道你施恩給我的主人了。」

老總管井旁遇利百加

15老總管的話還沒有說完,利百加肩上扛著水罐走出來。她是彼土利的女兒,彼土利亞伯拉罕的兄弟拿鶴密迦所生的兒子。 16利百加長得非常美麗,是個處女,沒有男人親近過她。她下到井旁,把水罐盛滿了水後上來。 17老總管跑上前去對她說:「求你給我一點水喝。」 18她回答說:「我主,請喝!」說完,立刻放下水罐,托在手上讓他喝。 19等他喝完以後,利百加又說:「我再為你的駱駝打水,讓牠們喝飽。」 20於是,她迅速把水罐裡的水倒進水槽裡,又跑到井邊為所有的駱駝打水。 21老總管默不作聲地注視著利百加,要看看耶和華是否使他此行順利。

22駱駝喝過水以後,老總管拿出一隻約六克重的金環和一對約一百一十克重的金鐲給利百加23對她說:「請問你是誰的女兒?你父親家裡有地方讓我們住宿嗎?」 24利百加回答說:「我是彼土利的女兒,我父親是拿鶴密迦的兒子。 25我家裡有充足的糧草,也有地方讓你留宿。」 26老總管聽了,就俯伏敬拜耶和華, 27說:「我主人亞伯拉罕的上帝耶和華當受稱頌,因為祂一直以慈愛和信實對待我的主人。耶和華也一路引導我走到我主人兄弟的家裡。」

28利百加跑回家中,把這事告訴了母親家的人。 29利百加有個哥哥名叫拉班30他看見妹妹的金環和手上的金鐲,聽了她敘述老總管的話,就跑到井旁,見老總管跟駱駝仍然站在那裡, 31便對他說:「你這蒙耶和華賜福的人,請到我家。為什麼站在外面呢?我已經為你預備好了房間,也為駱駝預備了地方。」 32老總管就到了拉班的家裡,拉班卸下駱駝背上的東西,給駱駝餵上草料,打水給老總管和隨行的人洗腳。 33然後晚餐準備好了,老總管卻說:「不,等我說明來意後再吃。」拉班說:「請說。」

34老總管說:「我是亞伯拉罕的僕人。 35耶和華賜給我主人極大的福氣,使他非常富有。耶和華賜給他牛群、羊群、金子、銀子、僕婢、駱駝和驢。 36我主人的妻子撒拉在晚年生了一個兒子,主人把所有的財產都給了他。 37主人要我起誓,他說,『你不可給我的兒子娶我居住的迦南當地女子為妻, 38你要到我家鄉的親族中為我兒子物色妻子。』 39我問我的主人,『如果那女子不願意跟我回來怎麼辦?』 40他說,『我忠心事奉的耶和華必派天使與你同行,使你一路順利,為我兒子在家鄉的親族中物色妻子。 41你去我親族那裡就是履行了你向我起的誓,如果我的親族不肯把女子交給你,你也算履行了你向我起的誓。』

42「今天我來到井旁時曾禱告說,『我主人亞伯拉罕的上帝耶和華啊,求你使我一路順利。 43我現在站在井旁,有女子出來打水的時候,我會對她說,請讓我喝一點你罐裡的水, 44如果她說,請喝,我也打水給你的駱駝喝,就讓她做你為我家主人的兒子預備的妻子吧。』

45「我心中的話還沒有說完,就看見利百加肩上扛著水罐到井旁打水。我上前向她要水喝, 46她就連忙放下肩上的水罐,說,『請喝,我也打水飲你的駱駝。』我喝了,她又打水飲駱駝。 47我問她是誰家的女兒,她說,『是拿鶴密迦的兒子彼土利的女兒。』我就給她戴上金鼻環和金手鐲, 48然後俯伏敬拜、頌讚我主人亞伯拉罕的上帝耶和華,祂引導我走對路,使我找到了我主人兄弟的孫女給我主人的兒子做妻子。 49現在,你們若願意以慈愛和信實對待我的主人,答應這門親事,請告訴我;如果不答應,也請告訴我,好讓我知道應該怎麼辦。」

50拉班彼土利回答說:「既然這是耶和華的安排,我們就無話可說了。 51你看,利百加就在這裡,你可以照耶和華的話,把她帶回去給你主人的兒子做妻子。」 52亞伯拉罕的老總管聽見這話,就俯伏在地上敬拜耶和華, 53然後拿出金銀首飾和衣裳送給利百加,又把貴重的禮物送給她的哥哥和母親。 54老總管和隨行的人用過晚飯以後,在那裡住了一夜。早晨,老總管說:「請讓我返回我主人那裡。」 55利百加的哥哥和母親說:「讓她和我們住上十來天再去吧!」 56可是,老總管說:「既然耶和華已經使我一路順利,請你們不要挽留我,請讓我回到我主人那裡。」 57他們說:「我們問問利百加的意見吧。」 58他們就叫來利百加,問她:「你願意跟這個人同去嗎?」利百加說:「我願意!」 59於是,他們讓妹妹利百加和她的奶媽跟老總管及隨行的人一同離去, 60並為利百加祝福,說:

「我們的妹妹啊,

願你成為千萬人之母!

願你的後裔佔領敵城!」

以撒與利百加成婚

61於是,利百加和她的婢女們準備妥當,騎上駱駝,跟著老總管離去。老總管就這樣帶著利百加走了。

62那時,以撒住在南地,他剛從庇耳·拉海·萊回來。 63傍晚的時候,以撒來到田間默想,他抬頭一看,見一隊駱駝迎面而來。 64利百加抬頭看見以撒,就從駱駝上下來, 65問老總管:「那從田間來迎接我們的是誰?」老總管說:「是我的主人!」利百加聽了就蒙上面紗。 66老總管向以撒講述整個事情的經過。 67以撒就帶利百加進入他母親撒拉的帳篷,娶她為妻,並且愛她。自從母親去世後,以撒這才得到安慰。

Kiswahili Contemporary Version

Mwanzo 24:1-67

Isaki Na Rebeka

124:1 Mwa 17:17; Yos 23:1; Mwa 12:2; Gal 3:9Wakati huu Abrahamu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, naye Bwana alikuwa amembariki katika kila njia. 224:2 Mwa 15:3; 39:4-6; 47:29Akamwambia mtumishi wake mkuu wa vitu vyote katika nyumba yake, yule aliyekuwa msimamizi wa vitu vyote alivyokuwa navyo, “Weka mkono wako chini ya paja langu, 324:3 Mwa 10:15-19; 47:31; 50:25; 14:19; Hes 20:14; 2Kor 6:14-17Ninataka uape kwa Bwana, Mungu wa mbingu na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia mwanangu mke kutoka binti za Wakanaani, ambao ninaishi miongoni mwao, 424:4 Mwa 12:1; 21:21; Amu 14:3bali utakwenda katika nchi yangu na jamaa zangu umpatie Isaki mwanangu mke.”

524:5 Ebr 11:15Yule mtumishi akamuuliza, “Je, kama huyo mwanamke atakataa kuja nami katika nchi hii? Je, nimpeleke mwanao katika hiyo nchi uliyotoka?”

6Abrahamu akasema, “Hakikisha kwamba hutamrudisha mwanangu huko. 724:7 Mwa 12:1, 7; 16:7; Rum 4:15; Gal 3:16Bwana, Mungu wa mbingu, aliyenitoa nyumbani kwa baba yangu na nchi yangu niliyozaliwa na aliyesema nami na akaniahidi kwa kiapo, akisema, ‘Nitawapa watoto wako nchi hii,’ atatuma malaika wake akutangulie ili umpatie mwanangu mke kutoka huko. 824:8 Yos 2:12-20; 9:20Kama huyo mwanamke asipokubali kufuatana nawe, basi utafunguliwa kutoka kiapo nilichokuapisha. Ila usimrudishe mwanangu huko.” 924:9 Mwa 32:4; 33:8Basi yule mtumishi akaweka mkono wake chini ya paja la bwana wake Abrahamu akamwapia kuhusu shauri hili.

1024:10 1Fal 10:2; 1Nya 12:40; Isa 30:6; Mwa 11:29; 43:11; 45:25; Hes 23:7; Kum 23:4; Amu 3:8Ndipo huyo mtumishi akachukua ngamia kumi miongoni mwa ngamia za bwana wake, akaondoka, akiwa amechukua aina zote za vitu vizuri kutoka kwa bwana wake. Akaelekea Aramu-Naharaimu24:10 Yaani Mesopotamia ya Kaskazini-Magharibi. na kushika njia kwenda mji wa Nahori. 1124:11 Kut 2:15-16; 1Sam 9:11; Yn 4:7; Mwa 29:2, 9-10Akawapigisha ngamia magoti karibu na kisima cha maji nje ya mji, ilikuwa inaelekea jioni, wakati ambapo wanawake wanakuja kuteka maji.

1224:12 Mwa 19:19; 26:24; 27:20; 28:13; 31:42, 53; 32:9; 43:23; 46:3; Kut 3:6; 1Fal 18:36; Za 75:9; 94:7; Neh 1:11; Yos 2:12; Ay 10:12Kisha akaomba, “Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, nipatie ushindi leo, uonyeshe huruma kwa bwana wangu Abrahamu. 13Tazama, nimesimama karibu na kisima hiki cha maji, nao binti za watu wa mji huu wanakuja kuteka maji. 1424:14 Amu 6:17, 37; 1Sam 14:10; 1Fal 13:3; Za 86:17; Isa 38:7; Yer 44:29Basi na iwe hivi, nitakapomwambia binti mmojawapo, ‘Tafadhali tua mtungi wako nipate kunywa maji,’ naye akisema, ‘Kunywa, nitawanywesha na ngamia wako pia.’ Basi na awe ndiye uliyemchagua kwa ajili ya mtumishi wako Isaki. Kwa hili nitajua umemhurumia bwana wangu.”

1524:15 Mwa 22:22-23; 11:29Ikawa kabla hajamaliza kuomba, Rebeka akatokea akiwa na mtungi begani mwake. Alikuwa binti wa Bethueli. Bethueli alikuwa mwana wa Milka aliyekuwa mke wa Nahori ndugu wa Abrahamu. 1624:16 Mwa 12:11; Kum 22:15-21Huyu msichana alikuwa mzuri sana wa sura, bikira, ambaye hakuna mtu aliyekuwa amekutana naye kimwili. Aliteremka kisimani, akajaza mtungi wake akapanda juu.

1724:17 1Fal 17:10; Yn 4:7Ndipo yule mtumishi akaharakisha kukutana naye akamwambia, “Tafadhali nipe maji kidogo katika mtungi wako.”

18Yule msichana akasema, “Kunywa, bwana wangu.” Akashusha kwa haraka mtungi mkononi mwake na akampa, akanywa.

19Baada ya kumpa yule mtumishi yale maji, akamwambia, “Nitateka maji kwa ajili ya ngamia zako pia mpaka wote watosheke.” 20Akafanya haraka kumimina maji kwenye birika ya kunyweshea wanyama, akakimbia kisimani kuteka maji mengine na akateka ya kuwatosha ngamia wake wote. 21Pasipo kusema neno, yule mtumishi akamtazama kwa makini aone kama Bwana ameifanikisha safari yake, au la.

2224:22 Mwa 41:42; Isa 3:21; Eze 16:11-12Ikawa ngamia walipokwisha kunywa wote, yule mtumishi akampa huyo msichana pete ya puani ya dhahabu yenye uzito wa beka moja24:22 Beka moja ya dhahabu ni sawa na gramu 5.5. na bangili mbili za dhahabu zenye uzito wa shekeli kumi.24:22 Shekeli 10 za dhahabu ni sawa na gramu 110. 2324:23 Amu 19:15; 20:4Kisha akamuuliza, “Wewe ni binti wa nani? Tafadhali uniambie, je, kuna nafasi katika nyumba ya baba yako tutakapoweza kulala?”

2424:24 Mwa 11:29Yule msichana akamjibu, “Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Milka aliyemzalia Nahori.” 2524:25 Amu 19:19Akaendelea kusema, “Kwetu kuna majani mengi na malisho, tena kuna nafasi kwa ajili yenu kulala.”

2624:26 Kut 4:31; 12:27; 1Nya 29:20; 2Nya 20:18Yule mtumishi akasujudu na kumwabudu Bwana, 2724:27 Mwa 14:20; 32:10; 47:29; Kut 18:20; Rut 4:14; 1Sam 25:32; 2Sam 18:28; 1Fal 8:56; Za 28:6; 41:13; 68:19; 98:3; 106:48; Yos 2:14; Lk 1:68akisema, “Atukuzwe Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye hakuondoa wema na uaminifu wake kwa bwana wangu. Mimi nami, Bwana ameniongoza safarini akanifikisha nyumbani kwa jamaa za bwana wangu.”

2824:28 Mwa 29:12Yule msichana akakimbia akawaeleza watu wa nyumbani mwa mama yake kuhusu mambo haya. 2924:29 Mwa 25:20; 27:43; 28:2-5; 29:5, 12-13Rebeka alikuwa na kaka aliyeitwa Labani, huyo akaharakisha kukutana na yule mtumishi kule kisimani. 3024:30 Eze 23:42Mara alipoiona ile pete puani, na bangili mikononi mwa dada yake na kusikia yale maneno Rebeka aliyoambiwa na huyo mtumishi, alimwendea huyo mtumishi, akamkuta amesimama karibu na ngamia wake pale karibu na kisima. 3124:31 Mwa 26:29; Rut 3:10; Za 115:15Akamwambia, “Karibu nyumbani wewe uliyebarikiwa na Bwana, kwa nini unasimama huko nje? Mimi nimekuandalia nyumba na mahali kwa ajili ya ngamia.”

3224:32 Mwa 18:4; Amu 19:21Hivyo yule mtumishi akaenda nyumbani, mizigo ikaondolewa juu ya ngamia. Majani na malisho yakaletwa kwa ajili ya ngamia na maji kwa ajili yake na watu wake ili kunawa miguu. 33Ndipo chakula kikaandaliwa kwa ajili yake, lakini akasema, “Sitakula mpaka niwe nimewaambia yale niliyo nayo ya kusema.”

Labani akasema, “Basi tuambie.”

3424:34 Mwa 15:3Hivyo akasema, “Mimi ni mtumishi wa Abrahamu. 3524:35 Mwa 12:2, 16; 23:6Bwana amembariki sana bwana wangu, amekuwa tajiri. Amempa kondoo na ngʼombe, fedha na dhahabu, watumishi wa kiume na wa kike, ngamia na punda. 3624:36 Mwa 17:17; 25:5; 26:14Sara mkewe bwana wangu amemzalia mwana katika uzee wake, naye amempa kila kitu alichokuwa nacho. 3724:37 Mwa 50:5Naye bwana wangu ameniapisha na akasema, ‘Kamwe usimtwalie mwanangu mke katika binti za Wakanaani, ambao ninaishi katika nchi yao, 3824:38 Mwa 21:21ila uende mpaka kwa jamaa ya baba yangu na ukoo wangu mwenyewe, ukamtwalie mwanangu mke huko.’

39“Kisha nikamuuliza bwana wangu, ‘Je, kama huyo mwanamke hatakubali kurudi nami?’

4024:40 Mwa 5:22; 12:1; 16:7“Akanijibu, ‘Bwana ambaye nimetembea mbele zake, atatuma malaika wake pamoja nawe, na kuifanikisha safari yako, ili uweze kupata mke kwa ajili ya mwanangu katika ukoo wangu na kutoka jamaa ya baba yangu. 41Kisha, utakapokwenda kwenye ukoo wangu, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu hata kama wakikataa kukupa huyo binti, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu.’

42“Nilipokuja kisimani leo nilisema, ‘Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ikikupendeza, naomba uifanikishe safari niliyoijia. 4324:43 Mit 30:19; Isa 7:14Tazama, ninasimama kando ya kisima hiki, kama mwanamwali akija kuteka maji nami nikimwambia, tafadhali niruhusu ninywe maji kidogo kutoka kwenye mtungi wako, 44naye kama akiniambia, “Kunywa, nami nitateka maji kwa ajili ya ngamia wako pia,” basi huyo awe ndiye mke ambaye Bwana amemchagulia mwana wa bwana wangu.’

4524:45 1Sam 1:13; Yn 4:7“Kabla sijamaliza kuomba moyoni mwangu, Rebeka akatokea, amebeba mtungi begani mwake. Akashuka kisimani akateka maji, nami nikamwambia, ‘Tafadhali nipe maji ninywe.’

46“Akafanya haraka kushusha mtungi wake begani na kusema, ‘Kunywa na nitawanywesha ngamia wako pia,’ basi nikanywa, akawanywesha na ngamia pia.

4724:47 Mwa 22:22; Isa 3:19; Eze 16:11-12“Nikamuuliza, ‘Wewe ni binti wa nani?’

“Akasema, ‘Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Nahori, Milka aliyemzalia.’

“Ndipo nilipotia pete puani mwake na bangili mikononi mwake, 48nikasujudu na nikamwabudu Bwana. Nikamtukuza Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, aliyeniongoza katika njia sahihi ili nimtwalie mwana na bwana wangu mke katika jamaa zake. 49Ikiwa mtaonyesha wema na uaminifu kwa bwana wangu, mniambie, la sivyo, mniambie, ili niweze kujua njia ya kugeukia.”

5024:50 Za 118:23; Mwa 22:22; 31:24-29; 48:16Labani na Bethueli wakajibu, “Jambo hili limetoka kwa Bwana, hatuwezi kukuambia jambo lolote baya au jema. 51Rebeka yuko hapa, mchukue na uende, awe mke wa mwana wa bwana wako, sawasawa na Bwana alivyoongoza.”

52Ikawa huyo mtumishi wa Abrahamu aliposikia waliyosema, alisujudu mpaka nchi mbele za Bwana. 5324:53 Mwa 45:22; Kut 3:22; 12:35; 2Fal 5:5Ndipo huyo mtumishi akatoa vitu vilivyotengenezwa kwa dhahabu na kwa fedha pamoja na mavazi, akampa Rebeka, pia akawapa zawadi za thamani kubwa nduguye na mamaye. 5424:54 Mwa 30:25Kisha yeye na wale watu waliokuwa pamoja naye wakala, wakanywa na kulala palepale.

Walipoamka asubuhi, yule mtumishi, akasema, “Nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”

5524:55 Amu 19:3-4Lakini ndugu yake Rebeka pamoja na mama yake wakajibu, “Acha binti akae kwetu siku kumi au zaidi, ndipo mwondoke.”

56Lakini yule mtumishi akawaambia, “Msinicheleweshe, kwa kuwa Bwana amefanikisha safari yangu, nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”

57Ndipo wakasema, “Acha tumwite huyo binti tumuulize, tusikie atakavyosema.” 5824:58 Rum 1:16Kwa hiyo wakamwita Rebeka na kumuuliza, “Je, utakwenda na mtu huyu?”

Akasema, “Nitakwenda.”

5924:59 Mwa 35:8Hivyo wakamwaga ndugu yao Rebeka aondoke, pamoja na mjakazi wake, mtumishi wa Abrahamu na watu wake. 6024:60 Mwa 17:16; 22:17; 27:4; 31:55; 48:9, 15, 20; Yos 22:6; Mit 27:11Wakambariki Rebeka, wakamwambia,

“Ndugu yetu, uwe wewe kumi elfu,

mara elfu nyingi,

nao wazao wako wamiliki

malango ya adui zao.”

6124:61 Mwa 16:1; 30:3; 46:25Rebeka na vijakazi wake wakajiandaa, wakapanda ngamia zao wakafuatana na yule mtu. Hivyo yule mtumishi akamchukua Rebeka akaondoka.

6224:62 Mwa 16:14; 12:9Basi Isaki alikuwa ametoka Beer-Lahai-Roi, kwa kuwa alikuwa anaishi nchi ya Negebu. 6324:63 Za 77:12; 119:15, 27; 143:5; 145:5; Mwa 18:2Isaki akatoka kwenda shambani kutafakari wakati wa jioni, alipoinua macho yake, akaona ngamia wanakuja. 6424:64 Mwa 31:17, 34; 1Sam 30:17Rebeka pia akainua macho akamwona Isaki. Akashuka kutoka kwenye ngamia wake 6524:65 Mwa 38:14; Wim 4:1-3; 6:7; Isa 47:2na akamuuliza yule mtumishi, “Ni nani mtu yule aliye kule shambani anayekuja kutulaki?”

Yule mtumishi akajibu, “Huyu ndiye bwana wangu.” Hivyo Rebeka akachukua shela yake akajifunika.

66Kisha yule mtumishi akamweleza Isaki mambo yote aliyoyatenda. 6724:67 Mwa 31:33; 18:9; 25:20; 49:31; 29:18-20; 23:1-2; 34:3; Amu 16:4Ndipo Isaki akamwingiza Rebeka katika hema la Sara mama yake, Isaki akamchukua Rebeka, hivyo akawa mke wake. Isaki akampenda, akafarijika baada ya kifo cha mama yake.