創世記 17 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

創世記 17:1-27

上帝再次與亞伯蘭立約

1亞伯蘭九十九歲那年,耶和華向他顯現說:「我是全能的上帝。你要遵行我的旨意,做純全無過的人。 2我要與你立約,我要使你子孫極其繁盛。」 3亞伯蘭就俯伏在地,上帝又對他說: 4「我要與你立約,你必成為萬族之父。 5以後你的名字不再叫亞伯蘭,要改為亞伯拉罕17·5 「亞伯拉罕」意思是「萬族之父」。,因為我已立你為萬族之父。 6我要使你生養眾多,民族必由你而生,君王必從你而出。 7我要和你並你的子子孫孫立永遠的約,我要做你和你子孫的上帝。 8我要把你現在寄居的整個迦南,賜給你和你的子孫永遠作產業,我也必做他們的上帝。」

9上帝又對亞伯拉罕說:「你和你的子孫世世代代都要遵守我的約。 10你們所有的男子都要受割禮,這是我與你和你的子孫所立的約,你們要遵守。 11你們都要割包皮,作為我與你們立約的記號。 12你們世世代代的男子,在出生後的第八日都要接受割禮,包括在你家裡出生的和用錢從外族人那裡買來的奴僕。 13不論是在你家裡生的,還是你用錢買來的男子,都要接受割禮,這樣我的約就在你們的肉體上成為永遠的約。 14任何沒有接受割禮的男子,要將他從民中剷除,因為他違背了我的約。」

15上帝對亞伯拉罕說:「你的妻子撒萊以後不要叫撒萊,她的名字要叫撒拉16我必賜福給她,讓她為你生一個兒子。我必賜福給她,讓她成為列國之母,列邦的君王必從她而出。」 17亞伯拉罕就俯伏在地,笑了起來,心想:「一百歲的人還能有孩子嗎?撒拉已經九十歲了,還能生育嗎?」 18亞伯拉罕對上帝說:「願以實瑪利蒙你賜福。」 19上帝說:「不,你妻子撒拉必為你生一個兒子,你要給他取名叫以撒,我必與他堅立我的約,作為他後代永遠的約。 20至於以實瑪利,我已聽見你的祈求,我必賜福給他,使他生養眾多、子孫極其繁盛。他必做十二個族長的父親,我必使他成為大國。 21撒拉必在明年這時候給你生以撒,我必向他堅守我的約。」 22上帝說完以後,便離開亞伯拉罕上升而去。

23亞伯拉罕就在那天照著上帝的吩咐,為兒子以實瑪利和家中所有的男子,不論是在家中出生的,還是買回來的,都行了割禮。 24亞伯拉罕接受割禮的時候九十九歲。 25他的兒子以實瑪利接受割禮的時候十三歲。 26他們父子二人就在那天接受了割禮。 27亞伯拉罕家裡所有的男子,包括家中出生的和買回來的,都一起接受了割禮。

Kiswahili Contemporary Version

Mwanzo 17:1-27

Agano La Tohara

117:1 Mwa 5:22; 12:4-7; 20:5; 28:3; 35:11; 43:14; 48:3; 49:25; Kut 6:3; 18:13; Rut 1:20; Ay 5:17; 6:4, 14; 22:21; 33:19; 36:16; Isa 13:6; Yoe 1:15; Mik 6:9; 1Fal 3:6; 9:4; Za 15:2; 18:23; 78:72; 101:2Abramu alipokuwa na miaka tisini na tisa, Bwana akamtokea akamwambia, “Mimi ndimi Mungu Mwenyezi;17:1 Mungu Mwenyezi hapa ni jina la Kiebrania, El-Shaddai (yaani Mungu Mwenye utoshelevu wote). enenda mbele zangu na uishi kwa unyofu. 217:2 Mwa 12:2; 15:18; 22:16-18Nami nitafanya Agano langu kati yangu na wewe, nami nitakuzidisha sana sana.”

317:3 Mwa 18:2; 19:1; 33:3; Kut 18:7; Hes 14:5; Yos 5:14; 7:6; Amu 13:20; Eze 1:28; 3:23Abramu akaanguka kifudifudi, naye Mungu akamwambia, 417:4 Mwa 15:18; 12:2; 25:23“Kwa upande wangu, hili ndilo Agano langu na wewe: Wewe utakuwa baba wa mataifa mengi. 517:5 Mwa 32:28; 35:10; 37:3, 13; 43:6; 46:2; 1Fal 18:31; 2Fal 17:34; 1Nya 1:34; Neh 9:7; Isa 48:1; Yn 1:42; Rum 4:17Jina lako hutaitwa tena Abramu, bali jina lako litakuwa Abrahamu,17:5 Abrahamu maana yake Baba wa watu wengi. kwa maana nimekufanya wewe baba wa mataifa mengi. 617:6 Mwa 1:28; 18:10; 21:1; 22:17; 26:22; 28:3; 35:11; 36:31; 41:52; 47:27; 48:4; 49:22; Law 26:9; Mt 1:6; Kum 7:13; Isa 51:2Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, kwako yatatoka mataifa nao wafalme watatoka kwako. 717:7 Mwa 6:18; 9:16; 18:15; Kut 6:7; 20:2; 29:45-46; Law 11:44-45; 18:2; 22:33; 25:38; 26:9, 12, 15; Hes 15:41; Kum 4:20; 7:6, 21; 29:13; 2Sam 7:24; Ebr 13:20; Yer 14:9; Ufu 21:7; Rum 9:8; Gal 3:16Nitalithibitisha Agano langu kama Agano la milele kati yangu na wewe na wazao wako baada yako na vizazi vijavyo niwe Mungu wako na Mungu wa wazao wako. 817:8 Mwa 10:19; 12:7; 15:7; 23:4; 28:4; 35:27; 37:1; Kut 6:4; Yer 31:1; 1Nya 29:15Nchi yote ya Kanaani, unakoishi sasa kama mgeni, nitakupa kuwa milki yako milele, na uzao wako, nami nitakuwa Mungu wao.”

917:9 Mwa 18:19; 22:18; Kut 19:5; Kum 5:2Ndipo Mungu akamwambia Abrahamu, “Kwa upande wako, lazima ushike Agano langu, wewe na wazao wako kwa ajili ya vizazi vijavyo. 1017:10 Mwa 21:4; Law 12:3; Yos 5:2-7; Rum 4:11; Yn 7:22; Mdo 7:8Hili ni Agano langu na wewe pamoja na wazao wako baada yako, Agano mtakalolishika: Kila mwanaume miongoni mwenu atatahiriwa. 1117:11 Kut 12:48; Kum 10:16; Mwa 9:12; Rum 4:11Mtafanyiwa tohara na hii itakuwa ni alama ya Agano kati yangu na ninyi. 1217:12 Mwa 9:12; 21:4; Law 12:3; Yos 5:2; Lk 1:59; 2:21Kwa vizazi vijavyo, kila mwanaume miongoni mwenu mwenye siku nane ni lazima atahiriwe, pamoja na watakaozaliwa nyumbani mwako au walionunuliwa kwa fedha kutoka kwa mgeni, wale ambao sio watoto wako. 1317:13 Kut 12:44-48; Mwa 9:16Awe amezaliwa nyumbani mwako au amenunuliwa kwa fedha yako, ni lazima watahiriwe. Agano langu katika mwili wako litakuwa ni Agano la milele. 1417:14 Kut 4:24-26; 12:15, 19; 30:33; Eze 44:7; Yos 5:2-8; Law 7:20, 25; 17:4; 18:29; 19:8; 20:17; Hes 9:13; 15:30; 19:13; Kum 17:12; Ay 38:15; Za 37:28Kila mwanaume asiyetahiriwa, ambaye hajapata tohara ya mwilini, atatengwa na watu wake, amelivunja Agano langu.”

1517:15 Mwa 11:29Pia Bwana akamwambia Abrahamu, “Kwa upande wa Sarai mkeo, hutamwita tena Sarai bali jina lake litakuwa Sara. 1617:16 Mwa 18:10; 24:60; Isa 29:22; Gal 4:31Nitambariki na hakika nitakupatia mwana kwake. Nitambariki na kwamba atakuwa mama wa mataifa, wafalme wa mataifa watatoka kwake.”

1717:17 Mwa 12:4; 18:11-13; 21:6, 7; 24:1, 36; Yer 20:15; Lk 1:18; Rum 4:19; Gal 4:23; Ebr 11:11Abrahamu akaanguka kifudifudi, akacheka na kusema moyoni mwake, “Je, mtu wa miaka mia moja aweza kuzaa mwana? Je, Sara atazaa mtoto katika umri wa miaka tisini?” 1817:18 Mwa 16:15; 21:11Abrahamu akamwambia Mungu, “Laiti Ishmaeli naye angeshiriki baraka yako!”

1917:19 Mwa 9:16; 16:11; 18:14; 21:2; 26:3; 50:24; Kut 13:11; Kum 1:8; Gal 3:16; 1Sam 1:20; Mt 1:21; Lk 1:13, 31Ndipo Mungu akasema, “Ndiyo, lakini mkeo Sara atakuzalia wewe mwana, nawe utamwita jina lake Isaki.17:19 Isaki maana yake Kucheka. Nitalithibitisha Agano langu naye kama Agano la milele kwa ajili yake na wazao wake baada yake. 2017:20 Mwa 13:16; 16:10; 25:12-18; 48:19Kwa upande wa Ishmaeli, nimekusikia: hakika nitambariki, nitamfanya awe na uzao mwingi na nitaongeza sana idadi yake. Atakuwa baba wa watawala kumi na wawili, nami nitamfanya awe taifa kubwa. 2117:21 Kut 34:10; Mwa 18:10-14; 21:2Lakini Agano langu nitalithibitisha kwa Isaki, ambaye Sara atakuzalia mwaka ujao majira kama haya.” 2217:22 Mwa 18:33; 35:13; Hes 12:9Wakati alipomaliza kuzungumza na Abrahamu, Mungu akapanda juu akaondoka kwa Abrahamu.

2317:23 Mwa 12:5Siku ile ile, Abrahamu akamchukua Ishmaeli mwanawe na wote waliozaliwa nyumbani mwake pamoja na walionunuliwa kwa fedha zake, kila mwanaume wa nyumbani mwake, akawatahiri, kama Mungu alivyomwagiza. 2417:24 Mwa 12:4; Rum 4:11Abrahamu alikuwa na umri wa miaka tisini na tisa alipotahiriwa, 2517:25 Mwa 16:16naye Ishmaeli mwanawe alitahiriwa akiwa na umri wa miaka kumi na mitatu. 26Abrahamu na Ishmaeli mwanawe walitahiriwa siku ile ile, 2717:27 Mwa 14:14Kila mwanaume nyumbani mwa Abrahamu, pamoja na wote waliozaliwa nyumbani mwake au aliyenunuliwa kwa fedha kutoka kwa mgeni, alitahiriwa pamoja naye.