马可福音 7 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

马可福音 7:1-37

传统与诫命

1有法利赛人和一些律法教师从耶路撒冷来见耶稣。 2他们看到祂的门徒有些吃饭前没有照礼仪洗手。 3因为法利赛人和所有的犹太人都拘守祖先的传统,总是先照礼仪洗手之后才吃饭; 4从市场回来也要先洁净自己,然后才吃饭。他们还拘守许多其他规矩,如洗杯、罐、铜器等。

5他们质问耶稣:“为什么你的门徒违背祖先的传统,竟用不洁净的手吃饭呢?”

6耶稣回答说:“以赛亚先知针对你们这些伪君子所说的预言一点不错,正如圣经上说,

“‘这些人嘴上尊崇我,

心却远离我。

7他们的教导无非是人的规条,

他们敬拜我也是枉然。’

8你们只知拘守人的传统,却无视上帝的诫命。” 9耶稣又对他们说:“你们为了拘守自己的传统,竟巧妙地废除了上帝的诫命。 10摩西说,‘要孝敬父母’,又说,‘咒骂父母的,必被处死。’ 11你们却认为人若对父母说,‘我把供养你们的钱财已经全部奉献给上帝了’, 12他就可以不奉养父母。 13你们就是这样为了拘守传统而废除上帝的道,类似的情形还有很多。”

内心的污秽

14耶稣又召集众人,教导他们说:“我的话,你们要听明白, 15从外面进去的不会使人污秽,只有从人里面发出来的才会使人污秽。 16有耳可听的,都应当听!”

17耶稣离开众人,进了屋子,门徒问祂这比喻的意思。 18耶稣说:“你们也不明白吗?你们不知道吗?从外面进去的,不会使人污秽, 19因为不能进入他的心,只能进他的肠胃,最后会排出来,也就是说所有的食物都是洁净的。 20从人里面发出来的才使人污秽, 21因为从里面,就是从人的心里能够生出恶念、苟合、偷盗、谋杀、 22通奸、贪婪、邪恶、诡诈、放荡、嫉妒、毁谤、骄傲、狂妄。 23这一切恶事都是从里面生出来的,能使人污秽。”

外族妇人的信心

24耶稣从那里启程去泰尔西顿地区。祂进了一户人家,原本不想让人知道,却无法避开人们的注意。 25-26当时有一个妇人的小女儿被污鬼附身,她听见耶稣的事,就来俯伏在祂脚前,恳求祂赶出她女儿身上的鬼。这妇人是希腊人,来自叙利亚腓尼基

27耶稣对她说:“要先让儿女们吃饱,因为把儿女的食物丢给狗吃不合适。”

28妇人说:“主啊,你说的对,但桌子下的狗也吃孩子们掉下来的碎渣呀!”

29耶稣说:“因为你这句话,你回去吧,鬼已经离开你的女儿了。”

30她回到家里,见女儿躺在床上,鬼已经离开了。

医治聋哑的人

31耶稣离开泰尔地区,经过西顿,来到低加坡里地区的加利利湖。 32有人带着一个又聋又哑的人来见耶稣,恳求祂把手按在这个人身上。 33耶稣就带他离开众人走到一边,用指头伸进他的耳朵,又吐唾沫抹他的舌头, 34望天长叹,对他说:“以法大!”意思是“开了吧!” 35他的耳朵立刻开了,舌头灵活了,说话也清楚了。 36耶稣吩咐他们不要将这事告诉人。可是耶稣越是这样吩咐,他们越是极力宣扬, 37听见的人都十分惊奇,说:“祂做的事好极了,甚至叫聋子听见,哑巴说话!”

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Marko 7:1-37

Kilicho Safi Na Kilicho Najisi

(Mathayo 15:1-20)

17:1 Mt 15:1Mafarisayo na baadhi ya walimu wa sheria waliokuwa wametoka Yerusalemu wakakusanyika mbele ya Yesu. 27:2 Mdo 11:8; Rum 14:14Wakawaona baadhi ya wanafunzi wake wakila chakula kwa mikono iliyo najisi, yaani, bila kunawa kama ilivyotakiwa na sheria ya dini ya Wayahudi. 37:3 Mk 7:5-13; Lk 11:38-39(Kwa kuwa Mafarisayo na Wayahudi wote hawali chakula pasipo kunawa kwa kufuata desturi za wazee wao. 47:4 Mt 23:25Wanapotoka sokoni hawawezi kula pasipo kunawa. Pia kuna desturi nyingine nyingi wanazofuata kama vile jinsi ya kuosha vikombe, vyungu na vyombo vya shaba.)

57:5 Gal 1:14; Kol 2:8Kwa hiyo wale Mafarisayo na walimu wa sheria wakamuuliza Yesu, “Mbona wanafunzi wako hawafuati desturi za wazee, na badala yake wanakula kwa mikono najisi?”

67:6 Isa 29:13; Mt 15:8Yesu akawajibu, “Nabii Isaya alisema ukweli alipotabiri juu yenu, ninyi wanafiki. Kama ilivyoandikwa:

“ ‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao,

lakini mioyo yao iko mbali nami.

77:7 Isa 29:13Huniabudu bure,

nayo mafundisho yao ni maagizo ya wanadamu tu.’

87:8 Mk 7:3Ninyi mmeziacha amri za Mungu na kushika desturi za watu.”

97:9 Mk 7:3Naye akawaambia, “Ninyi mnayo njia nzuri ya kukataa amri za Mungu ili mpate kuyashika mapokeo yenu! 107:10 Kut 20:21; Kum 5:16; Kut 21:17; Law 20:9Kwa mfano, Mose alisema, ‘Waheshimu baba yako na mama yako,’ na, ‘Yeyote amtukanaye baba yake au mama yake, na auawe.’ 117:11 Mt 23:16-18Lakini ninyi mwafundisha kwamba mtu akimwambia baba yake au mama yake, ‘Kile ambacho ningeweza kukusaidia ni Korbani’ (yaani kimewekwa wakfu kwa Mungu), 12basi hawajibiki tena kumsaidia baba yake au mama yake. 137:13 Ebr 4:12; Mk 7:3Kwa njia hiyo ninyi mnabatilisha neno la Mungu kwa mapokeo yenu mliyojiwekea. Nanyi mnafanya mambo mengi ya aina hiyo.”

147:14 Mt 15:10Yesu akaita tena ule umati wa watu, akawaambia, “Nisikilizeni, kila mmoja wenu na mwelewe jambo hili. 157:15 Mdo 10:14, 15Hakuna kitu kinachomwingia mtu kimtiacho unajisi, lakini kile kimtokacho ndicho kimtiacho unajisi. [ 167:16 Mt 11:15Kama mtu yeyote ana masikio ya kusikia na asikie.]”

177:17 Mk 9:28Akiisha kuuacha ule umati wa watu na kuingia ndani, wanafunzi wake wakamuuliza maana ya mfano ule. 18Akawajibu, “Je, hata nanyi hamwelewi? Je, hamfahamu kwamba kitu kimwingiacho mtu hakimtii unajisi? 197:19 Kol 2:16; 1Tim 4:3-5; Mdo 10:15Mtu akila kitu hakiingii moyoni mwake bali tumboni, na baadaye hutolewa nje ya mwili wake.” (Kwa kusema hivi, Yesu alivihalalisha vyakula vyote kuwa ni “safi.”)

20Akaendelea kusema, “Kile kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi. 217:21 Mwa 6:5; 8:21; Mt 15:21-28Kwa maana kutoka ndani ya moyo wa mtu hutoka mawazo mabaya, uasherati, wizi, uuaji, uzinzi, 227:22 Mt 20:15tamaa mbaya, uovu, udanganyifu, ufisadi, wivu, matukano, kiburi na upumbavu. 23Maovu haya yote hutoka ndani ya mtu, nayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi.”

Imani Ya Mwanamke Msirofoinike

(Mathayo 15:21-28)

247:24 Mt 21:21Ndipo Yesu akaondoka hapo akaenda sehemu za Tiro. Akaingia katika nyumba moja, naye hakutaka mtu yeyote ajue kwamba yuko humo. Lakini hakuweza kujificha. 257:25 Mt 4:24Mara mwanamke mmoja, ambaye binti yake mdogo alikuwa na pepo mchafu, akaja na kumpigia magoti miguuni pake. 26Basi huyo mwanamke alikuwa Myunani, aliyezaliwa Foinike ya Siria.7:26 Kulikuwa na Foinike ya Siria (ndio Shamu) na Foinike ya Libya. Akamsihi Yesu amtoe binti yake huyo pepo mchafu.

27Yesu akamwambia, “Waache watoto washibe kwanza, kwa maana si vyema kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.”

28Lakini yule mwanamke akamjibu, “Bwana, hata mbwa walio chini ya meza hula makombo ya chakula cha watoto.”

29Ndipo Yesu akamjibu, “Kwa sababu ya jibu lako, nenda zako nyumbani; yule pepo mchafu amemtoka binti yako.”

30Akaenda zake nyumbani akamkuta binti yake amelala kitandani, yule pepo mchafu akiwa amemtoka.

Yesu Amponya Mtu Aliyekuwa Kiziwi Na Bubu

317:31 Mt 11:21; 4:18-25; Mk 5:20Kisha Yesu akaondoka sehemu za Tiro, akapita katikati ya Sidoni, hadi Bahari ya Galilaya na kuingia eneo la Dekapoli. 327:32 Mt 9:32; Lk 11:14; Mk 5:23Huko, watu wakamletea Yesu mtu mmoja kiziwi, ambaye pia alikuwa na kigugumizi, wakamwomba aweke mkono wake juu ya huyo mtu na amponye.

337:33 Mk 8:23Baadaye Yesu akampeleka yule kiziwi kando mbali na watu, Yesu akatia vidole vyake masikioni mwa yule mtu. Kisha akatema mate na kuugusa ulimi wa yule mtu. 347:34 Mk 6:41; Yn 11:41; Mk 8:12Ndipo Yesu akatazama mbinguni, akavuta hewa ndani kwa nguvu akamwambia, “Efatha!” (yaani, “Funguka!”) 357:35 Isa 35:5-6Mara masikio yake yakafunguka na ulimi wake ukaachiliwa, akaanza kuongea sawasawa.

367:36 Mt 8:4Yesu akawaamuru wasimwambie mtu yeyote habari hizi. Lakini kadiri alivyowazuia, ndivyo walivyozidi kutangaza kwa bidii. 377:37 Isa 35:5Walistaajabu mno. Wakasema, “Amefanya mambo yote vizuri mno! Amewawezesha viziwi wasikie na bubu waseme!”