雅歌 2 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

雅歌 2:1-17

女子:

1我是沙仑平原的玫瑰花,

是谷中的百合花。

男子:

2我的爱人在众少女中,

就像荆棘中的一朵百合花。

女子:

3我的良人在众男子中,

好像林中的一棵苹果树。

我欢欢喜喜地坐在他的树荫下,

轻尝他香甜可口的果子。

4他带我走进宴席大厅,

众人都看见他对我充满柔情爱意。

5请用葡萄干来补充我的力气,

用苹果来提振我的精神,

因为我思爱成病。

6他的左手扶着我的头,

他的右手紧抱着我。

7耶路撒冷的少女啊!

我指着羚羊和田野的母鹿2:7 “羚羊和田野的母鹿”在希伯来文中与“万军之全能上帝”发音相似。吩咐你们,

不要叫醒或惊动爱情,

等它自发吧。

8听啊!是我良人的声音,

他攀过高岗,跃过山丘,

终于来了!

9我的良人好像羚羊和幼鹿。

看啊,他就在墙外,

正从窗户往里观看,

从窗棂间往里凝视。

10他对我说:

“我的爱人,起来吧!

我的佳偶,跟我来!

11你看!冬天过去了,

雨水止住了。

12大地百花盛开,

百鸟争鸣的季节已经来临,

田野也传来斑鸠的叫声。

13无花果快成熟了,

葡萄树也开满了花,

散发着阵阵芬芳。

我的爱人,起来吧;

我的佳偶,跟我来。”

男子:

14我的鸽子啊,

你在岩穴中,

在悬崖的隐秘处。

让我看看你的脸,

听听你的声音吧,

因为你的声音温柔,

你的脸庞秀丽。

15为我们抓住狐狸,

抓住破坏葡萄园的小狐狸,

因为我们的葡萄树正在开花。

女子:

16我的良人属于我,我也属于他。

他在百合花间牧放羊群。

17我的良人啊,

凉风吹起、日影飞逝的时候,

但愿你快快回来,

就像比特山的羚羊和小鹿一样。

Kiswahili Contemporary Version

Wimbo 2:1-17

Mpendwa

12:1 1Nya 27:29; Hos 14:5; Wim 5:13; Isa 55:1Mimi ni ua la Sharoni,

yungiyungi ya bondeni.

Mpenzi

2Kama yungiyungi katikati ya miiba

ndivyo alivyo mpenzi wangu katikati ya wanawali.

Mpendwa

32:3 Mwa 3:6; Wim 1:4, 14; 4:16Kama mti wa mtofaa miongoni mwa miti ya msituni

ndivyo alivyo mpenzi wangu

miongoni mwa wanaume vijana.

Ninafurahia kuketi kivulini mwa mwanaume huyu,

na tunda lake ni tamu kwangu.

42:4 Es 1:11; Hes 1:52Amenichukua mpaka kwenye ukumbi wa karamu,

na bendera ya huyu mwanaume

juu yangu ni upendo.

52:5 Wim 7:8; 5:8Nitie nguvu kwa zabibu kavu,

niburudishe kwa matofaa,

kwa maana ninazimia kwa mapenzi.

62:6 Wim 8:3Mkono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu,

na mkono wake wa kuume unanikumbatia.

72:7 Wim 5:8; 3:5; 8:4Binti za Yerusalemu, ninawaagiza

kwa paa na kwa ayala wa shambani:

Msichochee wala kuamsha mapenzi

hata yatakapotaka yenyewe.

Shairi La Pili

Mpendwa

82:8 Wim 8:14Sikiliza! Mpenzi wangu!

Tazama! Huyu hapa anakuja,

akirukaruka juu milimani

akizunguka juu ya vilima.

92:9 2Sam 2:18; Wim 8:14Mpenzi wangu ni kama paa au ayala kijana.

Tazama! Anasimama nyuma ya ukuta wetu,

akitazama kupitia madirishani,

akichungulia kimiani.

10Mpenzi wangu alizungumza na kuniambia,

“Inuka, mpenzi wangu,

mrembo wangu, tufuatane.

11Tazama! Wakati wa masika umepita,

mvua imekwisha na ikapita.

12Maua yanatokea juu ya nchi;

majira ya kuimba yamewadia,

sauti za njiwa zinasikika

katika nchi yetu.

132:13 Nah 3:12; Wim 7:122:13 Mik 7:1; Isa 28:4; Yer 24:2; Hos 9:10Mtini unatunga matunda yake ya mwanzoni,

zabibu zinazochanua zaeneza harufu nzuri.

Inuka, njoo mpenzi wangu.

Mrembo wangu, tufuatane.”

Mpenzi

142:14 Wim 8:13; Mwa 8:8; Wim 1:15Hua wangu penye nyufa za majabali,

mafichoni pembezoni mwa mlima,

nionyeshe uso wako,

na niisikie sauti yako,

kwa maana sauti yako ni tamu,

na uso wako unapendeza.

152:15 Amu 15:4; Wim 7:12; Eze 13:4; Za 80:13Tukamatie mbweha,

mbweha wale wadogo

wanaoharibu mashamba ya mizabibu,

mashamba yetu ya mizabibu yaliyochanua.

Mpendwa

162:16 Wim 7:10; 4:5; 6:3Mpenzi wangu ni wangu, nami ni wake,

yeye hujilisha katikati ya yungiyungi.

172:17 Wim 4:6; 1:14; Rum 13:12Mpaka jua linapochomoza,

na vivuli vikimbie,

rudi, mpenzi wangu,

na uwe kama paa,

au kama ayala kijana

juu ya vilima vya Betheri.