耶利米书 52 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

耶利米书 52:1-34

犹大的灭亡

1西底迦二十一岁登基,在耶路撒冷执政十一年。他母亲叫哈慕她,是立拿耶利米的女儿。 2西底迦约雅敬一样做耶和华视为恶的事。 3因此,耶和华向耶路撒冷犹大的人发怒,最终把他们从祂面前赶走。

后来,西底迦背叛了巴比伦王。 4在他执政第九年十月十日,巴比伦尼布甲尼撒率领全军攻打耶路撒冷,在城外安营,修筑围城的高台。 5城一直被围困到西底迦王执政第十一年。 6那年四月九日,城里饥荒非常严重,百姓无粮可吃。 7城被攻破,西底迦和士兵便在夜间从靠近御花园的两城墙中间的门逃往亚拉巴。当时迦勒底人仍四面包围着城。 8迦勒底的军队追赶西底迦,在耶利哥平原追上了他。他的军队都四散而逃。 9迦勒底人擒住西底迦,把他押到哈马利比拉去见巴比伦王。巴比伦王在那里审判他, 10当着他的面杀了他的众子和犹大所有的官员, 11又剜去他的双眼,把他用铜链锁着押往巴比伦,将他终生囚在牢里。

12巴比伦尼布甲尼撒执政第十九年五月十日,他的臣仆护卫长尼布撒拉旦进入耶路撒冷13放火焚烧耶和华的殿、王宫及耶路撒冷所有的房屋。他烧毁了所有重要建筑。 14他率领的迦勒底军队拆毁了耶路撒冷四围的城墙。 15护卫长尼布撒拉旦掳去最贫穷的人、城中的余民、那些投降巴比伦王的人和剩下的技工, 16只留下一些最贫穷的人,让他们照料葡萄园、耕种田地。

17迦勒底人打碎耶和华殿中的铜柱、铜底座和铜海,把铜运往巴比伦18并带走了盆、铲、灯剪、碗、碟及一切献祭用的铜器。 19护卫长还带走了杯、火鼎、碗、盆、灯台、碟和奠酒的杯等所有金银器皿。 20所罗门王为耶和华的殿所造的两根铜柱、一个铜海、铜海下面的十二头铜牛,以及一些铜底座,用的铜多得无法计算。 21两根铜柱中空,高八米,周长五米四,铜壁厚四指。 22铜柱有柱冠,柱冠高两米二,柱冠周围装饰着铜网和铜石榴。两根柱子都一样。 23每根铜柱周围装饰着九十六个石榴,网子四周共有一百个石榴。

24护卫长掳走祭司长西莱雅、副祭司长西番亚和三名殿门守卫, 25又从城中掳走一名统管士兵的将领、王的七个亲信、一名负责招兵的书记和城中找到的六十名平民, 26把他们带到利比拉去见巴比伦王。 27巴比伦王在哈马地区的利比拉处死了他们。犹大人就这样被掳去,离开了家园。

28以下是尼布甲尼撒掳去的人数:他执政第七年掳去三千零二十三名犹大人; 29他执政第十八年,从耶路撒冷掳去八百三十二人; 30他执政第二十三年,他的护卫长尼布撒拉旦掳去七百四十五名犹大人。总共四千六百人。

31犹大约雅斤被掳后第三十七年,即巴比伦以未·米罗达元年十二月二十五日,巴比伦王恩待约雅斤,释放了他, 32并好言相待,使他的地位高过被掳到巴比伦的其他各王。 33约雅斤脱去了囚服,终生与巴比伦王一起吃饭。 34在他有生之年,巴比伦王供应他每天的需用,直到他去世。

Kiswahili Contemporary Version

Yeremia 52:1-34

Anguko La Yerusalemu

(2 Wafalme 24:18–25:30)

152:1 2Fal 24:17-18; Yos 10:29; Hes 33:20; 2Fal 8:22Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna. 252:2 Yer 36:30Alifanya maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Yehoyakimu. 352:3 Eze 17:12-16; Kut 33:15; Mwa 4:14Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira ya Bwana haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake.

Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.

452:4 Zek 8:19; 2Fal 25:1-7; Yer 34:1; Eze 24:1-2; Kum 28:52-57Hivyo katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli akiwa na jeshi lake lote alifanya vita dhidi ya Yerusalemu. Wakapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote. 5Mji ulizungukwa na jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Mfalme Sedekia.

652:6 Law 26:26; Mao 1:11; Eze 4:16Ilipowadia siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ikazidi kuwa kali sana ndani ya mji, hadi hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu. 752:7 Mao 4:19Kisha ukuta wa mji ukavunjwa na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Wakakimbia kuelekea Araba. 8Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia Mfalme Sedekia na kumpata katika sehemu tambarare za Yeriko. Askari wake wote wakatengwa naye na kutawanyika, 952:9 Yer 21:7; 32:4; Hes 34:11; 13:21naye akakamatwa.

Akapelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu. 1052:10 Yer 22:30; 39:6-7Huko Ribla mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake. Pia akawaua maafisa wote wa Yuda. 1152:11 Eze 12:13; 17:16; Yer 34:4Kisha akayangʼoa macho ya Sedekia, akamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli, alipomweka gerezani mpaka siku ya kifo chake.

1252:12 Zek 8:19; Yer 39:9; Zek 7:5Mnamo siku ya kumi ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, aliyemtumikia mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu. 1352:13 2Nya 36:19; Kum 29:24; Mik 3:12; Za 74:8; Yer 19:13; Kum 13:16; Mao 2:6Alichoma moto Hekalu la Bwana, jumba la kifalme, na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu. 14Jeshi lote la Wakaldayo chini ya jemadari wa askari walinzi wa mfalme walivunja kuta zote zilizoizunguka Yerusalemu. 1552:15 2Fal 24:1; Yer 38:19; 1:3Nebuzaradani, jemadari wa askari walinzi, akawapeleka uhamishoni baadhi ya watu maskini sana na wale waliobaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa kawaida, na wale waliojisalimisha kwa mfalme wa Babeli. 16Lakini Nebuzaradani akawaacha mabaki ya wale watu maskini kabisa ili watunze mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.

1752:17 1Fal 7:15, 27-37; Yer 27:19-22Wakaldayo walivunja vipande zile nguzo za shaba, vile vishikilio vya shaba vilivyohamishika, na ile Bahari ya shaba, ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu la Bwana. Hivyo wakaichukua hiyo shaba yote na kuipeleka Babeli. 1852:18 Kut 27:3; 1Fal 7:45; Hes 4:14Wakachukua pia vyungu, masepetu, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, sahani na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika katika huduma ya Hekalu. 1952:19 Law 10:1; 1Fal 7:50; Hes 3:31; Kut 25:29; Hes 4:7; Dan 5:2; Ezr 1:7Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua yale masinia, vile vyetezo, yale mabakuli ya kunyunyizia, zile sufuria, vile vinara vya taa, zile sahani na yale mabakuli yaliyotumika kwa sadaka za vinywaji, vitu vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.

2052:20 1Fal 7:25, 47Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na wale mafahali kumi na mawili wa shaba waliokuwa chini yake, pamoja na vile vishikilio vilivyohamishika, ambavyo Mfalme Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana, ilikuwa na uzito usioweza kupimika. 21Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane, kimo chake na mzunguko dhiraa kumi na mbili, na unene wa nyanda nne, na zote zilikuwa wazi ndani. 2252:22 1Fal 7:15-16, 20, 47; Kut 28:33Sehemu ya shaba juu ya ile nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tano, na ilikuwa imepambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Ile nguzo nyingine pamoja na makomamanga yake ilifanana na hiyo ya kwanza. 23Kulikuwa na makomamanga tisini na sita pembeni; jumla ya makomamanga juu ya wavu uliokuwa umezunguka yalikuwa mia moja.

2452:24 2Fal 25:18; Yer 37:3; 21:1; 2Fal 12:9Yule jemadari wa askari walinzi akawachukua kama wafungwa Seraya kuhani mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo, na mabawabu watatu. 2552:25 Yer 36:10Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji, na washauri saba wa mfalme. Akamchukua pia mwandishi aliyesimamia uandikishaji wa watu wa nchi, pamoja na watu wake sitini waliopatikana ndani ya mji. 26Nebuzaradani jemadari akawachukua hao wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla. 2752:27 Yer 20:4; Law 26:33; Hes 34:11Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme wa Babeli akaamuru wanyongwe.

Hivyo Yuda wakaenda utumwani, mbali na nchi yao. 2852:28 2Fal 24:14-16; Neh 1:2; 2Nya 36:20; Kum 28:36Hii ndiyo hesabu ya watu ambao Nebukadneza aliwachukua kwenda uhamishoni:

katika mwaka wa saba,

Wayahudi 3,023;

29katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Nebukadneza,

watu 832 kutoka Yerusalemu;

3052:30 Yer 43:3; 13:19katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake,

Wayahudi 745 walichukuliwa kwenda uhamishoni na Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme.

Jumla ya watu wote walikuwa 4,600.

Yehoyakini Anaachiwa Huru

3152:31 2Fal 25:27-30; Mwa 40:13-20Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, katika mwaka ule ambao Evil-Merodaki52:31 Pia aliitwa Ameli-Mariduki. alifanyika mfalme wa Babeli, alimwacha huru Yehoyakini mfalme wa Yuda, na kumfungua kutoka gerezani siku ya ishirini na tano ya mwezi wa kumi na mbili. 32Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima zaidi kuliko wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli. 3352:33 2Sam 9:7, 13Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya mfungwa, na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula mezani mwa mfalme. 3452:34 2Sam 9:10Siku kwa siku mfalme wa Babeli alimpa Yehoyakini posho siku zote za maisha yake, hadi siku ya kifo chake.