约书亚记 5 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

约书亚记 5:1-15

在吉甲行割礼

1约旦河西岸一带的亚摩利众王和沿海一带的迦南众王,听说耶和华使约旦河成为干地、让以色列人穿过,都吓得胆战心惊,勇气尽失。

2那时,耶和华对约书亚说:“你要制作火石刀,再次给以色列人行割礼。” 3约书亚便制作火石刀,在割礼山给以色列人行了割礼。 4约书亚给他们举行割礼,是因为所有从埃及出来、能够作战的男子之后都死在旷野的路上。 5埃及出来的男子都受过割礼,而后来在旷野的路上出生的以色列人都没有受过割礼。 6以色列人在旷野飘泊了四十年,直到从埃及出来可以作战的男子都死了为止,因为他们不听从耶和华的话。耶和华曾向他们祖先起誓,要把奶蜜之乡赐给他们,但后来祂向他们起誓,不让他们看见那片土地。 7耶和华立他们的子孙代替他们。这些人没有受过割礼,因为在路上没有为他们行过割礼,约书亚就为他们行了割礼。

8全体民众受了割礼后,都留在自己的营内,直到康复为止。 9耶和华对约书亚说:“今天我除去了你们在埃及受的羞辱。”因此,那地方叫吉甲5:9 “吉甲”意思是“除去”。,沿用至今。

在迦南守逾越节

10以色列人都在耶利哥平原上的吉甲扎营,并于一月十四日傍晚在那里守逾越节。 11逾越节次日他们就吃当地的出产,包括无酵饼和烤麦穗。 12他们吃了当地出产后的第二天,吗哪便不再降下,以色列人再没有吗哪吃了。那一年他们开始吃迦南的出产。

耶和华军队的元帅

13约书亚走近耶利哥,举目看见一个人站在他面前,手里拿着拔出来的剑。约书亚上前去问道:“你是来帮助我们的,还是来帮助我们敌人的?” 14那人答道:“都不是,我来是做耶和华军队的统帅。”约书亚就俯伏下拜说:“我主,有什么话要吩咐仆人?” 15耶和华军队的统帅对约书亚说:“把你脚上的鞋脱下!因为你站的地方是圣洁的。”约书亚便把鞋脱下来。

Kiswahili Contemporary Version

Yoshua 5:1-15

15:1 Kut 4:25; Hes 13:29; Mwa 42:28; Yos 2:9-11; Kut 15:14; Za 48:6; Eze 21:7; 1Fal 10:5Basi wafalme wote wa Waamori magharibi ya Yordani na wafalme wote wa Kanaani waliokuwa kwenye pwani waliposikia jinsi Bwana alivyoukausha Mto Yordani mbele ya Waisraeli hata tulipokwisha kuvuka, mioyo yao ikayeyuka kwa hofu, wala hawakuwa na ujasiri kuwakabili Waisraeli.

Tohara Huko Gilgali

25:2 Kut 4:25; Mwa 17:10-14Wakati huo Bwana akamwambia Yoshua, “Tengeneza visu vya mawe magumu sana na uwatahiri Waisraeli tena.” 3Kwa hiyo Yoshua akatengeneza visu vya mawe magumu sana na kutahiri Waisraeli huko Gibeath-Haaralothi.5:3 Gibeath-Haaralothi maana yake ni Kilima cha Magovi.

45:4 Hes 1:3; Kum 2:14, 16; Hes 14:29; 26:64Hii ndiyo sababu ya Yoshua kufanya hivyo: Wanaume wote waliotoka Misri, wote wenye umri wa kwenda vitani, walikufa jangwani wakiwa njiani baada ya kuondoka Misri. 5Watu wote waliotoka Misri walikuwa wametahiriwa, lakini watu wote waliozaliwa jangwani wakiwa safarini toka Misri walikuwa hawajatahiriwa. 65:6 Hes 32:13; Yos 14:10; Za 107:4; Kut 16:35; Hes 14:23-35; Kum 2:14; Kut 3:8Waisraeli walitembea jangwani miaka arobaini mpaka wanaume wote wale waliokuwa na umri wa kwenda vitani wakati waliondoka Misri walipokwisha kufa, kwa kuwa hawakumtii Bwana. Kwa maana Bwana alikuwa amewaapia kuwa wasingeweza kuona nchi ambayo alikuwa amewaahidi baba zao katika kuapa kutupatia, nchi inayotiririka maziwa na asali. 75:7 Hes 14:31Kwa hiyo akawainua wana wao baada yao na hawa ndio hao ambao Yoshua aliwatahiri. Walikuwa hawajatahiriwa bado kwa sababu walikuwa safarini. 85:8 Mwa 34:25Baada ya taifa lote kutahiriwa, waliendelea kukaa kambini mpaka walipokuwa wamepona.

95:9 Kum 11:30; 1Sam 14:6; Law 18:3; Yos 24:14; Eze 20:7Bwana akamwambia Yoshua, “Leo nimeiondoa aibu ya Wamisri kutoka kwenu.” Basi mahali pale pakaitwa Gilgali hadi leo.

105:10 Kut 12:6; 12:11Jioni ya siku ya kumi na nne ya mwezi, wakiwa kambini huko Gilgali katika tambarare za Yeriko, Waisraeli wakaadhimisha Pasaka. 115:11 Hes 15:19; Kut 12:15; Law 23:14; Hes 9:5Siku iliyofuata Pasaka, katika siku ile ile, wakala mazao ya nchi, mikate isiyotiwa chachu na nafaka za kukaanga. 125:12 Kut 16:35Mana ilikoma siku iliyofuata baada ya Waisraeli kula chakula kilichotoka katika nchi; hapakuwa na mana tena kwa ajili ya Waisraeli, ila mwaka huo walikula mazao ya nchi ya Kanaani.

Jemadari Wa Jeshi La Bwana

135:13 Mwa 18:2; Hes 22:23; Mwa 32:24; Kut 23:23; Mdo 1:10; Zek 1:8Basi wakati Yoshua alipokuwa karibu na Yeriko, akainua macho, akaona mtu aliyesimama mbele yake, akiwa na upanga mkononi uliofutwa kwenye ala. Yoshua akamwendea na kumuuliza, “Je, wewe uko upande wetu au upande wa adui zetu?”

145:14 Mwa 17:3; 19:1; Dan 10:13; Ufu 2:17; Law 9:24; Hes 16:22Akajibu, “La, siko upande wowote, lakini mimi nimekuja nikiwa jemadari wa jeshi la Bwana.” Yoshua akaanguka kifudifudi hadi chini, akasujudu, akamuuliza, “Je, Bwana, una ujumbe gani kwa mtumishi wako?” 155:15 Mwa 28:17; Kut 3:5; Mdo 7:33; Kut 19:10-13; Za 22:3; 29:2; Isa 6:3; 1Nya 26:25-29; 1Sam 2:2Jemadari wa jeshi la Bwana akajibu, “Vua viatu vyako, kwa maana mahali hapa unaposimama ni patakatifu.” Naye Yoshua akafanya hivyo.