约书亚记 10 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

约书亚记 10:1-43

太阳停止

1耶路撒冷亚多尼·洗德听说约书亚夺取并毁灭了城,像对付耶利哥耶利哥王一样对付城和城的王,又听说基遍人已经跟以色列人缔结盟约,住在他们中间, 2便大为惊恐。因为基遍是一座大城,宏伟得像座都城,比城更大,城中的人都骁勇善战。 3耶路撒冷亚多尼·洗德便派遣使者去见希伯仑何咸耶末毗兰拉吉雅非亚伊矶伦底璧,说: 4“求你们上来帮助我攻打基遍,因为这城已经与约书亚以色列人缔结盟约。” 5于是,五位亚摩利王,就是耶路撒冷王、希伯仑王、耶末王、拉吉王和伊矶伦王,便联合起来,率领他们所有的军队在基遍附近扎营,攻打基遍

6基遍人派人去吉甲告诉约书亚说:“住在山区的亚摩利众王正联合起来攻打我们,求你赶快来救我们!不要不顾你的仆人。” 7于是,约书亚便率领全军,包括所有精兵,从吉甲上去。 8耶和华对约书亚说:“不要害怕,我已经把他们交在你手中,他们没有一人能抵挡你。” 9约书亚吉甲出发,连夜赶路,突袭敌人。 10耶和华使亚摩利联军阵脚大乱,以色列人就在基遍大败敌军,在去伯·和仑的上坡路上追杀他们,一直追到亚西加玛基大11敌人在从伯·和仑亚西加的下坡路上逃窜的时候,耶和华降下大冰雹,被冰雹砸死的人比以色列人用刀杀死的还要多。

12耶和华将亚摩利人交在以色列人手中,那天约书亚当众向耶和华祷告:

“太阳啊,停在基遍

月亮啊,停在亚雅仑谷!”

13果然太阳停住了,

月亮也不动了,

直到以色列人杀败敌人。

《雅煞珥书》记载了这事。约有一天的时间,太阳停留在天空,没有西沉。 14耶和华这样垂听一个人的祈求是空前绝后的,这是因为耶和华要为以色列争战。

15后来,约书亚率领以色列军返回了吉甲的营地。

亚摩利五王被杀

16那五王逃进玛基大的山洞里,躲藏起来。 17有人告诉约书亚那五个王藏在玛基大的山洞里, 18约书亚便下令说:“滚几块大石头堵住洞口,派人看守。 19你们不可停下来,要继续追杀敌人,不要让他们逃回城,你们的上帝耶和华已经把他们交在你们手中了。” 20约书亚以色列人把敌人杀得大败,几乎全军覆没,一些残余都逃进了坚固的城垒。 21以色列人都安然无恙地回到约书亚驻扎的玛基大营。再也没有人敢威胁以色列人了。

22约书亚说:“打开洞口,把里面的五个王押出来见我。” 23众人便把耶路撒冷王、希伯仑王、耶末王、拉吉王、伊矶伦王从洞里押出来,带到约书亚面前。 24约书亚召来全体以色列人,然后对那些跟他一起出征的将领说:“你们上前来,用脚踏在这些王的脖子上。”各将领便照着约书亚的吩咐做了。 25约书亚对他们说:“你们不要惊慌害怕,要刚强勇敢,因为耶和华要使你们攻打的所有仇敌都落此下场。” 26随后约书亚将这五个王杀死,把尸体分别挂在五棵树上,直到傍晚。 27日落时,约书亚才下令把尸体放下,扔在他们先前躲藏的山洞里,用大石头堵住洞口,石头至今还在那里。

28约书亚在当天占领了玛基大,把玛基大王和所有的居民都用刀杀了,一个没留。他对待玛基大王跟以前对待耶利哥王一样。

29约书亚以色列军又从玛基大出发,去攻打立拿30耶和华将立拿城和立拿王交在以色列人手中,他们用刀杀了全城的人,一个没留。他们对待立拿王跟以前对待耶利哥王一样。

31约书亚以色列军从立拿前往拉吉,他们在城外扎营,攻打拉吉32耶和华将拉吉交在以色列人手中,第二天约书亚便攻占了拉吉,用刀杀了全城的人,就像在立拿所行的一样。 33基色何兰前来支持拉吉,结果也被约书亚杀得一个不剩。

34约书亚又率领以色列全军从拉吉前往伊矶伦,在城外扎营,攻打伊矶伦35他们当天就攻陷该城,用刀杀了城内所有的人,就像在拉吉所行的一样。

36约书亚和全体以色列人又从伊矶伦去攻打希伯仑37他们攻陷该城及其附属城邑,用刀杀了希伯仑王和城邑中的居民,一个没留,就像在伊矶伦所行的一样。

38然后,约书亚和全体以色列人再回兵攻打底璧39攻取了该城及其附属城邑,擒获底璧王,用刀杀了城中所有的人,一个没留,就像对待希伯仑立拿立拿王一样。

40这样,约书亚征服了整个地区,包括山区、南地、丘陵和山坡及那里的众王。他按照以色列的上帝耶和华的吩咐,消灭了一切有生命气息的,一个没留。 41约书亚征服了各地,从加低斯·巴尼亚迦萨歌珊全境,直到基遍42约书亚能一鼓作气杀败诸王,征服他们的土地,都是因为有以色列的上帝耶和华为以色列人争战。 43之后,约书亚率领以色列人回到吉甲的营地。

Kiswahili Contemporary Version

Yoshua 10:1-43

Jua Linasimama

110:1 Yos 12:10; 15:8, 63; 18:28; Amu 1:7; Yos 8:1; Kum 20:16; Yos 8:22; 9:3, 15Baada ya haya Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu alisikia kuwa Yoshua alikuwa ameteka mji wa Ai na kuuangamiza kabisa, tena alikuwa ameua mfalme wake, kama alivyofanya huko Yeriko na mfalme wake, tena ya kuwa watu wa Gibeoni walikuwa wamefanya mapatano ya amani na Waisraeli, na walikuwa wakiishi karibu yao. 210:2 Kut 15:14-16; Kum 11:25; 28:10; Za 48:4-6; Mit 1:26, 27; Ebr 10:27, 31; Ufu 6:15-17Yeye na watu wake wakataharuki mno kwa kuwa Gibeoni ulikuwa mji mkubwa kama mmojawapo ya miji ya kifalme; ulikuwa mkubwa kuliko Ai, nao watu wake wote walikuwa mashujaa wa vita. 310:3 Mwa 13:18; Yos 12:11; 15:35; 21:29; Neh 11:29; Yos 12:11; 15:39; 2Fal 14:19; 2Nya 11:9; 25:27; 32:9; Neh 11:30; Isa 32:6; 37:8; Yer 34:7; Mik 1:13Hivyo Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu akaomba msaada kwa Hohamu mfalme wa Hebroni, Piramu mfalme wa Yarmuthi, Yafia mfalme wa Lakishi, na Debiri mfalme wa Egloni. 410:4 Yos 9:15Akawaambia, “Njooni mnisaidie kuipiga Gibeoni, kwa sababu imefanya mapatano ya amani na Yoshua na Waisraeli.”

510:5 Hes 13:29; Kum 1:7; Yos 9:2Ndipo hao wafalme watano wa Waamori, ambao ni wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni, wakaunganisha majeshi yao. Wakapanda na vikosi vyao vyote, nao wakajipanga dhidi ya Gibeoni na kuishambulia.

610:6 Kum 11:30Nao Wagibeoni wakatuma ujumbe kwa Yoshua kwenye kambi ya Gilgali na kumwambia, “Usiwatelekeze watumishi wako. Panda haraka uje kwetu kutuokoa! Tusaidie, kwa sababu wafalme wote wa Waamori wakaao kwenye nchi ya vilima wameunganisha majeshi yao pamoja dhidi yetu.”

710:7 Yos 8:1Basi Yoshua akaondoka Gilgali pamoja na jeshi lake lote, wakiwepo watu wote mashujaa wa vita. 810:8 Kum 3:2; Yos 1:9; 2:24; Kum 7:24; 7:24; 11:25; Yos 11:6; 23:9; Amu 4:14Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope watu hao, nimewatia mkononi mwako. Hakuna yeyote atakayeweza kushindana nawe.”

9Baada ya Yoshua kutembea usiku kucha kutoka Gilgali, akawashambulia ghafula. 1010:10 Kut 14:24; Kum 7:23; Yos 9:3; 16:3-5; 18:13-14; 21:22; 1Fal 9:17; 1Nya 6:68; 7:24; 2Nya 8:5; 25:13; Yos 15:35; 1Sam 17:1; 2Nya 11:9; Neh 11:30; Yer 34:7; Yos 12:16; 15:41Bwana akawafadhaisha mbele ya Waisraeli, nao wakawashinda kwa ushindi mkuu huko Gibeoni. Israeli wakawafukuza kuelekea njia iendayo Beth-Horoni wakiwaua mpaka kufikia njia iendayo Azeka na Makeda. 1110:11 Kut 9:18; Za 18:12; Isa 28:2; 17; 32:19; Eze 13:11; Amu 5:20Walipokuwa wakikimbia mbele ya Israeli kwenye barabara iteremkayo kutoka Beth-Horoni hadi Azeka, Bwana akawavumishia mawe makubwa ya mvua kutoka mbinguni, na wengi wao wakauawa na hayo mawe kuliko wale waliouawa kwa upanga wa Waisraeli.

1210:12 Amo 2:9; Yos 19:42; 21:24; Amu 1:35; 12:12; 1Sam 14:31; 1Nya 6:69; 8:13; 2Nya 11:10; 28:18Katika siku ile ambayo Bwana aliwapeana Waamori kwa Israeli, Yoshua akanena na Bwana akiwa mbele ya Waisraeli akasema:

“Wewe jua, simama juu ya Gibeoni,

wewe mwezi, tulia juu ya Bonde la Aiyaloni.”

1310:13 Hab 3:11; 2Sam 1:18; Isa 38:8Hivyo jua likasimama,

nao mwezi ukatulia,

hadi taifa hilo lilipokwisha

kujilipizia kisasi kwa adui wake,

kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Yashari.

Jua likasimama kimya katikati ya mbingu, likachelewa kuzama muda wa siku moja nzima. 1410:14 Yos 10:42; Kut 14:14; Za 106:43; 136:24; Isa 63:10; Yer 21:5; Isa 38:8; Kum 1:30; 3:22; 20:4; 33:29; Amu 1:19, 22; 2Nya 20:29; Neh 4:20; Isa 31:4; Zek 12:3Haijakuwepo siku nyingine kama hiyo kabla au baada, siku ambayo Bwana alimsikiliza mwanadamu. Hakika Bwana alikuwa akiwapigania Israeli.

15Ndipo Yoshua akarudi kambini huko Gilgali pamoja na Israeli yote.

Wafalme Watano Wa Waamori Wauawa

1610:16 Za 68:12Basi wale wafalme watano wakawa wamekimbia kujificha kwenye pango huko Makeda. 17Yoshua alipoambiwa kuwa wafalme hao watano wamekutwa wakiwa wamejificha ndani ya pango huko Makeda, 18akasema, “Vingirisheni mawe makubwa kwenye mdomo wa hilo pango, tena wekeni walinzi wa kulilinda. 19Lakini msiwaache! Wafuatieni adui zenu, washambulieni kutoka nyuma, wala msiwaache wafike kwenye miji yao, kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewatia mkononi mwenu.”

2010:20 Kum 20:16; 2Nya 11:10; Yer 4:5; 5:17; 8:14; 35:11Hivyo Yoshua pamoja na Waisraeli wakawaangamiza kabisa karibu wote, lakini wachache waliosalia walifika kwenye miji yao yenye maboma. 21Basi jeshi lote likarudi salama kwa Yoshua huko kambini Makeda, na hakuna yeyote aliyetoa neno kinyume cha Waisraeli.

22Ndipo Yoshua akasema, “Haya fungueni mdomo wa pango, mniletee hao wafalme watano.” 23Kwa hiyo wakawatoa hao wafalme watano nje ya pango: wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni. 2410:24 Kum 7:24; Mal 4:3; 2Sam 22:40; Za 110:1; Isa 51:23Walipokuwa wamewaleta hawa wafalme kwa Yoshua, akawaita watu wote wa Israeli, na kuwaambia majemadari wa vita waliokwenda pamoja naye, “Njooni hapa mweke nyayo zenu juu ya shingo za hawa wafalme.” Basi wakaja wakaweka nyayo zao shingoni.

2510:25 Kum 31:6; 1Sam 17:37; Za 63:9; 2Tim 4:17; Kum 3:21; 7:19Yoshua akawaambia, “Msiogope, wala msivunjike moyo. Kuweni hodari na wenye ushujaa. Hili ndilo Bwana atakalowatendea adui zenu wote mnaokwenda kupigana nao.” 2610:26 Hes 25:14; Yos 8:29; 2Sam 21:6-9; Es 2:23; Za 149:7-9Ndipo Yoshua akawapiga na kuwaua wale wafalme na kuwatundika juu ya miti mitano, nao wakaachwa wakiningʼinia juu ya ile miti hadi jioni.

2710:27 Kum 21:23; Mwa 35:20; Yos 8:9, 29Wakati wa kuzama jua Yoshua akaamuru, nao wakawashusha kutoka kwenye ile miti na kuwatupa kwenye lile pango ambalo walikuwa wamejificha. Kwenye mdomo wa lile pango wakaweka mawe makubwa, ambayo yapo hadi leo.

2810:28 Kum 20:16; Yos 6:21Siku ile Yoshua akateka Makeda. Akamuua kila mmoja katika ule mji, pamoja na mfalme wake kwa upanga. Hakubakiza mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Makeda kama vile alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.

Israeli Yaangamiza Miji Ya Kusini

2910:29 Hes 33:20; Yos 15:42; 21:13; 2Fal 8:22; 19:8Ndipo Yoshua akaondoka Makeda akiwa pamoja na Israeli yote mpaka mji wa Libna na kuushambulia. 30Bwana pia akautia huo mji wa Libna pamoja na mfalme wake mikononi mwa Israeli. Yoshua akaangamiza ule mji na kila mtu aliyekuwa ndani yake kwa upanga. Hakubakiza huko mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Libna kama alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.

3110:31 2Fal 14:19; Mik 1:13Kisha Yoshua akaondoka Libna kwenda Lakishi akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia. 32Bwana akautia Lakishi mikononi mwa Israeli, Yoshua akauteka siku ya pili. Yoshua akauangamiza mji na kila kilichokuwa ndani yake kwa upanga, kama tu vile alivyokuwa ameufanyia mji wa Libna. 3310:33 Yos 12:12; 16:3, 10; 21:21; Amu 1:29; 2Sam 5:25; 1Fal 9:15; 1Nya 6:67Wakati huo huo, Horamu mfalme wa Gezeri alikuwa amepanda ili kusaidia Lakishi, lakini Yoshua akamshinda pamoja na jeshi lake, hadi hapakubakia mtu yeyote.

34Ndipo Yoshua akaondoka Lakishi kwenda Egloni akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia. 3510:35 Hes 13:22; Amu 1:10; 2Sam 5:14Wakauteka mji huo siku ile ile, wakaupiga kwa upanga na kumwangamiza kila mmoja aliyekuwa ndani yake, kama vile walivyokuwa wameufanyia Lakishi.

3610:36 Mwa 13:18; Yos 14:13; 15:13; 20:7; 21:11; Amu 16:3Kisha Yoshua akapanda kutoka Egloni kwenda Hebroni akiwa pamoja na Israeli yote na kuushambulia. 37Wakauteka mji na kuupiga kwa upanga, pamoja na mfalme wake, vijiji vyake na kila mmoja aliyekuwa ndani yake. Hawakubakiza mtu yeyote. Kama vile huko Egloni, waliuangamiza kabisa pamoja na kila mmoja aliyekuwa ndani yake.

3810:38 Yos 15:15; Amu 1:11Ndipo Yoshua na Israeli wote wakageuka na kuushambulia Debiri. 39Wakauteka mji, mfalme wake na vijiji vyake, na kuupiga kwa upanga. Kila mmoja aliyekuwa ndani yake wakamwangamiza kabisa. Hawakubakiza mtu yeyote. Wakaufanyia Debiri na mfalme wake kama vile walivyokuwa wameifanyia miji ya Libna na Hebroni na wafalme wao.

4010:40 Mwa 12:9; Yos 12:8; 15:19-21; 18:25; 1Sam 30:27; Kum 1:7; 7:24; 20:16-17; Yos 15:21-63; 19:1-8; Kut 23:31-33Hivyo Yoshua akalishinda eneo hilo lote, ikiwa ni pamoja na nchi ya vilima, na Negebu, na sehemu ya magharibi chini ya vilima, materemko ya milima, pamoja na wafalme wake wote. Hakubakiza mtu yeyote. Akaangamiza kabisa kila kitu chenye pumzi, kama vile Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa ameamuru. 4110:41 Mwa 14:17; 10:19; Yos 11:16; 15:51; Hes 13:17; 32:8; Kum 2:23Yoshua akawashinda kuanzia Kadesh-Barnea hadi Gaza na kutoka eneo lote la Gosheni hadi Gibeoni. 4210:42 Yos 10:14; Za 44:2; 80:8Wafalme hawa wote pamoja na nchi zao Yoshua aliwashinda kwa wakati mmoja, kwa sababu Bwana, Mungu wa Israeli, aliwapigania Israeli.

4310:43 Yos 5:9; 1Sam 11:14; 13:12Ndipo Yoshua akarudi pamoja na Israeli yote kwenye kambi huko Gilgali.