箴言 11 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

箴言 11:1-31

1耶和华憎恶骗人的天平,

喜爱公平的砝码。

2傲慢带来羞辱,

谦卑者有智慧。

3正直人被诚实引导,

奸诈者被奸诈毁灭。

4在降怒之日,财富毫无益处,

唯有公义能救人免于死亡。

5纯全人行义走坦途,

恶人作恶致沉沦。

6正直人被义行所救,

奸诈者被私欲所掳。

7恶人一死,他的希望就破灭,

他对财势的冀望转眼成空。

8义人脱离患难,

恶人落入其中。

9不敬虔者张口败坏邻舍,

义人却因知识获得拯救。

10义人亨通,全城快乐;

恶人灭亡,人人欢呼。

11城因正直人的祝福而兴盛,

因恶人的口舌而倾覆。

12无知者轻视邻舍,

明哲保持缄默。

13嚼舌者泄露秘密,

忠信者守口如瓶。

14缺乏智谋,国必败亡;

谋士众多,战无不胜。

15为他人作保,必受亏损;

厌恶当保人,得享平安。

16贤淑的女子得到尊荣,

残暴的男子得到资财。

17仁慈的人造福自己,

残酷的人惹祸上身。

18恶人赚来的转眼成空,

播种公义的必获奖赏。

19坚持行义,必得生命;

追逐罪恶,终必灭亡。

20心术不正的人令耶和华憎恶,

纯全无过的人蒙耶和华喜爱。

21恶人终必受到惩罚,

义人的子孙必得拯救。

22女子貌美无内涵,

如同猪鼻挂金环。

23义人的愿望结出善果,

恶人的希望招致烈怒。

24有人乐善好施,反倒越来越富;

有人极其吝啬,反而越来越穷。

25慷慨好施的必得昌盛,

恩待他人的必蒙恩待。

26囤粮不卖,惹人咒诅;

乐意卖粮,必蒙祝福。

27寻求良善得恩惠,

追求罪恶遭祸患。

28倚仗财势者必衰败,

义人必兴旺如绿叶。

29祸害自家,必一无所有,

愚人必做智者的仆役。

30义人结果如生命之树,

智者深得人心。

31看啊!义人在世上尚且遭报11:31 “义人在世上尚且遭报”《七十士译本》作“义人尚且难以得救”,参见彼得前书4:18

更何况恶人和罪人呢!

Kiswahili Contemporary Version

Mithali 11:1-31

111:1 Law 19:36; Ay 6:2; Mit 16:11; Eze 45:10Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu,

bali vipimo sahihi ni furaha yake.

211:2 Dan 4:30; Mit 16:18; 18:12Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu,

bali unyenyekevu huja na hekima.

311:3 Mit 13:6Uadilifu wa wenye haki huwaongoza,

bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.

411:4 Ay 20:20; Eze 7:19; Sef 1:18Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu,

bali haki huokoa kutoka mautini.

511:5 1Fal 8:36; Mit 5:21-23; 13:6; 21:7Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka,

bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.

611:6 Es 7:9; 1Tim 4:8; Mhu 10:8Haki ya wanyofu huwaokoa,

bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.

711:7 Ay 8:13; Mit 10:28Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka;

yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.

811:8 Mit 21:8Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu,

naye mtu mwovu huingia humo badala yake.

911:9 Mit 12:6; Yer 45:5; Ay 8:13Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu

humwangamiza jirani yake,

bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.

1011:10 2Fal 11:20; Mit 28:12; Es 8:15Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi;

mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.

1111:11 Mit 14:34; 29:8Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa,

bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.

1211:12 Mit 14:21; Ay 6:24Mtu asiye na akili humdharau jirani yake,

bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.

1311:13 Law 19:16; 1Tim 5:13; Mit 20:19; 10:14Masengenyo husaliti tumaini,

bali mtu mwaminifu hutunza siri.

1411:14 Mit 20:18; 24:6; 2Sam 15:34; 1Fal 12:1; Mit 20:18; 2Sam 15:34; Mit 15:22; 24:6; 1Fal 12:1Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka,

bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.

1511:15 Mit 6:1; 17:18; 22:26-27Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka,

bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.

1611:16 Mit 31:31Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima,

bali wanaume wakorofi hupata mali tu.

1711:17 Mt 25:34Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe,

bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.

1811:18 Hos 10:12; Kut 1:20; Ay 4:8Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu,

bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.

1911:19 Kum 30:15; Mit 10:2; 1Sam 2:6; Za 89:48; Mit 1:18-19; Mhu 7:2; Yer 43:1Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima,

bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.

2011:20 1Nya 29:17; Za 52:7Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu,

bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.

2111:21 Mit 16:5; Za 112:2Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa,

bali wenye haki watakuwa huru.

22Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe

ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.

2311:23 Rum 2:8, 9Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema,

bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.

2411:24 Za 112:9Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi,

mwingine huzuia, lakini huwa maskini.

2511:25 Mit 22:9; 2Kor 9:6-9; Mt 5:7Mtu mkarimu atastawi;

yeye awaburudishaye wengine

ataburudishwa mwenyewe.

2611:26 Amo 8:5; Ay 29:13Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka,

bali baraka itamkalia kichwani kama taji

yeye aliye radhi kuiuza.

2711:27 Es 7:10; Za 7:15-16Yeye atafutaye mema hupata ukarimu,

bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.

2811:28 Yer 9:23; 17:8; Mk 10:25; Za 52:8Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka,

bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.

2911:29 Mhu 5:16; Mit 14:19Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo,

naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.

3011:30 Mwa 2:9; Yak 5:20Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima,

naye mwenye hekima huvuta roho za watu.

3111:31 Yer 25:29; 49:12; 1Pet 4:18Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani,

si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?