申命记 25 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

申命记 25:1-19

1“如果发生纠纷,双方告上法庭,审判官要判明是非。 2如果有罪的一方被判受鞭打,审判官要命令他当场伏在地上,按罪行轻重量刑。 3最多可以鞭打他四十下。如果超过四十下,你们就是在公开羞辱自己的同胞。

4“牛在踩谷时,不可笼住它的嘴。

为死亡的兄弟传宗接代

5“如果兄弟们住在一起,其中一个没有儿子便死了,死者的妻子不可改嫁外人。死者的兄弟要尽兄弟的责任娶她为妻。 6她生的第一个儿子要算为死者的儿子,免得死者在以色列无法留名。 7如果死者的兄弟不愿娶那寡妇,她要到城门口见长老们,告诉他们,‘我丈夫的兄弟不肯尽兄弟的责任娶我,不肯为我丈夫在以色列留名。’ 8本城的长老们要把死者的兄弟召来,与他商谈。如果他执意不肯, 9那寡妇要当着众长老的面,上前脱下他的鞋,吐唾沫在他脸上,说,‘这就是不肯为兄弟留后之人的下场。’ 10从此以后,他的家在以色列要被称为‘被脱鞋者之家’。

其他条例

11“如果两个男人打架,其中一人的妻子为帮助丈夫而伸手抓住另外一人的下体, 12就要砍掉她的手,不可怜悯她。

13“你们做买卖时,口袋里不可有一大一小两种砝码, 14家里也不可用一大一小两种量器。 15你们必须使用准确公正的砝码和量器,以便在你们的上帝耶和华要赐给你们的土地上得享长寿。 16因为你们的上帝耶和华憎恶行事诡诈的人。

灭绝亚玛力人的命令

17“你们要记住,你们从埃及出来的路上,亚玛力人是怎样对待你们的。 18他们趁你们疲惫不堪时,袭击你们当中掉队的人,毫不敬畏上帝。 19所以,当你们的上帝耶和华赐给你们那片土地作产业、使你们四境安宁时,要灭绝亚玛力人,抹去世人对他们的记忆。你们要切记!

Kiswahili Contemporary Version

Kumbukumbu 25:1-19

125:1 Kut 21:6; Kum 17:8-13; 19:17; Mdo 23:3; 1Fal 8:32; Kut 23:7; Kum 1:16-17Watu wanapokuwa na ugomvi, wapeleke mahakamani na waamuzi wataamua shauri hilo; watawaachia wasio na kosa na kuwahukumu wenye hatia. 225:2 Mit 10:13; 19:29; Lk 12:48-49Kama mtu mwenye hatia anastahili kuchapwa, mwamuzi atamwamuru alale chini ili achapwe mbele yake idadi ya viboko kulingana na kosa lake, 325:3 Mt 27:26; Yn 19:1; 2Kor 11:24; Ay 18:3; Yer 20:2lakini kamwe asichapwe zaidi ya viboko arobaini. Ikiwa atachapwa zaidi ya viboko arobaini, nduguyo atadhalilika machoni pako.

425:4 Hes 22:29; 1Kor 9:9; 1Tim 5:18Usimfunge maksai kinywa anapopura nafaka.

525:5 Rut 4:10-13; Mt 22:24; Mk 12:19; Lk 20:28Ikiwa ndugu wanaishi pamoja na mmoja wao akafa bila kuacha mwana, kamwe mjane wake asiolewe nje ya jamaa hiyo. Ndugu wa mumewe atamchukua, amwoe na kutimiza wajibu wa shemeji kwake. 625:6 Mwa 38:9; Rut 4:5, 10Mwana wa kwanza atakayemzaa atapewa jina la ndugu aliyekufa ili jina lake lisifutike katika Israeli.

725:7 Rut 1:15; 4:2-6; Mwa 23:10Hata hivyo, ikiwa ndugu huyo wa mume hataki kuoa huyo mke wa nduguye, mjane atawaendea wazee kwenye lango la mji na kusema, “Ndugu wa mume wangu anakataa kuendeleza jina la nduguye katika Israeli. Hataki kutimiza wajibu wa shemeji kwangu.” 8Ndipo wazee wa mji wake watamwita na kuzungumza naye. Kama atashikilia kukataa akisema, “Sitaki kumwoa,” 925:9 Yos 24:22; Rut 4:7-11; Hes 12:14; Ay 17:6; 30:10; Isa 50:6mjane wa nduguye atamwendea mbele ya wazee, atamvua kiatu kimoja na kumtemea mate usoni, na kusema, “Hivi ndivyo ambavyo hufanywa kwa mtu ambaye atakataa kuendeleza jamaa ya ndugu yake.” 1025:10 Mit 6:33; 1Tim 3:7Jamaa ya mtu huyo itafahamika katika Israeli kama Jamaa ya Aliyevuliwa Kiatu.

11Ikiwa watu wawili wanapigana na mke wa mmoja wao akaja kumwokoa mumewe na yule anayemshambulia, naye mke huyo akifika na kumkamata sehemu za siri, 1225:12 Kum 7:2; 19:13huyo mwanamke utamkata mkono wake. Usimhurumie.

1325:13 Mit 11:1; 20:23; Eze 45:10; Mik 6:11; Amo 8:5Usiwe na mawe ya kupimia ya aina mbili katika mkoba wako, moja zito na jingine jepesi. 1425:14 Law 7:20; Hos 9:4Usiwe na vipimo viwili tofauti katika nyumba yako, kimoja kikubwa, kingine kidogo. 1525:15 Kut 20:12Ni lazima uwe na uzito na vipimo sahihi na vya haki, ili upate kuishi maisha marefu katika nchi anayokupa Bwana Mungu wako. 1625:16 Mit 11:1; 20:23; Amo 8:9-11; Ufu 21:27; 1Tim 4:6; 1Kor 8:9-11Kwa maana Bwana Mungu wako humchukia yeyote ambaye hufanya mambo kama haya, yeyote anayetenda kwa udanganyifu.

1725:17 Mwa 36:12; Kut 17:8Kumbuka kile Waamaleki walichowatendea mlipokuwa njiani mkitoka Misri. 1825:18 Za 36:1; Rum 3:18; Mit 16:6Wakati mlipokuwa mmechoka na kuishiwa nguvu kwa safari yenu, wakawapiga wale wote waliokuja nyuma. Waamaleki hawakumwogopa Mungu. 1925:19 Kut 33:14; Ebr 3:18-19; Es 9:16; Mwa 36:12; 1Sam 15:2-3Bwana Mungu wako atakapokupa pumziko mbali na adui zako wote wanaokuzunguka katika nchi akupayo kuimiliki kuwa urithi, utafutilia mbali kumbukumbu lote la Waamaleki chini ya mbingu. Usisahau!