民数记 20 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

民数记 20:1-29

磐石出水

1一月,以色列全体会众抵达旷野,在加低斯安营。米利暗离世,葬在那里。 2会众没有水喝,就聚集起来反对摩西亚伦3他们埋怨说:“还不如当初跟我们的弟兄一起死在耶和华面前! 4你们为什么领耶和华的会众到这旷野来,要叫我们和牲畜都死在这里吗? 5你们为什么把我们领出埃及,带到这不毛之地?这里没有五谷、无花果树、葡萄树和石榴树,甚至没有水喝。” 6摩西亚伦离开会众到会幕门口,俯伏在地。耶和华的荣光向他们显现。 7耶和华对摩西说: 8“你拿着杖和你哥哥亚伦招聚会众,当着他们的面吩咐磐石流出水来,水就会从磐石流出,供会众和牲畜喝。” 9摩西遵命而行,从耶和华面前取了杖, 10然后和亚伦把会众招聚到磐石前,说:“你们这些叛逆之徒听着,非要我们叫磐石给你们流出水来吗?” 11接着,摩西举起手中的杖击打磐石两下,水便喷涌而出,会众和牲畜都喝了。

12耶和华对摩西亚伦说:“你们对我没有足够的信心,没有当着以色列人的面尊我为圣,所以你们不得带领会众进入我将要赐给他们的土地。” 13这地方叫米利巴泉,因为以色列人在那里埋怨耶和华,耶和华就向他们彰显了祂的圣洁。

以东王不借路

14摩西加低斯派使者去见以东王,说:“你的弟兄以色列人说,你知道我们遭遇的种种困难。 15我们祖先到埃及寄居多年,我们世代受埃及人虐待。 16但我们呼求耶和华,祂就垂听了我们的声音,差遣天使把我们领出埃及。现在我们来到你边境的加低斯城, 17求你容我们借道贵国。我们不会踏入田地和葡萄园,也不会喝井里的水,只走大路,不会偏离,直到走出贵国。” 18以东王却说:“你们不可从我这里经过,否则我必兵戎相见。” 19以色列人说:“我们只走大路,倘若我们和牲畜喝了你的水,我们会付钱。我们别无他求,只求步行穿过贵国。” 20以东王仍然不准,还率领大军严阵以待。 21由于无法从以东穿过,以色列人只好绕道。

亚伦离世

22以色列全体会众从加低斯出发,来到何珥山。 23耶和华在位于以东边界的何珥山对摩西亚伦说: 24亚伦要去他祖先那里了,他不能进入我赐给以色列人的土地,因为你们在米利巴泉违背了我的命令。 25摩西啊,你要带亚伦和他儿子以利亚撒何珥山, 26亚伦的圣衣脱下来给他儿子以利亚撒穿上,因为亚伦将死在那里。” 27摩西遵命而行。他们三人就当着全体会众的面上了何珥山。 28摩西亚伦的圣衣脱下,给以利亚撒穿上。随后亚伦在山顶离世。摩西以利亚撒便下了山。 29以色列全体会众得知亚伦离世,就为他哀悼了三十天。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 20:1-29

Maji Kutoka Kwenye Mwamba

(Kutoka 17:1-7)

120:1 Hes 13:21; 13:26; 33:36; Kum 1:46; Amu 11:17; Za 29:8; Kut 15:20Katika mwezi wa kwanza jumuiya yote ya Kiisraeli ilifika kwenye Jangwa la Sini, nao wakakaa Kadeshi. Miriamu akafa huko na kuzikwa.

220:2 Kut 15:22; 17:1; Hes 16:19Mahali hapo hapakuwa na maji kwa ajili ya jumuiya hiyo, nao wakakusanyika ili kumpinga Mose na Aroni. 320:3 Mwa 13:7; Kut 17:2; 21:18; 5:21; Hes 14:2; 16:31-35Watu wakagombana na Mose, na kusema, “Laiti tungelikufa wakati ndugu zetu walipoanguka na kufa mbele za Bwana! 420:4 Hes 14:2; Kut 14:11; Hes 14:3; 16:13Kwa nini mmeileta jumuiya ya Bwana kwenye jangwa hili, ili tufe humu, sisi na mifugo yetu? 520:5 Hes 13:23; 16:14; Kut 17:1Kwa nini mmetupandisha kutoka Misri mpaka mahali hapa pa kutisha? Hapa hakuna nafaka wala tini, zabibu au makomamanga. Wala hapa hakuna maji ya kunywa!”

620:6 Kut 40:2; Hes 14:5; 16:19Mose na Aroni wakaondoka pale kwenye kusanyiko mpaka kwenye mlango wa Hema la Kukutania na kuanguka kifudifudi, nao utukufu wa Bwana ukawatokea. 7Bwana akamwambia Mose, 820:8 Kut 4:2; 10:12-13; 17:6; Isa 41:18; 43:20; Yer 31:9“Chukua ile fimbo, na wewe na ndugu yako Aroni mkusanye kusanyiko pamoja. Nena na ule mwamba mbele ya macho yao, nao utatoa maji yake. Utatoa maji kutoka huo mwamba kwa ajili ya jumuiya ili wao na mifugo yao waweze kunywa.”

920:9 Hes 17:2; 17:10Kwa hiyo Mose akaichukua hiyo fimbo kutoka pale ilipokuwa mbele za Bwana kama alivyomwagiza. 1020:10 Za 106:32-33Mose na Aroni wakakusanya kusanyiko pamoja mbele ya huo mwamba, naye Mose akawaambia, “Sikilizeni, enyi waasi. Je, ni lazima tuwatoleeni maji kutoka mwamba huu?” 1120:11 Kut 17:6; Isa 33:21Ndipo Mose akainua mkono wake na kuupiga mwamba mara mbili kwa fimbo yake. Maji yakabubujika, nayo jumuiya na mifugo yao wakanywa.

1220:12 Hes 27:14; Kum 32:51; Isa 5:16; 8:13; Kum 3:27Lakini Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Kwa sababu hamkuniamini mimi kiasi cha kuniheshimu kama mtakatifu machoni pa Waisraeli, hamtaiingiza jumuiya hii katika nchi ninayowapa.”

1320:13 Kut 17:7; Law 10:3Haya yalikuwa maji ya Meriba,20:13 Meriba maana yake Kugombana. mahali pale ambapo Waisraeli waligombana na Bwana, naye akajionyesha mwenyewe huko kuwa mtakatifu katikati yao.

Edomu Wakatalia Israeli Kupita

1420:14 Hes 20:1, 16; Mwa 36:16; 25:30; 24:3; Kum 4:39; Yos 2:11; 9:9; Kut 18:8Mose akawatuma wajumbe kutoka Kadeshi kwenda kwa mfalme wa Edomu, akisema:

“Hili ndilo ndugu yako Israeli asemalo: Wewe unafahamu juu ya taabu zote ambazo zimetupata. 1520:15 Mwa 46:6; 15:13; Kut 1:14Baba zetu walishuka Misri, nasi tumeishi huko miaka mingi. Wamisri walitutesa sisi na baba zetu, 1620:16 Mwa 16:11; 21:17; Kut 2:23; 14:19; 12:42; Kum 26:8; Hes 33:37lakini tulipomlilia Bwana, alisikia kilio chetu na akamtuma malaika akatutoa Misri.

“Sasa tupo hapa Kadeshi, mji ulio mpakani mwa nchi yako. 1720:17 Hes 21:22; Kum 2:27; Amu 11:17Tafadhali turuhusu tupite katika nchi yako. Hatutapita katika shamba lolote, wala shamba la mizabibu, au kunywa maji kutoka kwenye kisima chochote. Tutasafiri kufuata njia kuu ya mfalme, na hatutageuka kulia wala kushoto mpaka tuwe tumeshapita nchi yako.”

1820:18 Hes 21:23Lakini mfalme wa Edomu akajibu:

“Hamtapita hapa; kama mkijaribu kupita, tutatoka na kuwashambulia kwa upanga.”

1920:19 Kut 2:23; Kum 2:6, 28Waisraeli wakajibu:

“Sisi tutafuata njia kuu; tena ikiwa sisi au mifugo yetu tutakunywa tone la maji yenu, tutalilipia. Sisi tunataka tu kupita kwa miguu, wala si kitu kingine chochote.”

20Watu wa Edomu wakajibu tena:

“Hamwezi kupita hapa.”

Ndipo watu wa Edomu wakatoka dhidi ya Waisraeli, jeshi kubwa lenye nguvu. 2120:21 Hes 21:23; 21:4; Kum 2:8; Amu 11:18Kwa kuwa Waedomu waliwakatalia Waisraeli kupita katika nchi yao, Israeli wakageuka, wakawaacha.

Kifo Cha Aroni

2220:22 Kum 1:46; Hes 33:37; 34:7; Kum 32:50Jumuiya yote ya Kiisraeli ikaondoka kutoka Kadeshi, wakafika kwenye Mlima Hori. 23Kwenye Mlima Hori, karibu na mpaka wa Edomu, Bwana akamwambia Mose na Aroni, 2420:24 Mwa 25; 8; Kut 17:7“Aroni atakusanywa pamoja na watu wake. Hataingia katika nchi ninayowapa Waisraeli, kwa sababu ninyi wawili mliasi dhidi ya agizo langu kwenye maji ya Meriba. 2520:25 Hes 33:38Watwae Aroni na Eleazari mwanawe, na uwapandishe juu katika Mlima wa Hori. 2620:26 Kut 28:1-4; 40:13; Law 16:4; Hes 27:13; 31:2Mvue Aroni mavazi yake, na umvike Eleazari mwanawe, kwa maana Aroni atakusanywa pamoja na watu wake; atakufa huko.”

2720:27 Hes 33:38Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza: Wakapanda Mlima Hori mbele ya macho ya jumuiya yote ya Kiisraeli. 2820:28 Kut 29:29; Hes 33:38; Kum 10:6; 32:50; Mwa 27:41; Law 10:6; Kum 34:8Mose akamvua Aroni mavazi yake na kumvika mwanawe Eleazari mavazi hayo. Naye Aroni akafia pale juu ya mlima. Kisha Mose na Eleazari wakateremka kutoka mlimani. 29Jumuiya yote ilipofahamu kwamba Aroni amekufa, jamaa yote ya Kiisraeli wakamwomboleza kwa siku thelathini.