士师记 6 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

士师记 6:1-40

士师基甸

1后来,以色列人又做耶和华视为恶的事,耶和华就把他们交在米甸人手下七年。 2米甸人势力强盛,以色列人只好躲进山里,藏在洞穴和营寨中。 3每当他们撒种的时候,米甸人、亚玛力人及东方人就前来进犯, 4在他们境内安营,摧毁他们远至迦萨一带的庄稼,不给他们留下任何粮食,也不留下一只羊、一头牛或驴。 5入侵者带着牲畜和帐篷像蝗虫一样涌来,人和骆驼不计其数,摧毁了整个地区。 6以色列人因米甸人的入侵而极其贫乏,就呼求耶和华。

7以色列人因米甸人的入侵而呼求耶和华的时候, 8耶和华就差遣先知对他们说:“以色列的上帝耶和华说,‘我曾把你们从受奴役之地埃及领出来, 9将你们从埃及人及一切欺压者的手中拯救出来,从你们面前赶走他们,把他们的土地赐给你们。’ 10我曾对你们说,‘我是你们的上帝耶和华。你们虽然住在亚摩利人的地方,但不可祭拜他们的神明。’你们却充耳不闻。”

11一天,耶和华的天使来到俄弗拉,坐在亚比以谢族人约阿施的橡树下。约阿施的儿子基甸因为要躲避米甸人,正躲在榨酒池里打麦子。 12耶和华的天使向基甸显现,对他说:“英勇的战士啊,耶和华与你同在。” 13基甸说:“我主啊,如果耶和华与我们同在,我们怎会有这些遭遇?我们的祖先说耶和华曾带他们出埃及,但如今祂那些奇妙的作为在哪里呢?现在祂已经丢弃我们,把我们交在米甸人手里。” 14耶和华转向他,说:“你尽自己的力量去从米甸人手中拯救以色列人吧,我现在派你去。” 15基甸说:“主啊,我出身于玛拿西支派最弱小的家族,在家里最微不足道,我怎能拯救以色列人呢?” 16耶和华说:“我必与你同在,你必如击打一人一样击打米甸人。” 17基甸说:“如果我在你面前蒙恩,求你给我一个凭据,使我知道与我说话的真是你耶和华。 18请你在这里等一等,让我回去拿礼物献给你。”耶和华说:“我必等你回来。”

19基甸回家预备了一只山羊羔,用十公斤面粉做了无酵饼,把肉放进篮子,把汤盛在壶中,然后拿到橡树下献上。 20上帝的天使对基甸说:“把肉和无酵饼放在这磐石上,把汤倒在上面。”他一一照做。 21耶和华的天使伸出手中的杖碰了一下饼和肉,火就从磐石中喷出来烧尽了它们。耶和华的天使也不见了。 22基甸发现他果然是耶和华的天使,便说:“唉!主耶和华啊,不好了,我面对面见了你的天使。” 23耶和华对他说:“放心吧,不要害怕,你不会死。” 24基甸在那里为耶和华筑了一座坛,称之为“耶和华赐平安”。这坛如今仍在亚比以谢族的俄弗拉

25那天晚上,耶和华吩咐基甸:“牵来你父亲的第二头牛,就是那头七岁的公牛,拆毁你父亲为巴力筑的祭坛,砍倒坛旁的亚舍拉神像。 26然后,在这座山顶上把石头堆放整齐,为你的上帝耶和华筑一座祭坛,用砍倒的亚舍拉神像作柴,把那头公牛献作燔祭。” 27于是,基甸带了十个仆人遵命而行。不过,他因为害怕家人和城中的人,不敢在白天行动,便在夜间行动。

28清早,城里的人起来后,发现巴力的祭坛已经被人拆毁,坛旁的亚舍拉神像被砍倒,第二头公牛被献在新建的祭坛上。 29他们彼此议论说:“这是谁干的?”他们仔细调查后得知是约阿施的儿子基甸所为, 30便对约阿施说:“把你儿子交出来!他拆毁了巴力的祭坛,砍倒了坛旁的亚舍拉神像,我们要处死他!” 31约阿施对气势汹汹的人群说:“你们这样做是要为巴力辩护吗?是要救它吗?谁为巴力辩护,今天早晨就处死谁。有人拆毁巴力的祭坛,如果它是神明,就让它为自己辩护吧!” 32因此,那天他们称基甸耶路·巴力,意思是“让巴力为自己辩护”,因为他拆毁了巴力的祭坛。

33那时,米甸人、亚玛力人及东方人会合在一起,过了约旦河,在耶斯列的平原安营。 34耶和华的灵降在基甸身上,他就吹响号角,号召亚比以谢族的人跟从他。 35他派人走遍玛拿西亚设西布伦拿弗他利各支派召集军队,人们纷纷前来会合。 36基甸对上帝说:“若如你所言,你要用我去拯救以色列人, 37求你给个凭据。我把一团羊毛放在麦场上,若明天早晨只是羊毛上有露水,地面却是干的,我就知道,如你所言,你要用我去拯救以色列人。” 38果然如此,基甸一早醒来,从羊毛中挤出满满一碗露水。 39基甸又对上帝说:“求你不要发怒,容许我再试一次,这次让羊毛是干的,地面有露水。” 40那天晚上,上帝就照他所求使地面布满露水,唯独羊毛是干的。

Kiswahili Contemporary Version

Waamuzi 6:1-40

Gideoni

16:1 Amu 2:11; Mwa 25:2; Hes 25:15-18Waisraeli wakafanya tena yaliyo maovu mbele za Bwana, naye kwa miaka saba Bwana akawatia mikononi mwa Wamidiani. 26:2 1Sam 13:6; Isa 5:30; 8:21; 26:16; 27:3; 2:19; Yer 48:28; 49:8; Ay 24:8; Yer 41:9; Ebr 11:38Mkono wa Midiani ukawa na nguvu dhidi ya Israeli na kwa ajili ya Wamidiani, Waisraeli wakajitengenezea mahali pa kujificha milimani, kwenye mapango na ngome. 36:3 Hes 13:29; Mwa 25:6; Isa 11:14; Yer 49:28Kila wakati Waisraeli walipopanda mazao mashambani, Wamidiani, Waamaleki na mataifa mengine ya mashariki walivamia nchi yao. 46:4 Law 26:16; Kum 28:30, 51; Isa 10:6; 42:22; Mwa 10:19Wakapiga kambi katika mashamba yao na kuharibu mazao ya nchi yote hadi kufikia Gaza, wala hawakuacha kiumbe chochote kilicho hai kwa Waisraeli, iwe kondoo au ngʼombe au punda. 56:5 Kum 28:42; Amu 8:10; Isa 21:7; 60:6; Yer 49:28Walipanda na mifugo yao na mahema yao, mfano wa makundi ya nzige. Ilikuwa haiwezekani kuwahesabu watu na ngamia zao; wakavamia nchi ili kuiharibu. 6Waisraeli wakafanywa kuwa maskini sana na Wamidiani, hata Israeli wakamlilia Bwana kuomba msaada.

76:7 Amu 3:9Waisraeli walipomlilia Bwana kwa sababu ya Wamidiani, 86:8 Kum 18:15; 1Fal 20:13, 22; 2Fal 17:13, 23; Neh 9:29; Yer 25:5; Ay 36:10; Eze 18:30-31; Amu 2; 1Bwana akawapelekea nabii, ambaye aliwaambia, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: Niliwapandisha mtoke Misri, toka nchi ya utumwa. 96:9 Neh 10:9; Za 136:24; 44:2Nikawanyakua kutoka mikononi mwa Wamisri na kutoka mikononi mwa watesi wenu wote. Nikawafukuza watoke mbele yenu nami nikawapa ninyi nchi yao. 106:10 Kut 20:5; Yos 24:15; Yer 10:2Nikawaambia, ‘Mimi ndimi Bwana Mungu wenu; msiiabudu miungu ya Waamori, ambayo mnakaa katika nchi yao!’ Lakini ninyi hamkuitii sauti yangu.”

116:11 Mwa 16:7; Yos 18:23; Amu 7:14; 8:13, 29; Hes 26:30; Amu 7:1; 8; 1; Ebr 11:32; Rut 2:17; 3:2; 1Sam 23:1; Neh 13:15; Isa 16:10; 63:3; Mao 1:15; Yoe 3:13Malaika wa Bwana akaja akaketi chini ya mti wa mwaloni huko Ofra, ambao ulikuwa mali ya Yoashi, Mwabiezeri, ambako Gideoni mwanawe alikuwa akipepeta ngano penye shinikizo la kukamulia zabibu, ili kuificha Wamidiani wasiione. 126:12 Yos 1:5; Rut 2:4; 1Sam 10:7; Za 129:8; Amu 11:1; Lk 1:11, 28Malaika wa Bwana alipomtokea Gideoni, akamwambia, “Bwana yu pamoja nawe, Ewe shujaa mwenye nguvu.”

136:13 Yos 3:5; 2Sam 7:22; Za 44; 1; 78:3; Kum 31:17; 2Nya 15; 2Gideoni akajibu, “Ee Bwana wangu, kama Bwana yu pamoja nasi, mbona mambo haya yote yametutokea? Yako wapi basi yale matendo yake makuu baba zetu waliyotusimulia juu yake waliposema, ‘Je, Bwana hakutupandisha kutoka Misri?’ Lakini sasa Bwana ametuacha na kututia katika mkono wa Midiani.”

146:14 Ebr 11:34; Amu 10:1; 1Fal 14:27Bwana akamgeukia na kusema “Enenda kwa uwezo wako huu, ukawaokoe Israeli kutoka mikononi mwa Wamidiani. Je, si mimi ninayekutuma wewe?”

156:15 Isa 60:22; 1Sam 9:20-21Gideoni akauliza, “Ee Bwana wangu, nitawezaje kuwaokoa Israeli? Ukoo wangu ndio dhaifu kuliko zote katika Manase, nami ndiye mdogo wa wote katika jamaa yangu.”

166:16 Kut 3:12; Hes 14:43; Yos 1:5Bwana akamjibu, “Nitakuwa pamoja nawe, nawe utawapiga Wamidiani kana kwamba walikuwa ni mtu mmoja.”

176:17 Mwa 24:14; Kut 3; 12; 4:8Gideoni akajibu, “Kama basi nimepata kibali machoni pako, nipe ishara kuonyesha kweli kwamba ni wewe unayesema nami. 18Tafadhali ninakuomba usiondoke hapa mpaka nitakaporudi na kukuletea sadaka yangu na kuiweka mbele yako.”

Naye Bwana akamwambia, “Nitangoja mpaka utakaporudi.”

196:19 Mwa 18:7-8; Law 19:36; Amu 13:15Gideoni akaingia ndani ya nyumba yake na kuandaa mwana-mbuzi pamoja na kuoka mikate isiyotiwa chachu kutokana na efa moja6:19 Efa moja ni sawa na lita 22. ya unga. Akaweka nyama kwenye kikapu na mchuzi kwenye chungu, akamletea huyo malaika hapo nje chini ya mti wa mwaloni na kumpa.

206:20 Amu 13:19Malaika wa Mungu akamwambia, “Itwae nyama na mikate isiyotiwa chachu, uviweke juu ya mwamba huu na umimine huo mchuzi juu yake.” Gideoni akafanya hivyo. 216:21 Kut 4:2; Law 9:24Malaika wa Bwana akainyoosha fimbo iliyokuwa mkononi mwake, ncha yake ikagusa ile nyama na ile mikate isiyotiwa chachu, nao moto ukatoka kwenye mwamba ukateketeza ile nyama na ile mikate. Malaika wa Bwana akatoweka kutoka machoni pake. 226:22 Kum 13:16; Mwa 32:30; 11:32Gideoni alipotambua kuwa ni malaika wa Bwana, akapiga kelele kwa mshangao, akasema, “Ole wangu, Bwana Mwenyezi! Kwa kuwa nimemwona malaika wa Bwana uso kwa uso!”

236:23 Dan 10:19; Mwa 16:13; Kum 5:26Lakini Bwana akamwambia, “Amani iwe kwako! Usiogope. Hutakufa.”

246:24 Mwa 22:14; Yos 18:23Hivyo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu mahali pale na kupaita, Yehova-Shalom.6:24 Yehova-Shalom maana yake Bwana ni Amani. Mpaka leo ingalipo imesimama huko Ofra ya Waabiezeri.

256:25 Kut 34:13; Amu 2:13; Kum 2:13; 7:5Usiku ule ule Bwana akamwambia, “Mchukue ngʼombe dume wa baba yako, yaani, yule wa pili mwenye miaka saba, na ubomoe madhabahu ya Baali aliyo nayo baba yako, na ukaikate Ashera iliyo karibu nayo. 266:26 Mwa 8:20Kisha mjengee Bwana Mungu wako, madhabahu halisi, kwa taratibu zake, juu ya huu mwamba. Kwa kutumia kuni za hiyo nguzo ya Ashera uliyoikatakata, mtoe sadaka huyo dume wa pili kuwa sadaka ya kuteketezwa.”

27Basi Gideoni akawachukua watumishi wake kumi na kufanya kama Bwana alivyomwambia. Lakini kwa kuwa aliwaogopa jamaa yake na watu wa mji, akafanya haya usiku badala ya mchana.

286:28 1Fal 16:32; 2Fal 21:3Watu wa mji walipoamka asubuhi, tazama madhabahu ya Baali imebomolewa na nguzo ya Ashera iliyokuwa karibu nayo imekatwakatwa na yule ngʼombe wa pili ametolewa sadaka juu ya madhabahu yaliyojengwa upya!

29Wakaulizana, “Ni nani aliyetenda mambo haya?”

Walipochunguza kwa makini, wakaambiwa, “Ni Gideoni mwana wa Yoashi, ndiye alitenda hivi.”

30Watu wa mji wakamwambia Yoashi, “Mlete mwanao hapa. Ni lazima afe, kwa sababu amebomoa madhabahu ya Baali na kukatakata nguzo ya Ashera iliyokuwa karibu nayo.”

316:31 1Sam 24:15; Za 43:1; Yer 30:13Lakini Yoashi akauambia ule umati uliokuwa umezunguka ukiwa kinyume naye, “Je, ninyi mtamtetea Baali? Mnajaribu kumwokoa? Yeyote mwenye kumpigania atauawa kufikia kesho asubuhi! Kama Baali ni mungu kweli, anaweza kujitetea mwenyewe wakati mtu anapobomoa madhabahu yake.” 326:32 Amu 7:1; 8:29, 35; 9:1; 1Sam 12:11Basi siku ile wakamwita Gideoni “Yerub-Baali,” yaani, “Baali na ashindane naye,” kwa sababu alibomoa madhabahu yake.

336:33 Hes 13:29; Mwa 25:6; Yos 15:56; Eze 25:4; Hos 1:5Basi Wamidiani wote, Waamaleki na mataifa mengine ya mashariki wakaunganisha majeshi yao, wakavuka ngʼambo ya Yordani na kupiga kambi katika Bonde la Yezreeli. 346:34 Amu 3:10; Yos 6:20; Amu 3:27; Yos 17:2Ndipo Roho wa Bwana akamjia Gideoni, akapiga tarumbeta, akiwaita Waabiezeri ili wamfuate. 356:35 Yos 17:7; Amu 4:6; 7:23Akatuma wajumbe waende katika Manase yote, akiwataka wachukue silaha na pia katika Asheri, Zabuloni na Naftali, nao wakakwea ili kukutana nao.

36Gideoni akamwambia Mungu, “Kama utawaokoa Waisraeli kwa mkono wangu, kama ulivyoahidi: 376:37 Ay 31:20; Hes 18; 27; 2Sam 6:6; 24:16; Mwa 24; 14tazama, nitaweka ngozi ya kondoo kwenye kiwanja cha kupuria nafaka, na kama utakuwepo umande juu ya ngozi tu, nayo ardhi yote ikiwa kavu, ndipo nitakapojua kuwa utaokoa Israeli kwa mkono wangu, kama ulivyosema.” 38Hivyo ndivyo ilivyotokea. Gideoni akaamka asubuhi na mapema kesho yake, akaikamua ile ngozi, umande ukatoka, maji ya kujaa bakuli.

396:39 Mwa 18:32Kisha Gideoni akamwambia Bwana, “Usinikasirikie. Ninaomba nifanye ombi moja lingine. Niruhusu nifanye jaribio jingine moja kwa ngozi hii. Wakati huu uifanye ngozi hii kavu na ardhi yote ifunikwe na umande.” 406:40 Kut 4:3-7; Isa 28:7Usiku ule Mungu akafanya hivyo. Ngozi ile ilikuwa kavu, nayo ardhi yote ikafunikwa na umande.