哈该书 2 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

哈该书 2:1-23

对新殿的应许

1七月二十一日,耶和华借先知哈该说: 2“你去告诉撒拉铁的儿子犹大省长所罗巴伯约撒答的儿子大祭司约书亚和所有的余民, 3‘你们幸存的人当中有谁见过这殿昔日的荣耀呢?现在你们看这殿如何?看上去岂不是无足轻重吗? 4所罗巴伯啊,你要刚强,这是耶和华说的。约撒答的儿子大祭司约书亚啊,你要刚强;这地方的所有百姓啊,你们要刚强。这是耶和华说的。你们要动工,因为我与你们同在。这是万军之耶和华说的。 5这是你们出埃及时我与你们立的约。不要惧怕,我的灵仍住在你们当中。

6“‘万军之耶和华说,不久,我要再次震动天地、海洋和旱地。 7万军之耶和华说,我要震动万国,万国的珍宝都要送到这殿,我要使这殿充满荣耀。 8万军之耶和华说,金子是我的,银子也是我的。 9万军之耶和华说,这殿后来的荣耀必大过从前的荣耀。万军之耶和华说,我要在这地方赐下平安。’”

指出百姓的罪

10大流士王执政第二年九月二十四日,耶和华对先知哈该说: 11“万军之耶和华说,‘你去问祭司律法怎么说, 12如果有人用衣服兜着祭肉,而衣服碰到饼、汤、酒、油或其他食物,这些被衣服碰到的食物会成为圣洁之物吗?’”祭司们答道:“不会。” 13哈该又说:“如果因碰过尸体而变得不洁净的人接触这些食物,这些食物会变得不洁净吗?”祭司答道:“会变得不洁净。” 14于是哈该说:“耶和华说,‘这百姓和这国家在我面前也是如此。他们手中的各样工作和他们在那里所献的都不洁净。’

耶和华应许赐福

15“‘你们现在要回想重建耶和华殿之前的光景。 16那时,有人盼望得到二十斗谷物,却只有十斗。有人盼望得到五十桶酒,榨酒池中却只有二十桶。 17我曾用虫灾、霉灾和冰雹毁灭你们的作物,你们仍没有归向我。这是耶和华说的。 18从今以后,也就是从九月二十四日起,你们要思想耶和华的殿奠基的日子,要认真思想。 19虽然粮仓里没有种子,葡萄树、无花果树、石榴树和橄榄树没结果子,但从今以后,我要赐福给你们。’”

拣选所罗巴伯

20同一天,耶和华第二次对哈该说: 21“你告诉犹大省长所罗巴伯,‘我必震动天地, 22推翻君王的宝座,消灭列国的势力,掀翻他们的战车和驾车的人,使战马跌倒、骑士自相残杀。 23万军之耶和华说,我的仆人——撒拉铁的儿子所罗巴伯啊,到那日,我必使你作我盖印的戒指,因为我拣选了你。这是万军之耶和华说的。’”

Kiswahili Contemporary Version

Hagai 2:1-23

Utukufu Ulioahidiwa Wa Nyumba Mpya

12:1 Law 23:34; Yn 7:37; Ezr 5:1Katika siku ya ishirini na moja ya mwezi wa saba, neno la Bwana lilikuja kupitia nabii Hagai, kusema: 22:2 Hag 1:12; 1Nya 6:15“Sema na Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, na mabaki ya watu. Uwaulize, 32:3 Ezr 3:12; Isa 60:7; Zek 4:10‘Ni nani miongoni mwenu aliyebaki ambaye aliiona hii nyumba katika utukufu wake wa mwanzo? Sasa inaonekanaje kwenu? Je, haionekani kwenu kama si kitu? 42:4 Zek 8:9; Hag 1:13; 1Sam 16:18; Mk 16:20; Rum 8:31; 1Nya 28:20; Efe 6:10; Kut 3:12; 33:14; Hes 14:9; Mdo 7:9; 2Sam 5:10Lakini sasa uwe imara, ee Zerubabeli,’ asema Bwana. ‘Kuwa imara, ee kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki. Mwe imara, enyi watu wote wa nchi,’ asema Bwana, ‘na mfanye kazi. Kwa kuwa mimi nipo pamoja nanyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. 52:5 Mwa 6:18; 15:1; Kut 29:46; Neh 9:20; Zek 4:6; 8:13; Isa 63:11; Ezr 5:2; 1Nya 28:20‘Hili ndilo nililoagana nanyi mlipotoka katika nchi ya Misri. Pia Roho wangu anadumu katikati yenu. Msiogope.’

62:6 Kut 19:18; Ay 9:6; Isa 10:25; 14:16; 34:4; Eze 38:19; Yer 4:26; Ebr 12:26“Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Baada ya muda kidogo kwa mara nyingine nitazitikisa mbingu na nchi, bahari na nchi kavu. 72:7 1Sam 9:20; Isa 60:7; Mwa 3:15; Kum 18:15; Za 24:7; Lk 2:32; Kut 16:7; 29:43Nitatikisa mataifa yote, nacho kile kinachotamaniwa na mataifa yote kitakuja, nami nitaujaza utukufu katika nyumba hii,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. 82:8 1Nya 29:2‘Fedha ni mali yangu na dhahabu ni mali yangu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. 92:9 Za 85:9; Isa 9:6; 11:10; 60:7, 17; Law 26:6; Ezr 3:12; Lk 11:31; 2:14; Yn 1:14‘Utukufu wa nyumba hii ya sasa utakuwa mkubwa kuliko utukufu wa ile nyumba ya mwanzoni,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. ‘Na mahali hapa nitawapa amani,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”

Baraka Kwa Watu Waliotiwa Unajisi

102:10 Hag 1:15Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilikuja kwa nabii Hagai: 112:11 Law 10:10-11; Kum 17:8-11; 33:8; Yer 18:18“Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Ulizeni makuhani jinsi sheria inavyosema: 122:12 Yer 11:15; Mwa 7:2Kama mtu akibeba nyama iliyowekwa wakfu katika pindo la vazi lake, kisha lile pindo likagusa mkate au mchuzi, divai, mafuta au chakula kingine, je, kitu hicho kitakuwa kimewekwa wakfu?’ ”

Makuhani wakajibu, “La hasha.”

132:13 Law 22:4-6; Hes 19:13Kisha Hagai akasema, “Je, kama mtu aliyetiwa unajisi kwa kugusa maiti akigusa mojawapo ya vitu hivi, kitu hicho kitakuwa kimetiwa unajisi?”

Makuhani wakajibu, “Ndiyo, huwa kimenajisiwa.”

142:14 Isa 1:13; 29:13; Tit 1:14-15; Za 51:17Kisha Hagai akasema, “ ‘Basi ndivyo walivyo machoni pangu hawa watu na taifa hili,’ asema Bwana. ‘Lolote wafanyalo na chochote watoacho hapo ni najisi.

152:15 Ezr 3:10; 4:24; Hag 1:5“ ‘Sasa fikirini kwa uangalifu kuanzia leo na kuendelea: tafakarini jinsi mambo yalivyokuwa kabla halijawekwa jiwe moja juu ya lingine katika Hekalu la Bwana. 162:16 Rut 3:7; Ay 24:11; Isa 5:2, 10; Hag 1:6; Kum 28:38Wakati mtu alipoendea lundo la nafaka la vipimo ishirini, kulikuwa na vipimo kumi tu. Wakati mtu alipoendea pipa la mvinyo ili kuchota vipimo hamsini, kulikuwa na vipimo ishirini tu. 172:17 Hag 1:11; Kut 9:18; Kum 28:22; Za 78:48; Isa 9:13; Amo 4:6; 1Fal 8:37; Yer 3:10; 5:3Kazi zenu zote za mikono nilizipiga kwa ukame, ukungu na mvua ya mawe, lakini hata hivyo, hamkunigeukia mimi,’ asema Bwana. 182:18 Zek 8:9; Hag 1:5; Ezr 3:11‘Tangu leo na kuendelea, kuanzia siku hii ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa, tafakarini siku ambayo msingi wa Hekalu la Bwana uliwekwa. Tafakarini: 192:19 Kut 28:33; Yoe 1:12; 2:14; Mwa 12:2; Law 25:21; Za 128:1-6Je, bado kuna mbegu iliyobakia ghalani? Mpaka sasa, hakuna mzabibu au mtini, mkomamanga wala mzeituni uliozaa tunda.

“ ‘Kuanzia leo na kuendelea, nitawabariki.’ ”

Zerubabeli Pete Ya Muhuri Ya Bwana

202:20 Ezr 1:5; Hag 1:15Neno la Bwana likamjia Hagai kwa mara ya pili katika siku ya ishirini na nne ya mwezi kusema: 212:21 Ezr 5:2; Isa 14:16; Eze 21:27; 38:19-20; Ebr 12:26“Mwambie Zerubabeli mtawala wa Yuda kwamba nitazitikisa mbingu na nchi. 222:22 Mwa 19:25; Ay 2:13; Dan 2:44; Mik 5:10; Mt 24:7; Kut 15:21; Eze 38:21; Amu 7:22Nitapindua viti vya enzi vya falme, na kuziharibu kabisa nguvu za falme za kigeni. Nitapindua magari ya vita pamoja na waendeshaji wake; farasi na wapanda farasi wataanguka, kila mmoja kwa upanga wa ndugu yake.

232:23 Zek 4:10; Kut 28:9; Dan 9:24-26; Mwa 38:18; 2Kor 1:22; Mt 1:12; Wim 8:6; Yer 22:24; Isa 2:11; 10:20; 20:3; 2:1“ ‘Katika siku ile,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nitakuchukua wewe, mtumishi wangu Zerubabeli mwana wa Shealtieli,’ asema Bwana. ‘Nitakufanya kama pete yangu ya muhuri, kwa kuwa nimekuchagua,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”