列王纪下 17 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

列王纪下 17:1-41

何细亚做以色列王

1犹大亚哈斯执政第十二年,以拉的儿子何细亚撒玛利亚登基做以色列王,执政九年。 2他做耶和华视为恶的事,不过没有他之前的以色列诸王那么败坏。 3亚述撒缦以色攻打以色列何细亚纳贡称臣。 4然而,何细亚差遣使者向埃及求援,不再像往年那样向亚述王进贡。亚述王发现后,把他抓起来囚在狱中。 5亚述王攻打以色列全境,并围困撒玛利亚三年。 6何细亚执政第九年,撒玛利亚沦陷。亚述王把以色列人掳到亚述,安置在哈腊歌散哈博河一带以及玛代人的各城。

以色列人的罪恶史

7以色列人之所以有如此下场,是因为他们的上帝耶和华领他们出埃及,从埃及王法老手中救出他们,他们却犯罪得罪祂。他们祭拜别的神明, 8效法耶和华在他们面前赶走的外族人的风俗和以色列诸王奉行的习俗。 9以色列人暗中做不义之事,冒犯他们的上帝耶和华。从瞭望塔到坚城,他们在各地建丘坛, 10在各高岗上、绿树下立神柱和亚舍拉神像, 11在各丘坛烧香,如同耶和华在他们面前赶走的外族人一样。他们邪恶的行为激怒了耶和华。 12尽管耶和华警告他们不可祭拜偶像,他们仍然执迷不悟。

13耶和华借着祂的众先知和先见警告以色列人和犹大人说:“你们要离开恶道,遵守我的诫命和律例,即我吩咐你们祖先遵守并借着我的仆人——众先知传给你们的律法。” 14但他们充耳不闻,像他们祖先一样顽固不化,不信靠他们的上帝耶和华, 15拒绝遵守祂的律例和祂与他们祖先所立的约,无视祂的警告。他们随从虚无的偶像,自己也变得虚无。他们违背耶和华的命令,去效法周围的外族人。 16他们把他们的上帝耶和华的诫命抛诸脑后,铸造了两个金牛犊,还造了亚舍拉神像。他们祭拜巴力和天上的万象, 17把自己的儿女烧死献作祭物。他们占卜,行邪术,出卖自己去做耶和华视为恶的事,惹祂发怒。

18因此,耶和华非常愤怒,从祂面前赶走以色列人,只留下犹大一个支派。 19犹大人也不遵守他们的上帝耶和华的诫命,反而效法以色列人的恶行。 20于是,耶和华弃绝了以色列全族,使他们饱尝痛苦,任人宰割,直至把他们从自己眼前赶走。 21祂使以色列大卫家分裂出来,以色列人便拥立尼八的儿子耶罗波安为王。耶罗波安诱使以色列人远离耶和华,使他们犯了大罪。 22以色列人沉溺于耶罗波安所犯的一切罪中,始终不肯回头, 23直到耶和华把他们从自己眼前赶走,正如祂借自己的仆人——众先知对他们的警告。这样,以色列人被掳到亚述,至今仍住在那里。

外族人移居撒玛利亚

24亚述王把巴比伦古他亚瓦哈马西法瓦音等地的一些居民迁移到撒玛利亚各城,代替以色列人。 25刚迁居到那里的时候,他们不敬拜耶和华,所以耶和华差遣狮子闯入他们当中,咬死了一些人。 26有人禀告亚述王说:“你迁移到撒玛利亚各城的那些人不知道当地神明的规矩,所以神明就差遣狮子闯入他们当中,咬死了一些人。” 27亚述王便下令:“派一位被掳来的祭司回去,让他住在那里,把当地神明的规矩教导给他们。” 28于是,有一位从撒玛利亚被掳走的祭司回去住在伯特利,教导他们怎样敬拜耶和华。

29可是,这些从各地迁来的民族都在所住的各城为自己制造神像,供奉在撒玛利亚人在高岗上建造的神庙中。 30巴比伦人造疏割·比讷神像,古他人造匿甲神像,哈马人造亚示玛神像, 31亚瓦人造匿哈他珥他神像,西法瓦音人焚烧儿女向他们的神明亚得米勒亚拿米勒献祭。 32他们也敬拜耶和华,却委任各种人做祭司,在高岗上的神庙为他们献祭。 33他们就这样既敬拜耶和华,又各按各的风俗供奉自己的神明。

34直到现在,他们仍然执迷不悟,不敬畏耶和华,也不遵行耶和华赐给雅各子孙的律例、典章、法度和诫命。耶和华曾给雅各取名叫以色列35与他的子孙立约,吩咐他们:“不可祭拜其他神明,不可跪拜和供奉他们,也不可向他们献祭。 36耶和华伸出大能的臂膀把你们领出埃及,你们要敬拜祂,要向祂跪拜、献祭。 37你们要永远谨遵祂所定的律例、典章、法度和诫命,不可祭拜其他神明。 38不可忘记我与你们立的约,不可祭拜其他神明。 39我是你们的上帝耶和华,你们要敬拜我,我必从一切仇敌手中救你们。” 40但是他们没有听从,依然仿效先前的风俗。 41那些移民到撒玛利亚各城的外族人既敬拜耶和华,又供奉自己的偶像。直到今日,他们的子孙仍是这样。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 17:1-41

Hoshea, Mfalme Wa Mwisho Katika Israeli

117:1 2Fal 15:30Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Ahazi mfalme wa Yuda, Hoshea mwana wa Ela akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, akatawala kwa miaka tisa. 217:2 Kum 4:25Akafanya maovu machoni pa Bwana, lakini si kama wafalme wengine wa Israeli waliomtangulia.

317:3 Hos 10:14; Amu 3:15Mfalme Shalmanesa wa Ashuru akainuka dhidi ya Mfalme Hoshea, ambaye hapo mbeleni alikuwa mtumwa wake na kumlipa ushuru. 417:4 Za 146:3; Hos 13:10Lakini mfalme wa Ashuru akagundua kuwa Hoshea alikuwa msaliti, kwa kuwa alikuwa ametuma wajumbe kwa So mfalme wa Misri, naye hakuendelea kulipa ushuru kwa mfalme wa Ashuru tena kama alivyokuwa anafanya kila mwaka. Kwa hiyo Shalmanesa akamkamata na kumtia gerezani. 5Mfalme wa Ashuru akaishambulia nchi yote, akapigana dhidi ya Samaria na kuizunguka kwa majeshi miaka mitatu. 617:6 2Fal 15:29; Isa 10:9Katika mwaka wa tisa wa Hoshea, mfalme wa Ashuru akaiteka Samaria na kuwahamishia Waisraeli huko Ashuru. Akawaweka huko Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi.

Israeli Inakwenda Uhamishoni Kwa Sababu Ya Dhambi

717:7 Yos 7:11; Kut 14:15-31Yote haya yalitokea kwa sababu Waisraeli walikuwa wametenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wao, ambaye alikuwa amewapandisha kutoka Misri akiwatoa chini ya utawala wa nguvu wa Farao mfalme wa Misri. Waliabudu miungu mingine 817:8 Law 18:3; Kum 9:4na kufuata desturi za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao, pamoja na desturi ambazo wafalme wa Israeli walizileta. 917:9 2Fal 18:8Waisraeli wakafanya vitu kwa siri dhidi ya Bwana Mungu wao, ambavyo havikuwa sawa. Kuanzia kwenye mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye maboma walijijengea wenyewe mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji yao yote. 1017:10 Kut 34:13; Mik 5:14Wakaweka mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti uliotanda. 11Wakafukiza uvumba kila mahali palipoinuka, kama yalivyofanya yale mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao. Wakafanya mambo maovu ambayo yalimghadhibisha Bwana. 1217:12 Kut 20:4Wakaabudu sanamu, ingawa Bwana alikuwa amesema, “Msifanye mambo haya.” 1317:13 1Sam 9:9; Yer 18:11; Zek 1:4Bwana akawaonya Israeli na Yuda kupitia kwa manabii na waonaji wake wote: “Acheni njia zenu mbaya. Shikeni amri na maagizo yangu, kufuatana na sheria yangu yote niliyowaagiza baba zenu kuitii ambayo niliileta kwenu kupitia kwa watumishi wangu manabii.”

1417:14 Kut 32:9; Mdo 7:15Lakini hawakusikiliza, walikuwa na shingo ngumu kama baba zao, ambao hawakumtegemea Bwana Mungu wao. 1517:15 Law 26:11; Kum 32:21Walizikataa amri zake, na agano alilokuwa amelifanya na baba zao, na maonyo aliyokuwa amewapa. Wakafuata sanamu zisizofaa, nao wenyewe wakawa hawafai. Wakayaiga mataifa yaliyowazunguka, ingawa Bwana alikuwa amewaonya akiwaambia, “Msifanye kama wanavyofanya,” nao wakafanya mambo ambayo Bwana alikuwa amewakataza wasifanye.

1617:16 Kut 32:4; Yer 2:5Wakayaacha maagizo yote ya Bwana Mungu wao na kujitengenezea sanamu mbili, walizozisubu katika sura ya ndama na nguzo ya Ashera. Wakasujudia mianga yote ya angani, na wakamtumikia Baali. 1717:17 Kum 18:10-12; Rum 7:14Wakawatoa kafara wana wao na mabinti zao katika moto. Wakafanya uaguzi na uchawi, nao wakajiuza wenyewe katika kutenda uovu machoni pa Bwana, wakamghadhibisha.

18Basi Bwana akawakasirikia sana Israeli na kuwaondoa kwenye uwepo wake. Ni kabila la Yuda tu lililobaki; 19na hata hivyo nao Yuda hawakuzishika amri za Bwana Mungu wao. Wakafuata desturi ambazo Israeli walikuwa wamezianzisha. 2017:20 2Fal 17:6Kwa hiyo Bwana aliwakataa watu wote wa Israeli; akawatesa na kuwaachia katika mikono ya wateka nyara hadi alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake.

2117:21 1Sam 15:27; 1Fal 12:20Alipokwisha kuwatenga Israeli mbali na nyumba ya Daudi, wakamfanya Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mfalme wao. Yeroboamu akawashawishi Israeli waache kumfuata Bwana na akawasababisha kutenda dhambi kuu. 22Nao Israeli wakadumu katika dhambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati, nao hawakuziacha 2317:23 Eze 39:23-24; Amu 6:8hadi Bwana alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake, kama vile alivyokuwa ameonya kupitia watumishi wake wote manabii. Hivyo watu wa Israeli wakaondolewa kutoka nchi yao kwenda uhamishoni Ashuru, nao wako huko mpaka sasa.

Samaria Inakaliwa Tena

2417:24 2Fal 18:34; Amo 6:2Mfalme wa Ashuru akawaleta watu kutoka Babeli, Kutha, Ava, Hamathi na Sefarvaimu na kuwaweka katika miji ya Samaria badala ya Waisraeli. Wakaimiliki Samaria na kuishi katika miji yake. 2517:25 Mwa 37:20; Yer 50:17Wakati walianza kuishi humo, hawakumwabudu Bwana, kwa hiyo akatuma simba miongoni mwao, wakawaua baadhi ya watu. 26Habari ikapelekwa kwa mfalme wa Ashuru, kusema: “Watu uliowahamisha na kuwaweka katika miji ya Samaria hawajui kile Mungu wa nchi hiyo anachokitaka. Ametuma simba miongoni mwao, ambao wanawaua, kwa sababu watu hawajui anachokitaka.”

27Ndipo mfalme wa Ashuru akaamuru hivi: “Mtwae mmoja wa makuhani uliowachukua mateka kutoka Samaria ili arudi kuishi humo na awafundishe watu kile ambacho Mungu wa nchi anataka.” 28Basi mmoja wa makuhani ambaye alikuwa amepelekwa uhamishoni kutoka Samaria akaja kuishi Betheli na kuwafundisha jinsi ya kumwabudu Bwana.

2917:29 Yer 2:28; Mik 4:5Hata hivyo, kila kikundi cha taifa lililoletwa Samaria kilitengeneza miungu yao wenyewe katika miji kadhaa mahali walipoishi, nao wakaiweka mahali pa ibada za miungu ambapo watu wa Samaria walikuwa wametengeneza katika mahali pa juu. 30Watu kutoka Babeli wakamtengeneza Sukoth-Benothi kuwa mungu wao, watu kutoka Kutha wakamtengeneza Nergali, na watu kutoka Hamathi wakamtengeneza Ashima; 3117:31 2Fal 17:24Waavi wakatengeneza Nibhazi na Tartaki, nao Wasefarvi wakachoma watoto wao kama kafara kwa Adrameleki na Anameleki, miungu ya Sefarvaimu. 3217:32 1Fal 12:31Walimwabudu Bwana, lakini pia waliteua aina zote za watu wao ili kuwawakilisha kama makuhani katika mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu pa ibada. 33Walimwabudu Bwana, lakini pia waliitumikia miungu yao kulingana na desturi za mataifa walikotoka.

3417:34 Mwa 17:5; 1Fal 18:31Mpaka leo wanashikilia desturi zao za zamani. Hawamwabudu Bwana wala kuzishika hukumu na maagizo, sheria na amri ambazo Bwana aliwapa uzao wa Yakobo, ambaye alimwita Israeli. 3517:35 Kut 20:3Wakati Bwana alipofanya Agano na Waisraeli, aliwaamuru akisema: “Msiiabudu miungu mingine yoyote wala kuisujudia, wala kuitumikia wala kuitolea dhabihu. 3617:36 Kum 3:20; Za 136:12Bali imewapasa kumwabudu Bwana aliyewapandisha kutoka Misri kwa uwezo wake mkuu na kwa mkono wake ulionyooshwa. Kwake yeye mtasujudu na kwake yeye mtatoa dhabihu. 3717:37 Kum 5:32; Law 19:37Imewapasa daima kuwa waangalifu kutunza hukumu na maagizo, sheria na amri alizowaandikia. Msiabudu miungu mingine. 3817:38 Kum 6:12Msisahau agano nililofanya nanyi, wala msiabudu miungu mingine. 39Bali, mtamwabudu Bwana Mungu wenu, kwani yeye ndiye atakayewakomboa kutoka mikononi mwa adui zenu wote.”

40Hata hivyo hawakusikiliza, lakini waliendelea na desturi zao za awali. 4117:41 1Fal 18:21; Mt 6:24Hata wakati watu hawa walipokuwa wanamwabudu Bwana, walikuwa bado wakitumikia sanamu zao. Mpaka leo watoto wao na watoto wa watoto wao wanaendelea kufanya kama baba zao walivyofanya.