出埃及记 30 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

出埃及记 30:1-38

造香坛的条例

1“你要用皂荚木造一座烧香用的坛。 2坛是四方形的,长宽各四十五厘米,高九十厘米,坛上面凸起的四角与坛连成一体。 3坛顶、坛的四面和坛上凸起的角要包上纯金,四周镶上金边。 4要在坛两侧的金边下面安两个金环,使横杠穿过金环,以便抬香坛。 5要用皂荚木造横杠,包上金。 6要把香坛放在约柜前幔子的外面,对着约柜上的施恩座,就是我要跟你会面的地方。

7亚伦每天早上料理灯台的时候,要在这坛上烧芬芳的香。 8黄昏点灯的时候,他也要在耶和华面前烧香,世世代代都要如此。 9不可在这香坛上烧别的香料,不可用这坛来献燔祭或素祭,也不可在上面浇奠祭。 10亚伦每年要用赎罪祭牲的血在坛的角上行一次赎罪礼,世代如此。这是耶和华至圣的坛。”

人丁的赎价

11耶和华对摩西说: 12“你统计以色列人口的时候,每一个被统计的男子都要缴付赎价给耶和华,赎回自己的性命,免得在统计人口期间发生灾祸。 13凡被统计的人都要付六克银子,即十季拉,以圣所的秤为准,作为献给耶和华的礼物。 14凡被统计的,年龄在二十岁以上的男子都要献此礼物给耶和华。 15富有的不用多缴,贫穷的也不可少付,每个人都要献六克银子给耶和华,用来赎自己的性命。 16要向以色列人收赎命的款项,供会幕使用,可以使以色列人在耶和华面前蒙眷顾,赎性命。”

洗濯盆

17耶和华对摩西说: 18“你用铜造一个洗濯盆和盆座,放在会幕和祭坛之间,盆里盛着水, 19亚伦父子们洗手洗脚, 20他们进会幕或到坛前给耶和华献火祭之前,一定要用水洗濯才可以供职,免得死亡。 21他们要洗手洗脚,免得死亡,这是亚伦及其子孙世代当守的永久律例。”

22耶和华对摩西说: 23“要用上等的香料,就是没药汁六公斤、香肉桂和菖蒲各三公斤、 24肉桂皮六公斤,都按圣所的秤为准,再加上橄榄油四升, 25按着调制香料的方法制作圣膏油。 26要用这些膏油来抹会幕、约柜、 27桌子和桌上所有的器具、灯台和灯台上的器具、香坛、 28燔祭坛和坛上所有的器具、洗濯盆和盆座。 29你要使这一切圣洁,成为至圣之物。凡碰到它们的都会圣洁。

30“你也要用这油来膏亚伦父子们,使他们分别出来,做圣洁的祭司事奉我。 31你要把我的话告诉以色列百姓,‘我要世世代代以这油为圣膏油。 32不要把这膏油用在普通人身上,也不可仿制,因为这是圣膏油,你们也要视之为圣物。 33任何人若仿制或用这油抹祭司以外的人,要将他从民中铲除。’”

34耶和华对摩西说:“要取各种芬芳的香料,就是苏合香、香螺、白松香和纯乳香,分量相同, 35用调制香料的方法调制,加上盐,做成纯净圣洁的香。 36你们要把一些香捣成极细的粉末,放在会幕内的约柜前面,就是我与你会面的地方,你们要视这香为至圣之物。 37你们不可用同样的配方为自己做香,要视它为耶和华的圣物。 38任何人若仿制这香,自己拿来私用30:38 “私用”希伯来文是“闻这香味”。,必从民中被铲除。”

Kiswahili Contemporary Version

Kutoka 30:1-38

Madhabahu Ya Kufukizia Uvumba

(Kutoka 37:25-28)

130:1 Kut 40:5, 26; Hes 4:11; 1Fal 6:20; Eze 41:22; Kut 25:6; 37:29; Lk 1:11; Ebr 9:4; Ufu 8:3“Tengeneza madhabahu kwa mbao za mshita kwa ajili ya kufukizia uvumba. 230:2 Kut 27:2; Ufu 9:13Madhabahu hayo yawe mraba, urefu na upana wake dhiraa moja,30:2 Dhiraa moja ni sawa na sentimita 45. na kimo cha dhiraa mbili,30:2 Dhiraa mbili ni sawa na sentimita 90. nazo pembe zake zitakuwa kitu kimoja nayo. 330:3 Kut 25:11Funika hayo madhabahu juu na pande zote na pia pembe zake kwa dhahabu safi, na uifanyizie ukingo wa dhahabu kuizunguka. 430:4 Kut 25:12Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya madhabahu chini ya huo ukingo, ziwe mbili kila upande, za kushikilia hiyo mipiko itumikayo kuibebea madhabahu. 530:5 Kut 25:13Tengeneza mipiko kwa miti ya mshita na uifunike kwa dhahabu. 630:6 Kut 25:22; 26:34Weka hayo madhabahu mbele ya lile pazia lililo mbele ya Sanduku la Ushuhuda, lililo mbele ya kiti cha rehema kilicho juu ya Sanduku la Ushuhuda, mahali ambapo nitakutana nawe.

730:7 Kut 26:6; 40:27; Hes 3:10; Kum 33:10; 1Sam 2:28; 1Nya 6:49; 2Nya 2:4; 26:18“Itampasa Aroni kufukiza uvumba wenye harufu nzuri juu ya madhabahu kila siku asubuhi wakati anapowasha zile taa. 830:8 Kut 25:37; 29:42Itampasa afukize uvumba tena wakati anapowasha taa wakati wa machweo ili uvumba ufukizwe daima mbele za Bwana kwa vizazi vijavyo. 930:9 Law 10:1; Hes 16:7, 40Usifukize uvumba mwingine wowote juu ya madhabahu haya au sadaka nyingine yoyote ya kuteketezwa wala sadaka ya nafaka, wala usimimine sadaka ya kinywaji juu yake. 1030:10 Law 16:2; 9:7; 16:18-19; 23:27-28; 25:9; Kut 29:14; Law 4:3; 6:25; 7:7; 8:2; 14; Hes 6:11; Kut 29:42Mara moja kwa mwaka Aroni atafanya upatanisho juu ya pembe za hayo madhabahu. Upatanisho huu wa mwaka lazima ufanywe kwa damu ya sadaka ya upatanisho kwa ajili ya dhambi kwa vizazi vijavyo. Ni takatifu sana kwa Bwana.”

Fedha Ya Upatanisho

11Naye Bwana akamwambia Mose, 1230:12 Kut 38:25; Hes 1:2, 49; 4:2, 29; 14:29; 14:29; 26:2; 31:26; 2Sam 24:1; 2Fal 12:4; Kut 38:26; Hes 31:50; Mt 20:28; Hes 14:12; Kum 28:58-61; 2Sam 24:13; 1Fal 8:37“Utakapowahesabu Waisraeli, kila mmoja lazima alipe kwa Bwana fidia kwa ajili ya nafsi yake wakati wa kuhesabiwa kwake. Ndipo hakutakuwa na pigo juu yao unapowahesabu. 1330:13 Kut 38:24-26; Law 15:15; 27:3; Hes 3:47; 7:13; 18:16; Eze 4:10; 45:12; Mt 17:24Kila mmoja anayekwenda upande wa wale waliokwisha hesabiwa atatoa nusu shekeli,30:13 Nusu shekeli ni sawa na gramu 6. kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, ambayo ina uzito wa gera ishirini.30:13 Gera 20 ni sawa na shekeli moja au gramu 12. Hii nusu shekeli ni sadaka kwa Bwana. 1430:14 Kut 38:26; Hes 14:29; 26:2; 32:11; 2Nya 25:5Wote wale wanaovuka, wenye umri wa miaka ishirini au zaidi, watatoa sadaka kwa Bwana. 1530:15 Mit 22:2; Efe 6:9Matajiri hawatalipa zaidi ya nusu shekeli, nao maskini hawatatoa pungufu wakati mnatoa sadaka kwa Bwana kwa kufanya upatanisho wa nafsi zenu. 1630:16 Kut 38:25-28; 2Nya 24:5; Hes 31:54Utapokea fedha ya upatanisho kutoka kwa Waisraeli na uzitumie kwa ajili ya huduma ya Hema la Kukutania. Itakuwa ni ukumbusho kwa Waisraeli mbele za Bwana kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu.”

Sinia La Kunawia

17Kisha Bwana akamwambia Mose, 1830:18 Kut 31:9; 35:16; 38:8; 39:39; 40:7, 30; 1Fal 7:38; 2Nya 4:6“Tengeneza sinia la shaba lenye kitako cha shaba kwa ajili ya kunawia. Liweke kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, kisha uweke maji ndani yake. 1930:19 Kut 40:31-32; Yn 13:10; Kut 29:4; 40:12; Law 8:6; Za 26:6; Ebr 10:22Aroni na wanawe watanawa mikono na miguu yao kwa maji yatokayo katika hilo sinia. 2030:20 Kut 28:43Wakati wowote wanapoingia katika Hema la Kukutania, watanawa kwa maji ili kwamba wasije wakafa. Pia, wanapokaribia madhabahu ili kuhudumu kwa kuleta sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, 2130:21 Kut 27:21; 28:43; 29:42watanawa mikono na miguu yao ili kwamba wasije wakafa. Hii itakuwa ni amri ya kudumu kwa ajili ya Aroni na wazao wake kwa vizazi vijavyo.”

Mafuta Ya Upako

2230:22 Mwa 43:11; 37:25; Mit 7:17; Wim 4:14; Isa 43:24; Yer 6:20Kisha Bwana akamwambia Mose, 2330:23 Wim 4:14; Eze 27:22; Za 45:8; Yer 6:20“Chukua vikolezi bora vifuatavyo: shekeli 50030:23 Shekeli 500 ni sawa na kilo 6. za manemane ya maji, shekeli 25030:23 Shekeli 250 ni sawa na kilo 3. za mdalasini wenye harufu nzuri, shekeli 250 za miwa yenye harufu nzuri, 2430:24 Za 45:8; Eze 27:19; Kut 29:40shekeli 500 za aina nyingine ya mdalasini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, pia hini30:24 Hini moja ni sawa na lita 4. ya mafuta ya zeituni. 2530:25 1Nya 9:30; Kut 37:29; 29:7; 1Sam 9:16; Hes 35:25; Za 133:2Vitengeneze vikolezi hivi kuwa mafuta matakatifu ya upako yenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato. Yatakuwa mafuta matakatifu ya upako. 2630:26 Kut 40:9; Law 8:10; Hes 7:1Kisha yatumie kupaka hilo Hema la Kukutania, Sanduku la Ushuhuda, 27meza na vifaa vyake vyote, kinara cha taa na vifaa vyake vyote, madhabahu ya kufukizia uvumba, 28madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake vyote na sinia pamoja na kitako chake. 2930:29 Law 8:10-11; 6:18, 27; Kut 29:37; Mt 23:17Utaviweka wakfu ili viwe vitakatifu sana na kila kitakachoigusa kitakuwa kitakatifu.

3030:30 Kut 29:7; Law 8:2, 12, 30; 10:7; 16:32; 21:10-12; 1Nya 15:12; Za 133:2; Kut 28:41“Mtie Aroni na wanawe mafuta na uwaweke wakfu ili waweze kunitumikia katika kazi ya ukuhani. 3130:31 Kut 29:7, 42Waambie Waisraeli, ‘Haya yatakuwa mafuta matakatifu yangu ya upako kwa vizazi vijavyo. 32Usiyamimine juu ya miili ya wanadamu wala usitengeneze mafuta ya aina nyingine kwa utaratibu huu. Ni mafuta matakatifu na ni lazima myaone kuwa ni matakatifu. 3330:33 Mwa 17:14; Law 7:20, 21Mtu yeyote atakayetengeneza manukato kama hayo na yeyote atakayeyamimina juu ya mtu yeyote ambaye si kuhani atakatiliwa mbali na watu wake.’ ”

Uvumba

3430:34 Wim 3:6; Kut 25:6; 37:29Kisha Bwana akamwambia Mose, “Chukua vikolezi vyenye harufu nzuri vifuatavyo: natafi, shekelethi, kelbena na uvumba safi vyote vikiwa na vipimo sawa, 3530:35 Kut 25:6pia tengeneza mchanganyiko wa uvumba wenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato. Utiwe chumvi ili upate kuwa safi na mtakatifu. 3630:36 Kut 29:37; Law 2:3Saga baadhi yake kuwa unga na uweke mbele ya Sanduku la Ushuhuda ndani ya Hema la Kukutania, mahali ambapo nitakutana nawe. Itakuwa takatifu sana kwenu. 37Msitengeneze uvumba mwingine wowote wa namna hii kwa ajili yenu wenyewe; uoneni kuwa ni mtakatifu kwa Bwana. 38Yeyote atakayetengeneza uvumba kama huu ili kufurahia harufu yake nzuri lazima akatiliwe mbali na watu wake.”