使徒行传 6 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

使徒行传 6:1-15

选立执事

1那时,门徒的人数与日俱增。当中有些讲希腊话的犹太人埋怨讲希伯来话的犹太人,说对方在日常分配食物的事上怠慢了他们的寡妇。 2于是,十二使徒召集所有的门徒,对他们说:“我们不应该忽略传上帝的道,去管理膳食。 3弟兄姊妹,请从你们中间选出七位声誉良好、充满圣灵和智慧的人来负责膳食, 4而我们要专心祈祷和传道。”

5大家一致同意,便选出充满信心和圣灵的司提凡,此外还有腓利伯罗哥罗尼迦挪提门巴米拿,以及曾信过犹太教、来自安提阿的外族人尼哥拉6大家将这七个人带到使徒面前。使徒为他们祷告并按手在他们身上。

7上帝的道兴旺起来,耶路撒冷的门徒大大增多,连许多祭司也归信了。

司提凡被捕

8司提凡满有恩典和能力,在百姓中间行了惊人的神迹奇事。 9但有些来自古利奈亚历山大基利迦亚细亚、属于“自由人6:9 “自由人”指的是原为奴隶,后来获得自由的人。会堂”的犹太人联合起来与司提凡辩论。 10他们无法驳倒司提凡,因为他靠着智慧和圣灵说话。

11于是,他们暗中唆使一些人诬告司提凡说:“我们听见他说亵渎摩西和上帝的话!” 12又煽动百姓、长老和律法教师抓住司提凡,把他押到公会。 13他们还派人作伪证说:“司提凡常常讲侮辱圣地6:13 “圣地”指“圣殿”。和律法的话。 14我们听见他说那个拿撒勒人耶稣要毁坏圣殿,还要更改摩西传给我们的规矩。” 15公会在座的人都盯着司提凡,只见他的面容好像天使的面容。

Kiswahili Contemporary Version

Matendo 6:1-15

Mateso Na Kuenea Kwa Injili

(6:1–9:31)

Saba Wachaguliwa Kuhudumu

16:1 Mdo 2:21; 4:35; 9:29, 39-41; 1Tim 5:3Basi ikawa katika siku hizo, wakati idadi ya wanafunzi ilipokuwa ikiongezeka sana, palitokea manungʼuniko kati ya Wayahudi wa Kiyunani, dhidi ya Waebrania kwa sababu wajane wao walisahaulika katika mgawanyo wa chakula wa kila siku. 26:2 Mdo 11:26; Ebr 4:12; Kut 18:17Wale mitume kumi na wawili wakakusanya wanafunzi wote pamoja wakasema, “Haitakuwa vyema sisi kuacha huduma ya neno la Mungu ili kuhudumu mezani. 36:3 Mdo 1:14-16; Lk 1:15; Kut 18:21; Neh 13:13; 1Tim 3:7, 8Kwa hiyo ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, watu wenye sifa njema, waliojawa na Roho Mtakatifu na hekima, ambao tunaweza kuwakabidhi kazi hii, 46:4 Mdo 2:42nasi tutatumia muda wetu kuomba na huduma ya neno.”

56:5 Mdo 11:19; 22:20; 8:5-40; 21:8; Lk 1:15Yale waliyosema yakawapendeza watu wote, nao wakamchagua Stefano (mtu aliyejawa na imani na Roho Mtakatifu) pamoja na Filipo, Prokoro, Nikanori, Timoni, Parmena na Nikolao, mwongofu kutoka Antiokia. 66:6 Mdo 13:3; 2Tim 1:6; Hes 27; 18; Mk 5:23Wakawaleta watu hawa mbele ya mitume, nao wakawaombea na kuwawekea mikono juu yao.

76:7 Mdo 12:24; 19:20Neno la Mungu likazidi kuenea. Idadi ya wanafunzi ikazidi kuongezeka sana katika Yerusalemu hata makuhani wengi wakaitii ile imani.

Kukamatwa Kwa Stefano

86:8 Yn 4:48Stefano, akiwa amejaa neema na nguvu za Mungu, alifanya ishara na miujiza mikubwa miongoni mwa watu. 96:9 Mt 27:32; 22:3; 23:34; 2:9Hata hivyo, ukainuka upinzani wa watu wa Sinagogi la Watu Huru (kama lilivyokuwa linaitwa), la Wayahudi wa Kirene na wa Iskanderia, na wengine kutoka Kilikia na Asia. Watu hawa wakaanza kupingana na Stefano. 106:10 Lk 21:15; Mdo 5:39Lakini hawakuweza kushindana na hekima yake wala huyo Roho ambaye alisema kwake.

116:11 2Fal 21:10; Mt 26:59-61Ndipo kwa siri wakawashawishi watu fulani waseme, “Tumemsikia Stefano akisema maneno ya kufuru dhidi ya Mose na dhidi ya Mungu.”

Stefano Afikishwa Mbele Ya Baraza

126:12 Mt 5:22Wakawachochea watu, wazee na walimu wa Sheria, nao wakamkamata Stefano wakamfikisha mbele ya baraza. 136:13 Mt 24:15; Mdo 7:48Wakaweka mashahidi wa uongo ambao walishuhudia wakisema, “Mtu huyu kamwe haachi kusema dhidi ya mahali hapa patakatifu na dhidi ya Sheria. 146:14 Mdo 26:3; 28:17Kwa maana tumemsikia akisema kwamba Yesu wa Nazareti atapaharibu mahali patakatifu na kubadili desturi zote tulizopewa na Mose.”

156:15 Mt 5:22Watu wote waliokuwa wameketi katika baraza wakimkazia macho Stefano, wakaona uso wake unangʼaa kama uso wa malaika.