但以理书 12 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

但以理书 12:1-13

末日

1“那时,守护你同胞的天使长米迦勒必挺身而出。将有一段灾难时期,是开国以来从未有过的。那时,你同胞中凡名字记在册子上的,必得拯救。 2许多长眠地下的人必醒过来,有些得到永生,有些蒙受羞辱,永远被憎恶。 3智者必发出光辉,如耀眼的穹苍;引导多人归向公义的人必如闪亮的星辰,直到永永远远。 4但以理啊,这些话要保密,要把这书封起来,直到末了。许多人必四处探究,因而知识必增多。”

5但以理观看,看见另有两个人分别站在河的两岸。 6其中一人问身穿细麻衣、站在河水之上的人:“这奇异的事何时才应验呢?” 7我听见身穿细麻衣、站在河水之上的人向天举起双手,凭永活者起誓说:“再过三年半,等摧毁圣民的权势结束时,这一切事都要成就。” 8我听见这话,却不明白,就问他:“我主啊,这些事的结局会怎样呢?” 9他说:“但以理啊,你走吧,因为这些事要保密,要被封起来,一直到末了。 10许多人必被净化、洗涤、炼净。但恶人必依旧作恶,他们无人明白,只有智者能明白。 11从废除日常献的祭、设立带来毁灭的可憎之物算起,必经过一千二百九十天。 12能等候一千三百三十五天的人有福了! 13你要坚持到底。你必得到安息,到了末后的日子,你必起来承受你的产业。”

Kiswahili Contemporary Version

Danieli 12:1-13

Nyakati Za Mwisho

112:1 Dan 10:13; Yud 9; Dan 9:12; Lk 10:20; Yer 17:13; Mt 24:21; Mk 13:19; Yer 30:7; Za 56:8; Kut 32:32“Katika wakati huo Mikaeli, mtawala mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwako wakati wa taabu ambao haujatokea tangu mwanzo wa mataifa hadi wakati huo. Lakini wakati huo, watu wako, kila mmoja ambaye jina lake litakutwa limeandikwa kwenye kitabu, ataokolewa. 212:2 Isa 26:19; Yn 5:28-29; Mt 25:46; Yn 11:24Wengi ambao wamelala kwenye mavumbi wataamka, baadhi yao kwa uzima wa milele, wengine kwa aibu na kudharauliwa milele. 312:3 Dan 11:33; Yn 5:35; Flp 2:15; Mit 4:18; 1Kor 15:42; Mt 13:43Wale wenye hekima watangʼaa kama mwanga wa mbingu, nao wale ambao huwaongoza wengi kutenda haki, watangʼaa kama nyota milele na milele. 412:4 Isa 8:16; Ufu 22:10; Yer 5:1Lakini wewe Danieli, yafunge na kuyatia muhuri maneno ya kitabu hiki mpaka wakati wa mwisho. Wengi watakwenda huku na huko, na maarifa yataongezeka.”

512:5 Dan 10:4Ndipo mimi Danieli nikaangalia, nako mbele yangu walisimama wengine wawili, mmoja katika ukingo huu wa mto, na mwingine ukingo wa pili wa mto. 612:6 Eze 9:2; Dan 8:13; Za 74:9Mmoja wao akasema na yule mtu aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, “Je, itachukua muda gani kabla mambo haya ya kushangaza hayajatimizwa?”

712:7 Dan 6:26; Ufu 10:5-7; Lk 21:24; Dan 8:24; 8:24; Ufu 11:2; Mwa 14:22Kisha mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, akainua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni, nami nikamsikia akiapa kwa jina lake yeye aishiye milele, akisema, “Itakuwa wakati, nyakati mbili, na nusu wakati.12:7 Wakati, nyakati mbili na nusu wakati maana yake mwaka mmoja, miaka miwili, na nusu mwaka, yaani miaka mitatu na nusu. Nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimevunjwa kabisa, ndipo mambo haya yote yatakapotimizwa.”

8Nilisikia, lakini sikuelewa. Kwa hiyo nikauliza, “Bwana wangu, matokeo ya haya yote yatakuwa nini?”

912:9 Isa 29:11Akajibu, “Danieli, enenda zako, kwa sababu maneno haya yamefungwa na kutiwa muhuri mpaka wakati wa mwisho. 1012:10 Isa 1:25; Zek 13:9; Hos 14:9; Isa 32:7; Ufu 22:11; Dan 11:35Wengi watatakaswa, na kuondolewa mawaa na kufanywa safi, lakini waovu wataendelea kuwa waovu. Hakuna mmoja wa waovu atakayefahamu, lakini wale wenye hekima watafahamu.

1112:11 Mk 13:14; Dan 8:11; 9:27; Mt 24:15; Kut 29:38; Ufu 11:2“Tangu wakati ule wa kukomeshwa dhabihu ya kila siku na kusimamishwa kwa chukizo la uharibifu, kutakuwako siku 1,290. 1212:12 Isa 30:18; Eze 4:5-6; Dan 8:14Amebarikiwa mtu yule atakayevumilia hadi kufikia mwisho wa hizo siku 1,335.

1312:13 Isa 57:2“Lakini wewe, enenda zako mpaka mwisho. Utapumzika, nawe ndipo mwisho wa hizo siku utafufuka ili kuupokea urithi uliowekewa.”