以赛亚书 56 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

以赛亚书 56:1-12

外族人蒙拯救

1耶和华说:

“你们当坚持正义,

秉行公义,

因为我的救恩快要来临,

我的公义快要彰显。

2谨守而不亵渎安息日、

不做恶事的人有福了!”

3皈依耶和华的外族人啊,

不要以为耶和华会把你和祂的子民分开,

太监也不要觉得自己只是一棵枯树。

4因为耶和华说:

“如果太监遵守我的安息日、

做我喜悦的事、

持守我的约,

5我必在我的殿中、

墙内赐给他们纪念碑和名号,

使他们胜过有儿女的人。

我必赐给他们永远不会被除去的名号。

6至于那些皈依耶和华、

事奉祂、爱祂的名、

做祂的仆人、

谨守而不亵渎安息日、

持守祂的约的外族人,

7我必领他们到我的圣山,

到向我祷告的殿内,

使他们欢欣。

他们献上的燔祭和其他祭物必蒙悦纳,

因为我的殿必被称为万民祷告的殿。”

8招聚以色列流亡者的主耶和华说:

“除了这些被招聚回来的人以外,

我还要招聚其他人。”

以色列昏庸的首领

9田野和林中的走兽啊,

来吞吃吧!

10以色列的守望者瞎眼无知,

是不会叫的哑巴狗,

只喜欢躺下睡觉做梦。

11这些人就像贪吃的狗,

不知饱足,

又像什么都不懂的牧人,

人人各行其是,

追求自己的利益。

12他们说:“来吧,我去拿酒,

让我们喝个痛快!

明天会跟今天一样,

甚至更丰盛。”

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 56:1-12

Wokovu Kwa Ajili Ya Wengine

156:1 Yer 22:3; Rum 13:11; Za 85:9; Dan 9:24; Yer 23:6; Isa 26:8Hili ndilo asemalo Bwana:

“Dumisheni haki

na mkatende lile lililo sawa,

kwa maana wokovu wangu u karibu

na haki yangu itafunuliwa upesi.

256:2 Kut 20:8-10; Isa 58:3; Za 119:2Amebarikiwa mtu yule atendaye hili,

mtu yule alishikaye kwa uthabiti,

yeye ashikaye Sabato bila kuinajisi,

auzuiaye mkono wake usifanye uovu wowote.”

356:3 Law 21:20; Mdo 8:27; Kut 12:43; 1Fal 8:41; Zek 8:20-23; Yer 38:7; Kum 23:3Usimwache mgeni aambatanaye na Bwana aseme,

“Hakika Bwana atanitenga na watu wake.”

Usimwache towashi yeyote alalamike akisema,

“Mimi ni mti mkavu tu.”

456:4 Yer 38:7; Kut 31:13Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana:

“Kwa matowashi washikao Sabato zangu,

ambao huchagua kile kinachonipendeza

na kulishika sana agano langu:

556:5 1Tim 5:13; Isa 60:18; 48:19; 55:13; Ufu 3:12; Hes 32:42; 1Sam 15:12; Isa 47:3hao nitawapa ndani ya Hekalu langu na kuta zake

kumbukumbu na jina bora

kuliko kuwa na watoto wa kiume na wa kike:

nitawapa jina lidumulo milele,

ambalo halitakatiliwa mbali.

656:6 1Nya 22:2; Isa 61:5; Kut 12:43; 1Fal 8:41; Isa 60:7-10Wageni wanaoambatana na Bwana

ili kumtumikia,

kulipenda jina la Bwana,

na kumwabudu yeye,

wote washikao Sabato bila kuinajisi

na ambao hushika sana agano langu:

756:7 Eze 20:40; Rum 12:1; Isa 19:21; Flp 4:18; Mt 21:13; Mk 11:17; Isa 19:21; Lk 19:46hawa nitawaleta kwenye mlima wangu mtakatifu

na kuwapa furaha ndani ya nyumba yangu ya sala.

Sadaka zao za kuteketeza na dhabihu zao

zitakubalika juu ya madhabahu yangu;

kwa maana nyumba yangu itaitwa

nyumba ya sala kwa mataifa yote.”

856:8 Eze 34:12; Yn 10:16; Efe 1:10; Kum 30:4; Isa 11:12; 60:3-11Bwana Mwenyezi asema, yeye awakusanyaye

Waisraeli waliohamishwa:

“Bado nitawakusanya wengine kwao

zaidi ya hao ambao wamekusanywa tayari.”

Mashtaka Ya Mungu Dhidi Ya Waovu

956:9 Yer 12:9; Eze 34:5-8; Isa 18:6; Eze 39:17-20Njooni, enyi wanyama wote wa kondeni,

njooni mle, ninyi wanyama wote wa mwituni!

1056:10 Mt 15:14; Eze 3:17; Nah 3:18; Isa 52:8; 62:6; Yer 6:17; 31:6; 14:13-14Walinzi wa Israeli ni vipofu,

wote wamepungukiwa na maarifa;

wote ni mbwa walio bubu,

hawawezi kubweka;

hulala na kuota ndoto,

hupenda kulala.

1156:11 Yer 23:1; 8:10; Eze 34:2; Mik 3:11; Isa 53:6; Hos 4:7-8; Isa 57:17Ni mbwa wenye tamaa kubwa,

kamwe hawatosheki.

Wao ni wachungaji waliopungukiwa na ufahamu;

wote wamegeukia njia yao wenyewe,

kila mmoja hutafuta faida yake mwenyewe.

1256:12 Za 10:6; Lk 12:18-19; Law 10:9; Mit 23:20; Isa 42:25Kila mmoja hulia, “Njooni, tupate mvinyo!

Tunywe kileo sana!

Kesho itakuwa kama leo,

au hata bora zaidi.”