以赛亚书 49 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

以赛亚书 49:1-26

主的仆人

1众海岛啊,听我说!

远方的列邦啊,要留心听!

我还没有出生,

耶和华就呼召我;

我还没有离开母腹,

祂就提及我的名。

2祂使我的口像利剑,

用祂的手荫庇我;

祂使我成为磨亮的箭,

把我藏在祂的箭囊中。

3祂对我说:“以色列啊,

你是我的仆人,

我要借着你彰显我的荣耀。”

4但我说:“我虚耗精力,

徒劳无功。

然而,耶和华必公正地待我,

我的报酬在我的上帝那里。”

5我在母腹之中,耶和华便塑造我做祂的仆人,

叫我带领雅各归向祂,

以色列人召集到祂那里。

我在耶和华眼中是尊贵的,

我的上帝是我的力量。

6祂对我说:“我不单单只是让你做我的仆人,

去复兴雅各的众支派,

使以色列得保全的人重归故土。

我还要使你成为外族人的光,

好把我的救恩带到地极。”

7以色列的救赎主和圣者耶和华对受藐视、

被本国人憎恨、

遭官长奴役的那位说:

“因着信实的耶和华——拣选你的以色列的圣者,

君王一见你必肃然起立,

首领一见你必俯伏下拜。”

以色列的复兴

8耶和华说:

“在悦纳的时候,我应允了你;

在拯救的日子,我帮助了你。

我要保护你,

使你做我跟民众立约的中保,

复兴这片土地,

分配荒凉的产业。

9你要对被囚禁的人说,

‘出来吧!’

要对黑暗中的人说,

‘你们自由了。’

他们在路上必有吃的,

光秃的山岭上必有食物。

10他们不再饥渴,

也不再被热风和烈日灼伤,

因为怜悯他们的那位必引导他们,

领他们到泉水边。

11我要使我的群山变为通途,

修筑我的大路。

12看啊,他们必从远方来。

有的来自北方,有的来自西方,

还有的来自希尼49:12 “希尼”可能指遥远的东方或南方某地。。”

13诸天啊,要欢呼!

大地啊,要快乐!

群山啊,要歌唱!

因为耶和华安慰祂的子民,

怜悯祂受苦的百姓。

14锡安说:“耶和华撇弃了我,

主把我忘了。”

15耶和华说:“母亲岂能忘记自己吃奶的婴儿,

不怜悯自己亲生的孩子?

就算有母亲忘记,

我也不会忘记你。

16看啊,我已经把你铭刻在我的手掌上,

你的墙垣时刻在我的看顾之下。

17你的儿女必很快回来,

毁灭和破坏你的必离你而去。

18举目四下看看吧,

你的儿女正聚集到你这里。

我凭我的永恒起誓,

你必把他们作为饰物戴在身上,

如新娘一样用他们妆扮自己。

这是耶和华说的。

19“你那荒废、凄凉、

遭到毁坏之地现在必容不下你的居民,

那些吞灭你的人必远远地离开你。

20你流亡期间所生的子女必在你耳边说,

‘这地方太小了,

再给我们一些地方住吧。’

21你会在心里问,‘我丧失了儿女、

不再生育,流亡在外,漂流不定,

谁给我生了这些儿女?

谁把他们养大?

我孤身留下,

他们是从哪里来的?’”

22主耶和华说:

“看啊,我必向列国招手,

向万民竖立我的旗帜,

他们必抱着你的儿子、

背着你的女儿回来。

23列王必做你的养父,

王后必做你的乳母。

他们必向你俯伏下拜,

舔你脚上的尘土。

那时你便知道我是耶和华,

仰望我的必不致羞愧。”

24勇士抢去的能夺回来吗?

暴君掳走的能救回来吗?

25但耶和华说:

“勇士掳去的必被夺回,

暴君抢去的必被救出。

我必与你的对头作对,

拯救你的儿女。

26我要使那些欺压你的人吞吃自己的肉,

喝自己的血喝得酩酊大醉,

好像喝酒一样。

那时候,世人都必知道我耶和华是你的救主,

是你的救赎主,

雅各的大能者。”

Kiswahili Contemporary Version

Isaya 49:1-26

Mtumishi Wa Bwana

149:1 Isa 44:24; Yer 1:5; Lk 1:15; Isa 33:13; 11:11; Mt 1:20; Isa 7:14; 9:6; Kut 33:12Nisikilizeni, enyi visiwa, sikieni hili,

ninyi mataifa mlio mbali:

Kabla sijazaliwa, Bwana aliniita,

tangu kuzaliwa kwangu, amelitaja jina langu.

249:2 Za 64:3; Hos 6:5; Efe 6:17; Ay 40:18; Ufu 1:16; Kut 33:22; Zek 9:13Akafanya kinywa changu kuwa kama upanga ulionolewa,

katika uvuli wa mkono wake akanificha;

akanifanya kuwa mshale uliosuguliwa,

na kunificha katika podo lake.

349:3 Isa 20:3; Zek 3:8; Law 10:3; Isa 44:23Akaniambia, “Wewe u mtumishi wangu,

Israeli, ambaye katika yeye

nitaonyesha utukufu wangu.”

449:4 Eze 3:19; Law 26:20; Isa 35:4; Ay 27:2; Isa 55:2; 65:23; 45:25; 54:17Lakini nilisema, “Nimetumika bure,

nimetumia nguvu zangu bure bila faida.

Hata hivyo linalonistahili liko mkononi mwa Bwana,

nao ujira wangu uko kwa Mungu wangu.”

549:5 Kum 30:4; Isa 11:12; 43:4; Za 139:13; Gal 1:15; Za 18:1Sasa Bwana asema:

yeye aliyeniumba tumboni kuwa mtumishi wake,

kumrudisha tena Yakobo kwake

na kumkusanyia Israeli,

kwa maana nimepata heshima machoni pa Bwana,

naye Mungu wangu amekuwa nguvu yangu;

649:6 Zek 8:22; Lk 2:32; Yn 11:52; Isa 9:2; Yon 1:9; Isa 26:18; Kum 30:4; Mdo 13:47yeye asema:

“Je, ni jambo dogo sana wewe kuwa mtumishi wangu

ili kurejeza makabila ya Yakobo,

na kuwarudisha wale Waisraeli niliowahifadhi?

Pia nitakufanya uwe nuru kwa ajili ya watu wa Mataifa,

ili upate kuleta wokovu wangu hata miisho ya dunia.”

749:7 Isa 48:17; Za 69:7-9; Isa 52:15; Mwa 27:29; Za 22:6, 29; 86:9; Kum 7:9Hili ndilo asemalo Bwana,

yeye Mkombozi na Aliye Mtakatifu wa Israeli,

kwake yeye aliyedharauliwa na kuchukiwa na taifa,

kwa mtumishi wa watawala:

“Wafalme watakuona na kusimama,

wakuu wataona na kuanguka kifudifudi,

kwa sababu ya Bwana, aliye mwaminifu,

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, aliyekuchagua wewe.”

Kurejezwa Kwa Israeli

849:8 Za 69:13; 2Kor 6:2; Law 25:10; Za 37:9; Isa 60:10; 41:10; 26:3; 5:249:8 Isa 44:28; Neh 2:17Hili ndilo asemalo Bwana:

“Wakati wangu uliokubalika nitakujibu,

nami katika siku ya wokovu nitakusaidia;

nitakuhifadhi, nami nitakufanya

kuwa agano kwa ajili ya watu,

ili kurudisha nchi

na kugawanyia urithi tena wale waliokuwa ukiwa,

949:9 Lk 4:19; Isa 41:18; Zek 9:12; Isa 42:7; Za 107:10kuwaambia mateka, ‘Tokeni nje,’

nao wale walio gizani, ‘Kuweni huru!’

“Watajilisha kando ya barabara

na kupata malisho yao juu ya kila kilima kilicho kitupu.

1049:10 Isa 33:16; Ufu 7:16; Isa 35:7; Za 21:6; Isa 42:16; 33:21Hawataona njaa wala kuona kiu,

wala hari ya jangwani au jua halitawapiga.

Yeye mwenye huruma juu yao atawaonyesha njia,

na kuwaongoza kando ya chemchemi za maji.

1149:11 Isa 11:6; Yer 31:9; Isa 40:4Nitaifanya milima yangu yote kuwa barabara,

na njia kuu zangu zitainuliwa.

1249:12 Isa 2:3; 43:5-6; 59:19; Mt 8:11Tazama, watakuja kutoka mbali:

wengine kutoka kaskazini, wengine kutoka magharibi,

wengine kutoka nchi ya Sinimu.”49:12 Sinimu hapa ina maana ya Aswani.

1349:13 Za 98:4; 71:21; 2Kor 1:4; Isa 48:20; Za 96:11; 65:12-13; 9:12Pigeni kelele kwa furaha, enyi mbingu;

furahi, ee dunia;

pazeni sauti kwa kuimba, enyi milima!

Kwa maana Bwana anawafariji watu wake,

naye atakuwa na huruma kwa watu wake walioumizwa.

1449:14 Isa 40:9; Za 9:10; Isa 27:8; Za 71:11Lakini Sayuni alisema, “Bwana ameniacha,

Bwana amenisahau.”

1549:15 Mt 7:11; Isa 44:21; 1Fal 3:26; Isa 66:13“Je, mama aweza kumsahau mtoto

aliyeko matitini mwake akinyonya,

wala asiwe na huruma

juu ya mtoto aliyemzaa?

Ingawa anaweza kusahau,

mimi sitakusahau wewe!

1649:16 Wim 8:6; Kut 28:9; Za 48:12-13; Isa 62:6; Mwa 38:18Tazama, nimekuchora kama muhuri

katika vitanga vya mikono yangu,

kuta zako zi mbele yangu daima.

1749:17 Isa 49:19Wana wako wanaharakisha kurudi,

nao wale waliokuteka wanaondoka kwako.

1849:18 Mit 17:6; Rum 14:11; Hes 14:21; Yer 2:32; Isa 11:12; 43:5; 54:9; 45:23Inua macho yako ukatazame pande zote:

wana wako wote wanakusanyika na kukujia.

Kwa hakika kama vile niishivyo,

utawavaa wote kama mapambo,

na kujifunga nao kama bibi arusi,”

asema Bwana.

1949:19 Law 26:33; Isa 62:4; Zek 10:10; Eze 36:10-11; Zek 2:4; Isa 60:18; 1:20“Ingawa uliangamizwa na kufanywa ukiwa,

na nchi yako ikaharibiwa,

sasa nafasi itakuwa finyu kwa ajili ya watu wako,

nao wale waliokuangamiza watakuwa mbali sana.

2049:20 Mt 3:9; Rum 11:11, 12Watoto waliozaliwa wakati wa msiba wako

bado watakuambia,

‘Mahali hapa ni finyu sana kwetu,

tupe eneo kubwa zaidi la kuishi.’

2149:21 Isa 5:13; Lk 15:5; Isa 60:4; 29:23; 66:7-8; 47:8; Yer 10:20; Mwa 15:2Ndipo utasema moyoni mwako,

‘Ni nani aliyenizalia hawa?

Nilikuwa nimefiwa, tena tasa;

nilikuwa nimehamishwa na kukataliwa.

Ni nani aliyewalea hawa?

Niliachwa peke yangu,

lakini hawa wametoka wapi?’ ”

2249:22 Isa 60:10-11; Hes 11:12; Mwa 3:14; Za 72:9; Kut 6:2; Mik 7:17; Mwa 3:14Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi:

“Tazama, nitawaashiria watu wa Mataifa,

nitainua bendera yangu kwa mataifa;

watawaleta wana wako mikononi yao,

na kuwabeba binti zenu juu ya mabega yao.

23Wafalme watakuwa baba zenu wa kuwalea,

na malkia wao watakuwa mama zenu wa kuwalea.

Watasujudu mbele yako nyuso zao zikigusa ardhi;

wataramba mavumbi yaliyo miguuni mwako.

Ndipo utajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana;

wale wanaonitumaini mimi hawataaibika.”

2449:24 Mt 12:29; Mk 3:27; Lk 11:21Je, nyara zaweza kuchukuliwa kutoka kwa mashujaa wa vita,

au mateka kuokolewa kutoka kwa watu wakali?

2549:25 Yer 50:33-34; Isa 14:2; 25:9; Mk 3:27; Isa 13:11; 25:4-9; 1Sam 24:15Lakini hili ndilo asemalo Bwana:

“Naam, mateka watachukuliwa kutoka kwa mashujaa,

na nyara zitapokonywa kutoka kwa watu wakali.

Nitashindana na wale wanaoshindana nawe,

nami nitawaokoa watoto wako.

2649:26 Isa 9:4, 20; Nah 1:10; Ufu 16:6; Eze 39:7; Hes 23:24; Yer 25:27; Isa 11:9; Ay 19:25; Isa 48:17; Mwa 49:24; Za 132:2Nitawafanya wale wanaokuonea kula nyama yao wenyewe,

watalewa kwa damu yao wenyewe,

kama vile kwa mvinyo.

Ndipo wanadamu wote watajua

ya kuwa Mimi, Bwana, ni Mwokozi wako,

Mkombozi wako, niliye Mwenye Nguvu wa Yakobo.”