以西结书 19 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

以西结书 19:1-14

以色列的哀歌

1“你要为以色列的首领唱哀歌, 2说,

“‘你的母亲像什么?

她就像狮群中的母狮,

卧在雄壮的狮子中养育幼狮。

3母狮养大一头幼狮,

使它成为一头猛狮。

它学会了捕猎和吃人。

4列国的人知道后,

便设陷阱捉住它,

用钩子拉到埃及

5母狮盼着它回来,

眼见指望落空,

便又养育一头幼狮,

使它成为一头猛狮。

6它出入狮群,

长成一头猛狮,

学会了捕食和吃人。

7它夷平列国的堡垒,

使他们的城邑沦为废墟,

遍地都因它的咆哮而震惊。

8于是,列国便从四面围攻它,

设网罗捕捉它。

它落入他们的陷阱。

9他们用钩子钩住它,把它关进笼里,

解送到巴比伦王那里囚禁起来。

于是,在以色列的山岭上再也听不见它的吼声。

10“‘你母亲像葡萄园中的一棵葡萄树,

栽在溪水旁,

枝繁叶茂,硕果累累,

因为水源充沛。

11它的枝子粗壮,可作王的杖。

它的树干高大,直插云霄,

枝叶茂密,远远可见。

12但它被愤怒地连根拔起,

抛在地上。

东风吹干了它的果实,

粗壮的枝干折断枯干,

被火焚烧。

13现在,它被栽种在干旱的旷野。

14火从枝干蔓延,

烧毁了它的果实,

没有留下一根粗壮的枝干可作王的杖。’

“这是一首哀歌,可作哀悼之用。”

Kiswahili Contemporary Version

Ezekieli 19:1-14

Maombolezo Kwa Ajili Ya Wakuu Wa Israeli

119:1 Yer 7:29; 2Nya 24:6; Eze 26:17; Yer 9:10, 20; Eze 27:32; 28:12“Wewe fanya maombolezo kuhusu wakuu wa Israeli 219:2 Hes 23:24; Mwa 49:9na useme:

“ ‘Tazama jinsi gani mama yako alivyokuwa simba jike

miongoni mwa simba!

Alilala katikati ya wana simba

na kulisha watoto wake.

319:3 Eze 19:6; 2Fal 23:31, 32Alimlea mmoja wa watoto wake,

naye akawa simba mwenye nguvu.

Akajifunza kurarua mawindo

naye akala watu.

419:4 2Nya 36:4; Mao 4:20; Ay 41:2; 2Fal 23:33-34Mataifa wakasikia habari zake,

naye akanaswa katika shimo lao.

Wakamwongoza kwa ndoana

mpaka nchi ya Misri.

519:5 2Fal 23:34; Mwa 49:9“ ‘Mama yake alipongoja na kuona tumaini lake halitimiziki,

nayo matarajio yake yametoweka,

akamchukua mwanawe mwingine

na kumfanya simba mwenye nguvu.

619:6 Yer 22:13; 2Nya 36:9; 2Fal 24:9Alizungukazunguka miongoni mwa simba,

kwa kuwa sasa alikuwa simba mwenye nguvu.

Akajifunza kurarua mawindo

naye akala watu.

719:7 Eze 29:10; 30:12Akabomoa ngome zao

na kuiharibu miji yao.

Nchi na wote waliokuwa ndani yake

wakatiwa hofu kwa kunguruma kwake.

819:8 2Fal 24:2, 11; Mao 4:20; Eze 12:13; 2Fal 24:11Kisha mataifa wakaja dhidi yake

kutoka sehemu zilizomzunguka.

Wakatanda nyavu zao kwa ajili yake,

naye akanaswa katika shimo lao.

919:9 2Fal 25:7; 24:15; 2Nya 36:6; 2Fal 19:28; Zek 11:3Kwa kutumia ndoana wakamvutia kwenye tundu

na kumleta mpaka kwa mfalme wa Babeli.

Wakamtia gerezani, hivyo kunguruma kwake

hakukusikika tena

katika milima ya Israeli.

1019:10 Za 80:8-11; Eze 15:2; Yer 17:8; Mwa 49:22“ ‘Mama yako alikuwa kama mzabibu

katika shamba lako la mizabibu

uliopandwa kando ya maji,

ukiwa unazaa sana na wenye matawi mengi

kwa sababu ya wingi wa maji.

1119:11 Eze 31:3; Dan 4:11Matawi yake yalikuwa na nguvu,

yaliyofaa kuwa fimbo ya enzi ya mtawala.

Ulikuwa mrefu kupita miti mingine

katikati ya matawi manene;

ulionekana kwa urahisi

kwa ajili ya urefu wake

na wingi wa matawi yake.

1219:12 Kum 29:28; Eze 17:10; Hos 13:15; Isa 27:11; Eze 28:17; Mwa 41:6Lakini ulingʼolewa kwa hasira kali

na kutupwa chini.

Upepo wa mashariki uliufanya usinyae,

matunda yake yakapukutika,

matawi yake yenye nguvu yakanyauka

na moto ukayateketeza.

1319:13 Eze 20:35; Hos 2:14; 2:3Sasa umepandwa jangwani

katika nchi kame na ya kiu.

1419:14 Amu 9:15; Eze 20:47; 15:4Moto ulienea kuanzia katika mmojawapo ya matawi yake makubwa

na kuteketeza matunda yake.

Hakuna tawi lenye nguvu lililobaki juu yake

lifaalo kuwa fimbo ya enzi ya mtawala.’

Hili ndilo ombolezo, na litumike kama ombolezo.”