Левит 9 – CARST & NEN

Священное Писание (Восточный перевод), версия для Таджикистана

Левит 9:1-24

Священнослужители начинают служение

1На восьмой день Мусо позвал Хоруна с его сыновьями и старейшин Исроила. 2Он сказал Хоруну:

– Возьми телёнка для жертвы за грех и барана для всесожжения, обоих без изъяна, и поставь их перед Вечным. 3Скажи исроильтянам: «Возьмите козла для жертвы за грех, телёнка и ягнёнка – годовалых и без изъяна – для всесожжения, 4и вола9:4 Или: «корову», также в ст. 18 и 19. с бараном для жертвы примирения, чтобы принести их в жертву Вечному вместе с хлебным приношением, смешанным с маслом. Ведь сегодня вам явится Вечный».

5То, что велел Мусо, принесли к шатру встречи, и всё общество подошло и встало перед Вечным. 6Мусо сказал:

– Вечный повелел вам сделать это, чтобы вам явилась слава Вечного.

7Мусо сказал Хоруну:

– Подойди к жертвеннику и принеси свою жертву за грех и всесожжение, чтобы очистить себя и народ. Сделай приношение за народ, чтобы очистить его, как повелел Вечный.

8Хорун подошёл к жертвеннику и заколол телёнка в жертву за свой грех. 9Сыновья подали ему кровь, он обмакнул в кровь палец и помазал рога жертвенника. Остальную кровь он вылил к основанию жертвенника. 10На жертвеннике он сжёг жир, почки и сальник с печени из жертвы за грех, как повелел Мусо Вечный. 11Мясо и шкуру он сжёг за лагерем.

12Следом он заколол жертву всесожжения. Сыновья подали ему кровь, и он окропил ею жертвенник со всех сторон. 13Они подавали ему жертву всесожжения кусок за куском, включая голову, и он сжёг это на жертвеннике. 14Он вымыл требуху и ноги жертвы и сжёг их на жертвеннике поверх всесожжения.

15Потом Хорун принёс жертву за народ. Он взял козла – приношение за грех народа, заколол его и принёс в жертву за грех, как и первое всесожжение.

16Он принёс жертву всесожжения и всё сделал по установлению. 17Ещё он принёс хлебное приношение, взял из него пригоршню и сжёг на жертвеннике в добавление к утреннему всесожжению.

18Он заколол вола и барана в жертву примирения. Сыновья подали ему кровь, и он окропил ею жертвенник со всех сторон. 19Но жир вола и барана – курдюк, слой жира вокруг почек и сальник с печени – 20он положил на грудь жертвы, а потом сжёг на жертвеннике. 21Хорун потряс грудину и правое бедро жертвы перед Вечным как приношения потрясания, как повелел Мусо.

22Хорун поднял руки над народом и благословил его. Принеся жертву за грех, всесожжение и жертву примирения, он сошёл с жертвенника.

23Мусо и Хорун вошли в шатёр встречи. Выйдя, они благословили народ, и народу явилась слава Вечного. 24Вечный послал огонь, который сжёг всесожжение и жир на жертвеннике. Увидев это, все закричали от радости и пали лицом на землю.

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Walawi 9:1-24

Makuhani Waanza Huduma Yao

19:1 Eze 43:27; Law 4:15Katika siku ya nane, Mose akawaita Aroni na wanawe, na wazee wa Israeli. 29:2 Law 4:3; 8:14-18Akamwambia Aroni, “Chukua ndama dume kwa ajili ya sadaka yako ya dhambi, na kondoo dume kwa sadaka yako ya kuteketezwa, wote wawili wasiwe na dosari, nao uwalete mbele za Bwana. 39:3 Law 4:3, 32; 10:16; Ezr 6:17; Isa 53:10; Rum 8:3; 1Pet 2:24Kisha waambie Waisraeli: ‘Chukueni mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na ndama na mwana-kondoo, wote wawili wawe wa umri wa mwaka mmoja, na wasio na dosari, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, 49:4 Law 4:10; Kut 32:6; 29:43; 9:6; 16:7; 24:16; 40:34-35; 1Fal 8:10-12na pia maksai na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya amani, ili kutoa dhabihu mbele za Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka iliyochanganywa na mafuta. Kwa kuwa leo Bwana atawatokea.’ ”

5Wakavileta vile vitu Mose alivyowaagiza mbele ya Hema la Kukutania, nalo kusanyiko lote likakaribia na kusimama mbele za Bwana. 6Ndipo Mose akasema, “Hili ndilo Bwana alilowaagiza mlifanye, ili utukufu wa Bwana upate kuonekana kwenu.”

79:7 Law 16:6; Kut 30:10; Ebr 4:1-4; 7:27; 1Sam 3:14Mose akamwambia Aroni, “Njoo madhabahuni ili utoe dhabihu yako ya sadaka ya dhambi na sadaka yako ya kuteketezwa, ufanye upatanisho kwa ajili yako mwenyewe na kwa ajili ya watu. Kisha utoe sadaka ya upatanisho kwa ajili ya watu, kama vile Bwana alivyoagiza.”

89:8 Law 4:1-12; 10:19; 9:9; Kut 29:12; Eze 43:20; Law 4:7; 8:15Hivyo Aroni akaja madhabahuni na kumchinja yule ndama kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe. 9Wanawe wakamletea damu, naye akachovya kidole chake katika hiyo damu, akaitia kwenye pembe za madhabahu, nayo damu iliyobaki akaimwaga chini ya madhabahu. 10Juu ya madhabahu akateketeza mafuta, figo na mafuta yanayofunika ini kutoka kwenye hiyo sadaka ya dhambi, kama Bwana alivyomwagiza Mose. 119:11 Law 4:11-12Akateketeza nyama na ngozi nje ya kambi.

129:12 Law 10:19Kisha Aroni akachinja sadaka ya kuteketezwa. Wanawe wakamletea damu, naye akainyunyiza pande zote za madhabahu. 139:13 Law 1:8-9Wakamletea sadaka ya kuteketezwa kipande kwa kipande, pamoja na kichwa, naye akaviteketeza juu ya madhabahu. 149:14 Isa 53:10; 1Kor 15:3; 2Kor 5:21; Gal 1:4; Ebr 2:17; 1Pet 2:24; 3:18Akasafisha sehemu za ndani na miguu, akaviteketeza juu ya sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu.

159:15 Law 4:27-31Kisha Aroni akaleta sadaka ile iliyokuwa kwa ajili ya watu. Akachukua yule mbuzi wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya watu, akamchinja na kumtoa kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kama alivyofanya kwa ile ya kwanza.

169:16 Law 1:1-13Aroni akaleta sadaka ya kuteketezwa na kuitoa kama ilivyoelekezwa. 179:17 Law 2:1-2; 3:5; Kut 29:38; 9:18; Law 3:1-11Pia akaleta sadaka ya nafaka, akachukua konzi moja na kuiteketeza juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya kuteketezwa ya asubuhi.

18Akachinja maksai na kondoo dume kama sadaka ya amani kwa ajili ya watu. Wanawe Aroni wakampa ile damu, naye akainyunyiza kwenye madhabahu pande zote. 19Lakini sehemu zile za mafuta ya yule maksai na kondoo dume, yaani mafuta ya mkia, mafuta yaliyofunika tumbo, ya figo na yaliyofunika ini, 20hivi vyote wakaviweka juu ya vidari, kisha Aroni akayateketeza hayo mafuta ya wanyama juu ya madhabahu. 219:21 Kut 29:24-26; Law 7:30-34Aroni akaviinua vile vidari na paja la kulia mbele za Bwana ili viwe sadaka ya kuinuliwa, kama Mose alivyoagiza.

229:22 Mwa 48:20; Kut 39:43; Lk 24:50Kisha Aroni akainua mikono yake kuwaelekea watu na kuwabariki. Naye baada ya kutoa dhabihu ya sadaka ya dhambi, sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya amani, akashuka chini.

239:23 Kut 40:2; 24:16; 2Sam 6:18; 2Nya 16:2; Hes 16:19Kisha Mose na Aroni wakaingia kwenye Hema la Kukutania. Walipotoka nje, wakawabariki watu. Nao utukufu wa Bwana ukawatokea watu wote. 249:24 Kut 19:18; Amu 6:21; 13:20; 1Fal 18:39; Mwa 15:17; 2Nya 7:1; Ezr 3:1Moto ukaja kutoka uwepo wa Bwana, ukairamba ile sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sehemu ya mafuta yaliyokuwa juu ya madhabahu. Watu wote walipoona jambo hili, wakapiga kelele kwa furaha na kusujudu.