Zaburi 94:1-11
Zaburi 94
Mungu Mlipiza Kisasi Kwa Ajili Ya Wenye Haki
94:1 Mwa 4:24; Za 80:1; Rum 12:19; Kum 33:2Ee Bwana, ulipizaye kisasi,
Ee Mungu ulipizaye kisasi, uangaze sasa.
94:2 Mwa 18:25; Yak 5:9; Hes 10:35; Za 31:23Ee Mhukumu wa dunia, inuka,
uwalipize wenye kiburi kama wanavyostahili.
94:3 Za 13:2; Mwa 20:3Hata lini, waovu, Ee Bwana,
hata lini waovu watashangilia?
94:4 Yer 43:2; Za 52:1; Yud 15Wanamimina maneno ya kiburi,
watenda mabaya wote wamejaa majivuno.
94:5 Za 28:9; 44:2; 74:8; Isa 3:15; Yer 8:21Ee Bwana, wanawaponda watu wako,
wanawaonea urithi wako.
94:6 Kum 10:18; 20:19; Isa 1:17Wanamchinja mjane na mgeni,
na kuwaua yatima.
94:7 Ay 22:14; Mwa 24:12Nao husema, “Bwana haoni,
Mungu wa Yakobo hafahamu.”
94:8 Kum 32:6; Za 73:22Sikizeni, enyi wajinga miongoni mwa watu;
enyi wapumbavu, lini mtakuwa na hekima?
94:9 Kut 4:11; Mit 20:12Je, aliyeweka sikio asisikie?
Aliyeumba jicho asione?
94:10 Za 39:11; Ay 35:11; Yn 6:45; Isa 2:3; 28:26; Kut 35:34Je, anayeadhibisha mataifa asiadhibu?
Je, awafundishaye wanadamu asiwe na maarifa?
94:11 Za 139:2; Mt 15:26; 9:4; 1Kor 3:20; 1:21Bwana anajua mawazo ya mwanadamu;
anajua kwamba ni ubatili.