Zaburi 89:1-8
Zaburi 89
Wimbo Wakati Wa Taabu Ya Kitaifa
Utenzi wa Ethani Mwezrahi.
89:1 Za 59:16; 36:5; 40:10Nitaimba juu ya upendo mkuu wa Bwana milele;
kwa kinywa changu nitajulisha uaminifu wako
ujulikane kwa vizazi vyote.
89:2 Za 36:5Nitatangaza kuwa upendo wako unasimama imara milele
na uaminifu wako umeuthibitisha mbinguni.
89:3 Eze 34:23; Hes 3:5; Ebr 7:21; Mdo 2:30Ulisema, “Nimefanya agano na mteule wangu,
nimemwapia mtumishi wangu Daudi,
89:4 2Sam 7:12-16; Lk 1:32, 33; Mt 1:1; Isa 9:6, 7; Rum 1:3; 1Fal 9:5; 8:16; Eze 37:24, 25; Za 132:11, 12‘Nitaimarisha uzao wako milele
na kudumisha ufalme wako kwa vizazi vyote.’ ”
89:5 Za 19:1; 1:5Ee Bwana, mbingu zinayasifu maajabu yako,
uaminifu wako pia katika kusanyiko la watakatifu.
89:6 Mwa 1:26; Kut 9:14; Za 18:31; 113:5Kwa kuwa ni nani katika mbingu
anayeweza kulinganishwa na Bwana?
Ni nani miongoni mwa viumbe vya mbinguni
aliye kama Bwana?
89:7 Ay 5:1; Za 11:1; 47:2Katika kusanyiko la watakatifu, Mungu huogopwa sana,
anahofiwa kuliko wote wanaomzunguka.
89:8 Isa 6:3; Za 71:19Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote,
ni nani aliye kama wewe?
Ee Bwana, wewe ni mwenye nguvu,
na uaminifu wako unakuzunguka.