Zaburi 78:1-8
Zaburi 78
Mungu Na Watu Wake
Utenzi wa Asafu.
78:1 Kut 19:5; Kum 32:29; Isa 51:4; 55:3Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu,
sikilizeni maneno ya kinywa changu.
78:2 Za 49:4; Mt 13:35Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo,
nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
78:3 Za 44:1; Amu 6:13yale ambayo tuliyasikia na kuyajua,
yale ambayo baba zetu walituambia.
78:4 Kut 12:26; Yos 4:6, 7; Kum 4:9; 11:19; 32:7; Za 71:18; 26:7; 71:17Hatutayaficha kwa watoto wao;
tutakiambia kizazi kijacho
matendo yastahiliyo sifa ya Bwana,
uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
78:5 Za 19:7; 81:5; 147:19Aliagiza amri kwa Yakobo
na akaweka sheria katika Israeli,
ambazo aliwaamuru baba zetu
wawafundishe watoto wao,
78:6 Za 22:31; 102:18ili kizazi kijacho kizijue,
pamoja na watoto ambao watazaliwa,
nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
78:7 Kum 6:12; 5:29Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu,
nao wasingesahau matendo yake,
bali wangalizishika amri zake.
78:8 2Nya 30:7; Kut 32:9; 23:21; Kum 21:18; Isa 30:9; 65:2Ili wasifanane na baba zao,
waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi,
ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake,
ambao roho zao hazikumwamini.