Zaburi 78:1-8 NEN

Zaburi 78:1-8

Zaburi 78

Mungu Na Watu Wake

Utenzi wa Asafu.

78:1 Kut 19:5; Kum 32:29; Isa 51:4; 55:3Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu,

sikilizeni maneno ya kinywa changu.

78:2 Za 49:4; Mt 13:35Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo,

nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:

78:3 Za 44:1; Amu 6:13yale ambayo tuliyasikia na kuyajua,

yale ambayo baba zetu walituambia.

78:4 Kut 12:26; Yos 4:6, 7; Kum 4:9; 11:19; 32:7; Za 71:18; 26:7; 71:17Hatutayaficha kwa watoto wao;

tutakiambia kizazi kijacho

matendo yastahiliyo sifa ya Bwana,

uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.

78:5 Za 19:7; 81:5; 147:19Aliagiza amri kwa Yakobo

na akaweka sheria katika Israeli,

ambazo aliwaamuru baba zetu

wawafundishe watoto wao,

78:6 Za 22:31; 102:18ili kizazi kijacho kizijue,

pamoja na watoto ambao watazaliwa,

nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.

78:7 Kum 6:12; 5:29Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu,

nao wasingesahau matendo yake,

bali wangalizishika amri zake.

78:8 2Nya 30:7; Kut 32:9; 23:21; Kum 21:18; Isa 30:9; 65:2Ili wasifanane na baba zao,

waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi,

ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake,

ambao roho zao hazikumwamini.

Read More of Zaburi 78