Zaburi 70:1-5 NEN

Zaburi 70:1-5

Zaburi 70

Kuomba Msaada

(Zaburi 40:13-17)

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Maombi.

70:1 Za 35:4; 6:10; 35:26; 71:12; 109:29; 129:5Ee Mungu, ufanye haraka kuniokoa;

Ee Bwana, njoo hima unisaidie.

70:2 Za 35:2Wale wanaotafuta kuuondoa uhai wangu,

waaibishwe na kufadhaishwa;

wote wanaotamani kuangamizwa kwangu,

warudishwe nyuma kwa aibu.

Wale waniambiao, “Aha! Aha!”

warudi nyuma kwa sababu ya aibu yao.

70:4 Za 31:6, 7; 35:27; 32:11; 118:24; 9:10Lakini wote wakutafutao

washangilie na kukufurahia,

wale wapendao wokovu wako siku zote waseme,

“Mungu na atukuzwe!”

70:5 Za 109:22; 141:1; 30:10; 86:1; 33:10; 18:2; 119:60Lakini bado mimi ni maskini na mhitaji;

Ee Mungu, unijie haraka.

Wewe ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu;

Ee Bwana, usikawie.

Read More of Zaburi 70