Zaburi 68:28-35
68:28 Kut 9:16; Za 29:11; Isa 26:12; 29:23; 45:11; 60:21; 64:8Ee Mungu, amuru uwezo wako,
Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako,
kama ulivyofanya hapo awali.
68:29 2Nya 9:24; 32:23Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu
wafalme watakuletea zawadi.
68:30 Isa 27:1; 34:7; 51:9; Ay 40:21; Eze 29:3; Za 22:12; 18:14; 120:7; 89:10; 140:2; Yer 50:27Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi,
kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa.
Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea.
Tawanya mataifa yapendayo vita.
68:31 Isa 19:19; 43:3; 45:14; 11:11; 18:1; Sef 3:10Wajumbe watakuja kutoka Misri,
Kushi68:31 Kushi hapa ina maana maeneo ya Naili ya juu, yaani Ethiopia. atajisalimisha kwa Mungu.
68:32 Za 46:6; 67:4; 7:17Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia,
mwimbieni Bwana sifa,
68:33 Kum 33:26; Kut 9:23; Za 29:3, 4; Isa 30:30; 33:3; 66:6; 45:3mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu,
yeye angurumaye kwa sauti kuu.
68:34 Za 68:28; 45:3Tangazeni uwezo wa Mungu,
ambaye fahari yake iko juu ya Israeli,
ambaye uwezo wake uko katika anga.
68:35 Mwa 28:17; Isa 40:29; 41:10; 50:2; Za 66:20; 18:1; 29:11; 28:6; 2Kor 1:3; Kum 7:21Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako,
Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu.
Mungu Asifiwe!