Zaburi 68:21-27
68:21 Za 74:14; 110:5; Hab 3:13Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake,
vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
68:22 Ay 36:30; Mt 18:6Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani;
nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
68:23 Za 58:10; 1Fal 21:19; 2Fal 9:36ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako,
huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
68:24 Za 63:2Ee Mungu, maandamano yako yameonekana,
maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu,
yakielekea patakatifu pake.
68:25 1Nya 15:16; 6:31; 2Nya 5:12; Ufu 18:22; Mwa 31:27; Isa 5:12Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda,
pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
68:26 Za 22:22; Ebr 2:12; Law 19:2Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa,
msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
68:27 1Sam 9:21; Hes 34:21; Amu 5:18Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza,
wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda,
hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.