Zaburi 50:1-15
Zaburi 50
Ibada Ya Kweli
Zaburi ya Asafu.
50:1 Yos 22:22; Za 113:3Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana,
asema na kuiita dunia,
tangu mawio ya jua
hadi mahali pake liendapo kutua.
50:2 Za 2:6; 48:2; Mao 2:15; Kum 33:2Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu,
Mungu anaangaza.
50:3 Isa 30:28; 42:14; 64:12; 29:6; 65:6; Za 18:8; 107:25; 96:13; 83:15; 147:18; Ay 37:9; Yn 1:4; Nah 1:3Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya,
moto uteketezao unamtangulia,
akiwa amezungukwa na tufani kali.
50:4 Kum 4:26; 31:26; Isa 1:2; Ebr 10:30; Mik 6:1, 2Anaziita mbingu zilizo juu,
na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
50:5 Kum 7:6; Za 18:25; Kut 24:7; 1Kor 6:2; 2Nya 6:11; Isa 13:3; 1The 3:13; Ebr 8:6; Yud 14; Mwa 24:7; Isa 59:20, 21“Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu,
waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
50:6 Za 19:1; Ay 9:15; Mwa 16:5Nazo mbingu zinatangaza haki yake,
kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
50:7 Ebr 2:4; Kut 20:2; Za 48:14“Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema,
ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu:
Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
50:8 2Sam 22:16; Za 40:6Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako,
au sadaka zako za kuteketezwa,
ambazo daima ziko mbele zangu.
50:9 Hes 32:16; Law 1:5; 16:5; Mdo 17:25; Mik 6:6; Isa 43:23Sina haja ya fahali wa banda lako,
au mbuzi wa zizi lako.
50:10 Za 104:20, 24; Isa 56:9; Mik 5:8Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu,
na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
50:11 Mt 6:26; Za 8:7; 80:13Ninamjua kila ndege mlimani,
nao viumbe wa kondeni ni wangu.
50:12 Kut 19:5; Kum 10:14; Ay 3:11; Za 24:1; 1Kor 10:26Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi,
kwa maana ulimwengu ni wangu,
pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
Je, mimi hula nyama ya mafahali
au kunywa damu ya mbuzi?
50:14 Ezr 1:4; Za 27:6; 66:13; 76:11; 7:8; Hes 30:2Toa sadaka za shukrani kwa Mungu,
timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
50:15 Zek 13:9; Isa 55:6; 58:9; Za 4:1; 3:7; 81:7; 69:17; 142:2; 86:7; 22:23; 107:6; Yak 5:13; Yn 15:8na uniite siku ya taabu;
nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”