Zaburi 44:1-12
Zaburi 44
Kuomba Ulinzi Wa Mungu
Kwa mwimbishaji. Utenzi wa wana wa Kora.
44:1 2Sam 7:22; 1Nya 17:20; Yer 26:11; Amu 6:13; Kum 32:7; Ay 37:23Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu,
baba zetu wametueleza
yale uliyotenda katika siku zao,
siku za kale.
44:2 Kut 15:17; Kum 7:1; Yos 10:42; 3:10; Mdo 7:45; Isa 60:21; Amu 4:23; 2Nya 14:13; Za 80:9; Yer 32:23Kwa mkono wako uliwafukuza mataifa
na ukawapanda baba zetu,
uliangamiza mataifa
na kuwastawisha baba zetu.
44:3 Yos 24:12; Kut 15:16; Za 78:54; 77:15; 79:11; 89:10, 15; Isa 40:10; 52:10; 63:5; Kum 4:37Sio kwa upanga wao waliipata nchi,
wala si mkono wao uliwapatia ushindi;
ilikuwa ni kitanga cha mkono wako wa kuume,
na nuru ya uso wako,
kwa kuwa uliwapenda.
44:4 Za 24:7; 5:2; 21:5; 74:12Wewe ni mfalme wangu na Mungu wangu,
unayeamuru ushindi kwa Yakobo.
44:5 Yos 23:5; Za 60:12; 108:13; Dan 8:10Kwa uwezo wako tunawasukuma nyuma watesi wetu;
kwa jina lako tunawakanyaga adui zetu.
44:6 Za 33:16; Hos 1:7; Mwa 48:22Siutumaini upinde wangu,
upanga wangu hauniletei ushindi;
44:7 Kum 20:4; Ay 8:2bali wewe unatupa ushindi juu ya adui zetu,
unawaaibisha watesi wetu.
44:8 1Kor 1:3; Rum 2:17; Za 34:2; 52:1; 30:12; 2Kor 10:17Katika Mungu wetu tunajivuna mchana kutwa,
nasi tutalisifu jina lako milele.
44:9 Kum 8:3; 31:17; Za 43:2; 107:39; 108:11; Isa 5:15; Yos 7:12Lakini sasa umetukataa na kutudhili,
wala huendi tena na jeshi letu.
44:10 Law 26:17; Amu 2:14; Kum 28:25Umetufanya turudi nyuma mbele ya adui,
nao watesi wetu wametuteka nyara.
44:11 Yer 12:3; 32:37; Law 26:33; Zek 2:6; Kum 4:27; Eze 6:8; Lk 21:24; Za 9:11; 60:1; 2Fal 17:6Umetuacha tutafunwe kama kondoo
na umetutawanya katika mataifa.
44:12 Kum 32:30; Isa 50:1; 52:3; Yer 15:13Umewauza watu wako kwa fedha kidogo,
wala hukupata faida yoyote kwa mauzo yao.