Zaburi 35:11-18 NEN

Zaburi 35:11-18

35:11 Kut 23:1; Mt 26:60Mashahidi wakatili wanainuka,

wananiuliza mambo nisiyoyajua.

35:12 Yer 18:20; Za 38:20; 109:5; Mit 17:13Wananilipa baya kwa jema

na kuiacha nafsi yangu ukiwa.

35:13 2Sam 3:31; 1Fal 20:31; Za 30:11; 69:10, 11; 109:24; Ay 30:25Lakini walipokuwa wagonjwa, nilivaa nguo ya gunia

na nikajinyenyekesha kwa kufunga.

Maombi yangu yaliponirudia bila kujibiwa,

35:14 Za 38:6; 42:9; 43:2niliendelea kuomboleza

kama vile wao ni rafiki au ndugu.

Niliinamisha kichwa chini kwa huzuni

kama ninayemwombolezea mama yangu.

35:15 Ay 31:29; 16:10Lakini nilipojikwaa,

walikusanyika kwa shangwe;

washambuliaji walijikusanya dhidi yangu

bila mimi kujua.

Walinisingizia pasipo kukoma.

35:16 Za 22:7; Mk 10:34; 9:18; Ay 16:9; Mdo 7:54Kama watu wasiomcha Mungu, wamenidhihaki,

wamenisagia meno.

35:17 Za 6:3; 22:20, 21; 57:4; 58:6Ee Bwana, utatazama mpaka lini?

Niokoe maisha yangu na maangamizi yao,

uhai wangu wa thamani

kutokana na simba hawa.

35:18 Za 22:20, 25; 42:4; 109:30Nami nitakushukuru mbele ya kusanyiko kubwa,

nitakusifu katikati ya watu wengi.

Read More of Zaburi 35